Ridhiwani kaenda Ukerewe?

Ridhiwani kaenda Ukerewe?

Mwanakijiji amepoteza dira kabisa sasa kama amefuata Mkuyati au kumvuta aliye mbali sisi inatuhusu nini?

Kwa kweli hii inaonesha demise ya JF, yaani hata hao wachache akina Mwanakijiji wameanza kuandika hizi pumba..tume finish.
 
Last edited by a moderator:
Kumbukumbu zako zitakuwa zinakudanganya sana. Utawala wa Hitler ndo aliopelekea vita kuu ya pili ya dunia ambayo ilimalizaika mwaka 1945 na Ujerumani kupoteza makoloni yake yote ikiwemo Tanganyika ambayo ilikaliwa na Mwingereza.
wajerumani waliondoka baada ya vitaya kwanza ya dunia 1918 kipindi hicho Hitler alikuwa jeshini .....
 
Mwanakijiji ni mbea mkubwa aliwahi kuja na thread yake ya eti wana picha za mzee kikwete akibanjua amri ya sita na shori mmoja majuu yeye na shogake Mwafrika wa kike.....walibanwa mbavu picha hazikutoka na thread ikafungwa na shigake Invisible baada ya kuona hali mbaya kwa shogake......

natabiri....mwanakijiji akibanwa sana hii thread itafungwa au kuwa hiden isionekane alafu huu umbea utakufa kimya kimya.......
Tabia za kinafiki na kimbea mbea ni kawaida na mwanakijiji hasa akiona populality yake inaanza kupungua akishirikiana na shogake Invisible......hakuna hot doc siku hizi wewe unafikiria umaarufu wa Invisible na mwanakijiji utakujaje nowadays?

Thread ya kidaku
 
Ana maana yake....huyu jamaa huwa hakurupuki.

wakerewe wanasifika sana kwa matibabu ya wanaume wasiokuwa na nguvu za kiume,ila sidhani kama mzee mwanakijiji anamaanisha hivyo. Mwacheni huyo dogo atembelee sehemu zenye historia kama huko Ukerewe a.k.a UK
 
Kumbukumbu zako zitakuwa zinakudanganya sana. Utawala wa Hitler ndo aliopelekea vita kuu ya pili ya dunia ambayo ilimalizaika mwaka 1945 na Ujerumani kupoteza makoloni yake yote ikiwemo Tanganyika ambayo ilikaliwa na Mwingereza.
Ujerumani alipoteza makoloni yake baada ya vita vya kwanza vya dunia mwaka 1918,Hitler aliingia madakani 1933 na kudhamiria kurudisha makoloni ya Ujerumani hivyo kuanzisha WW2 kwa lengo hilo,Hivyo Morinyo yuko sahihi mkuu!
 
Mashehe wote na wachawi anaowatumia kumrogea sijui kumrogesha huko bagamoyo hawatoshi ama wamedunda? Sasa ukara laba kaende kwenye mashetani yaliyoko kwibutuke!
Mkuu mashehe wanaroga kwani?
 
Watanzania wanajua kinachoendelea; usidhani hawajui. Nimedokeza kidogo tu na watu wameanza kufunguka so the bottom line ni kuwa inawezekana kweli kuna hazina ilifichwa wakati wa Mjerumani?


Hii ni hekaya nyingine ya kusadikika. Hazina hii imepatikana wapi? Nani amewahi kuipata? It is just an imaginary treasure.

Hii ni twist tu ya idea kuwa dogo ameenda kupata rupia ya mjerumani au hiyo hazina ili ahalalishe (justify) uporaji alioufanya.

HATUDANGANYIKI
 
Ujerumani alipoteza makoloni yake baada ya vita vya kwanza vya dunia mwaka 1918,Hitler aliingia madakani 1933 na kudhamiria kurudisha makoloni ya Ujerumani hivyo kuanzisha WW2 kwa lengo hilo,Hivyo Morinyo yuko sahihi mkuu!

Asante mkuu.
 
Ujerumani alipoteza makoloni yake baada ya vita vya kwanza vya dunia mwaka 1918,Hitler aliingia madakani 1933 na kudhamiria kurudisha makoloni ya Ujerumani hivyo kuanzisha WW2 kwa lengo hilo,Hivyo Morinyo yuko sahihi mkuu!

