Safari za Kikwete zazaa matunda...

Safari za Kikwete zazaa matunda...

Acha uzushi mtoa mada hawa walikuwepo kutoka enzi hizo mie nilisoma kipindi cha Mkapa tulikuwa na walimu wa Physics,Biology na Chemistry kutoka USA na kwingineko usihadae watu kwa kuwa wewe ndo uko shule ya kata sasa au mwanao yuko huko hii system ilikuwepo tangu enzi hizo na hao walimu wenyewe huko kwao wanafanya mazoezi na wala sio walimu ambao wako na uzoefu hivyo nakumbuka wakati huo mwalimu wetu wa Physics alikuwa mkali sana kuliko yule Mmarekani kwa hiyo hizo safari za Kikwete zisikutie kiwewe ati zimezaa matunda au ndo unampigia debe????
 
Mwaka huu wakati wa Kikwete kwa mara ya kwanza tunaona kampuni za uchimbaji dhahabu zikianza kulipa kodi, au hujui hilo?

Unafikiri wawekezaji wajinga? waje, wawekeze mali zao, mitambo na muhimu zaidi ni ujuzi wao halafu wakuwachie wewe kila kitu? NO. Kwanza wanahakikisha wanarudisha wanachowekeza, halafu wanapata faida halafu ndio mgawane faida sio kabla. Kama hutaki, kachimbe na kucha.

Mishahara kama haiwatoshi waende wakafanye nchi zitakazowapa mishahara ya kuwatosha au wasubiri tunaenda kwa kuongezana hivyo hivyo kidogo kidogo. Huwezi kulazimisha kitu hakiwezekani kwa mara moja.

Wameshaambiwa kaeni, msiwe na shaka tutaongezana kidogo kidogo na kila muda unavyokwenda tutaongezana, hutaki wacha. Wewe ukisema ya nini wenzako wanauliza ntaipata lini.

nadhani we sio zomba ni zombi hiyo i ya mwisho umeireplace na a maana comment zako ni kama unaishi kuzimu vile.haiwekani mtu wa kawaida ukawa na mawazo kama haya if you are not pretending.
 
Kuna wakati ambao Tanzania inapata vyuo vya aina zote vingi na kuboreshwa kama huu wa Kikwete? umelala upo macho? Bila kuwaleta waliokuzidi kielimu kukufundisha unafikiri utaelimika? kwa lipi jipya? Wakati wa Kikwete ni wastani wa zaidi ya vyuo vikuu viwili kila mwaka. Upo hapo ulipo? ni nani mwingine aliyefanya hivyo?

Wakati mwingine ukiandika usiwe unafikiri kila mmoja anafikiri kwa umbali wa pua. Ukiacha pesa za NSSF zilizojenga UDOM ni chuo gani tuaambie serikali ya Kikwete ina contribution from when it the process began mpaka kikawa chuo. Vingi ni vya makanisa tena vimeanza kama taaisisi za elimu ya cheti na shahada na baadae vikafikia vigezo vya transformation into university status na sioni mkono wa Kikwete wala serikali yake. Na vingi kati ya hivi quality ya elimu yake bado ni questionable lakini hili la thread nyingine. Tujikite kwenye upotoshaji wako. Usipende kumpa mtu sifa asizokuwa nazo. Kwenye elimu mpe sifa ya shule za kata na primary kama iliyoonyeshwa jana uko Morogoro yenye mwalimu mmoja na ambaye ndiye walimu mkuu anafundishwa madarasa mawili ndani ya cumba kimoja na wakati mmoja. Sasa hata kama vyuo angejenga Kikwete kama unavyotaka tuamini hawa wa Mvomero watakwenda vyuo hivyo?
 
I don't buy chip things because chip is always expensive and short cut will always cut you short......kuimport waalimu kutoka nje ya nchi huku wa kwenu mnashindwa kuwalipa ni kutafuta vitu rahisi...by the way siamini kuwa hao wa nje wanakuja bure....gharama yao mtaitambua baada ya uranium yenu na mali asili nyingine kutwaliwa live mbele ya macho yenu
Nachukia sana vitu vya msaada au vya bure!

mtoa hoja,kachemka anaowatumia post ajue ni interlectures hivyo angalia uhitaji wa walimu wasayansi tunao wahitaji+no yawanafunzi wanao hitaji huduma hiyo.walimu wa sayansi wapo ila namna gani wanatumiwa?je mazingira ya meboreshwa?
 
Hayo ndiyo maendeleo?? Mtegemea cha nduguye...... na nguo ya kuazima.......
Tunawapuuza madaktari wetu na walimu wetu kwa msaala wa kimarekani upitaooo!
 
