Sakata la Bomu: Pengo afichua siri

Sakata la Bomu: Pengo afichua siri

Pengo kwa hili amekurupuka, ni kiongozi wangu wa dini ila kwa hili napingana nae! hata upelelezi haujaanza yeye tayari ana majibu ya nani kahusika, na kwamba sio tukio la kidini? mbona wasimbulie stendi ya mabasi ai baa wakasahambulie kanisani tena wakati balozi wa papa akiwa anaongoza ibada ya kutabaruku kanisa??anawaogoba hawa wabeba majambia au vipi??
 
Tumekamata watu saba na mkristo mmoja,, Bongo bana!!mambo tambaraaaaaaare.
 
Nimepoteza imani yangu kwa Pengo,sikutegemea kauli hii ktk mauaji makubwa ya kidini yaliyokuwa yakimlenga Balozi wa Papa.
 
Sasa hapa serikali Inajipongeza kanisa kuridhika Ngoma hii Lazima Tusukumiwe chadema..MASIKINI TANZANIAAAA
 
Nimesikiliza maelezo ya Cardinal Pengo kwa makini sana.
Nahisi kwa kauli hiyo kaingilia uchunguzi wa polisi kama inavyojulikana.
Nahisi kama tukio lile lingekuwa la kigaidi kawaida bila malengo maalumu, basi lingefanyika eidha maeneo kama mashuleni, masokoni, vituo vya mabasi na train, vyuo vikuu, mabaa na maclubs, mahotelini, shorpping centres n.k kwenye mikusanyiko mikubwa mda wote.
 
Sijui kwanini huwa haamini kuwa ni uhasama wa kidini, hata kule Zanzibar hakutoa tamko la maana.
Sijui mpaka akoswekoswe kwanza!
 
Nimesikiliza maelezo ya Cardinal Pengo kwa makini sana.
Nahisi kwa kauli hiyo kaingilia uchunguzi wa polisi kama inavyojulikana.
Nahisi kama tukio lile lingekuwa la kigaidi kawaida bila malengo maalumu, basi lingefanyika eidha maeneo kama mashuleni, masokoni, vituo vya mabasi na train, vyuo vikuu, mabaa na maclubs, mahotelini, shorpping centres n.k kwenye mikusanyiko mikubwa mda wote.
Kwa hiyo humuamini kiongozi wako wa kiroho?
 
Sijui kwanini huwa haamini kuwa ni uhasama wa kidini, hata kule Zanzibar hakutoa tamko la maana.
Sijui mpaka akoswekoswe kwanza!

mkuu, siasa zimeingia mpaka kwenye majumba ya Ibada!
 
Kardinali Pengo ametoa tamko kuwa shambulio la bomu kule kanisani Arusha ambalo limeua mpaka sasa watu watatu na kujeruhi takribani 40 sio la kidini yaani halihusiani na UDINI ndani ya Tanzania kwa sababu baadhi ya waliokamatwa ni wana majina ya kikristo na pia kuna watu walienda kumweleza wahusika na anawaamini.

Kwanza akiwa kama mtumishi wa Mungu nilifikiri angefunuliwa na Roho wa Bwana badala ya kutueleza eti kuna watu walienda kumweleza au watu hao walikuwa ni wajumbe wa Mungu kama ilivyokuwa kwa Abraham? watu hao ni akina nani na wanafanya nini? Pili, hivi shambulizi la kidini dhidi ya dini nyingine ni mpaka mtu awe na jina la dini ile? Je, hao akina Ambrose, David na Joseph ni wakristo kweli? ni wa dhehebu gani? kama ni wakatoliki walibatizwa wapi? je, wanahudhuria jumuiya ndogo ndogo? je ni bado wakristo? Na wale waarabu ni wakristo? je sio wale waarabu wamewapa fedha ili kutekeleza hazima ya dini nyingine?

Tatu, anasisitiza kusema ukweli wakati yeye mwenyewe anaficha ukweli, kwa nini asisimulie a whole story?

