Regia Mtema is No More!

Regia Mtema is No More!

Status
Not open for further replies.
habari mbaya sana hizi lakini haitufai kitu kulalama na kulia kwani yashatokea. Yote ni kumshukuru Mungu na kuomba rehema zake kwa ajili yetu sote tulobaki tuongeze uchaji kwake kwani hakuna ajuaye siku wala saa.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa na Jina la Bwana libarikiwe. Apumzike kwa Amani mpendwa wetu mh regia mtema
 
its true bana,MUNGU ampumzishe kwa amani mpiganaji wetu....amen
Habari zilizothibitishwa na JF ni kuwa Regia Mtema (mb) amepata ajali na Kufariki dunia eneo la Ruvu Darajani.

Ndugu wa Karibu wanasema alikuwa kaenda kukagua Kiwanja alichopewa na Wazazi wake na baadae kwenye mkutano wa CHADEMA huko Kibaha.

Habari hizi zimethibitishwa.
 
Ni Kama vile ailona kifo chake kwani tarehe 31 December 2011 aliweka in record mambo yote aliyowafanyia watu wa jimbo lake kwenye jamii forums. check in detail trend yenye ttile "Niliyoyafanya tangu niwe Mbunge-Shukrani kwa WanaJF".
rip Regina
 
.......For a while nimepata mental block. Kwa upeo wetu wanadamu, sometimes ni vigumu sana kumuelewa Mungu! Inatia uchungu usio kifani kuona wale wale wanaojitoa kwa moyo wote pasipo hila kuwasemea wanyonge wa nchi hii ndio wanaoondoka mapema sana. Regia had a vision that we could all see. Aliwafikiria watanzania mno katika maisha yake. Alikuwa si wa watu wa Kilombelo tu, wala wa walemavu tu. Regia alikuwa ni Mbunge wa watanzania wote. Jimbo lake kiukweli lilikuwa ni Tanzania nzima. Kuthibitisha hili soma thread yake aliyokuwa ameanzisha hivi juzijuzi alipoomba yeyote mweye hoja ambayo anadhani inahitaji kusemewa ndani ya Bunge na CDM aiwakilishe kwake.
Nakumbuka siku moja Mchungaji Msigwa Mbunge wa Iringa alisema unapokuwa Mbunge wa CDM unakuwa na kazi mbili. Moja ni kuliwakilisha jimbo lako lakini pili ni kuwawakilisha watanzania wote. Tumeyaona haya kwa Dr Slaa, Mh Mnyika, Mh Mbowe, Mh Tundu Lisu, Mh Zito na wengine wengi. This was also true for our beloved sister Regia Mtema. Japo tuna majonzi sana lakini tukumbuke tumeagizwa na mwenyezi Mungu kuwa tushukuru kwa yote. Yeye ndiye anayejua kwa nini anamchukua huyu na kwa nini anamuacha huyu. RIP our beloved sister Regia Mtema. Na jina la BWANA lihimidiwe.
 
TUNAOMBA MUONGOZO WA INVISIBLE ..INAPOTOKEA MEMBER KAMA HUYU KATUTOKA HASA WALE AMBAO WAMEAMUA KUWA MSTARI WA MBELE KWA KUWEKA MAJINA YAO DHAHIRI.....BASI KWENYE HOME PAGE TUKIFUNGUA TUONE PICHA YAKE KWA SIKU ZITAKAZOKUBALIKA...NA BENDERA YA JF..ambayo ina nembo ya JF ..IONESHWE IKIPEPEA NUSU MLINGOTI..

NAOMBA KUTOA HOJA!!!

mkuu umeniwahi. sioni sababu ya kutofanya hivi...
 
[h=2]Niliyoyafanya tangu niwe Mbunge-Shukrani kwa WanaJF[/h]
Wakuu habari!

Ni matumani yangu kuwa tumejiandaa kumaliza mwaka vizuri na kuplan vizuri for next year.

Tukiwa tunafunga mwaka nimeona niandike kwa kifupi yale niliyoyafanya kwa kipindi Cha mwaka mmoja tangu kuapishwa kuwa Mbunge wa Vitimaalum Nov 12,2010.

Taarifa hii inaonyesha utekelezaji wa Kazi za Ubunge,Kazi za chama Wilayani Kilombero na Kazi za Chama Kitaifa.

