Rostam aibukia kanisani!

Rostam aibukia kanisani!


Samahani kwakuvamia hili jikwaa mimi sio mwanasiasa ila imenibidi niseme kidogo maana naona sasa ni KERO KUBWA,Napenda mzidi kutambua majukumu ya mlinziwetu,Baba mwenye Muji eeeh! maana Yupe na mali inapo potea mlinzi ndio anajibu kwa boss wake muajili yaani mwajili ni mwananchi.

Nawapa pongezi wotee mnao post kuhusu Rostam,ila ukweli utabaki palepale maana mimi sielewi kabisa yaani watu wanaacha kuongelea mambo yanayo husu taifa wizi unafanyika waziwazi na wezi wenu wanajulikana wezi wa EPA mnakaa eti Rostam kaiba Nadhani tunashida tena kubwa kama mambo ya EPA tumeamu kuya samehe nakuanza kumfuatilia huyu Muhindi MTZ nawashangaa Hii nyumba inamwenyewe bwana eeeh! kama Ropstam Mwizi hii nyumba inamlinzi na Baba mwenye nyumba Pia yupo.

Kwani ninani kati yetu ambaye ajui kuwa watu weupe ni wajanja eeh! naamini Rostam anafanya kwakutumia akili ndio maana utasikia Richmond yake,Mara Voda lakini anayo haki yakuwa navyo hivyo vitu maana si ni akili Yake ndio anaotumia kutafuta.

Mimi nadhani sisi tufatilie yetu tuachane na huyu Muhindi maana atatupotezea muda Ukweli hatuwezi kumfanya chochote tutaishia tu kumchafulia jina ila Watu wa Igunga wamemzimikia sana hawaambiwi wala hawasikii wanampenda mtu wao.

Hata kama ungekuwa wewe Hauwezi kukaa sehemu kijinga wakati opportunity yakupata mshiko ipo eti ukaacha kupata pesa eti kisa watu watachonga hiyo haisaidii mimi nadhani huyu jamaa aendelee tu na mabusiness yake kama NMyumba haina mlinzi Basi ijulikana kama tumempa jukumu la kulinda nyumba alafu tunamlipa itakuwa je mali ziibiwe sizitalipwa na huyo mlinzi wasiwasi nininini?

Mimi nasema tena kama KKKT wangetulia tu hiyo pesa wafanyie kazi ya Mungu,Maana Mungu anainua watu kwa njia mbalimbali kutegemeza kazi yake mimi nadhani hapo hakuna jipya ni huyo Rostam akae kimya tu kama Ben,
Maana inakuwa Kero sasa jamaa anakuwa kama DILI sasa tunasahau mpaka mambo ya muhimu.

hamna jipya.
 
Hmmmh! hilo kanisa kweli wanashangaza kualika mtu kama " ROAST THEM" after all the turmoil ... but anyway with us Tanzanians ndivyo tulivyo .. wa Monduli alikaribishwa kama mfalme, wa bariadi ndiyo usiseme na matarumbeta sasa huyu si ajabu ... maana tunawalea wenyewe
 
Mtikila ananuka kwa ufisadi kama Rostam na Lowassa, sasa anyamaze tu kuna kina Nape, hao wameanza huko UV-CCM sasa tusubirie nao hao vipi, lakini Mtikila sasa ni political history.

Sasa ni zamu ya kina dogo kama Nape!
 
kaaz kweli kweli
lakini si alipokea hela??? haijalishi kakopa au kamfisadisha ila cha msingi kapokea mijisenti and he's at it... let him face it

Mtikila alipokea hela ya RA akijua kabisa ni zakifisadi angenyamaza kimya kwenye issue hii.Naye amejidhlilisha.
 

Samahani kwakuvamia hili jikwaa mimi sio mwanasiasa ila imenibidi niseme kidogo maana naona sasa ni KERO KUBWA,Napenda mzidi kutambua majukumu ya mlinziwetu,Baba mwenye Muji eeeh! maana Yupe na mali inapo potea mlinzi ndio anajibu kwa boss wake muajili yaani mwajili ni mwananchi.