Nne, anaonekana kutuliza wakristo hasa wakatoliki kwa njia ambayo inatiwa wasiwasi. Mwisho, hivi vita ya udini haiko duniani? Tanzania sio sehemu ya dunia hii? Hivi ni kitabu gani cha dini gani kinasema maadui wakubwa wa dini yao ni Myaudi na Mkristo?!

Sources: Nipashe na Mwananchi 8/5/2013
 
Kardinali Pengo ametoa tamko kuwa shambulio la bomu kule kanisani Arusha ambalo limeua mpaka sasa watu watatu na kujeruhi takribani 40 sio la kidini yaani halihusiani na UDINI ndani ya Tanzania kwa sababu baadhi ya waliokamatwa ni wana majina ya kikristo na pia kuna watu walienda kumweleza wahusika na anawaamini.

Kwanza akiwa kama mtumishi wa Mungu nilifikiri angefunuliwa na Roho wa Bwana badala ya kutueleza eti kuna watu walienda kumweleza au watu hao walikuwa ni wajumbe wa Mungu kama ilivyokuwa kwa Abraham? watu hao ni akina nani na wanafanya nini? Pili, hivi shambulizi la kidini dhidi ya dini nyingine ni mpaka mtu awe na jina la dini ile? Je, hao akina Ambrose, David na Joseph ni wakristo kweli? ni wa dhehebu gani? kama ni wakatoliki walibatizwa wapi? je, wanahudhuria jumuiya ndogo ndogo? je ni bado wakristo? Na wale waarabu ni wakristo? je sio wale waarabu wamewapa fedha ili kutekeleza hazima ya dini nyingine?

Tatu, anasisitiza kusema ukweli wakati yeye mwenyewe anaficha ukweli, kwa nini asisimulie a whole story?

Nne, anaonekana kutuliza wakristo hasa wakatoliki kwa njia ambayo inatiwa wasiwasi. Mwisho, hivi vita ya udini haiko duniani? Tanzania sio sehemu ya dunia hii? Hivi ni kitabu gani cha dini gani kinasema maadui wakubwa wa dini yao ni Myaudi na Mkristo?!

Sources: Nipashe na Mwananchi 8/5/2013

Wewe na hao nipashe wote mpo nyuma ya wakati kitu ambacho ni hatari sana, Yerico Nyerere alileta kanusho hapa jamvini mara mbili, moja ikiwa ni usiku wa manane lkn yote hii ni baada ya kuwasiliana na idaraa ya habari ya TEC, ambayo inafanya kazi chini ya Kardinali Pengo.

Sasa nipashe wanapokuja na hii habari ambayo siyo reliable ina maanisha nn kwa watanzania?
 
Kama Kardinal kiongozi wako wa dini una mkataa.Hata Yesu akisema utamkataa.Manake kichwani mwako umeshajiweka maadui wa dini yako ni Waislamu tu.Peleka upuuzi wako huko
 
Wanataka wasikie waliokamatwa ni Athumani, Said, Addul qadri ili yale malengo na Mission zao zikamilike.Uislam haufutwi kwa Propaganda!
 
Kardinali Pengo ametoa tamko kuwa shambulio la bomu kule kanisani Arusha ambalo limeua mpaka sasa watu watatu na kujeruhi takribani 40 sio la kidini yaani halihusiani na UDINI ndani ya Tanzania kwa sababu baadhi ya waliokamatwa ni wana majina ya kikristo na pia kuna watu walienda kumweleza wahusika na anawaamini.

Kwanza akiwa kama mtumishi wa Mungu nilifikiri angefunuliwa na Roho wa Bwana badala ya kutueleza eti kuna watu walienda kumweleza au watu hao walikuwa ni wajumbe wa Mungu kama ilivyokuwa kwa Abraham? watu hao ni akina nani na wanafanya nini? Pili, hivi shambulizi la kidini dhidi ya dini nyingine ni mpaka mtu awe na jina la dini ile? Je, hao akina Ambrose, David na Joseph ni wakristo kweli? ni wa dhehebu gani? kama ni wakatoliki walibatizwa wapi? je, wanahudhuria jumuiya ndogo ndogo? je ni bado wakristo? Na wale waarabu ni wakristo? je sio wale waarabu wamewapa fedha ili kutekeleza hazima ya dini nyingine?

