Kardinali Pengo ametoa tamko kuwa shambulio la bomu kule kanisani Arusha ambalo limeua mpaka sasa watu watatu na kujeruhi takribani 40 sio la kidini yaani halihusiani na UDINI ndani ya Tanzania kwa sababu baadhi ya waliokamatwa ni wana majina ya kikristo na pia kuna watu walienda kumweleza wahusika na anawaamini.
Kwanza akiwa kama mtumishi wa Mungu nilifikiri angefunuliwa na Roho wa Bwana badala ya kutueleza eti kuna watu walienda kumweleza au watu hao walikuwa ni wajumbe wa Mungu kama ilivyokuwa kwa Abraham? watu hao ni akina nani na wanafanya nini? Pili, hivi shambulizi la kidini dhidi ya dini nyingine ni mpaka mtu awe na jina la dini ile? Je, hao akina Ambrose, David na Joseph ni wakristo kweli? ni wa dhehebu gani? kama ni wakatoliki walibatizwa wapi? je, wanahudhuria jumuiya ndogo ndogo? je ni bado wakristo? Na wale waarabu ni wakristo? je sio wale waarabu wamewapa fedha ili kutekeleza hazima ya dini nyingine?
Tatu, anasisitiza kusema ukweli wakati yeye mwenyewe anaficha ukweli, kwa nini asisimulie a whole story?
Nne, anaonekana kutuliza wakristo hasa wakatoliki kwa njia ambayo inatiwa wasiwasi. Mwisho, hivi vita ya udini haiko duniani? Tanzania sio sehemu ya dunia hii? Hivi ni kitabu gani cha dini gani kinasema maadui wakubwa wa dini yao ni Myaudi na Mkristo?!
Sources: Nipashe na Mwananchi 8/5/2013