Nawapa pongezi wotee mnao post kuhusu Rostam,ila ukweli utabaki palepale maana mimi sielewi kabisa yaani watu wanaacha kuongelea mambo yanayo husu taifa wizi unafanyika waziwazi na wezi wenu wanajulikana wezi wa EPA mnakaa eti Rostam kaiba Nadhani tunashida tena kubwa kama mambo ya EPA tumeamu kuya samehe nakuanza kumfuatilia huyu Muhindi MTZ nawashangaa Hii nyumba inamwenyewe bwana eeeh! kama Ropstam Mwizi hii nyumba inamlinzi na Baba mwenye nyumba Pia yupo.

Kwani ninani kati yetu ambaye ajui kuwa watu weupe ni wajanja eeh! naamini Rostam anafanya kwakutumia akili ndio maana utasikia Richmond yake,Mara Voda lakini anayo haki yakuwa navyo hivyo vitu maana si ni akili Yake ndio anaotumia kutafuta.

Mimi nadhani sisi tufatilie yetu tuachane na huyu Muhindi maana atatupotezea muda Ukweli hatuwezi kumfanya chochote tutaishia tu kumchafulia jina ila Watu wa Igunga wamemzimikia sana hawaambiwi wala hawasikii wanampenda mtu wao.

Hata kama ungekuwa wewe Hauwezi kukaa sehemu kijinga wakati opportunity yakupata mshiko ipo eti ukaacha kupata pesa eti kisa watu watachonga hiyo haisaidii mimi nadhani huyu jamaa aendelee tu na mabusiness yake kama NMyumba haina mlinzi Basi ijulikana kama tumempa jukumu la kulinda nyumba alafu tunamlipa itakuwa je mali ziibiwe sizitalipwa na huyo mlinzi wasiwasi nininini?

Mimi nasema tena kama KKKT wangetulia tu hiyo pesa wafanyie kazi ya Mungu,Maana Mungu anainua watu kwa njia mbalimbali kutegemeza kazi yake mimi nadhani hapo hakuna jipya ni huyo Rostam akae kimya tu kama Ben,
Maana inakuwa Kero sasa jamaa anakuwa kama DILI sasa tunasahau mpaka mambo ya muhimu.

hamna jipya.

kazi kwenu
 
Siasa ni mchezo wa draft na RA kishaingia kingi, Mchungaji akubali kushindwa mchezo uishe. Kwa sasa hoja za mchungaji dhidi ya RA ni upuuzi mtupu! anachotakiwa nikuzitupa fedha na kisha kujinyonga kama Yuda.

namshauri RA sikunyingine wakimwalika kwenye mnuso aende na waandishi wa habari na kufanya caverage kwa TV.
 
Mkanya inaelekea una wazo lakini unashindwa kuliwasilisha vizuri. au point yako haijaeleweka. Vinginevyo hutaki Rostam aongelewe. Je na ufisadi usiongelewe.

Hapa point ya msingi Rostam ni moja wa mafisadi katika nyumba hii suala la kuwa ni muhindi au mzungu si mjadala uliopo. Mjadala wetu ni mafisadi.. Sasa kama baba mwenye nyumba naye ni mwizi basi mtoto asiongelewe au asikanywe. Nafikiri cha msingi hapa suala la mafisadi litafutiwe ufumbuzi na hata katika kusemwa huku nina uhakika ya kwamba hata waliokuwa mbioni kufanya ufisadi mkubwa wanapata wasiwasi ya kuchafuliwa na wananchi na hata kuchukiwa na wananchi kwa ujumla.

Hata ndugu yangu Mtikila ni mwanasiasa safi tatizo kubwa hapa ni huu ukame ndio unatusumbua watanzania. kutaka makubwa kwa njia ya mkato. Nafikiri ingekuwa bora zaidi hata angeenda hata kukopa Bank na si pesa ambazo zina harufu ya ufisadi.

Kuhusu kuchangia kanisa kila mtu anaweza kuchangia kanisa. Kwani nani anafahamu wapi watu wanapata pesa za kupeleka madhabahuni kama sadaka. Na wakati mwingine wazee wakanisa ndo hao hao wala rushwa. Wacha kazi ya Mungu isonge mbele na ili hali pesa hizo zibarikiwe na Mwenye Enzi Mungu ndiye muaamuzi kama hapo pana baraka au la. Hata kama ingekuwa ni mwaliko rami its ok, Lakini tatizo ni hotuba ya kujisafisha as reported.
 
