Ni kweli sisi sote ni members, na tuna michango yetu ndani ya JF.
Lakini mchango wa RegiA umetuzidi sana sisi wote kutokana na sababu zifuatazo!
1.Aliweza kufanya majukumu ya kibunge, lakini hapohapo kutumia vyema muda wake kutuhabarisha yanayojiri, akishawishi na kuleta mrejesho wa anachofanya katika eneo-Bunge lake.
2.Jina lake la awali (GenderSensitive), pamoja na kuwa lilikuwa ni anonymous, lilikuwa linampa hadhi fulani, na mimi nilipolisoma kwa mara ya kwanza nilihisi kuwa ni mtu makini!..Lakini hata niliposoma michango yake niligundua kuwa ni mwanaharakati wa juu sana wa ukombozi wa gender ya kike na binadamu kwa ujumla!
3. Kuna wakati alitoa nafasi kwa wasichana hapa JF kuungana naye katika safari za mikoani, huenda alikuwa akizunguka kufanya research fulani(sikuwahi kufahamu alikuwa ana mission gani) lakini hilo tu lilidhihirisha kuwa alikuwa ni mtu aliyejaa fursa kwa wanawake, wasichana na binadamu wenzake wanaomzunguka.
4. Kitendo cha kutushirikisha sisi Jamiiforums kwenye kutoa kero zinazoigusa jamii ya Watanzania(alichokifanya juzi tu hapa jamvini) kilikuwa nicha heshima sana kwetu..ni wazi wa kumponda hawawezi kukosekana, japo alifurajia sana challenges!
Amini usiamini kwa ufahamu wangu hakuna Mbunge ambaye amefanya kitendo cha ujasiri kiasi hicho..inagharimu usafi fulani kuwaconfront Great Thinkers wa JF kuwataka ushauri, ukiwa fisadi utapata majibu In No Time!
KWA HAYA MACHACHE NASHAURI ADMINISTRATION YA JAMIIFORUMS IANGALIE UWEZEKANOWA KUPRINT TSHIRT ZENYE BAADHI YA MANENO NA KAULI ZAKE ALIZOZITOA MAJUKWAANI NA KUZIUZA KWA MEMBERS...NAAMINI HAKUNA ATAKAYEPENDA KUKOSA MEMENTO YA AINA HII.
NAWASILISHA.