Ni ndugu yangu mtu mzima, namwita shangazi, sijawahi gombana nae, na binafsi namwona ni mtu mwema kwangu, na nimefahamiana naye toka utoto wangu hadi utu uzima huu, kipindi cha likizo nlikuwa nashinda kwake miezi mingi kabla ya kwenda home, ila kipindi cha hivi karibuni amekua na tabia ambazo zimefanya roho yangu ianze kumkataa.
Kila mwezi atanipigia simu, hili la kunipigia simu sina shida nalo, Maana hata mm huwa nampigiaga simu.
TATIZO LINAPOANZIA:
Kila nikiongea naye kwenye simu, ananiuliza maswali ambayo mara nyingi mm binafsi sipo huru (comfortable) Kuyajibu daaah..
1)Kila akinipigia simu lazima aniulize nipo wapi, nikikwepesha kumjibu atanisisitiza mpaka nimwambie niko wapi..
2)Nikimwambia napigaa mishe za kilimo, simu zitakazofuata ataniuliza mara nne nne kilimo kiliendaje.
3)Muda mwingine ananiuliza kama biashara nilizofungua bado zipo
4)Kila akinipigia ananiuliza kazi nlizo-apply zimeendaje
Kutokana na hayo maswali hapo juu, yani nimeanza kujitenga naye kimya kimya mpaka yeye Kuna siku aliniuliza mbona najitenga nae, ila nahic hajajua kwanini namkwepa, ila in general shangazi yangu tangu nimfahamu amekuwa ni mtu mkarimu Sana kwangu.
Huyu shangazi yangu Huwa anasema baadhi ya ndugu Zake wengine hawapokeagi simu zake, nahisi ni kwasababu ya hii tabia yake ya kuuliza maswali.
Labda mm ndio nina tatizo, Wenye uzoefu naombeni mnipe mawazo yenu kwenye hili, ili kama nina makosa nijirekebishe
Naomba nikujali
Shauri yake..Wengi walioonekana ni wema kwetu, walituliza, anyway Mwamini Mungu tu mkuu
Si ndio hapo sasa, siwapendi watu wa tabia hiiWengine wanakuuliza tu hata msaada hawakupi
Mkuu umesema kitu cha ukweliKila kitu lazima kuwa na KIASI na binadamu yeyote mwenye kutaka kufika mbali lazima ajifunze kutunza SIRI na Kuheshimu sauti ya ndani.
Yaani kama kuna mambo nafsi yako inasita kuzungumza kwa mtu fulani, acha usizungumze.
Tofauti na hayo mtu mzima anayetafuta siyo busara kuhoji kila hatua anayopitia katika maisha yake binafsi na ya utafutaji kiujumla.
Mkuu huna tatizo ila sauti yako ya ndani ndiyo unayotakiwa kuisikiliza.
Unapotamka malengo yako yote kwa mtu unakuwa kama upo uchi na hata hamasa ya kupambania lile lengo inashuka.
ni kweli kaka lakini kwanini tuwe na hofu na kila mja, hivi ni kweliKila kitu lazima kuwa na KIASI na binadamu yeyote mwenye kutaka kufika mbali lazima ajifunze kutunza SIRI na Kuheshimu sauti ya ndani.
Yaani kama kuna mambo nafsi yako inasita kuzungumza kwa mtu fulani, acha usizungumze.
Tofauti na hayo mtu mzima anayetafuta siyo busara kuhoji kila hatua anayopitia katika maisha yake binafsi na ya utafutaji kiujumla.
Mkuu huna tatizo ila sauti yako ya ndani ndiyo unayotakiwa kuisikiliza.
Unapotamka malengo yako yote kwa mtu unakuwa kama upo uchi na hata hamasa ya kupambania lile lengo inashuka.
Una point ya msingi kiukweli, ila elewa tu katika maisha ya kawaida na maisha ya utafutaji kuna namna unatakiwa kuishi na watu unakutana nao na wale unaowaamini kwa kuwaita ndugu.ni kweli kaka lakini kwanini tuwe na hofu na kila mja, hivi ni kweli
kila hatima zetu zipo mikononi mwa watu wabaya
mm nimekuwa mtu muwazi sana kwenye maisha yangu sijafanikiwa bado ila pia bado sijaona changamoto za hawa wapumbavu katika maisha yangu, Nina dada yangu naye msimamo wake ni huo kiasi kwamba mpaka kujua anafanya nini kwa sasa ni vigumu mno.Una point ya msingi kiukweli, ila elewa tu katika maisha ya kawaida na maisha ya utafutaji kuna namna unatakiwa kuishi na watu unakutana nao na wale unaowaamini kwa kuwaita ndugu.
Usiwe na Hofu na mtu yeyote ila jifunze kuwa MAKINI na kila mmoja unayekutana naye au kuishi naye.
Zaidi ya yote ishi maisha ya kujiwekea mipaka na ukiasi katika kufanya na kuongea pia mambo yanayogusa maisha yako moja kwa moja.
Adui wa kweli ni mjanja sana kuliko unavyofikiri na wakati mwingine anaweza kuwa yule unayemwamini sana kupita kiasi.
Point ya msingi : Adui wa kweli ni mjanja sana.
Kuna mambo mengine maisha yanakufundisha muda unapofika.mm nimekuwa mtu muwazi sana kwenye maisha yangu sijafanikiwa bado ila pia bado sijaona changamoto za hawa wapumbavu katika maisha yangu, Nina dada yangu naye msimamo wake ni huo kiasi kwamba mpaka kujua anafanya nini kwa sasa ni vigumu mno.
Hapa kuna cha kujifunza. Hivi watu damu zikiendana unakuta wanaelewana sana?Huenda damu yako na yake zinaendana so usichukilie vingine na hongera kwakukujari