Bangi na Mchicha uliokaangwa unamadhara makubwa kwa binadamu. Inaelekea uliamka asubuhi na kukosa cha ku-post uka2wekea uchuro huo. Walimu 47 wanatosha kata moja tu! Za kwako changanya na za mkeo.
 
Hao waalimu wanakuja kufundisha sayansi katika maabara zipi? Za shule ya kata au?
 
achana na uwezo mdogo wa kuwaza na kutafakari mambo mbona huangalii upande wa pili wa madini yetu yanayopotea kwa ziara zake za kuwaita wazungu waje kuchukua madini bure?
 
Waalim wa sayansi 47 kutoka USA wameapishwa leo ubalozi wa Merekani. Wamejitolea kuja kufundisha shule za Sekondari za Tanzania baada ya kuombwa rasmi na Mheshimiwa Rais Kikwete.

Ahsante Kikwete. Inanikumbusha wakati nasoma, enzi hizo, tulikuwa na Waalim kutoka Australia, India, Uingereza kwa uchache na mambo yallikuwa swaafi kabisa,

Hii ni fursa kubwa kwa Waalim wetu kujifundisha mbinu za wenzetu nasi kuwaonesha uwezo wetu nao wajifunze kutoka kwetu.

Haya wanafunzi, kazi kwenu na Mungu awasaidie muwe wanafunzi wazuri wa kuigwa na hawa Wamerekani wapeleke salaam njema kwao ili waje na wengine wanaosuasua.
hii ni nzuri sana, salamu kwa wale wote wanaobeza safari za JK.
 
Kweli njaa ni noma.Watu wako tayari kuuza utu kusifia upuuzi kama huu.Wakati nasoma tosamaganga nilifundishwa hesabu na walimu wa aina hii.Alikuwa na degree ya algebra.likuwa tabu tupu kwenye topic zingine ,matokeo yake baada ya huyo mwalimu kuondoka, ilibidi mwalimu wetu wa hesabu(mbongo) arudie topic zote alizofundisha mmarekani ndo tukaelewa.
 
hawa watu wana sera ya kuwatafutia watu wao ajira nje ya nchi...wamukutana na omba omba wakaamua kumbebesha zigo la misumari.......... HONGERA SANA JK....
 
Zomba,

..walionifundisha mimi walikuwa waalimu wa masomo ya Science na hisabati.

..tena kuna kwa miaka tofauti walikuwepo wanatokea Australia, Ujerumani, India, Marekani, na Uingereza.

..waalimu 47 wont make much difference kama waalimu wenzao wazalendo wataendelea kukatishwa tamaa kama inavyotokea sasa hivi.

JokaKuu,
nakubaliana kabisa na wewe. Hata hivyo, wanadamu hapa na pale tu wasahaulifu sana...but any general in the army who try to use the most skilled warrior who has lost his heart, while knowing he is of little use in the battle must be crazy. Tanzania haitajengwa na wamarekani....tunacheka makosa ya wenzutu ilihali sisi tunayarudia kama vile yalivyo. We have to motivate our working force. These guys can't teach us how to fly rockets....they can teach us how to depend on them so that they could continue to screw us.
 
Akili yako, ya mtoa mada na huyo unayemsifia zote sawa................
ungesema kwa nn ningekujibu. kwani rais kusafiri ni lazima, lkn kwa mtizamo wako wewe unafikiri mtu akisafiri anaenda kula bata tu, au ni ktkt lile kundi la ukosoaji hata mazuri lkn wewe hata zuri moja la mfano huna. pole.
 
Maabara zpo kwenye vijiwe vyetu a.k.a shule za kata?
 
Gharama ya kwenda kuwaomba marekani ni mara mbili na zaidi kusomesha wa hapa
 
Nataka nijue safari zake ni ngapi na zimetugharimu kiasi gani.This is for "cost-benefit analysis purposes"...Ni sawa na mtoto aliyetumwa dukani akapoteza kila kitu,ila akarudi na embe dodo kuonyesha kuwa safari yake ya dukani ilikuwa na manufaa.
 
Kuleta walimu kutoka Western countries kuwalipa in terms of dollars huku kuna migomo ya walimu ambao hawalipwi it is just a nonsensical decision.
 
Hivi unapogundua kuwa baba ako kaenda kuwachukua watu baki ili waje kula pilau iliyopikwa na wewe mwenyewe alafu wewe ukakosa ila kukiwa na mlenda anajifanya anakupenda!!!huo ni unafiki uliopitiliza!!!
 
Back
Top Bottom