Mchungaji anapaswa kurudi na kwenda kutubu, kwani kama aliweza kuhongwa ili aweze kulipeleka Mwanahalisi mahakamani anafikiri siri haijafichukua?

siri imefichuka ,siri imefichuka , mchungaji kahongwa na sasa imekuwa kizaazaa,
 
Kesi ya Mtikila dhidi ya mwanahalisi ni namba 55.
Kesi ya Rostam dhidi ya Mwanahalisi ni namba 54.
Kesi ya Mtikila dhidi ya Tanzania Daima ni namba 57.

Kesi hizi zimefunguliwa mwaka huu mwezi April ,kumbuka huyu mchungaji alipewa fedha muda na siku hizo hizo.

Nawatakia tafakuri ya kina.
 
Last edited:
We have nothing 2 urge on this ! Mtikila kapokea fedha ambazo yeye mwenyewe kakiri hivyo kwa hiyo kumtuhumu rostam juu ya yale anayoendelea kusema ni upuuzi mtupu! na ushauri zaidi kwa mtikila kwa taaluma na kipaji chake aelewe utaratibu wa kulipa madeni baada ya kukopa maana kama mchungaji aweza kopa hela asilipe naogopa sana mbingu anayotuhubiria kwenda kwenye nchi ya Maziwa na Asali ipo wapi!
 
We have nothing 2 urge on this ! Mtikila kapokea fedha ambazo yeye mwenyewe kakiri hivyo kwa hiyo kumtuhumu rostam juu ya yale anayoendelea kusema ni upuuzi mtupu! na ushauri zaidi kwa mtikila kwa taaluma na kipaji chake aelewe utaratibu wa kulipa madeni baada ya kukopa maana kama mchungaji aweza kopa hela asilipe naogopa sana mbingu anayotuhubiria kwenda kwenye nchi ya Maziwa na Asali ipo wapi!

Yes mtikila kakopa za RA na kweli ni za kifisadi na kwa hili mtikila kakosea ndiyo.

Lakini hii bado haimpi uhalali Rostamu kwenda kwenye mimbali ya kanisa na kuanza kusema wanao sema ni mafisadi ni waongo na wana chuki/wivu.

Hapo ndipo nasema big nooooo! kwa RA, yeye kutoa vijisenti hakumuhalarishii kwenda popote kujisafisha eti kwa vile alisha wapa wengine vijisenti, pale ni patakatifu siyo pa kwenda kusema uchafu wa siasa!

Hata hivo ieleweke wazi mafisadi wametufikisha pabaya sana watanzania kwa kufanya maisha yetu yazidi kuwa magumu, kwahiyo mtu akiona pesa ya nje nje lazima udenda umtoke!

Nionavyo mie pesa wakileta mafisadi zichukueni kwani si zao ni zetu wametuibia, ila mkisha zichukua zisiwazibe midomo, wasemeni na endeleeni kuwakosoa na kuwashikisha adabu!.

Na tusiishie hapa tu, tujiandae hata hiyo 2010 mafisadi wapo wanakusanya shilingi za kutumwagia ili tuwape kura, mihela yetu walo tuibia wakileta tuchukue saana tu, ila kwenye mabox ya kura tuwamalizie mbali.

mtazamo wangu tu wakuu
 

Samahani kwakuvamia hili jikwaa mimi sio mwanasiasa ila imenibidi niseme kidogo maana naona sasa ni KERO KUBWA,Napenda mzidi kutambua majukumu ya mlinziwetu,Baba mwenye Muji eeeh! maana Yupe na mali inapo potea mlinzi ndio anajibu kwa boss wake muajili yaani mwajili ni mwananchi.

Nawapa pongezi wotee mnao post kuhusu Rostam,ila ukweli utabaki palepale maana mimi sielewi kabisa yaani watu wanaacha kuongelea mambo yanayo husu taifa wizi unafanyika waziwazi na wezi wenu wanajulikana wezi wa EPA mnakaa eti Rostam kaiba Nadhani tunashida tena kubwa kama mambo ya EPA tumeamu kuya samehe nakuanza kumfuatilia huyu Muhindi MTZ nawashangaa Hii nyumba inamwenyewe bwana eeeh! kama Ropstam Mwizi hii nyumba inamlinzi na Baba mwenye nyumba Pia yupo.

