Ruling Kuhusu Kesi ya Lema ni Leo!!

Ruling Kuhusu Kesi ya Lema ni Leo!!

Leo ni leo kusuka ama kunyoa HIGH COURT DAR, kamanda Lema anaweza akarudishiwa ubunge au akaukosa, hilo linategemea maamuzi ya jopo la majaji wa mahakama kuu ikiongozwa na jaji mkuu. Kwa hiyo hapa kunaweza kutokea ya OBAMA au ya ROMNEY (GOD FORBID)
Uongo mtupu. angalia hapo kwenye RED.
 
Wameumia wakina nani tena? Tuache mahakama iamue tu kama haki ipo basi itakuwepo tu haina shida muhimu ni kuomba Mungu haki itendeke kwa pande zote!
Watakaotoa hukumu ambao wameteuliwa na serikali ambayo imetokana nachama ambacho kila siku kinatafuta namna ya kusambaratisha watu wanaowaona wachungu kwao,Mungu humsaidia mtu ambaye naye anajisaidia na kumuomba peke yake bila kufanya kitu haisaidii.
 
Kesi imeahirishwa.Mahakama imekubali kuna kosoro kwa upande wa mahakama

Baada ya siku 14 marekebisho yatafanyika halafu kesi itarudi tena mahakamani

Heee ama kwa hakika maajabu hayatakaa yaishe nchini Tanzania hasa huko mahakamani.
Kwanini hawakurekebisha hizo kasoro mapema kabla ya kupanga tarehe ya kutoa hukumu ya pingamizi?
Walikuwa na sababu gani ya kubadili tarehe toka 29/11 ya awali hadi 8/11 wakati wakijua kuna kasoro kwa upande wa mahakama?
 
Wanabodi na wanaushirika.

Tujenge utamaduni wa kuheshimu uhuru wa mahakama tukubali hukumu yoyote itakayotolea na mahakama.
Sawa mkuu,kuheshimu uhuru wa mahakama ni jambo muhimu sana .Lakini ninyi mnatutia wasiwasi,kwanini kesi hii mmeiamishia DAR?
 
Makamanda wanasizitiza ni matembezi ya miguu sasa hatupandi gari kutoka mahakamani

Mkuu mnaelekea wapi sasa na joto la Dar na mmevaa magwanda mnatachemka inabidi makamanda kila mmoja abebe chupa ya maji.
 
Tafadhali Yericko Nyerere naomba uifanye siku yangu leo iwe njema kwakutupa matokeo hapo mahakamani!
 
Uongo mtupu. angalia hapo kwenye RED.

Unajua nami nimekuwa nafuatilia huu uzi toka mwanzo naona kama hata waliokwenda mahakamani hawakujua wamekwenda "Kuchukua" nini. Leo nijuavyo mimi (istand to be corrected) ilikuwa siku ya kutolewa maamuzi dhidi ya mapingamizi yaliyowekwa na pande zote wala haikuwa siku ya hukumu!!

 
Kesi imeahirishwa.Mahakama imekubali kuna kosoro kwa upande wa mahakama

Baada ya siku 14 marekebisho yatafanyika halafu kesi itarudi tena mahakamani

huu ni ushindi kwa Lema na chadema kwa ujumla.!
 
hii kesi naona inawaumiza kichwa sana! hawa waiahirishe mara 100, ukweli utakuja kujitenga tu siku moja!

naona uchakachuaji wanaotaka kufanya unashindikana ndio maana wanapiga dana dana tu....
 
Kweli Lema na CDM kwa ujumla wamekosa mvuto kila mahali na hapa JF. Nimeamin ule msemo kuwa ngoma ikilia sana hupasuka. Nakumbuka kuna kipindi ikianzishwa thread inayomhusu Lema au CDM inakuwa na wachangiaji zaidi ya 200+. but now nashangaa hata posts 30 hazifiki!!! Am happy watanzania wamepevuka!!!

Leo tunachoma wapi mkuu?

Post yako ni ya 32 na ile ya chini yake ya 33..halau unasema posts 30 hazifiki.
 
Back
Top Bottom