mgeni wenu
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 3,664
- 1,730
Habari zilizothibitishwa na JF ni kuwa Regia Mtema (mb) amepata ajali na Kufariki dunia eneo la Ruvu Darajani. Ndugu wa Karibu wanasema alikuwa kaenda kukagua Kiwanja alichopewa na Wazazi wake na baadae kwenye mkutano wa CHADEMA huko Kibaha. Habari hizi zimethibitishwa. Maneno ya Regia ya kufunga mwaka 2011 (Disemba 31, 2011)
Marehemu Regia Estelatus Mtema,
Gari lililochukua uhai wake (baada ya ajali)
Naomba nichukue fursa hii pia kuwashukuru wanaJF wote kwa support yenu kwangu kwa hakika ninawashukuru sana tena sana. JF imekuwa ni nyumbani, JF imekuwa ni darasa, Vile vile JF imekuwa ni Tanuru la Moto maana wakati mwingine huwa ninaingizwa kwenye moto hasa. Na mwisho nichukue fursa hii kuwaomba radhi wale wote niliowakwaza kwa namna moja ama nyingine, tuanze upya mwaka ujao.. With Love Regia