Dares Salaam/Arusha.Kadinali Pengo alisema amepata taarifa kutoka kwa watu ambao hana na shaka nao.
Jana (juzi), niliongeleakwamba suala zima la tukio la Arusha halihusiani na imani yoyote ya kidini.Tamko hilo nilitamka kutokana na taarifa nilizofikishiwa na watu ambao sikuwezakuwa na shaka kwamba wanaoniambia ni kweli na sidhani kama ningekuwa na sababuya kusema wamefika kwa kunidanganya kwa hiyo tamko litakuwa limesimama juu yamsimamo huo, alisema Kadinali Pengo na kuongeza:
Lengo la msingi kabisa,langu na la kanisa ni kwamba tukio lolote lile liwe kwa nia mbaya au nzuri kwaupande wetu isiwe ni sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu waamani katika nchi yetu, alisema Pengo.
Alisema kuwa kilaanayehusika ajue amani ya kweli ya taifa lolote haiwezi ikapatikana isipokuwaikijengwa juu ya ukweli na ukweli kabisa bila kufuta au kujaribu kupotoshaukweli kwa namna yoyote ile.
Tusipojua kusema ukweliulivyo hatuwezi kufaulu kuleta amani katika taifa letu. Kwa hiyo pamoja nakuendelea kuwaomba waumini wa Katoliki pamoja na watu wenye mapenzi memakuendelea kumwomba Mwenyezi Mungu arehemu taifa letu na mapambano ya ainayoyote ile. Tuendeleze nia yetu njema ya kusema ukweli, haidhuru ukweli huuunamgusa nani, alisema Pengo.
Alisema kujaribu kufichaukweli na kupotosha ni njia sahihi kwa ibilisi kuleta vurugu katika jumuiya yawatu na ieleweke hivyo.
Naomba kila mtuakubaliane na tamko langu haidhuru pana kosa, amani ya taifa letu ni jambo lamsingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusemaukweli kama ulivyo, alisema.
Source: Mwananchi la Leo