Suala la Bandari TEC hawakupata kama walivyozoea

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,264

Anachojaribu kukifanya huyu msemaji ni kutaka wasiokuwa Wakatoliki waamini kuwa Kanisa Katoliki bado lina nguvu ile ile iliyokuwanayo kabla ya sakata la "Waarabu" na Bandari ya Dar-es-Salaam.

Kanisa Katoliki katika sakata hili halikupata kile ambacho wamezoea kupata kuanzia wakati wa ukoloni hadi kufikia hili la bandari kupewa "Waarabu," katika Tanganyika huru.

TEC imefedheheka na hili limewaumiza na kwa mara ya kwanza wameshindwa kupata walichotaka kama ilivyokuwa mazoea.

Hawa walikuwa wakikataa kitu basi hakipiti.

Hawakuitaka EAMWS.
Hawakuitaka OIC.

Hawakuitaka Mahakama ya Kadhi.

Hili la bandari hawakulitaka kama ilivyo kawaida.

Wameshindwa safari hii kwa mara ya kwanza.

"Waarabu" wamekabidhiwa bandari.

Imekuwaje kwa TEC kushindwa?

Imeshindwa kwa sababu kuu moja ingawa zipo nyingi.

Hapa nitaeleza hii sababu moja kuu.

Waislam katika sakata la bandari walijikusanya pamoja na kujiweka mbali sana na wale ambao kila wamuonapo "Mwarabu" wao wanauona Uislam ambao lazima upigwe vita kwa hali yoyote ile.

Lakini kulikuwa na kitu kilichoongeza ladha katika kachumbari iliyokuwa ikitengenezwa na TEC.

Waliokuwa wanapinga Waarabu kuendesha bandari walikuwa wa imani moja na pamoja na CHADEMA.

Mifano iko mingi lakini hapana haja kueleza yote hapa.

Waislam kimya kimya wakaiunganisha CHADEMA katika orodha yao.

Chama hiki kikawekwa kundi moja na TEC na hii haikuwa kazi kubwa ya kumtoa mtu jasho la kwapa.

Ndani ya serikali na CCM kuna watu waliona mapema kabisa asubuhi kuwa nchi imeshagawanyika mapande mawili katika misingi ya imani.

Walio ndani ya serikali na CCM iliwadhihirikia kuwa Waislam wamejitenga wako mbali na wanaowapiga vita "Waarabu" na kwa mara ya kwanza kwa namna ya ajabu kabisa Waislam wakawa wanasubiri muda uwadie wapambane na TEC na mwenza wake CHADEMA.

Zikavuja taarifa kuwa Waislam nje ya BAKWATA wanajiandaa kwenda mahakamani kuhoji mengi yanayowasibu ndani ya serikali.

Waliokuwa serikalini na CCM walitambua watuhumiwa watakuwa nani.

Wenye akili zilizotimia ndani ya serikali na CCM haraka wakajiuliza tumefikaje hapa?

Hawa Waswahili si ndiyo waliopigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana?

Wenye akili timamu wakatambua vipi wamefika hapo.

Waingereza wana msemo, "You do it once too often."

Wakatoliki wamejidekeza kupita kiasi kwa kuhodhi kila kitu kuanzia serikali yenyewe, bunge, vyama vya siasa na kila kitu bila ya kukutana na kizingiti chochote.

Waislam wako nje na katika hili la "Waarabu," na bandari wamejiweka pembeni makusudi ili Ukristo ndani ya Tanzania ujivue nguo wenyewe hadharani.

Wametishika na wakarudi nyuma.

Hatari iliyokuwa inawakabili waliitambua.

Serikali ikatimiza maamuzi yake.
Taifa likabakia limetulia.

Kanisa likabakia limefedheheka.

Ile nguvu waliyodhani bado TEC inayo kumbe haipo tena.

TEC bila shaka imejiuliza baada ya haya nini kitafuatia?

Sababu ya kushindwa kwao wanaijua fika.

Sasa msemaji anasema Vatican siyo iliyomwalika Rais wa Tanzania bali serikali imeombwa ialikwe Vatican.

Nani mwenye kawaida ya kuongopa?

Kinachotafutwa hapa ni kujaribu kujifuta tope baada ya kuanguka.

Inataka ieleweke kuwa Rais wa Tanzania ana hofu na amejisalimisha Vatican.

Msemaji ananadi kuwa Kanisa Katoliki lina nguvu si watu wa kupuuzwa.

