Balqior
JF-Expert Member
- Jun 8, 2021
- 1,724
- 5,749
Ni ndugu yangu mtu mzima, namwita shangazi, sijawahi gombana nae, na binafsi namwona ni mtu mwema kwangu, na nimefahamiana naye toka utoto wangu hadi utu uzima huu, kipindi cha likizo nlikuwa nashinda kwake miezi mingi kabla ya kwenda home, ila kipindi cha hivi karibuni amekua na tabia ambazo zimefanya roho yangu ianze kumkataa.
Kila mwezi atanipigia simu, hili la kunipigia simu sina shida nalo, Maana hata mm huwa nampigiaga simu.
TATIZO LINAPOANZIA:
Kila nikiongea naye kwenye simu, ananiuliza maswali ambayo mara nyingi mm binafsi sipo huru (comfortable) Kuyajibu daaah..
1)Kila akinipigia simu lazima aniulize nipo wapi, nikikwepesha kumjibu atanisisitiza mpaka nimwambie niko wapi..
2)Nikimwambia napigaa mishe za kilimo, simu zitakazofuata ataniuliza mara nne nne kilimo kiliendaje.
3)Muda mwingine ananiuliza kama biashara nilizofungua bado zipo
4)Kila akinipigia ananiuliza kazi nlizo-apply zimeendaje
Kutokana na hayo maswali hapo juu, yani nimeanza kujitenga naye kimya kimya mpaka yeye Kuna siku aliniuliza mbona najitenga nae, ila nahic hajajua kwanini namkwepa, ila in general shangazi yangu tangu nimfahamu amekuwa ni mtu mkarimu Sana kwangu.
Huyu shangazi yangu Huwa anasema baadhi ya ndugu Zake wengine hawapokeagi simu zake, nahisi ni kwasababu ya hii tabia yake ya kuuliza maswali.
Labda mm ndio nina tatizo, Wenye uzoefu naombeni mnipe mawazo yenu kwenye hili, ili kama nina makosa nijirekebishe
Kila mwezi atanipigia simu, hili la kunipigia simu sina shida nalo, Maana hata mm huwa nampigiaga simu.
TATIZO LINAPOANZIA:
Kila nikiongea naye kwenye simu, ananiuliza maswali ambayo mara nyingi mm binafsi sipo huru (comfortable) Kuyajibu daaah..
1)Kila akinipigia simu lazima aniulize nipo wapi, nikikwepesha kumjibu atanisisitiza mpaka nimwambie niko wapi..
2)Nikimwambia napigaa mishe za kilimo, simu zitakazofuata ataniuliza mara nne nne kilimo kiliendaje.
3)Muda mwingine ananiuliza kama biashara nilizofungua bado zipo
4)Kila akinipigia ananiuliza kazi nlizo-apply zimeendaje
Kutokana na hayo maswali hapo juu, yani nimeanza kujitenga naye kimya kimya mpaka yeye Kuna siku aliniuliza mbona najitenga nae, ila nahic hajajua kwanini namkwepa, ila in general shangazi yangu tangu nimfahamu amekuwa ni mtu mkarimu Sana kwangu.
Huyu shangazi yangu Huwa anasema baadhi ya ndugu Zake wengine hawapokeagi simu zake, nahisi ni kwasababu ya hii tabia yake ya kuuliza maswali.
Labda mm ndio nina tatizo, Wenye uzoefu naombeni mnipe mawazo yenu kwenye hili, ili kama nina makosa nijirekebishe