Sakata la Bomu: Pengo afichua siri

Sakata la Bomu: Pengo afichua siri

Pengo ni mzoefu wa taratibu za undeshaji Serikali, na pia nadhani ana saikolojia. Hata mimi siamini kama tukio la ARusha ni kidini, na kama litakuwa la kidini litakuwa kosa kubwa sana kuwahi kutokea Tanzania kwa vile ni wazi kwamba "mbaya" wa waislam si wakristo, ni serikali yenyewe kupitia Bakwata, so hawawezi kushambulia watu walio kwenye ibada ilihali humo ndani yake kuna watoto, wanwake ambao uwezo wao wa kukimbia hatari ni mdogo. Siamni kama kuna muislam atakayekuwa na imani hiyo iwapo ni timilifu wa akili. Pengo yuko sahihi, lets wait!
 
Mi naona Pengo alifanya hivyo kupunguza hasira wakristu dhidi ya waislamu. Ikumbukwe baada ya lile tukio humu jamvini na mitaani, watu washajenga chuki na waislamu kitendo ambacho kingehatarisha amani. Mi binafsi na'pongeza kwa kuona mbali.
 
Sijui kwanini wakiristo hawa wa chini wasifate mawazo pengo kiukweli anaona mbali baadhi ya wakati
 
Sijui kwanini wakiristo hawa wa chini wasifate mawazo ya pengo kiukweli anaona mbali baadhi ya wakati
 
Pengo huenda anajua kua ndani ya nyumba zetu za ibada kumejaa chuki na magomvi hivyo tunawezaa kulipuana wenyewe kwa wenyewe!!
 
Mi naona Pengo alifanya hivyo kupunguza hasira wakristu dhidi ya waislamu. Ikumbukwe baada ya lile tukio humu jamvini na mitaani, watu washajenga chuki na waislamu kitendo ambacho kingehatarisha amani. Mi binafsi na'pongeza kwa kuona mbali.

muadhama sio Mpum.bav kama wewe kusema uongo ili kufurahisha au kutuliza makundi, mbona hakusema hivyo alivyouawa Padr? Tulieni muone majibu yatavyoshusha nyuso zenu kwa Aibu!
 
Isije ikawa kauli ya Pengo kuwahisha hitimisho la mlipuko wa Arusha ni jaribio la kuzuia uchunguzi wa kina wa vyombo vya kijasusi katika suala hilo. Tukizingatia kuwa kuna uvumi wa baazi ya wastahiki fulani nchini kujihusisha na dawa za kulevya.
Hili nalo linabaki kuwa speculation bado.
.
 
Kama ni tukio la kigaidi mrusha bomu angekwenda kulirusha pale kilombero sokoni au soko kuu ambako kuna mkusanyiko mkubwa zaidi wa watu.Funika kombe mwanaharamu apite.
 
Mkuu mtoa mada, tamko la Pengo lilikuwa ni ombi la Serikali ili kuondoa hali ya chuki baina ya wakritu na waislam ili kuimalisha amani. Hivyo alihamua kutumia busara nae akakubali. Kwa hiyo msijiangaishe na ilo tamko. Kama wewe ni mkristu hakikisha kuwa haumchukii mwaislam. Upendo ni mafunzo kutoka kwa Yesu. Ndiyo maana hata baada ya kuteswa aliwaombea adui zake kwa kusema ''BABA WASAMEHE KWA KUWA HAWAJUI WALITENDALO"
 
