FP,
Kwa kweli, waliokupatia majina (kwa hali yoyote ile) wamekosa. Binafsi, mimi nimekujibu vyema (natumaini hili) na sikukuita jina lolote kwa vile mimi nakufahamu (kupitia mitandao hii) kwa muda mrefu.
Wakati mwingine, huwezi kucontrol kila kitu kinachoandikwa hapa. Watu wamekuwa very angry na kilichofanywa na ccm kwenye kamati ya Mwinyi na kile kinachofanyika Chadema wakati huu.
Watu wanakata tamaa so wakati mwingine hizi flairs zitakuwepo. Cha kufanya ni wewe kuendelea kufanya vile umekuwa unafanya miaka yote. Kuendelea kujadili hoja.
Hayo mengine achana nayo - ingawa mimi nitakuwa nawajibu kipuuzi wale wote wanaokuja kipuuzi kwangu. Kwangu mimi hakuna high road kwa mtu ambaye hana high road to begin with.
Mwafrika you are right,
lakini umeanza kuni attack mimi wakati nilikuwa nauliza maswali na kuleta hoja, rudi nyuma angalia post yako ya kwanza kunijibu hukutakiwa kunijibi vile
Lingine, napenda na ninatamani CCM waondoke hata kesho, lakini lazima tujenge chama kizuri.There is no life in CCM
wapigaji kura hawamo humu JF, wengi wetu kwanza tuko nje, na hata hizo kura mwakani hatutapiga
Makosa yoyote ya Chadema ndiyo yanayotumika na CCM kuwakosesha kura chadema! hivyo kwa hali ya sasa chadema lazima wawe waangalifu katika kila wakifanyacho ili adui zao CCM wasipate mwanya wa kuwazidi
Wapiga kura hawana upeo wako MWAFRIKA, wao wakiimbiwa nyimbo na Komba au na khadika kopa wanavutika tu.
Tuhuma za chama za kiukoo, kikabila n.k ni ishu ambazo ama kwa hakika wewe na mimi tunajua hazipo, lakini wapiga kura ambao ni waamuzi wa mwisho ndio wafungaji magoli
Tunaposema humu na kupose challenge kwa chadema is for good, maana hawatapita bila hizi challenge.
Nisemapo mimi sina chama jamani na matumaini yangu ni Chadema, angalau kuna mwanga
Tukidanganyana humu na kupakana mafuta as if hatujui field kuko vipi tunapoteza muda.
Nimewafanyia kampeni chadema jimbo la ubungo, sikuwa na kadi na nilipiga kura yangu kwa mbunge mtarajiwa,
na katika kupiga kampeni tulielezana sana umuhimu wa kwenda ndani zaidi 'ubungo vijijini' amani usiamini ubungo kubwa ile
Tulizani tutashinda kwa matumaini ya usoni(superficial) ukiona
to be honest tangu muda ule nimevunjika sana moyo, kushangiliwa hakutoshi
MWAFRIKA nimelala na njaa na kukosa chips mara mbili usiku nikiwa napiga kampeni ubungo
Nilikaa chini na kutafakari nikagundua kosa liko wapi
tunaongea mno vitabuni na kwenye e-mail mikutano n.k lakini kule kwa watu hatuooneani CCM wakizusha chochote kile wananchi kuamini ni rahisi
Niko nje na natarajia kuchukua kadi rasmi ya chadema , lakini katu sitapoteza muda kama matarajio yangu naamini kabisa ni zero!
Mkuu wwe chadema, lakini mimi nimeifanyia kazi, kwa mapenzi sikuwa mwanachama simply kwa sababu ya sababu nisizoweza kuandika hapa.
sitakujibu tena, ila furaha ya watanzania wengi ni kuona chama kipya kinaingia madarakani, tusiubebe unafiki na kujipa moyo kuwa ukiwashinda kwa hoja watu humu basi NDIO UMEPATA KURA, my friend things there are different.watanzania hawa mtu unamweleza ubaya wa CCM baada ya kumaliza mazungumzo anakuambia nitaipigia CCM , nimevishuhudia hivi vitu ndugu yangu, people are hard there than you can imagine
wanaosema CCM itachukua muda mrefu wako sahihi kabisa, thats is the facts and to change it is not easy, truth ni kuwa kila kitu kinawezekana!
uwezekano huo ni chadema kufanya move za uhakika, undisputable and clean!
Hii ni reality
I will write to you after election marks this words,
sehemu ambazo chadema wanashinda, jamii ya hiyo sehemu wameshalishwa uchadema na siyo rahisi kuwabadilisha hawa watanzania ndugu, kuwabadilisha maeneo mengine ni kazi sana, ushahidi unao
Chadema inaweza, tunapondika post humu wakisoma akina mbowe, slaa na wanapata picha ya kujipanga field, tukiwapa moyo na matarajio hewa, tunapoteza muda humu kaka
kazi njema