Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 359,899
- 828,507
Nina deni kubwa kwa Valentina na sijui nitalilipaje.. Labda kwa kichanga alichokiacha😭 Mungu nisaidie🙏🏿
Marehemu Valentina ndiye Mwana JF wa kwanza kufanya naye mawasiliano ya simu wayback 2013... Baadae nikawa mmoja wa wana JF aliowashirikisha kwenye fursa mbalimbali za kutafutq pesa na ajira.. Alipenda sana kuwa mbunifu wa fursa za pamoja japo nadhani wengi kama si wachache hawakumuelewa..
Tuliendelea kuwasiliana na akatamani tuonane ana kwa ana.. Lakini kila nilipokuwa na safari za Arusha mambo yangu yakawa mengi hivyo nikakosa kabisa muda wa kuonana naye😪
Mwaka 2021 nikiwa nafanya kazi Kigamboni Kibadq akanijulishq kwamba kwasasa yuko Dar.. Nikamuelekeza nilipo lakini akaniambia kwa situation yake hawezi kutumia usafiri wa jumuiya.. Nikaahidi kumchukulia usafiri wa binafsi ama mimi nimtembelee alipo lakini sikufanikiwa kufanya yote mawili mpaka naondoka Kigamboni🥱
Nadhani harakati na changamoto za maisha zinatunyima nafasi adhimu za upendo na kujali... Tuliendelea kuwasiliana mara moja moja lakini mwishowe mawasiliano yakakatika kabisa mpaka nililokuja kusoma hii taarifa ya kutwaliwa kwake!
Kwa moyo wa dhati naamini nina deni kwake.. Lakini naamini kuna siku nitalilipa. Pumzika kwa amani rafiki mwema😪
Marehemu Valentina ndiye Mwana JF wa kwanza kufanya naye mawasiliano ya simu wayback 2013... Baadae nikawa mmoja wa wana JF aliowashirikisha kwenye fursa mbalimbali za kutafutq pesa na ajira.. Alipenda sana kuwa mbunifu wa fursa za pamoja japo nadhani wengi kama si wachache hawakumuelewa..
Tuliendelea kuwasiliana na akatamani tuonane ana kwa ana.. Lakini kila nilipokuwa na safari za Arusha mambo yangu yakawa mengi hivyo nikakosa kabisa muda wa kuonana naye😪
Mwaka 2021 nikiwa nafanya kazi Kigamboni Kibadq akanijulishq kwamba kwasasa yuko Dar.. Nikamuelekeza nilipo lakini akaniambia kwa situation yake hawezi kutumia usafiri wa jumuiya.. Nikaahidi kumchukulia usafiri wa binafsi ama mimi nimtembelee alipo lakini sikufanikiwa kufanya yote mawili mpaka naondoka Kigamboni🥱
Nadhani harakati na changamoto za maisha zinatunyima nafasi adhimu za upendo na kujali... Tuliendelea kuwasiliana mara moja moja lakini mwishowe mawasiliano yakakatika kabisa mpaka nililokuja kusoma hii taarifa ya kutwaliwa kwake!
Kwa moyo wa dhati naamini nina deni kwake.. Lakini naamini kuna siku nitalilipa. Pumzika kwa amani rafiki mwema😪