A. KAZI ZA KIBUNGE
Tangu nimeapishwa nimefanikiwa kufanya Kazi mbalimbali za Kibunge Wilayani Kilombero,Jimbo ambalo niligombea na kupata Kura 38,550 sawa na asilimia 45 ya kura zote zilizopigwa. utekelezaji wa awamu hii ulikuwa ni QUICK WINS. Quick zifuatazo zimefanyika;
1. Nimepigania bei ya Sukari ishuke -Kuna maeneo Bei imeshuka lakini maeneo mengine hali bado ni mbaya. Kilombero ni Wilaya inayozalisha Sukari, Kiwanda Cha Illovo hivyo bei ya Sukari unapaswa kuwa chini kuliko maeneo yasiyodhalisha Sukari.
2. Nimepigania kituo Cha Polisi Cha Wilaya kiboreshwe-kimeboreshwa
3. Nimepigania kituo Cha afya Cha Mlimba kipatiwe Maji na Ambulance lirudishwe hivi vyote vimefanyika.Ambulance ilikuwa gereji zaidi ya miezi Sita mwaka 2010.
4. Nimepigania utekelezaji wa huduma bure kwa Wajawazito,Watoto chini ya Miaka Mitano,Wazee na Wenye Ulemavu-Kuna maeneo imefanikiwa maeneo mengi bado.
5. Nimetetea haki za Wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari Na KPL-Baadhi ya Kero zimetekelezwa lakini nyingine bado-Suala la Maslahi bado ni tete,suala la Usalama Kazini bado ni tete.
6. Nimetetea na kusimamia kero ya Wakulima na Wafanyabiashara ya kuongezeka kwa Ushuru bila kushirikishwa katika hatua zote muhimu.
7. Nimepigania haki ya Umeme kwa Wananchi wa Kilombero kwani tunavyanzo viwili ya umeme,Kihansi na Kidatu.REA imeenda kule ila inasua sua sana lakini Wizara imetuhakikishia kuwa inatekeleza azma yake ya kupeleka umeme maeneo yote ya karibu na vyanzo vya umeme.
8. Nimepigania barabara ya Kidatu-Ifakara kwa kiwango Cha lami-imeshindikana kwa mwaka wa fedha 2011-2012.
9. Nimesomesha Wanafunzi 86 Sekondari,13 Vyuo Vikuu hawa wa Vyuo Vikuu walihitaji kutoa advance ili waweze kusajiliwa then wapate Mkopo
10. Nimeezeka madarasa mawili(2) ya shule ya Msingi Mkula
11. Nimegharamia Visima viwili vya maji
12. Nimehudumia Baba aliyekuwa kipofu kwa miaka 8 akaweza kuona tena kupitia hospitali ya CCBRT
13. Nimesaidia wagonjwa wengine zaidi ya 42 wakapata huduma za afya na kupona
14. Nimesaidia Jezi kwa Vijana katika Kata 12 Kati ya 23 za Wilaya ya Kilombero
15. Nimefanikisha ligi Mbili katika Kata Mbili-Ligi za Mpira wa Miguu na Netboli
16. Nimeshiriki kwenye fundraising katika Misikiti 3 na Makanisa 4
17. Nimekuwa sehemu ya kufanikisha Uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishirki Cha Mt Fransisco
18. Nimeshiriki kuwasaidia Wahanga wa Mafuriko Wilayani Kilombero
19. Nimefanikisha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kushirki Umitashumta ngazi ya Wilaya,Mkoa na Taifa
20. Nimefanikisha Vikundi Viwili vya kina Mama Wajane kuweza Kujiajiri na kuendesha maisha yao wenyewe.
21. Nimefanikisha Vikundi 5 vya kina mama kuweza Kujiajiri.
22. Nimefanikisha Vikundi 3 vya wenye ulemavu Kujiajiri wenyewe.
23. Nimefanya Mikutano ya Hadhara ya Elimu ya Uraia pamoja na Shukrani zaidi ya 20.

Na mengine madogo madogo mengi.

B. KAZI ZA CHAMA WILAYANI KILOMBERO

Katika kukuza chama Wilayani Kilombero nimefanikiwa kufanya yafuatayo;
1. Nimelipia na kufungua Ofisi za CHADEMA katika Kata 5
2. Nimefungua na Kuzindua Matawi 13 yaliyojengewa na yenye Uongozi wa Kudumu
3. Nimeingiza Wanachama zaidi ya 8,000

C. KAZI ZA CHAMA ZA KITAIFA
1. Nimeshiriki Maandamano ya CHADEMA Kanda ya Ziwa katika Mikoa yote ya Kanda hiyo katika kupigania haki za watanzania.
2. Nimeshiriki Maandamano ya CHADEMA Nyanda za Juu Kusini kasoro (Mikoa ya Iringa na Ruvuma) katika kupigania haki za watanzania.
3. Nimeshiriki kwenye Kazi za Siasa Arusha - Sakata la Kuvuliwa Uanachama Madiwani kusaka muafaka.
4. Nimeshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Igunga
5. Nimeshiriki kutoa Mafunzo ya Mapungufu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba 2011 katika Mkoa wa Ruvuma
6. Nimeshiriki kwenye Siasa za Vyuo Vikuu, Makongamano, Mikutano ya Hadhara na Uzinduzi wa Matawi
7. Nimeshiriki kwenye Siasa za Dodoma, Singida na Morogoro.

Natambua nilipaswa kuyafanya zaidi ya haya lakini kutokana na sababu mbalimbali hayo ndio niliyofanikiwa kuyafanya. Angalau nimefanikiwa kufanya karibu asilimia 70 ya niliyopanga kuyafanya kwa mwaka huu 2011 kama Mbunge wa Vitimaalum Wilayani Kilombero.