Kwani ninani kati yetu ambaye ajui kuwa watu weupe ni wajanja eeh! naamini Rostam anafanya kwakutumia akili ndio maana utasikia Richmond yake,Mara Voda lakini anayo haki yakuwa navyo hivyo vitu maana si ni akili Yake ndio anaotumia kutafuta.

Mimi nadhani sisi tufatilie yetu tuachane na huyu Muhindi maana atatupotezea muda Ukweli hatuwezi kumfanya chochote tutaishia tu kumchafulia jina ila Watu wa Igunga wamemzimikia sana hawaambiwi wala hawasikii wanampenda mtu wao.

Hata kama ungekuwa wewe Hauwezi kukaa sehemu kijinga wakati opportunity yakupata mshiko ipo eti ukaacha kupata pesa eti kisa watu watachonga hiyo haisaidii mimi nadhani huyu jamaa aendelee tu na mabusiness yake kama NMyumba haina mlinzi Basi ijulikana kama tumempa jukumu la kulinda nyumba alafu tunamlipa itakuwa je mali ziibiwe sizitalipwa na huyo mlinzi wasiwasi nininini?

Mimi nasema tena kama KKKT wangetulia tu hiyo pesa wafanyie kazi ya Mungu,Maana Mungu anainua watu kwa njia mbalimbali kutegemeza kazi yake mimi nadhani hapo hakuna jipya ni huyo Rostam akae kimya tu kama Ben,
Maana inakuwa Kero sasa jamaa anakuwa kama DILI sasa tunasahau mpaka mambo ya muhimu.

hamna jipya.

Kweli Mtu haachi asili....

Si katika sura tu utamtambua kuwa ni mweusi au mweupe bali hata katika maandishi!!
 
Twamshangaa Rostam, lakini makanisa yetu ni machafu

Johnson Mbwambo Julai 16, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo

NIANZE ninachotaka kujadili leo kwa kusema mapema kwamba ingawa sifahamu mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ana washauri binafsi wangapi; lakini yeyote aliyemshauri kuutumia Usharika wa KKKT Kinondoni kusafisha jina lake kutokana na tuhuma za kuhusishwa na kampuni ya kifisadi ya Richmond, hakumtakia mema.

Niliamini kwamba mahali pazuri ambako Mheshimiwa Rostam alistahili kujieleza (kujisafisha) kuhusu tuhuma hizo ni kwenye mkutano na vyombo vya habari (press conference).

Huko ndiko mtu unaweza kujieleza kwa mapana na marefu na kisha kuwapa waandishi wa habari fursa ya kuuliza maswali yanayosumbua vichwa vya wananchi kuhusu mahusiano yake na Richmond na hata masuala mengine kama vile EPA n.k

Kanisani hapakuwa mahali pazuri kwake kujisafisha kwa sababu huko unazungumza tu na wala hakuna fursa ya kuulizwa maswali. Na hata kama angetoa fursa ya kuulizwa maswali, hakuna washarika ambao wangemuuliza maswali magumu, kwa sababu sana sana walichomwitia pale ni mchango wake (milioni saba) kwa Usharika huo. Ndiyo maana naamini njia sahihi kwake ni press conference.

Kwa hiyo lilikuwa jambo jema kwake kuitisha Press Conference Jumapili iliyopita na kujieleza. Japo waandishi hawakumbana kweli kweli kwa maswali mazito kama vile ya kumtaka aeleze ni vipi watu ambao wako karibu na yeye kimahusiano walimtaja katika ripoti ya Kamati ya Dk. Mwakyembe kuwa ana mahusiano na kampuni ya Richmond n.k, mwanga kidogo umepatikana.

Japo utetezi wake, kwa namna inayoshangaza, unafanana kidogo na wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa (wivu na kukwamisha uteuzi wa watu katika nafasi mbalimbali za uongozi), bado naamini Watanzania wamepata mwanga kidogo kufahamu iwapo ni haki kumtuhumu Rostam Aziz au ni “chuki na wivu tu wa kijinga” kama alivyosema.