Ukweli ni kuwa hakika Kanisa limehodhi serikali kwa uwiano wa 80% kwa 20%.

Hali hii leo si mtaji tena kwao kwa sababu zilizo wazi kwani mengi yasiyopendeza yanaelezwa dhidi ya Kanisa na hatari yake ishajitokeza.

TEC imedhoofika bila yenyewe kutambua.

Hii ndiyo sababu ya TEC na CHADEMA kujikuta wako peke yao katika sakata la bandari na vita yao dhidi ya "Waarabu."

Iwe iwavyo hali ya siasa imebadilika.

Hizi propaganda kuwa Rais wa Tanzania ana hofu hazitasaidia kitu.

Zinaweza zikaamsha makubwa ambayo hawayategemei.

Zinaweza hizi propaganda pengine zikazua makubwa kuliko ule ukimya walioonesha Waislam wakati wa sakata la bandari.

Wasisahau ukimya mwingi una kishindo.
 


Anachojaribu kukifanya huyu msemaji ni kutaka wasiokuwa Wakatoliki waamini kuwa Kanisa Katoliki bado lina nguvu ile ile iliyokuwanayo kabla ya sakata la "Waarabu" na Bandari ya Dar-es-Salaam.

Kanisa Katoliki katika sakata hili halikupata kile ambacho wamezoea kupata kuanzia wakati wa ukoloni hadi kufikia hili la bandari kupewa "Waarabu," katika Tanganyika huru.

TEC imefedheheka na hili limewaumiza na kwa mara ya kwanza wameshindwa kupata walichotaka kama ilivyokuwa mazoea.

Hawa walikuwa wakikataa kitu basi hakipiti.

Hawakuitaka EAMWS.
Hawakuitaka OIC.

Hawakuitaka Mahakama ya Kadhi.

Hili la bandari hawakulitaka kama ilivyo kawaida.

Wameshindwa safari hii kwa mara ya kwanza.

"Waarabu" wamekabidhiwa bandari.

Imekuwaje kwa TEC kushindwa?

Imeshindwa kwa sababu kuu moja ingawa zipo nyingi.

Hapa nitaeleza hii sababu moja kuu.

Waislam katika sakata la bandari walijikusanya pamoja na kujiweka mbali sana na wale ambao kila wamuonapo "Mwarabu" wao wanauona Uislam ambao lazima upigwe vita kwa hali yoyote ile.

Lakini kulikuwa na kitu kilichoongeza ladha katika kachumbari iliyokuwa ikitengenezwa na TEC.

Waliokuwa wanapinga Waarabu kuendesha bandari walikuwa wa imani moja na pamoja na CHADEMA.

Mifano iko mingi lakini hapana haja kueleza yote hapa.

Waislam kimya kimya wakaiunganisha CHADEMA katika orodha yao.

Chama hiki kikawekwa kundi moja na TEC na hii haikuwa kazi kubwa ya kumtoa mtu jasho la kwapa.

Ndani ya serikali na CCM kuna watu waliona mapema kabisa asubuhi kuwa nchi imeshagawanyika mapande mawili katika misingi ya imani.

Walio ndani ya serikali na CCM iliwadhihirikia kuwa Waislam wamejitenga wako mbali na wanaowapiga vita "Waarabu" na kwa mara ya kwanza kwa namna ya ajabu kabisa Waislam wakawa wanasubiri muda uwadie wapambane na TEC na mwenza wake CHADEMA.

Zikavuja taarifa kuwa Waislam nje ya BAKWATA wanajiandaa kwenda mahakamani kuhoji mengi yanayowasibu ndani ya serikali.

Waliokuwa serikalini na CCM walitambua watuhumiwa watakuwa nani.

Wenye akili zilizotimia ndani ya serikali na CCM haraka wakajiuliza tumefikaje hapa?

Hawa Waswahili si ndiyo waliopigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana?

Wenye akili timamu wakatambua vipi wamefika hapo.

Waingereza wana msemo, "You do it once too often."

Wakatoliki wamejidekeza kupita kiasi kwa kuhodhi kila kitu kuanzia serikali yenyewe, bunge, vyama vya siasa na kila kitu bila ya kukutana na kizingiti chochote.

Waislam wako nje na katika hili la "Waarabu," na bandari wamejiweka pembeni makusudi ili Ukristo ndani ya Tanzania ujivue nguo wenyewe hadharani.

Wametishika na wakarudi nyuma.

Hatari iliyokuwa inawakabili waliitambua.

Serikali ikatimiza maamuzi yake.