Well, zoezi zima la kuingia Hitler na Nazi ktk utawala lilikuwa likionekana mapema sana na kuleta hofu sana Ulaya.Si vyema sana kumfanya Hitler ni central issue,kwani uncertainty ya siasa za Ujerumani na usalama wa mali za mabepari wa kijerumani chini siasa za Nazi ilionekana wazi.Kabla hata Hitler hajaingia.Sidhani kama kuna mtu atapata shida predict baadhi ya mambo kwa uhakika kabisa Iwapo ushabiki/propaganda unaonekana kulalia upande wa CUF na hivyo kuongeza uwezekano wa kuchaguliwa.Nazi ndani ya ujerumani waliishi kama wageni waliokuja tawala wenyeji, kuna wajerumani wengin tuu walionja joto ya jiwe na walihitaji ukimbizi.Mojawapo ya watu Hitler aliwapania ni matajiri.


Wajerumani hawakuwa na time ya kuhamisha vitu kwa pleasure, pia hawakua na ulinzi tena wa kuweza jiaminisha safirisha maliza dhamani kupeleka ujerumani ambapo nako siasa hazikuwa zikiaminika.


Pia Ujerumani walipaswa weka mipango na siri muhimu na markings zao ili kusaidia vizazi vyao vya baadaye kuendeleza yale yaliyoanzishwa na wazee wao.

kwa wengi wanaweza wasione ugumu wa maisha na wasiwasi wa nchi za ulaya kipindi hiki hadi pale mtakapokuja sikia habari ya UK, walipoamua kukusanya zao documents za siri zote ktk meli moja, kw ajili ya kuzipeleka US.Waingereza walishakata tamaa kabisa wakasema kama wataangamia basi kuliko German wachukue ni bora taifa rafiki kam US wachukue na kuzitumia.Suez canal ilikuwa katika hatihati miaka kibao kutekwa na mataifa mengi sana ili kujihakikishia usalama wa mali ghafi na silaha.

Bado kuna mengi sana ya kujifunza kuhusu mienendo ya wajerumani, na mipango yao ya miaka mingi.Cha kushangaza pamoja na kuwepo kwa hizi tetesi na hata watu kufanya majaribio ya kuvunja structures za zege za wajerumani bado serikali yetu na wasomi hewa hawajafanya mengi kufanya tafiri.
 
Kumbukumbu zangu zinaonyesha kua, Hitler aliingia madarakani wakati wajerumani wameshatoka Tanganyika. Kama ni kweli yalifanyika, basi yalifanyika kabla yake.

Siasa za Nazi zilikuwa zinajulikana na kuinuka kwa Hitler kulikuwa kukiangaliwa sana kwa makini na wazungu wa ulaya pamoja US.Mataifa mengi yalikuwa yakikusanya silaha kwa bidii sana ,ingawa kasi ya wajerumani kukusanya ilikuwa kubwa zaidi.

Nazi hawakuibuka tuu walifanya propaganda na kufanikiwa ingiwa, ni kama leo malema aibuke ndani ya ANC na aanze kusanya watu na kuongeza ushawishi wa kuchukua nchi,wazungu watakuwa wanajua wazi nini kinafuatia.Au leo CUF upepo uanze wagukia kuelekea 2015, wapo watu watakuw awakijandaa ondoka nchini.Wajerumaniw alikuwa wakiona hali inapokwenda, na tishio lililokwepo.
 