Lakini mjadala wangu leo si kuhusu Rostam Aziz na tuhuma zinazomwandama; bali ni kuhusu usafi wa Kanisa kwa ujumla.

Nimesema kwamba aliyemshauri Rostam kulitumia jukwaa la KKKT Kinondoni kujisafisha, hakumtakia mema. Nimesema hivyo kwa sababu kama mshauri huyo angelifanya home work yake vizuri; angelijua kwamba uongozi wa Usharika huo tayari umegubikwa na tuhuma za ufisadi, na hivyo kwenda kwake huko kumeongeza tu chumvi kwenye kidonda.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwepo na tuhuma za ufisadi dhidi ya uongozi wa Usharika huo, na mwezi uliopita tu ulisambazwa waraka wa wanakwaya kwa washarika uliotumwa kwa uongozi wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ambao uliorodhesha tuhuma mbalimbali za ufisadi unaoendeshwa na uongozi wa Usharika.

Ingawa zilifanyika juhudi za kuzima tuhuma hizo na kuukejeli waraka huo, hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba uongozi wa Dayosisi ulilazimika kutuma ‘mjumbe’ Jumapili moja ili kuwatuliza washarika na kuwaahidi kwamba uchunguzi wa madai hayo unafanyika na kwamba wangepewa taarifa pindi ukikamilika.

Sasa wakati washarika bado wakisubiri mrejesho wa uchunguzi wa Dayosisi kuhusu tuhuma hizo za ufisadi, linaibuka suala jipya la Rostam kualikwa usharikani na uongozi huo huo unaotuhumiwa kwa ufisadi, na yeye Rostam akaamua kuitumia fursa hiyo kujisafisha!

Nina hakika mshauri wa Rostam angeliyajua hayo mapema pengine angemtafutia kanisa jingine ‘salama’ zaidi kuliko KKKT Kinondoni. Na kama angefanya hivyo (Rostam), pengine kauli yake hiyo ya kujisafisha aliyoitoa KKKT Kinondoni isingekanwa na kutotambuliwa na Dayosisi ya Mashariki na Pwani kama ilivyotokea.

Kwa ufupi, Kanisa la KKKT Kinondoni ambako Mheshimiwa Rostam alichagua kwenda kujisafisha si safi; kwani lenyewe linachunguzwa na Dayosisi kwa tuhuma mbalimbali za ufisadi!

Ninachojaribu kueleza hapa ni kwamba tunaweza kumlaumu Rostam kwa kuutumia Usharika wa KKKT Kinondoni kujisafisha, tunaweza kufurahia tamko la Dayosisi ya Mashariki na Pwani la kumkana Rostam, lakini ukweli unabaki pale pale. Na ukweli huo ni kwamba makanisa yetu yenyewe ni machafu kweli kweli.

Sitaki kuyazungumzia makanisa mengine nchini (na yanaibuka kama uyoga kila kukicha), lakini hili la KKKT Tanzania ambalo mimi ni msharika, nadiriki kusema nalo si safi.

Labda niwaulize Walutheri wenzangu, ni askofu wa kanisa gani aliyeshiriki katika mapokezi ya Edward Lowassa siku aliporudi Monduli baada ya kujiuzulu uwaziri mkuu kutokana na suala hilo hilo la Richmond analotuhumiwanalo Rostam?

Je si kweli kwamba askofu huyo ni Laizer na ni wa KKKT? Si kweli kwamba alipopewa fursa ya kuzungumza, alisema maneno yaliyolenga katika kumsafisha Lowassa? Na kama hivyo ndivyo, kwa nini tushangae ya KKKT Kinondoni?

Ukweli ni kwamba baadhi ya wachungaji na baadhi ya maaskofu wetu wanawapapatikia mno wakubwa; kiasi kwamba usafi wao kimaadili na kiroho unatia shaka.

Nimepata kusali katika makanisa tofauti ya KKKT na katika miji tofauti, lakini ninachokiona huko ni kile kile – wenye pesa na madaraka makubwa wanaheshimiwa mno kuliko waumini masikini. Na hili linakwenda hata katika ngazi ya kijiji!