Jana katika kujadiri azimio la bunge katika kulaani na kupinga kitendo cha kigaidi kilichofanywa na watu wasio julikana katika kanisa katoliki huko Arusha, wabunge wote bila kujari itikadi za vyama vyao wala imani zao za kidini walionyesha kuamini kuwa tukio hilo linatokana na imani za kidini kulaani na kuonya juu ya mtafaruku unaoendelea kujitokeza kati ya wakristu na waislam.Hii ni tofauti kabisa na tamko la kardinali Pengo ambaye kwa intelijensia yake ametamka kuwa shambulizi hilo alihusiani na na maswala ya kiimani.Lakini mimi naomba kujua, hivi msimamo wa bunge na tamko la Pengo haviingilii uchunguzi wa polisi?Hii ni kutokana na kwamba bunge lishajiaminisha na kuamisha watanzania walio wengi kwamba shamulizi hilo linatokana na mpasuko wa kidini unaolikumba taifa letu na huku Pengo kajenga imani na kuaminisha wengine kwamba shambulizi hilo halina mahusiano yoyote na maswala ya kiimani.Wakuu mie naona pande zote mbili yaani Pengo na bunge wamewahi mno kutoa kauli zao kwani polisi inaweza kuja na matokeo ya uchunguzi yakiwa kinyume kabisa na imani ya matamko yao, je watakubali?
Tatizo lenu wengi hamtafakari matamko haya yanayotolewa kwa dhati. Mnachukua literally tu. Kardinali alichosema kilikuwa kinalenga kuonyesha kuwa wakristu na waislamu Tanzania hawana uadui. Waliofanya tenfo hili ni lazima wana nia ingine zaidi ya kuchonganisha uislamu na ukristu Tanzania. Alisisitiza taarifa sahihi matokeo ya uchunguzi, hii ni kutaka watu wasiendelee kuaminishwa kuwa kuna ugomvi wa kidini Tanzania.Bunge kwa upande wake wanaona dhairi kuna mmomonyoko wa mahusiano yanayosababishwa na kikundi cha watu kuuchochea ukristu na uislamu. Wanalenga Serkali kuchukua hatua stahili ikiwemo kutunga sheria. Kwa upande mwingine Bunge linailaumu serkali kwa kuzembea.
 
kwa sasa matumaini yetu yamebaki kwa fbi. Pengine wanaweza kuwa na jibu. Ingekuwa rahisi sana kama gprs ilichukuwa eneo la tukio na kama tanzania inatumika.
 
Pengo ametumika kupoza upepo.

mbona baada ya tukio la Arusha matamko makali ya kukemea udini yanafuata.

kwa nini
 
Ndugu ni kwamba chuki za KIDINI zimeshaenea mpaka vijijini,majuzi wakati wa tukio la arusha nilipigiwa simu ndugu yangu alieko huko kijijini na kuniambi 'tumesikia waislamu wamelipua kanisa huko arusha,akaendelea leo wakati watu wanatoka makanisani wametangaziwa kuwa macho na waislamu wanaonekana ktk maeneo yao.na kama kuna mtu anawahifadhi afichuliwe mara moja'. Ninachosema hapa ni kuwa maeneo ninayotoka mimi wala haujawahi kuonekana msikiti,hivyo hofu yangu ni kuwa watakapopita waislamu maeneo hayo na utambulisho wao mfano KANZU na BARAGHASHIA inaweza kuwa hatari kwao...TANZANIA NOW IS DANGEROUS THAN WE THINK..
 
Pengo ametumika kupoza upepo.

mbona baada ya tukio la Arusha matamko makali ya kukemea udini yanafuata.

kwa nini

usilo lijua sawa na usiku wa giza tafuta uji unywe ulale kwanza.
 
Kuna haja ya kuwa na minimum qualification bungeni
Haya mambo ya maswali magumu kujibiwa na majibu mepesi inataka kuwa tabia zoelefu

Kongosho, tatizo tulilonalo hapa TZ kwa sasa ni kuwa siasa imeingilia kila kitu. Hakuna kitu cha maana kinachofanyika zaidi ya watu kuongea na kisha kuishia hewani.
Nikuulize swali la kipuuzi, ni tume ngapi zimeundwa kuchunguza mambo mbali mbali na zipi zimetoa matokeo yaliyofanyiwa kazi? Mangapi yanajadiliwa bungeni na ni mangapi yanatekelezwa? Juzi juzi tu jengo lilianguka na kutafuna makumi ya watu hupo kariakoo. Niambie ni hatua gani thabiti zimechukuliwa kufuatilia, kuchunguza na kuyabomoa majengo yenye sifa duni (chini ya kiwango)? Ni siasa, siasa siasa kwenye kila kitu!!!