Tatu, anasisitiza kusema ukweli wakati yeye mwenyewe anaficha ukweli, kwa nini asisimulie a whole story?

Nne, anaonekana kutuliza wakristo hasa wakatoliki kwa njia ambayo inatiwa wasiwasi. Mwisho, hivi vita ya udini haiko duniani? Tanzania sio sehemu ya dunia hii? Hivi ni kitabu gani cha dini gani kinasema maadui wakubwa wa dini yao ni Myaudi na Mkristo?!

Sources: Nipashe na Mwananchi 8/5/2013

Mi kaniacha hoi pale alipo sema anawaamini walio enda kumwambia hizo habari
 
Pengo atakua anajua kitu...tatizo hizi information wanazitoa kidogo kidogo kama dozi..
Hata hayo majina kwanini wanaficha kutoa full name eti joseph, david...kha..!!
 
Wanataka wasikie waliokamatwa ni Athumani, Said, Addul qadri ili yale malengo na Mission zao zikamilike.Uislam haufutwi kwa Propaganda!
acha propaganda...hata kwa vita uislamu haufutikiki.
 
"naisi ni mapema sana kwa kiongozi huyu kutoa tamko kama hili" may be he was forced to do so.
 
Kadinali Pengo alisema amepata taarifa kutoka kwa watu ambao hana na shaka nao.



“Jana (juzi), niliongelea kwamba suala zima la tukio la Arusha halihusiani na imani yoyote ya kidini. Tamko hilo nilitamka kutokana na taarifa nilizofikishiwa na watu ambao sikuweza kuwa na shaka kwamba wanaoniambia ni kweli na sidhani kama ningekuwa na sababu ya kusema wamefika kwa kunidanganya kwa hiyo tamko litakuwa limesimama juu ya msimamo huo,” alisema Kadinali Pengo na kuongeza:



“Lengo la msingi kabisa, langu na la kanisa ni kwamba tukio lolote lile liwe kwa nia mbaya au nzuri kwa upande wetu isiwe ni sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu wa amani katika nchi yetu,” alisema Pengo.


Alisema kuwa kila anayehusika ajue amani ya kweli ya taifa lolote haiwezi ikapatikana isipokuwa ikijengwa juu ya ukweli na ukweli kabisa bila kufuta au kujaribu kupotosha ukweli kwa namna yoyote ile.




“Tusipojua kusema ukweli ulivyo hatuwezi kufaulu kuleta amani katika taifa letu. Kwa hiyo pamoja na kuendelea kuwaomba waumini wa Katoliki pamoja na watu wenye mapenzi mema kuendelea kumwomba Mwenyezi Mungu arehemu taifa letu na mapambano ya aina yoyote ile. Tuendeleze nia yetu njema ya kusema ukweli, haidhuru ukweli huu unamgusa nani,” alisema Pengo.




Alisema kujaribu kuficha ukweli na kupotosha ni njia sahihi kwa ibilisi kuleta vurugu katika jumuiya ya watu na ieleweke hivyo.




“Naomba kila mtu akubaliane na tamko langu haidhuru pana kosa, amani ya taifa letu ni jambo la msingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusema ukweli kama ulivyo,” alisema.

Chanzo: Gazeti Mwananchi Leo.
 
Mambo kama haya huanza kidogokidogo. Wanasiasa walianza chama fulani ni cha waislam, watu wakaaminishwa wakaamini. Uchaguzi uliofuatia propaganda zikaendelea tena chama hiki kingine ni cha wakristo na hasa wakatoliki, watu wakaaminishwa na wakaamini. Matokeo yake baadhi ya watu wameshaanza kujenga imani kuwa kuna chama cha dini yetu. Na wengine wanafikra za kuchukia chama fulani kwa kuwa si cha dini yao. Walioanza haya ni wanasiasa. Watanzania popote tulipo tupinge hisia hizi potofu kwa mustakabali wa nchi yetu. Vita yoyote haina macho. Turudi kwenye misingi ya taifa letu: undugu, upendo, mshikamano etc.
 
Back
Top Bottom