Unapofikia uchaguzi wa wazee wa kanisa utaona jinsi wachungaji wanavyohaha kuhakikisha wafanyabiashara wenye mapesa na wakubwa wenye madaraka serikalini au katika makampuni makubwa wanachaguliwa kuwa wazee wa kanisa; bila hata kujali uadilifu wao.

Wanafanya hivyo kwa sababu wanataka wawe karibu nao kwa kuwa wanatoa mapesa mengi kwenye Harambee za Kanisa; lakini pia kwa kuwa wanataka wawe wafadhili wao binafsi na wa familia zao.

Kwa hakika hata hapa Dar es salaam, kwenye Kanisa Kuu la Azania Front, kuna viti maalumu ambavyo ingawa haijatamkwa rasmi popote, lakini vinafahamika kwamba ni vya wakubwa au matajiri fulani. Utaambiwa hapa ni pa fulani, pale ni pa fulani n.k.

Je, hivyo ndivyo Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufunza kubagua kondoo wake kwa misingi ya pesa na madaraka? Je, si kweli kwamba utajiri, uwaziri, ukuu wa mkoa, ubunge, ujaji, ufundi cherehani, ung’arishaji viatu, udereva, umakenika na hata umachinga, ni nje ya kanisa, na kwamba ndani ya kanisa wote tu sawa mbele za Mungu?

Na ukitaka kuona ni kiasi gani wachungaji wetu wamepoteza maadili ya kanisa kwa kupenda mno pesa, hudhuria misa za wiki chache kabla ya Sikukuu ya Mavuno. Baadhi ya mahubiri ya wachungaji wa KKKT ya kuhamasisha mavuno yanatia kichefuchefu.

Utasikia Baba Mchungaji akiwahamasisha washarika wake kuleta mavuno kwa kusema: “Leteni kila kitu na tutakibariki kwa jina la Yesu. Leteni mavuno yenu yanayotokana na biashara zenu na tutayabariki. Haijalishi kama pesa zako zinatokana na biashara ya baa au ukahaba. Ukishazileta hapa tunazibariki madhabahuni katika Jina la Yesu, na zinakuwa safi! Bwana Asifiwe!”

Bila shaka Mchungaji anayetoa mahubiri ya namna hii anachokiona mbele yake ni pesa tu. Hawaonei huruma hao makahaba au wauza pombe, na wala hajali kwamba wajibu wake ni kuwaombea waokoke; bali anachokiona ni pesa zao tu!

Mchungaji anayependa pesa kiasi hicho lazima ni fisadi, na lazima atawapapatikia kupita kiasi waumini ambao ni matajiri; hata kama anajua kwamba ni mafisadi.

Nasikia katika kanisa moja mtuhumiwa wa ujambazi naye ni mzee wa kanisa kwa kisingizio kuwa “ameokoka”, lakini inadaiwa bado hajaacha shughuli yake hiyo ya zamani.

Aidha, kuna mfanyabiashara mmoja mkubwa jijini, aliye msharika wa KKKT, amechukizwa mno na kitendo cha KKKT Kinondoni kumwalika Rostam Aziz kanisani. Lakini yeye amechukia si kwa sababu Rostam anahusishwa na Richmond, lakini kwa sababu ya kuhofia kwamba Rostam anaweza kumpokonya nafasi yake ya kuwa mchangiaji mkuu katika hafla mbalimbali nchini za KKKT.

Na ukiachilia suala la pesa zake, wala mfanyabiashara huyo aliyeudhiwa na kitendo hicho cha Rostam, mwenyewe hana usafi wowote kimaadili wa kuhalalisha heshima anayopewa na kanisa hilo. Je huo nao si ufisadi?

Nimalizie tafakuri yangu kwa kusema kwamba haitoshi tu kwa Dayosisi ya Mashariki na Pwani ya KKKT kutoa tamko la kumkana Rostam Aziz; kwani sote tunajua kwamba ufisadi na uchafu wa kila aina umetawala makanisa yake. Kinondoni ni mfano mmoja tu.

Kwa ufupi, makanisa yetu yajitazame kwanza yenyewe usafi wao kabla hayajaanza kuwanyooshea wengine vidole. Si tumefunzwa katika Biblia kwamba tutoe kwanza boriti kwenye macho yetu kabla ya hatujaangalia vibanzi kwenye macho ya wengine?

Tafakari.
 
Rostam amburuta Mtikila kortini


*Wasiosikia waomba fedha zake ziwasaidie
*Asema hataki tena mjadala aichia korti

Na Waandishi Wetu, Dar, Iringa

WAKATI Mbunge wa Igunga, Bw. Rostam Aziz, ametangaza kufunga mjadala kwa kumfungulia mashitaka Mwenyekiti wa DP, Bw. Christopher Mtikila, Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) mkoa wa Iringa, kimeomba kupewa fedha zilizotolewa na Mbunge huyo ili ziwasaidie.

Katika taarifa yake jana, Bw. Aziz alisema hana la kuongeza zaidi ya kufunga mjadala na kama kuna mtu amejificha nyuma ya vyombo vya habari aache kutuhumu na kuhukumu badala yake aende kwenye vyombo vya sheria.

Akitaka kuthibitisha hilo, alisema jana alifungua kesi namba 103/2008 katika Mahakama Kuu Tanzania, dhidi ya Bw. Mtikila akitaka athibitishe madai kuwa Mbunge huyo si raia wa Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi, Dar es Salaam, Bw. Mtikila alidai kuwa Bw. Aziz si raia wa Tanzania na kwamba ni raia wa Irani.

Akizungumza na Majira jana katika ukumbi wa SIDO mjini Iringa baada ya kufunga warsha ya mafunzo ya siku tano ya kutengeneza chaki yaliyotolewa kwa wanachama wa CHAVITA kutoka wilaya zote za Iringa, Mwenyekiti wa CHAVITA wa Mkoa wa Iringa, Bw. Shaibu Juma, alisema anashangazwa kuona watu wakivutana kwa ajili ya misaada ya mbunge huyo.

Kwani alisema yawezekana KKKT na Bw. Mtikila wanageuza suala hilo kuwa ajenda ya kisiasa, wakati kundi la watu wenye ulemavu, likiendelea kuhitaji watu wenye moyo kama wa Bw. Rostam kujitokeza kuwasaidia.

Alisema kinachoendelea sasa katika suala hilo la Bw. Rostam ni aibu kubwa kwa Taifa na kama Serikali haitaingilia kati suala hilo, kuna uwezekano mkubwa wahisani wakaogopa kujitokeza kuchangia miradi ya maendeleo kwa kukwepa aibu kama aliyoipata Mbunge huyo.

Kamanda Juma alisema wapo wafanyabiashara wengi ambao ni wanajitolea kusaidia jamii yenye matatizo lakini tangu jina la ufisadi lianze kujitokeza, kila mtu anayejitokeza kuchangia anapachikwa jina hilo, jambo ambalo linakwamisha moyo wa watu hao kuendelea kujitolea.

Alisema mtu wa kwanza kulaumiwa katika suala la Bw Aziz ni uongozi wa KKKT ambao ndio ulioanzisha mashambulizi dhidi ya mbunge huyo ambaye pia ni mfanyabiashara.

Kwani alisema Bw. Aziz alifika kanisani hapo kwa mwaliko wa kikundi cha kwaya katika Kanisa hilo, ambacho kilikuwa kikifanya uzinduzi wa Albamu yake na kumtaka mbunge huyo kuwa mgeni rasmi, sasa imegeuka kuwa nongwa kwa mbunge huyo eti kwa kuwa aliongea katika uzinduzi huo na kuchangia.

Mwenyetiki huyo alisema huenda wafanyabiashara wakubwa ambao ni viongozi katika Taifa, wakafika sehemu wakaogopa kutoa misaada na sadaka makanisani kwa kukwepa aibu kama aliyoipata Mbunge huyo.

Mbali ya Mwenyekiti huyo, pia walemavu wengi ambao walikuwa washiriki katika warsha hiyo na wakazi wa wilaya ya Ludewa, ambako ni kwao Bw. Mtikila, walisema walimshangaa ndugu yao, Mtikila, kwa kumshambulia Bw. Aziz wakati fedha zake pia alipokea.

