Yes,
Katika siku nilizotaabika sana ni leo.
USHUHUDA:
Kwa ufupi, Regia amekuwa rafiki yangu tokea mwaka 2009, JF ikiwa ndiyo chanzo cha kufahamiana.
Ilikuwa kila akija Arusha alitutaarifu, na alisababisha sisi marafiki wa JF tukutanike pamoja naye jioni hiyo na kukaa hadi usiku tukichatt naye kwa furaha na bashasha za aina yeke...tunalikumbuka sana hilo, na ni sababu ya sisi kuomboleza kwa machungu.
Lakini sura ya mwisho akiwa hai nilikuwa Dodoma kiofisi, na yeye alikuwa Bungeni, ilikuwa tarehe 17/11/2011!
Nilimpigia nikimjulisha kuwa nipo Dom, alifurahi sana kusikia, akaniomba tuonane jioni Dodoma Hotel, ambapo katika muda tuliokubaliana nilikuta ameshafika, akiwa na Godbless Lema, na mke wa Lema...
Tuliongea mambo mengi sana, ya kisiasa, kijamii na kirafiki...tukapata kinywaji na mlo pamoja, na baadaye tuliagana pale nje ya hoteli, wao wakaingia kwenye gari iliyokuwa inaendeshwa na Lema,wakatokomea...sijamwona tena hata dakika hii!
Appreciation:
Namshukuru Mungu kuwa niliongea naye, mtu ambaye anapendwa na jamii na kuheshimika sana kwa misimamo yake na moyo usiokata tamaa!
Kwa mtizamo wangu, kazi aliyofanya inatosha kabisa, alistahili kupokewa, na nahisi alikuwa anachoka sana!...Acha apumzike.
Kama hatujaiga na kujifunza toka kwake, basi sisi ni wapumbavu!
RIP REGIA-MAXIMUM RESPECT!