Kwa kuwa nimesoma historia ya vita mbili maarufu za dunia, nakubaliana kwa kiasi kikubwa na maelezo hayo hapo juu. Baada ya kumalizika vita ya pili ya dunia mnamo mwaka 1918, mkutano mkubwa wa upatanishi ulifanyika kule Versailles Ufaransa. Katika kutafuta chanzo cha vita, ikaonekana Ujerumani walikuwa ni chanzo cha vita. Hata hivyo Wajerumani, kwa wakati huo walikuwa na nguvu na utajiri mkubwa sana, na uwezo wa silaha pia. Sasa basi, ili kuwapunguza nguvu, wakapokonywa makoloni yao Afrika, ambayo yalikuwa chanzo cha nguvu zao za kiuchumi. Wakalazimika pia kulipa faini kubwa ya pauni milioni tano za Uingereza. Makoloni hayo waliyopokonywa ni Tanganyika (German East Afrika Co. - zikiwemo Rwanda na Burundi), Togo na Namibia (kwenye madini mengi). Kwa kuwa Wajerumani hawakuweza kunusa kwamba wangepokonywa makoloni baada ya usuluhishi kule Ufaransa, hawakubeba chochote cha thamani toka kwenye makoloni yao, kwa kujua kwamba wangerudi tena kuendelea na shughuli za maendeleo baada ya vita.
Kwa mantiki hii, uvumi wa kwamba waliacha mali nyingi inawezekana ikawa na ukweli mkubwa kwa kuwa waliwekeza sana katika makoloni yao (ikiwemo reli ya Mwakyembe) na majengo maarufu kama Ikulu. Kwa hiyo inawezekana ni kweli kwamba kuna mahali pamechimbiwa dhababu na vito vingine, na himzi habari zipo almost mikoa yota ya Tanzania. Kule kwa akina Bujibuji na PakaJimmy, Njowepo, masopakyindi wanaamini kwamba yule Mmisionari Lehner amekuja kuchukua utajiri wa mababu zake ulioachwa miaka hiyo. Imani hii ipo mapaka leo.
Nawasilisha
Mkuu nakubaliana na wewe kwa kuwa hili suala si tu historical lakini vile vile academic.
Ila nisingependa unichanganye katika mada na jamaa mmoja ambaye basically ni uncouth and uncivilised, na si yeyote kati ya uliowataja hapo juu.

Si wengi wanafahamu historia ya Lehner wa Mbeya, lakini ukifuatilia kumbukumbu wazazi wake walikuwa wammissionari wa sehemu hizo na vitega uchumi vyake vipo sehemu zinazo aminika kuwa kuna utajiri wa madini(inaaminika hospitali aliyojenga Mbalizi iko sehemu ambayo kuna veins za dhahabu)

Wazazi wangu walifanya kazi sehemu hizo, hasa Utengule Mission, Mbeya ambako Mission hiyo inaaminika kuwa katika sehemu yenye dhahabu.

Hizo ni tetesi zinaweza kuwa kweli au uongo.
 
Vibahasha aka wachumia tumbo team rejeo ndio alichukua nafasi ya nepe nini? Hahaha I love the pic



Hawa jamaa si walikuwa na mkutano
attachment.php
 
hii familia ni janga kwa taifa letu kama kweli alienda inasikitisha kutakuwa na kitu alifuatilia huko labda baba yake alimtuma maana ni familia ya matapeli si mama, baba hata watoto
 
Kama JF ingekuwa ni mkutano wa live ktk chumba kuna wengine tungekuwa tumeuwawa.Na types za akina Ritz,ambao wakisikia kitu kischosupport waliyoyazoea basi hukurupuka na natusi,sijui wangefanyaje kama wangekuwa wanaweza wafikia watu ambao wanaongea wasichopenda.Kweli inernete ni balaa na hofu kwa wababe .
 
Eeeeeeeeeehee life is full of surprise!!!

Haya mambo MMK kwa tabia yetu watanzania yanaonekana ya kipuuzi sana,lakini kwa hao anayoyaona ni ya kipuuzi basi ufahamu wao ni mdogo sana.Yaweza kuwa jambo hili ni tetesi lakin pia tetesi hizo zikawa ndio au hapana.

Binafsi najua hizi simulizi,ambazo binafsi nimeshakutanazo nikiwa na miaka kumin na nne, lakini si ukelewe, ila ninapo unga dot najalibu kuimagine kuwaona gold and treasurer hunters wakimfuata mtoto wa Mkuu wa Nchi nakumlisha maneno matamu,kisha nae katika umri huo ambao yeye binafsi alipaswa kupima kuyatenda ama kuyatenda.Kwa kuwa kwa yeye kuyatenda na ikafahamika kuwa alishiriki kwenye hisia hizo basi hato angaliwa yeye kama Riz bali ataangaliwa yeye kama Mtoto wa Rais aliyeko Madarakani.