Hao waloharibu vyanzo vya maji wako wapi? walioiba wanyama wamechukuliwa hatua gani? Wala rushwa? Richmond? Ile ishu ya jairo? nk nk. Ni siasa siasa siasa!!!
 
kama polisi wanajua kazi yao barabara wanatakiwa wamkamate Pengo kama shahidi namba moja

Ni vizuri ukasoma tena na tena kauli ya Guru Pengo, yule ni mwanafalsafa. Anasema, kauli yake imejengwa kwenye misingi ya taarifa alizopewa na anaamini waliompa hawawezi kuongopa, na waliompa taarifa zile ni Jeshi la Polisi na Serikali. Ilibidi atoe ufafanuzi jana, kuna ka-siri fulani, kama vile hakubaliani na kauli yake mwenyewe lakini anasema yeye anaheshimu Mamlaka na Mamlaka ndiyo iliyomwambia hivyo! Naam endapo itakuwa tofauti, yeye yuko salama....nilimsikiliza sana!
 
Kaka eti unasemaje, Makanisa yalipochomwa, zanzibar na Mbagala, hiyo nayo nini? Kuuawa na kupigwa risasi kwa Padri Znzibar nayo nini? Kama adui wa Waislamu ni Serikali mbona Chama kinachoongoza serikali hiyo kilifanyiwa kampeni ya ubenge huko Igunga. Na je kwa nini mashambulizi yasilenge Taasisi za serikali na Bakwata, zihamie makanisani? Unataka kumdanganya nani hapa. Nilishaema wivu, uvivu na ujinga unaopenyeza kati ya Wanaharakati wa Kiislamu ndio chanzo. Kama muislamu anaweza kulipua bomu msikitini unasemaje kuwa ana huruma na watoto walio Kanisani? Please you cant play me smart Zidane. Ulichofanya kwenye Avart yako ndio aklili yako.
Pengo ni mzoefu wa taratibu za undeshaji Serikali, na pia nadhani ana saikolojia. Hata mimi siamini kama tukio la ARusha ni kidini, na kama litakuwa la kidini litakuwa kosa kubwa sana kuwahi kutokea Tanzania kwa vile ni wazi kwamba "mbaya" wa waislam si wakristo, ni serikali yenyewe kupitia Bakwata, so hawawezi kushambulia watu walio kwenye ibada ilihali humo ndani yake kuna watoto, wanwake ambao uwezo wao wa kukimbia hatari ni mdogo. Siamni kama kuna muislam atakayekuwa na imani hiyo iwapo ni timilifu wa akili. Pengo yuko sahihi, lets wait!
 
Tunaendeshwa na siasa, afu waloko siasani baadhi yao vilaza

So tatizo linakuwa kubwa zaidi

Bora wangekuwa na akili wangeweza fuatilia

Kongosho, tatizo tulilonalo hapa TZ kwa sasa ni kuwa siasa imeingilia kila kitu. Hakuna kitu cha maana kinachofanyika zaidi ya watu kuongea na kisha kuishia hewani.
Nikuulize swali la kipuuzi, ni tume ngapi zimeundwa kuchunguza mambo mbali mbali na zipi zimetoa matokeo yaliyofanyiwa kazi? Mangapi yanajadiliwa bungeni na ni mangapi yanatekelezwa? Juzi juzi tu jengo lilianguka na kutafuna makumi ya watu hupo kariakoo. Niambie ni hatua gani thabiti zimechukuliwa kufuatilia, kuchunguza na kuyabomoa majengo yenye sifa duni (chini ya kiwango)? Ni siasa, siasa siasa kwenye kila kitu!!!

Hao waloharibu vyanzo vya maji wako wapi? walioiba wanyama wamechukuliwa hatua gani? Wala rushwa? Richmond? Ile ishu ya jairo? nk nk. Ni siasa siasa siasa!!!
 
Back
Top Bottom