Saa ishirini na nne za Nusrat Hanje kutia doa Mihimili mitatu ya Nchi

Ila kwa kweli ki ubinadamu, mtu yoyote angakuwa amevaa viatu vya nusrat hanje asingekubali kukaataa ubunge na kuendelea kusota jela.

Tuwe tu wakweli saa nyingine
Mkuu, unataka tuubariki huu uhuni simply kwa kuwa Nusrat kawekwa huru?

Kama binadamu tena ninayemfahamu Nusrat in person nimefarijika kutoka kwake jela tena kutokana na kunyimwa dhamana kwa hila, ila tukio lililo nyuma ya utolewaji wake si kitu cha kuungwa mkono.
 
Kwa waliowahi kutumia manati, unamlenga ndege umevuta manati yako hadi mwisho halafu kipago kinachomoka mkononi kinakurudia usoni. Balaa lake usiombe.

Mwisho mzuri wa hili jambo ni pande zote kukaa mezani waongee kama watu wenye akili, hiki kinachoendelea ni kuzidi kujitia aibu tu.
 
CCM bhana sijui akili walishazipeleka wapi? Mahera anadai majina ya covid 19 yaliletwa na chadema ndio hayo aliyoyapeleka kwa Ndugai.

1. Mahera anadai CHADEMA iliwasilisha hayo majina tarehe 19 November 2020. Tarehe 20 Nov 2020 huyohuyo Mahera akiwa Azam tv alidai tume haijapokea majina ya viti maalumu kutokea CHADEMA. (Angalieni hizi tarehe mtaona nani muongo). Wanasema ukiwa muongo jitahidi uwe na kumbukumbu maana hii ni aibu.

2. Nusrat Hanje: tufanye basi ni kweli Mahera anasema ukweli kuwa Chadema iliwasilisha majina ya viti maalumu. Swali la kujiuliza: Nusrat Hanje alikuwa mahabusu, Chadema wana mamlaka gani nchi hii ya kuweka jina la Nusrat kwenye orodha ya viti maalumu na kuhakikisha wanamtoa mahabusu ili akaapishwe? Hapa ndio ninapowaona ccm either walishatuona watanzania hatuna akili au wao ndio hawana akili. Chadema ina mamlaka gani ya kumtoa mwanachama wake mahabusu ili awahi kuapishwa?

Ushauri wangu kwa chadema. Fungueni kesi mahakamani. Hii kesi ni rahisi sana kushinda. CCM imepanga huu mchezo kiboya sana.

Tunashukuru Nusrat Hanje ametoka mahabusu. Sasa dada wa watu yupo huru.
Mahakama ipi?kwani hujui kuwa mahakama zote zipo mfukoni
 
Tatizo la hawa ccm hawajui hesabu. Wanapenda namba ila hesabu hawajui.
Angalau mzee wa lupaso yeye alitumia vyote nguvu na akili sio kwa ccm mpya wao nguvu mwanzo mwisho.Chek walivyoiba kizembe Hadi hata teja anajua.Wangewaachia hata cdm wabunge 50 tena wapya wasio na majina hapa wangefuta ushahidi wa wizi na kuwahadaa cdm na wafadhili na sio hii ya ushindi wa kishindo Leo umegeuka shubiri Hadi wanahaha kufoji viti maalumu feki.Aibu kweli.
 
Swali la kujiuliza. Hawa ccm ndio hawana akili au ccm watanzania washatuona hatuna akili ndio maana wanatengeneza movie bila hata kuihariri?
Washatuona cc watanzania HATUNA AKILI! Kwa 7bu anaweza akasimama kiongozi anayeaminika na pia ni MSOMI mzuri kabisa lkn akaongea kitu ambacho hata mtu mwwnye Akili ya kawaida AKAMSHANGAA! Haya mambo kuna wengine WANAYAFURAHIA kbs lkn TUSIPOPIGA kelele ya KUKEMEA ipo siku tutakuja kuona MAAJABU zaidi ya haya! Maana hata Mimi naweza nikamteua mke wangu awe mmbunge na akaapishwa na kusifanyike chichote! MUNGU atusaidie maana huko tuendako kila mtu atakuwa kambare!
 
Hii imemgharimu hata Polepole , imeshauriwa atimuliwe
katimuliwa kwa kupewa ubunge 😁😁😁. Ukowa sio mfia chama, maisha raha sana.
Fanya kazi mkuu upige pesa sio kutetea wanasiasa, utaonekana mnafiki kama wao tu, shauri zako.
TL anapiga pesa huko saa hizi. Polepole amekuwa mbunge. Wewe bado mpiga zumari tuu.
Mungu akusaidie, akuondoe tongotongo kama mimi.
 
CCM bhana sijui akili walishazipeleka wapi? Mahera anadai majina ya covid 19 yaliletwa na chadema ndio hayo aliyoyapeleka kwa Ndugai.

1. Mahera anadai CHADEMA iliwasilisha hayo majina tarehe 19 November 2020. Tarehe 20 Nov 2020 huyohuyo Mahera akiwa Azam tv alidai tume haijapokea majina ya viti maalumu kutokea CHADEMA. (Angalieni hizi tarehe mtaona nani muongo). Wanasema ukiwa muongo jitahidi uwe na kumbukumbu maana hii ni aibu.

2. Nusrat Hanje: tufanye basi ni kweli Mahera anasema ukweli kuwa Chadema iliwasilisha majina ya viti maalumu. Swali la kujiuliza: Nusrat Hanje alikuwa mahabusu, Chadema wana mamlaka gani nchi hii ya kuweka jina la Nusrat kwenye orodha ya viti maalumu na kuhakikisha wanamtoa mahabusu ili akaapishwe? Hapa ndio ninapowaona ccm either walishatuona watanzania hatuna akili au wao ndio hawana akili. Chadema ina mamlaka gani ya kumtoa mwanachama wake mahabusu ili awahi kuapishwa?

Ushauri wangu kwa chadema. Fungueni kesi mahakamani. Hii kesi ni rahisi sana kushinda. CCM imepanga huu mchezo kiboya sana.

Tunashukuru Nusrat Hanje ametoka mahabusu. Sasa dada wa watu yupo huru.
Tatizo ccm imwadharau watanzania wote kwa kiwango cha kutisha mno, CCM wao hujiona wenye haki ya kufikiri kwa niaba ya watanzania wote japo fikra zao zimejaa uzandiki, uonevu, manyanyaso na mambo yote ya hovyo hovyo yasiyo na tija kwa Taifa, iweje NECCCM Tumeccm ifikiri kwa niaba ya chadema? iweje Mwanasheria mkuu wa CCM afikiri kwa niaba ya chadema? iweje Ndungai na polepole wenye washauri vilaza akina cyprian Musiba le mutuz na wajinga jinga kibao wafikiri kwa niaba ya chadema na kwa watanzania kwa ujumla? CCM acheni kuwaza kufikiri vitu vya hovyo hovyo kwa niaba ya wananchi
 
Hata shetani alipoingia bustani ya Eden alianza na Hawa,kusudi amnase Adam kirahisi.
(Shetani) alianza na covid 19 (Hawa) ili kumnasa CDM (Adam).
Mpaka hapo Shetani kashindwa!
 
Back
Top Bottom