Aidha walisema kuwa kwa upande wa Kanisa halina sababu ya kuhoji uhalali wa fedha hizo, kwani wapo waumini wanaotoa sadaka kutokana na fedha za wizi na hata za mauaji, lakini kila kinachotolewa katika Kanisa husafishwa na kuwa chema na kuwa iwapo watasema mafisadi watengwe, basi hata wenye dhambi wasiruhusiwe kuingia makanisani.

Hata hivyo waliomba Serikali na makanisa kushirikiana kuchunguza upya uzinduzi wa albamu za wasanii wa nyimbo za injii ambao wamekuwa wakitaka kuchangiwa fedha kwani hata fedha hizo wanazozipata kwa kulazimisha watu kuingia kuangalia uzinduzi huo hazina tofauti na fedha za kifisadi.
 
Spika apiga marufuku mjadala wa Pinda



SPIKA wa Baraza la Wawakilishi, Bw. Pandu Ameir Kificho, amepiga marufuku mjadala uliozuka katika Baraza la Wawakilishi ukipinga kauli ya Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, kwamba Zanzibar si nchi.

Bw. Kificho alisema suala hilo kwa sasa linashughulikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano, kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, ambayo tayari imetoa maelekezo katika kulipatia ufumbuzi tatizo hilo.

"Wajumbe wa Baraza, kuanzia sasa napiga marufuku mjadala uliozuka kwamba Zanzibar si nchi au ni nchi ... suala hili kwa sasa linashughulikia na Ofisi ya Waziri Mkuu," alisema Bw. Kificho.

Alisema tayari Waziri Mkuu ametoa maelekezo na kuwataka wanasheria wakuu wawili kutoka Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutoka Zanzibar kukutana na kulipatia ufumbuzi tatizo hilo, ambalo linatokana na tafsiri ya Katiba.

Bw. Kificho alikuja juu baada ya mjadala huo ambao uliibuliwa na Bw. Pinda Dodoma baada ya kuulizwa swali na Mbunge wa Chwaka, Bw. Yahya Kassim Issa, aliyeuliza kama Zanzibar ni nchi kamili na kuzusha malumbano katika chombo hicho.

Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walianzisha tena mjadala huo katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba pamoja na Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, kusisitiza kwamba Zanzibar ni nchi kamili.

Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Bw. Mzee Ali Ussi, alimtaka Waziri Mkuu Pinda, kuliandikia barua Baraza la Wawakilishi na si kuwataka Wanasheria Wakuu wa Zanzibar na wa Muungano kukutana.

Bw. Kificho alitumia nasaha hizo kwa lengo la kupunguza kasi na munkari ya wajumbe wa Baraza ambao walionesha wazi kukasirishwa na kauli ya Bw. Pinda.

Kauli ya Waziri Mkuu Pinda kwamba Zanzibar si nchi imezusha mtafaruku mkubwa kwa wananchi wengi wa kawaida wa Unguja na Pemba ambao wameelezea hofu yao sasa ya kumezwa na Bara.
Tuma kwa Rafik
 
Kesi ya Mtikila dhidi ya mwanahalisi ni namba 55.
Kesi ya Rostam dhidi ya Mwanahalisi ni namba 54.
Kesi ya Mtikila dhidi ya Tanzania Daima ni namba 57.

Kesi hizi zimefunguliwa mwaka huu mwezi April ,kumbuka huyu mchungaji alipewa fedha muda na siku hizo hizo.

Nawatakia tafakuri ya kina.
Mh mh mh! I see
 
hawa wawili hawatofikishana mahakamani.. this is the biggest scam of all times.. hawa wanacheza mchezo wa "good cop bad cop"...
 
Kesi ya Mtikila dhidi ya mwanahalisi ni namba 55.
Kesi ya Rostam dhidi ya Mwanahalisi ni namba 54.
Kesi ya Mtikila dhidi ya Tanzania Daima ni namba 57.

Kesi hizi zimefunguliwa mwaka huu mwezi April ,kumbuka huyu mchungaji alipewa fedha muda na siku hizo hizo.

Nawatakia tafakuri ya kina.

Makubwa!!! Kumbe hili ni soo kubwa!! Yetu macho na masikio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom