Ridhiwan anapewa escort; Kwanini?

Ridhiwan anapewa escort; Kwanini?

Kwa sheria za nchi jirani ya Rwanda, watoto na mke wa raisi wanatakiwa kupewa ulinzi mkali ikiwezekana na mitutu. Sema Rwanda hali ni tofauti na TZ kwa ajili ya uhasama tangu 1994.

Hatujui sheria inasemaje kwa first family ya TZ, kwa wanaojua ni ulinzi kiasi gani wanastahili watoto wa raisi aliyeko madarakani watueleze.
 
Binafsi sina tatizo juu ya kupewa escort Riz1. Tatizo ni jinsi gani wanatumia mali ya umma kwa fujo. Fikiria, hata kama ana threats Je, gari moja ya Polisi isingetosha? Hapa si ulaya Bwana! Atumie mali ya watanzania kwa kiasi, hapo tutamwona kidogo mstaarabu.
Mtoa mada ameona jumla ya gari 5 zikimpeleka riz1 uwanja wa ndege! hebu fikiria jamani... Kweli tunamwonea wivu?

Riz1, ungetuliza mapepe kwani sisi si wapiga kura wako. Shuka huko ulipo matawini!

Mkuu Ulaya nina uhakika hawana huo ujinga, nilishuhudia mwenyewe kwa macho yangu raisi wa sasa wa ujerumani akitoka Bellevue (ikulu yake) na gari moja tu na piki piki. Tena hamna mbwe mbwe kama za Kikwete hadi ambulance ya knight support inamsindikiza na kusababisha foleni Dar. This is wastage of resources.
 
Members of the 1st family deserve state-sponsored personal security during the tenure of their parent/president. Ask Jenna & Barbara Bush or Chelsea Clinton, and they will explain this argument to you.
 
Wakati wa kampeni, baba alimtuma mwana ...sasa baba anamlipa mwana kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kuksanya wadhamini...
Ubia wa Urais! Ingawaje mkulu alisema urais wake hauna ubia.
Baba Rais, watoto wanapewa ulinzi kwa usalama wao...hayo hufanywa katika nchi za wenzetu sijui sisi huwa tuna mfumo upi.
Nakubaliana na wewe!Kwasababu kabla ya uchaguzi wengi walisema kampeni ilikuwa ni ya kifamilia zaidi kuliko ya kichama.Hata hivyo wameshinda,ina maana hata kama ingekuwa ni Ridhwani mwenyewe kwenye uchaguzi wa rais angeshinda pia,so naona ni baba anarudisha shukrani.Kwa wengine mnaoshangaa,ndo bongo yenu hiyo, mtafanyaje?
 
Ridhwan kavunja kipengere kipi cha katiba au sheria? Tusiendeshe nchi bila kufuata sheria kamwe hatutaweza kuwa viongozi bora wa baadaye.

Ridhwan hajavunja kipengele chochote lakini aliyeidhinisha hayo magari kavunja!

 
kwa kuwa hatuoni Ridhwan akipewa escort wakati wote inawezeka siku hiyo ilikuwa inahitaji escort ili aweze kwenda na muda. Ni viongozi wangapi wanatumia magari ya umma kwa kubebea nyasi, na kupeleka watoto shule na kwingineko? Ajabu ni nini kwa hili?

Makosa lazima yasemwe mkuu!
 
Members of the 1st family deserve state-sponsored personal security during the tenure of their parent/president. Ask Jenna & Barbara Bush or Chelsea Clinton, and they will explain this argument to you.

You must be crazy You want to compare Riz1 with Chelsea?
 
Kuna habari kuwa kuna family business ya madawa ya kulevya na yeye ndio dealer mkuu
 
sasa jamani mlitaka apande dcm la gongo la mboto?
this is so funny, but a poignant point. Lakini angeweza kupanda dcm la gongo la Mboto, kina Makongoro walikuwa wanatembea mguu kwenda na kurudi shule Upanga-Msasani. Ndio maana mpaka kesho baba yao anaheshimika na Watanzania kama vile mtume wa Mwenyezi Mungu.