Na kwa picha hiyo na kwa tendo hilo,hisia hizo ambazo, upelekwa kwenye tresuary hiyo ni utajiri mkubwa usio na matumizi ya nguvu, bali matumizi ya imani [Spirtul] zaidi, kwa hazina ambayo yasemekana kuwa ipo [Binafsi sikulazimishi mchangiaji kuamini lakini mimi naamini uwepo wa vitu vya aina hiyo kwani si muda mlefu uliopita dunia ililipuka kwa taarifa ya kupatikana kwa New World Tresure kutoka Spanish Colonial coins hivyo haya mambo yapo].

Binafsi nilifikwa na incident nikiwa mdogo miaka kumi na nne, watu wazima wakatamanishwa habari hizo kuwa ikipatikanika rupia ya zamani, ambayo mimi binafsi sijawai iona,basi watu wazima wale watakuwa matajiri.Basi watu wazima wale ikimuhusisha mama mmoja mkubwa wa familia yangu wakakumbushana kuwa wakiwa wadogo kijijini kwao walipata kuiona fedha ya namna hiyo kwa baba yao aliyepigana vita vya wajerumani. Watu wazima wakathibitishiana kuwa wanajua alipokuwa anaiweka karibu na kiko chake kipendwa kwenye moja ya nyumba aliyokuwa anapenda kuvutia.Kwa wengi wetu mnatambua nyumba nyingi za vijiji vyetu ni za udongo.Babu yangu huyo alikufa mwaka 1974, mimi nimekuja kubebwa kwenda tukio husika kuchukua mzigo nikiwa na mika kumi na nne 14 mwaka 1989.Da uwezi amini waliokuwa wametoka kijijini mwa babu yangu na kuthibitisha kuwa nyumba aliyokuwa anatumia babu yangu huyo kumpumzika na kuvuta kiko chake, walithibitisha kuwa Nyumba hiyo hipo, na wa kuweza kuichukua ni mtu kama mimi.

Basi wakubwa wale wakanibeba mzega mzega ukizingatia utoto unafuata wakubwa wanachokutuma, mimi binafsi nakumbuka raha yangu kubwa ni kusafiri kwamba kuwa naenda rikizo nje ya nyumbani, tena kijijini ambako nina nasaba nako,raha ya utoto kuwa nikiludi nyumbani nina jipya la kuhadithia huko story za matembezi yangu hayo!!.Kwa nilichokishuhudia kwa umri wangu ule wa miaka 14, ile siku tunafika kijinini nakumbuka tuliingia usiku, asubuhi napelekwa eneo la tukio natamalaki kuona wakubwa wanashangaa nyumba yote iko chini na vifaa vyote vilivyokuwemo watu walishasawazisha baada ya mvua kali iliyokuwa imemwagika siku mbili zilizopita kuidodonsha nyumba iliyoacha na babu kama sehemu yake ya kupumzikia toka mwaka 1974 sijazaliwa mpaka natayarishwa kuwa nitasafiri kwenda kijijini Nyumba ilikuwepo, ila kwa siku tatu za kusafiri toka nilikokuwa mpaka kufika kijijini zingatia usafiri wa miaka ile nyumba hiyo ilidondoka na Rupia sikuiona, wala kiko chake,ila kwangu sikuwa na habari zaidi ya kuwaza furaha yangu kuwa niko likizo kijijini.

Kwa watu wazima ilikuwa imekula kwao na ndoto za utajiri zikawa ndio,zimeyeyuka na waliingia hasara ikiwemo wao kusafiri,ila labda ilikuwa wanipeleke mimi kwenda kuona nyumba ya babu yangu, namuita rafiki ambae sikupata kumuona ikidondoka.

MMK nimeadithia haya kwako ili kuunganisha dot,kuwa kama tukio hili ni kweli basi Ritz nae kwa kujua ndiye mtoto ambae kwa sasa Baba yake anazamana ya kusimamia mali ya Watanzania ,hivyo kushirikishwa yeye, ama kwa kujua ukilinganisha na umri wake kuwa mtu mzima, au kwa kutokujua maisha ya kisasa zaidi, basi matamanio ya kuibuka na hazina [Treasure] isiyokuwa na matumizi ya nguvu basi.

Haya mambo mwanakijiji yapo,ila binafsi yanawafikia na kuwatokea wale ambao hawana kabisa kusudio la UTAJIRI kama SIFA, bali wapate hazina hiyo itumike kwa lengo kusudio la MANUFAA YA JAMII.Na ndio maana wale ambao wanazitaka kwa kusudio la SIFA uishi kuaambiwa masharti kibao,ikiwemo yale yenye harufu ya tishio la uhai wa binadamu mwenzie.

Na kwa ujumla mambo hayo bila nafasi za wazee wa Jadi, simaanishi waganga wa kienyeji, nazungumzia wale ambao wanadhamana za kijadi za eneo husika wao ndio kuanzisha mada kwa mujibu wa initution zao ,na si mtu nje ya eneo husika kuja kuanzisha mada kuwa wanataka kitu fulani na kweli wakafanikiwa.Na waha wajerumani kweli waliacha mark nyingi sana za hazina walizokwapua toka kwenye ardhi za mababu na kwa kuwa ardhi za mababu hazikutaka waondoke nazo waliishia kuondoka patupu wakiwa na ramani za Milima , miti mikubwa, mito na vijito, mawe n.k kama ishara ya hazina hizo.

Yawezakuwa alirubuniwa kutumika au la ni rumors za mijini!!! Yapo na yanatokea.
 
Well, zoezi zima la kuingia Hitler na Nazi ktk utawala lilikuwa likionekana mapema sana na kuleta hofu sana Ulaya.Si vyema sana kumfanya Hitler ni central issue,kwani uncertainty ya siasa za Ujerumani na usalama wa mali za mabepari wa kijerumani chini siasa za Nazi ilionekana wazi.Kabla hata Hitler hajaingia.Sidhani kama kuna mtu atapata shida predict baadhi ya mambo kwa uhakika kabisa Iwapo ushabiki/propaganda unaonekana kulalia upande wa CUF na hivyo kuongeza uwezekano wa kuchaguliwa.Nazi ndani ya ujerumani waliishi kama wageni waliokuja tawala wenyeji, kuna wajerumani wengin tuu walionja joto ya jiwe na walihitaji ukimbizi.Mojawapo ya watu Hitler aliwapania ni matajiri.


Wajerumani hawakuwa na time ya kuhamisha vitu kwa pleasure, pia hawakua na ulinzi tena wa kuweza jiaminisha safirisha maliza dhamani kupeleka ujerumani ambapo nako siasa hazikuwa zikiaminika.


Pia Ujerumani walipaswa weka mipango na siri muhimu na markings zao ili kusaidia vizazi vyao vya baadaye kuendeleza yale yaliyoanzishwa na wazee wao.

kwa wengi wanaweza wasione ugumu wa maisha na wasiwasi wa nchi za ulaya kipindi hiki hadi pale mtakapokuja sikia habari ya UK, walipoamua kukusanya zao documents za siri zote ktk meli moja, kw ajili ya kuzipeleka US.Waingereza walishakata tamaa kabisa wakasema kama wataangamia basi kuliko German wachukue ni bora taifa rafiki kam US wachukue na kuzitumia.Suez canal ilikuwa katika hatihati miaka kibao kutekwa na mataifa mengi sana ili kujihakikishia usalama wa mali ghafi na silaha.

Bado kuna mengi sana ya kujifunza kuhusu mienendo ya wajerumani, na mipango yao ya miaka mingi.Cha kushangaza pamoja na kuwepo kwa hizi tetesi na hata watu kufanya majaribio ya kuvunja structures za zege za wajerumani bado serikali yetu na wasomi hewa hawajafanya mengi kufanya tafiri.

Nicholas naomba urafiki nawe wa kupewa habari za kihistoria mkuu. Waweza kunipatia majina ya documents au documentaries ambazo Wajerumani zinazohusia na matukio haya. Nitashukuru sana mkubwa.
 