Taifa likabakia limetulia.

Kanisa likabakia limefedheheka.

Ile nguvu waliyodhani bado TEC inayo kumbe haipo tena.

TEC bila shaka imejiuliza baada ya haya nini kitafuatia?

Sababu ya kushindwa kwao wanaijua fika.

Sasa msemaji anasema Vatican siyo iliyomwalika Rais wa Tanzania bali serikali imeombwa ialikwe Vatican.

Nani mwenye kawaida ya kuongopa?

Kinachotafutwa hapa ni kujaribu kujifuta tope baada ya kuanguka.

Inataka ieleweke kuwa Rais wa Tanzania ana hofu na amejisalimisha Vatican.

Msemaji ananadi kuwa Kanisa Katoliki lina nguvu si watu wa kupuuzwa.

Ukweli ni kuwa hakika Kanisa limehodhi serikali kwa uwiano wa 80% kwa 20%.

Hali hii leo si mtaji tena kwao kwa sababu zilizo wazi kwani mengi yasiyopendeza yanaelezwa dhidi ya Kanisa na hatari yake ishajitokeza.

TEC imedhoofika bila yenyewe kutambua.
Wrwe
Hii ndiyo sababu ya TEC na CHADEMA kujikuta wako peke yao katika sakata la bandari na vita yao dhidi ya "Waarabu."

Iwe iwavyo hali ya siasa imebadilika.

Hizi propaganda kuwa Rais wa Tanzania ana hofu hazitasaidia kitu.

Zinaweza zikaamsha makubwa ambayo hawayategemei.

Zinaweza hizi propaganda pengine zikazua makubwa kuliko ule ukimya walioonesha Waislam wakati wa sakata la bandari.

Wasisahau ukimya mwingi una kishindo.

Wewe mzee ni mtu wa hovyo yafaa upuzwe licha kuandika vitabu na kusoma vitabu vingi kama unavyojinasibu lakini Bado hujajikomboa kifikra kama biashara ya utumwa ingekuwa Bado inaendelea wewe ni Moja ya watu ambao mgejifunga minyororo na kulazimishwa kuuzwa kwa waarabu
 


Anachojaribu kukifanya huyu msemaji ni kutaka wasiokuwa Wakatoliki waamini kuwa Kanisa Katoliki bado lina nguvu ile ile iliyokuwanayo kabla ya sakata la "Waarabu" na Bandari ya Dar-es-Salaam.

Kanisa Katoliki katika sakata hili halikupata kile ambacho wamezoea kupata kuanzia wakati wa ukoloni hadi kufikia hili la bandari kupewa "Waarabu," katika Tanganyika huru.

TEC imefedheheka na hili limewaumiza na kwa mara ya kwanza wameshindwa kupata walichotaka kama ilivyokuwa mazoea.

Hawa walikuwa wakikataa kitu basi hakipiti.

Hawakuitaka EAMWS.
Hawakuitaka OIC.

Hawakuitaka Mahakama ya Kadhi.

Hili la bandari hawakulitaka kama ilivyo kawaida.

Wameshindwa safari hii kwa mara ya kwanza.

"Waarabu" wamekabidhiwa bandari.

Imekuwaje kwa TEC kushindwa?

Imeshindwa kwa sababu kuu moja ingawa zipo nyingi.

Hapa nitaeleza hii sababu moja kuu.

Waislam katika sakata la bandari walijikusanya pamoja na kujiweka mbali sana na wale ambao kila wamuonapo "Mwarabu" wao wanauona Uislam ambao lazima upigwe vita kwa hali yoyote ile.

Lakini kulikuwa na kitu kilichoongeza ladha katika kachumbari iliyokuwa ikitengenezwa na TEC.

Waliokuwa wanapinga Waarabu kuendesha bandari walikuwa wa imani moja na pamoja na CHADEMA.

Mifano iko mingi lakini hapana haja kueleza yote hapa.

Waislam kimya kimya wakaiunganisha CHADEMA katika orodha yao.

Chama hiki kikawekwa kundi moja na TEC na hii haikuwa kazi kubwa ya kumtoa mtu jasho la kwapa.

Ndani ya serikali na CCM kuna watu waliona mapema kabisa asubuhi kuwa nchi imeshagawanyika mapande mawili katika misingi ya imani.

Walio ndani ya serikali na CCM iliwadhihirikia kuwa Waislam wamejitenga wako mbali na wanaowapiga vita "Waarabu" na kwa mara ya kwanza kwa namna ya ajabu kabisa Waislam wakawa wanasubiri muda uwadie wapambane na TEC na mwenza wake CHADEMA.

Zikavuja taarifa kuwa Waislam nje ya BAKWATA wanajiandaa kwenda mahakamani kuhoji mengi yanayowasibu ndani ya serikali.

Waliokuwa serikalini na CCM walitambua watuhumiwa watakuwa nani.

Wenye akili zilizotimia ndani ya serikali na CCM haraka wakajiuliza tumefikaje hapa?

Hawa Waswahili si ndiyo waliopigania uhuru wa Tanganyika hadi ukapatikana?

Wenye akili timamu wakatambua vipi wamefika hapo.

Waingereza wana msemo, "You do it once too often."

Wakatoliki wamejidekeza kupita kiasi kwa kuhodhi kila kitu kuanzia serikali yenyewe, bunge, vyama vya siasa na kila kitu bila ya kukutana na kizingiti chochote.

Waislam wako nje na katika hili la "Waarabu," na bandari wamejiweka pembeni makusudi ili Ukristo ndani ya Tanzania ujivue nguo wenyewe hadharani.

Wametishika na wakarudi nyuma.

Hatari iliyokuwa inawakabili waliitambua.

Serikali ikatimiza maamuzi yake.

Taifa likabakia limetulia.

Kanisa likabakia limefedheheka.

Ile nguvu waliyodhani bado TEC inayo kumbe haipo tena.

TEC bila shaka imejiuliza baada ya haya nini kitafuatia?

Sababu ya kushindwa kwao wanaijua fika.

Sasa msemaji anasema Vatican siyo iliyomwalika Rais wa Tanzania bali serikali imeombwa ialikwe Vatican.

Nani mwenye kawaida ya kuongopa?

Kinachotafutwa hapa ni kujaribu kujifuta tope baada ya kuanguka.

Inataka ieleweke kuwa Rais wa Tanzania ana hofu na amejisalimisha Vatican.

Msemaji ananadi kuwa Kanisa Katoliki lina nguvu si watu wa kupuuzwa.

Ukweli ni kuwa hakika Kanisa limehodhi serikali kwa uwiano wa 80% kwa 20%.

Hali hii leo si mtaji tena kwao kwa sababu zilizo wazi kwani mengi yasiyopendeza yanaelezwa dhidi ya Kanisa na hatari yake ishajitokeza.

TEC imedhoofika bila yenyewe kutambua.

Hii ndiyo sababu ya TEC na CHADEMA kujikuta wako peke yao katika sakata la bandari na vita yao dhidi ya "Waarabu."

Iwe iwavyo hali ya siasa imebadilika.

Hizi propaganda kuwa Rais wa Tanzania ana hofu hazitasaidia kitu.

Zinaweza zikaamsha makubwa ambayo hawayategemei.

Zinaweza hizi propaganda pengine zikazua makubwa kuliko ule ukimya walioonesha Waislam wakati wa sakata la bandari.

Wasisahau ukimya mwingi una kishindo.

Mzee usingizie CHADEMA huwa wanafuata haki na kama kweli mkataba ndio umebadilishwa basi CDM nao wapewe kongole . Mzee pamoja na usomi wako ila udini unakufanya heshima yako ipungue
 
😂😂ila hili lizee linapitia kipindi kigumu sana....yaan jambo la kawaida kabisa atalitafutia mtazamo wa kidini lionekane kama Kuna competition flan hv ya waislamu na wakristo...
Ndiyo sababu Waafrika tuko masikini, hatujui vipaumbele vyetu na wakati huo kuruhusu wasiopenda tupate maendeleo ya haraka kuendelea kutugawa kwa tofauti za kiimani. Pakistani na Iran wanarushiana makombola je wana imani tofauti. Ni busara kuwa macho kwa wanaopenda kutugawa bila kujali rangi yao au imani yao. Mwisho wa siku Afrika itaendelea kudidimia kwenye dimbwi la umasikini.
 
Ndiyo sababu Waafrika tuko masikini, hatujui vipaumbele vyetu na wakati huo kuruhusu wasiopenda tupate maendeleo ya haraka kuendelea kutugawa kwa tofauti za kiimani. Pakistani na Iran wanarushiana makombola je wana imani tofauti. Ni busara kuwa macho kwa wanaopenda kutugawa bila kujali rangi yao au imani yao. Mwisho wa siku Afrika itaendelea kudidimia kwenye dimbwi la umasikini.
Petrol,
Misingi ya umoja iliwekwa tokea mapema wakati wazee wetu hapa Dar es Salaam mwaka wa 1929 wanaunda African Association.

Waasisi walikuwa hawa: Cecil Matola (President), Kleist Abdallah Sykes (Secretary), Mzee bin Sudi, Ibrahim Hamisi, Ali Said Mpima, Zibe Kidasi, Suleiman Majisu, Rawkes Kusi na Rawson Watts.

AA ikawa imetawaliwa na Waislam na wakawa wanapitisha baadhi ya matatizo yao katika AA.

Wazee wetu wakaona hii haifai kwani walataka AA kiwe chama kisichofungamana na imani za wanachama wao.

Wakaamua mwaka wa 1933 kuunda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) President akiwa Mzee bin Sudi na Secretary Kleist Abdallah Sykes ili mashauri ya Waislam yapitishwe huko.

Sasa mwaka wa 1950 harakati za kutaka kuunda chama cha siasa.
Msimamo wa Hamza Mwapachu ulikuwa nafasi ya President wa chama hicho awe Mkristo ili chama kichukue sura ya umoja wa Watanganyika wote.

Wakati ule TAA ili ilikuwa imeshikwa na Waislam na Wengine walikuwa wachache sana katika siasa kwa kuwa Kanisa lilijiweka mbali sana na harakati za ukombozi wa Tanganyika.

Historia hii nimeieleza mara nyingi sana hapa.

Hivi ndivyo Julius Nyerere alivyochaguliwa kuwa President wa TAA mwaka wa 1953 katika uchaguzi ulifanyika Arnautoglo Hall Julius Nyerere na Abdul Sykes wakigombea nafasi hiyo.

Hii ni katika historia muhimu ya TANU ambayo Nyerere hakupata kuieleza na matokeo yake ikawa haifahamiki hadi pale kilipochapwa kitabu cha maisha ya Abdul Sykes (1997).

TANU ikaingia kupigania uhuru wa Tanganyika Nyerere akiwa kiongozi wa harakati hizi na nchi ikawa imeshikamana.

Ushahidi ni picha za kupigania uhuru.
Picha zote Nyerere kazungukwa na Waislam wake kwa waume.

Uhuru ukapatikana mwaka wa 1961 nchi ikiwa na umoja.
Nani aliyekuja kutugawa na kuuvunja umoja huu?

Ndugu yangu Petrol,
Unalo jibu?

Unamjua adui huyu?

Angalia picha hizo hapo chini na kwa makusudi sitaweka maelezo ila mwaka wa picha kwani picha zinajieleza zenyewe:

1706105095070.png

1955
1706105220419.png

1957
1706105275056.png

1962​
 
Ukweli utakuweka huru,hongera sana Sheikh Mohamed Said
Chifu...
Ahsante sana ndugu yangu.

Nimeweka makala hiyo hapo juu labda huenda ndugu zetu wakakaa kitako na kutafakari.

Kuna watu hapa wananitukana na wanapandisha hamaki na kuropoka ovyo wenyewe huandika 'hovyo.''

Angalia picha hii ambayo nayo sitaweka maelezo:


1706105630551.png

1955/56​
 
Duh! Nimemsoma mleta mada kwa kutulia, ila sijamwelewa kwa kweli! 😄

Nakiri wakati mwingine miye si mwepesi wa kuelewa haraka.
Peace...
Nina rafiki yangu mtu wa kujiweza sana.

Ameondoka Tanzania miaka mingi iliyopita.

Kila akija Tanzania hakosi kunitembelea nyumbani.

Siku alipokuja Maktaba akaniuliza kwa nini hadi leo sijatundika picha ya Mwalimu Julius Nyerere aliyopiga na Baraza la Wazee wa TANU mwaka 1957.

Picha hii yeye katundika ofisini kwake.

Nikamjibu kuwa haijanipitikia kufanya hivyo.

"Mohamed nipatie picha ya Nyerere kapiga na maaskofu wakati wa kupigania uhuru kama alivyopiga na Baraza la Wazee wa TANU nitakupa milioni 1."

Sijaweza kupata picha hii na yeye kila akiniuliza kuhusu picha namjibu sijapata.

Yeye hucheka kisha akapandisha dau juu.

Bei ya picha hii sasa thamani yake inakaribia shilingi za Kitanzania 10m.

Nadhani huyu rafiki yangu anajua kama picha hii haipo ndiyo maana anapandisha dau kila mwaka bila wasiwasi.
 
Back
Top Bottom