Kama mtoto wa Kikwete hana hadhi ya kupanda gobole la Gongo la Mboto, sawa, apande hata msururu wa helikopta kumpeleka airport, mradi uwe usafiri wake binafsi, sio akamue hela yetu mbuzi ya walipa kodi.
 
Members of the 1st family deserve state-sponsored personal security during the tenure of their parent/president. Ask Jenna & Barbara Bush or Chelsea Clinton, and they will explain this argument to you.

Hatuzungumzii usalama wao....hakika huo unahitajika....tunaongelea hili '' Re: Ridhiwan anapewa escort; Kwanini?'' yaani kwa nini mtoto wa Rais awe namsafara (sio ulinzi)
 
sioo sisi tuliomchagua yeye! maisha yanakwenda wakulu yana mwisho haya.
 
Katika mambo mengine huwa nilitofautiana na Mwl. Nyerere lakini kama kuna jambo ambalo nilimpa heshima basi ni jinsi alivyoiweka familia yake muda wote wa utawala wake. Mama na watoto waliweza kutambua, kukubali na kutenga taasisi ya Urais aliyoitumikia Nyerere na mambo yao binafsi.

Ndio maana leo (kwa tarifa nilizo latest ni za mwaka 2004) hakuna mtoto wa Mwl. aliye na madudu dizaini ya Riziwani nk. Sijasikia kapewa Waziri au nani katika wa mojawapo ya matawi ya ccm. Lakini Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete kwa eneo hili nadhani hakuna mwenye kumkaribia Nyerere.

Lazima kuwepo na mipaka katika hili. WaTz wanahitaji Katiba Mpya haraka.....lakini pamoja nayo lazima nchi iwe na mfumo wa elimu utoe watu wenye maadili na uwezo wa akili wa kuongoza nchi.
 
Mtoto wa raisi is a prince, au mtoto wa bosi ni bosi hamjui hilo? ana haki zote, LOL labda alikuwa amechelewa ndege so ikabidi awahi.
 
Nijuavyo mimi watoto wa marais wengi tu duniani(wanaounda first family) hupewa ulinzi na ama polisi,jeshi,secret service ama chombo chochote kinachosimamia usalama wa viongozi kwa nchi husika(ikiwa ni pamoja na kuwa na motorcade yenye escort ya walinzi) so Ridhwan kama mmojawapo wa watoto wanaounda first family ulinzi ni stahili yake...

Duniani? Katika nchi za Africa na nchi zenye udikteta jambo hilo hutumika tofauti na katika nchi zilzo na ustawi mzuri wa democrasia. Tofauti ni ufujaji kwa jina la usalama, ulinzi nk.
 
Kwa maadui alionao (Bashe, Masauni, Yanga-anti Nchunga nk nk) kwa nini asipewe ulinzi?....
 
MAWAZO BINAFSI: Ridhwan kwa sasa si miongoni mwa wategemezi wa Rais, yeye ana maisha yake binafsi pamoja na mkewe, moja kwa moja anakuwa sawa na raia mwingine wa Tanzania, si haki kutumia ofisi ya mzazi wake, hata kama atataka kutibiwa inabidi atumie taratibu zake binafsi au za mwajiri wake ambaye si IKULU.
 
Mkuu Ulaya nina uhakika hawana huo ujinga, nilishuhudia mwenyewe kwa macho yangu raisi wa sasa wa ujerumani akitoka Bellevue (ikulu yake) na gari moja tu na piki piki. Tena hamna mbwe mbwe kama za Kikwete hadi ambulance ya knight support inamsindikiza na kusababisha foleni Dar. This is wastage of resources.

Nilikuwa Netherlands mwaka 1998-2000, na waziri mkuu aliitwa Wim Kok. Alikuwa na siku mojawapo kila wiki ambayo alikuwa akienda ofisini kwa baiskeli, kama sehemu ya kampeni yake ya kulinda mazingira na kuhimiza 'a healthy lifestyle'. Wala hakukuwa na hata robo tu ya hizi mbwembwe tunazoona kwa viongozi wetu huku bongo. Maofisa wachache tu walimsindikiza kwa baiskeli tena kwenye cycle lane hiyohiyo wakifuatana nakuchanganyika na raia.
 
Back
Top Bottom