Nicholas naomba urafiki nawe wa kupewa habari za kihistoria mkuu. Waweza kunipatia majina ya documents au documentaries ambazo Wajerumani zinazohusia na matukio haya. Nitashukuru sana mkubwa.

wajerumani hawaku document,chochote kwa kusudio la kuweka pubic haya mambo.Wameweka mambo mengine ya Kanisa, historia fulani fulani,walichoona wajerumani wa mwanzo nani walikuwa E.A na ayo yapo ktk machapisho library ya mlimani.Ukisoa historia ya Ukristu sehemu mbali mabli Tanzania, ukisoma explorer wa kijerumani, ukiishi na wajerumani wanaokuja Africa, ukitembelea makazi yaliyokuwa na ngome za wajerumani, ukiongea na wazee walioishi na mjerumani au kusikia habari za mjerumani.Kisha uunganishe dot.Document nyingine ni siri kama ilivyo kwa madini, na vitu vingine,tena hiz docuement ndio zimehifadhiwa kwa umakini sana na ndio core ya kila kitu.Dhahabu, alamsi na vingine havikuwa vingi kiasi cha kushindwa bebwa na meli,ila hizo document ambazo zina map vitu muhimu kwa wajerumani ktk hii nchi, vinvyomap profiling ya raia wa hii nchi, tafiti walizofanya, na malengo ya mwanzo kabisa ktk hii nchi,hizo hata wao hawakuwa salama kuzibeba na kupita nazo ktk bahari iliyokuwa si salama.

Mimi binafsi nimeishi maeneo yenye masalia ya wajerumani, nimeziona hizo hela zinazowapagaisha watu, nimeona ujenzi wa kuchekesha sana ktk site zao, na nimejaribu tembelea restaurant chache zilizokuwa makao ya wajerumani ktk eneo husika.niemongea nao,hasa wanafunzi wanaosoma journalism, history na culture, ni watu wanaotaka sana mtu ukiongea nao uwe na umakini uwe, unakumbuka, uwe unaweza chelewa waaonyesh aunajua,ili wasiwe wanagalifu sana na kukukwepa.Wanapenda sana kuulizi vitu kwa mzaha,na next day watakuwambia walishfika pale.hawapendi sana uongelea historia yao ktk baadhi ya maeneo kwa vile wameshaambiwa inasomeka vibaya kwa watu wa africa hasa linapokuja suala la unyongaji na site zilizopo walizokuwa wakitumia kunyogea.

Kwa ujumla nimechunga mbuzi juu chamber nyingi tuu zenye masalia ya wajerumani, mengine yalikuwa yamebomolewa na wakware.ila mengine yalikuwa na masalia ya risasi, ambayo tulitengenezea vichupa vya kulipulia baruti za viberiti (huwa tulivitengeneza kwa kuweka ktk mpini wa mbao kama bunduki, halafu na msumari unawekewa mpira au sping ya kufyatua na hivyo msumari kugonga baruti kama kinyundo)kwa siku za mwaka mpya na shrehe nyingine.Ila kwa vile haikuwa ni utafiki na umri ulikuwa mdogo zikuweza komaa na mambo sana.

Niliwahi shuhudia kifo cha mbibi aliyekuwa kiishi mwenyewe ,baada ya kuuwawa na hawa treasure hunters,wakachukua na viungo vyake ili kuweka matambiko.Bado hawakufanikiwa sana.Kwa mtu makini ukiwasikiliza wazee wanapoongea utapata clue.Wajerumani walikuwa wakiwaua watu wanaokwenda nao kuficha vitu vyao, waliwafukio hukohuko.Watu walitafsiri kuwa jamaa wanawazika ili wawe mizimu wa kulinda hayo maficho,hii story ilinunulika kwa vile hata machifu wetu nao huwa walizika watu hai na watu wa kichifu ili wakapate walinzi na vibarua.Ila ukweli ni kwamba waliwaua ili siri ipotee na si vinginevyo.Kw ajinis nilivyoona ni kwamba hawa jamaa walificha vitu kwa patterns tofauti sana.

Wazee wengi wanasema kila wakichimba huwa wanakuta mashimo mengine yamejengewa boxi za zege ila ndani patupu, basi wao hutafsiri kwamba mizimu inahamisha kila wakifuata.Hapa panaleta hisi nyingine kuwa hawa jamaa mashimo mengine yanakuwa ni patterns tuu za kuweka alama kama si yaliandaliwa kwa kazi ya baadaye ila hayakutumika tena.Haya ndio maeneo wasomi wetu wanapaswa fanya utafiki mkubwa kabla wazee wengi hawajafa.na pia kujaribu tumia scanners na metal detectors ili kuweza track vitu.Wasome historia ya coins, na metal compositions zao ktk kipindi hicho, ili kuwasiadia sana kujihakikishia kila waendapo.
 
Back
Top Bottom