Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 80
mhariri wa Mtanzania leo ameamua kuwavaa Mnyika na Mrema akiwahusisha na kutenguliwa uteuzi wa Kafulila na Danda. Mhariri huyo katika habari yake ya leo ya ukurasa wa mbele ameeleza kwamba vijana hawana walikuwa na uhusiano wa karibu na Zitto Kabwe lakini wamgeuka na kuwa karibu na Mbowe. Mhariri huyo ameeleza kwamba kugeuka kwao kumetokana na ukabila na maslahi binafsi. Mwandishi wa habari huyo amewataja wakurugenzi hawa wawili wa chama hicho kuwa wote ni wachagga. Habari hiyo imewahusisha wabunge wa CHADEMA na wakurugenzi wa chama hicho kuwa wote wako kwenye mkakati wa kummaliza kisiasa Zitto Kabwe kwa ajili ya kuisaidia CCM.
.......ndiyohiyo
Habari hiyo ilipikwa na Balille kwa kushauriana na Kafulila kabla hata ya Sekretariati ya CHADEMA kukaa. Hebu ileteni habari yenyewe ichambuliwe, ilichoongezewa kipya ni nukuu moja tu toka kwa Kafulila. Ugomvi wa Balille na Mnyika ulianzia toka akiwa Rai https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/16440-mnyika-balille-rostam-aziz-na-kisa-cha-sms.html; kwa sasa huyu ndio Mhariri wa Mtanzania. Hapa NHC, Muhingo na Balille wanamamlaka makubwa sana. Sijui wamemlisha nini Manyerere jana akaipitisha hio stori
PM