Naomba nichukue fursa hii pia kuwashukuru wanaJF wote kwa support yenu kwangu kwa hakika ninawashukuru sana tena sana.JF imekuwa ni nyumbani, JF imekuwa ni darasa, Vile vile JF imekuwa ni Tanuru la Moto maana wakati mwingine huwa ninaingizwa kwenye moto hasa. Na mwisho nichukue fursa hii kuwaomba radhi wale wote niliowakwaza kwa namna moja ama nyingine, tuanze upya mwaka ujao..

With Love
Regia


HUU NAUCHUKULIA KAMA WOSIA WAKE WA MWISHO KWETU WANA JF NA TAIFA KWA UJUMLA, HII ILIKUWA TAREHE 31/12/2011.​
 
Nimekumbuka sana Mh. Amina, Salome na hivi leo Regia. Mungu tuokoe na ajali mwaka huu.Poleleni sana Watanzania bila kujali Chama na itikadi.RIP

 
Taa imezimika ghafla...............!


Poleni Watanzania
Poeni wana Kilombero
Poleni vijana wa Tanzania!
 
Hii gari ni balaa,haifai kabisa kujifundishia hasa huku mkono mmoja unapost kwenye JF.Baadhi ya kampuni za bima wanakwepa kuziwekea bima kwa vile uwezekano wa ajali ni mkubwa.
Hata hivyo nasema InnaLILLAAH WA INNA ILAIHI RAAJIUUN.

Acha dhihaka katika mambo mazito kama haya!
 
Oooh my God! Jembe limetutoka, jf tumempoteza mtu mhimu sana!
 
Nimekuwa JF tokea mwaka 2007 immediately baada ya kifo cha Amina Chifupa. I was shocked by her untimely departure, since then I have been receiving news about death and health of different people but today I am really shocked and feel the pain of losing a loved one. I did not know Regia personally but her charm and activities in JF and Tanzania's politics made me feel like I lost my very very very important close relative.

Rest in Peace Regia. We belong to Allah and to him shall we return!¬: Poleni wanasiasa wote wa Tanzania wenye nia njema na nchi, she was one of those people.
 
Hii nimeinyofoa kwenye Thread alitoianzisha kamanda Regia mwenyewe" Tunakusanya kero ambazo ungependa zisemwe Bungeni na nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA"


Regia : Ha ha ha!Umenichekesha.Kuna Siri katika Shukrani Mkuu,Mbwembwe nazo ni muhimu vile vile ni katika kunogesha Hotuba...Anyway limepokelewa na litafikishwa mahali husika.



quote_icon.png
By Ngongo
Regia.

Bado naendelea ..........

[23] Wabunge/Mawaziri punguzeni mbwembwe wakati wa kuwasilisha hoja mbali mbali mjengoni.Utasikia Mheshimiwa Spika namshukuru Mume/Mke wangu atataja jina,kisha ataendela na utaratibu wa mbwe mbwe namshuruku watoto wangu Ngongo anasoma Alberta University Canada,PakaJimmy anafanyakazi UNICTR Arusha ,Regia yuko hapa hapa mjengoni,ritz anapiga mzigo BOT.Akimaliza anahamia Wizara anayoisimamia Namshukuru sana Katibu Mkuu anamtaja jina ..........Muda wa salamu na pongezi unachukua zaidi ya dakika kumi.

Sikuwahi kukutana nae hata mara moja, lakini kwa hiyo msg yake kwako Ngongo, it seems she was charming, funny and good to chat with. Anyway, ninachoweza kusema kwa sasa ni 'tuungane katika kumuomba Mungu ampumzishe kwa amani! maana kazi za Mungu HAZITAFAKARIKI! tuamini na tupokee. RIP Regia, you lived your life in your own way n style, you struggled n reached a point where some people will never achieve in next 50 yrs of independence, so u died a hero!! To you JF members 'Lets live our life, coz we don know about tomorrow. RIP Reggy.
 
This is too sad.

Siamini mtani wangu Regia Mtema kanitoka.


Nilikufahamu humu humu ndani ya JF. Nilikufahamu kwa jina lako na nasikitika kuwa umeondoka bila kunifahamu mie SIKONGE.

Nilikuzoea kama dada yangu ambaye tumezaliwa pamoja wakati ukweli hatutaonana tena ana kwa ana.

Nduguzo na jamaa wako wote lazima wawe very proud kwako. Wazazi wako kwa kulea na kutunza mtoto kama wewe.

Kweli wema hawana maisha. Mungu akupe mapumziko mema huko ulikotangulia, AMEN.

 
Last edited by a moderator:
Inasemekena ni kweli,hata mimi nimepeta taarifa hapa mwanza najribu kuwasiliana na watu wa kibaha kuthibitisha
 
Watu wazuri tu ndio wanawahi kutuacha, sad indeed.
RAHA YA MILELE UMPE EH BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI
 
Bwana ametoa, Bwana ametwaa. Jina la Bwana Libarikiwe. Amen
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom