Ni kweli Haki na Usawa chini ya Utawala wa Sheria uzaa Demokrasia halisi. Si kweli kwamba uchaguzi wa Urais wa USA uliompa ushindi Baraka Obama ni kwa sababu Democratic party wametumia pesa nyingi kama Mweshimiwa Pinda anavyotaka kuuaminisha Umma wa wanzania.
Kama sikumwelewa vizuri lakini niimani yangu kuwa Mweshimiwa PINDA alimaanisha kuwa kwa sasa CCM watumie fedha nyingi kwenye chaguzi ila tu waziweke pamoja ili kuweza kustrategize kwa mamoja kama Chama.
Hii si sahihi na haiwezekani ktk mazingira ya Kitanzania kwa sababu Pesa Zinazotumiwa na CCM iwe ndani ya chaguzi za chama au chaguzi kuu zinazohusiha vyama vya upinzani ni fedha HARAMU ambazo hazina uhalali wowote na vyanzo vyake kila mtu anajua ni fedha za walipa kodi, wanyonge, waliokata tamaa ambazo uchotwa bila huruma na kwenda kufichwa nje ya nchi huku zikisubiria kununua madaraka.
Rais Baraka Obama ameshinda Marekani si kwa sababu chama chake au yeye mwenyewe ametumia fedha nyingi kwa kuwaonga wapiga kura au kununua kadi za kupigia kura bali ni sera nzuri za chama chake na jinsi alivyozitekeleza kama ahadi zake ya 2008.
Lakini si kama tunavyoona hapa kwetu mgombea kila anapokwenda kucampaign anatoa ahadi mpya ambazo hazitekelezeki. Nipata kuwepo Marekani wakati wa uchaguzi 2008 kwa miezi miwili kabla ya uchaguzi ule lakini sikuwahi kuona wapambe au wapenzi wa mgombea yoyote akigawa pesa kama hapa kwetu.
Ni aibu sana kwa viongozi wa CCM kuwa watu wa kwanza kuongelea Demokrasi na uchaguzi wa Marekani huku NAPE akirusha kombora kwa Vyama vya upinzani eti Wameona wapinzani wenzao wanavyokubali matokeo kirahisi.
Hii ni dhana potovu kwa kijana kama huyu kwani anajua fika kwamba kama tume si huru, watu kukimbia na masanduku ya kura, watu kitishwa na film za mauaji, mabomu ya machozi yasiyokuwa na sababu kura na kutanganza matokea na kuapishana chapuchapu ni baadhi tu ya matukio ya kawaida.
CCM kama chama Tawala wanapaswa kujifunza mengi toka kwa wamarekani. pale kwenye uchaguzi wa marekani juzi hakuna aliyepata hata kusukumwa, hapakuwepo na mabomu ya machozi na watu hawakupewa rushwa na kutishiwa picha za mauaji ya Rwanda na Burudi eti mkiwachagua wapizani tutakuwa kama hivi au vile.
Mwisho siasa za sasa hivi Shule ni muhimu na siyo tu kutumia uzoefu usioendana na uhalisia.
CCM kwa mjibu wa Mweshimiwa PINDA ni kama inatafuta ni jinsi gani ya kuhalalisha RUSHWA kwa eti imeona wamarekani safai hii wametumia fedha nyingi sana kwenye kumpata raisi wao.
HAPANA RUSHWA NI RUSHWA ( TANZANIA) na MATUMIZI YA FEDHA NI KITU KINGINE MAREKAN). PILI VYANZO VYA PESA HIZO NDILO JAMBO LA MUHIMU HAPA NA MATUMIZI YAKE ( TANZANIA).