RC mpya wa Geita ashangaa stendi kuu ya Mkoa kuwa ya matope wakati kuna utajiri wa dhahabu

Hapo hapo chato kwa walima furu kuna uwanja wa ndege wa kuchezea bata na mwewe.

Hii nchi ilikua kwenye full fascism
Acha dharau ata Geita ni Tanzania pia tujifunze ata kwa wakenya wanavyopendana na wanavyopenda maeneo ya nchi yao.
 
Tunachosahau watanzania ni ukweli kwamba sisi tunapita njia.

Huo uwanja utakuja kutumika siku fursa za maeneo hayo zikifunguka kwa mapana yake.

Walipo jenga minara ya São Paulo na Paris miaka mingi nyuma kwa wakati ule walionekana wajinga lakini leo hii ni vyanzo vya pesa za utalii za Brazil na france.

Tatizo letu waafrika ni kudhani maisha ni ya kwetu tu.
Yaani uache kujenga miundombinu yenye manufaa kwa sasa ujenge miundombinu kwa ajili ya kizazi kijacho, je umeshafikia mahitaji ya kizazi cha sasa? Mfano ndio huo wa stendi tope.
 
Mimi nafikiri shida inaanzia kwenye vipaumbele ( first things first). Unaanzaje kujenga stendi (uwanja) ya ndege kabla ya stendi ya magari, hali ukijua asilimia kubwa ya wananchi wa eneo husika wanatumia usafiri wa barabara?
Uwanja wa ndege na stendi vyote viwili vinaweza kujengwa sambamba. Mpanda ndege anaweza akawa ni mgeni kutoka nje na stendi ikajengwa kwa ajili ya abiria wa eneo husika.

Vyote viwili ni vichocheo vya maendeleo, inategemea na mtazamo wa mtu mmoja mmoja.
 
Yaani uache kujenga miundombinu yenye manufaa kwa sasa ujenge miundombinu kwa ajili ya kizazi kijacho, je umeshafikia mahitaji ya kizazi cha sasa? Mfano ndio huo wa stendi tope.
Mkuu viwanja vya ndege vinaifungua nchi kimataifa wakati stendi zinaifungua nchi kwa ajili ya abiria wa ndani. Vyote viwili ni muhimu kuwepo, ndege sio anasa kama tunavyojaribu kudanganyana tunapokuwa kwenye mijadala yetu.
 
Mkuu viwanja vya ndege vinaifungua nchi kimataifa wakati stendi zinaifungua nchi kwa ajili ya abiria wa ndani. Vyote viwili ni muhimu kuwepo, ndege sio anasa kama tunavyojaribu kudanganyana tunapokuwa kwenye mijadala yetu.
Kama hakuna stendi mabasi ya kuifungua nchi hayaji au?
 
Zile mbwembwe za musukuma kumbe stendi yake ni tope tupu kama Bukoba!!
Mnyonge mnyongeni Mkuu lakini haki yake apate..Alipinga mno ufisadi uliofanyika pale lakini wapi...almanusura avue gamba na avae gwanda enzi Zile...ikawa apokwe tena kadi ya CCM na wao...mara akatwe...nk.Acha kabisa CCM inawenyewe,...mwisho akaulizwa ni Ubunge Wa Geita mjini tu au!?.Basi tunaligawa kutakuwa na Jimbo la Geita Vijijini,nenda huko..akatulia.!Hupiga kampeni bila sapoti ya Chama Chake huko...Acha kabisa
 
Mkuu mpya wa mkoa wa Geita Mheshimiwa Rose amesema ameshangazwa sana kukuta mkoa wa Geita una stendi kuu ya mabasi ya matope.

RC Rose amesema stendi ndio reception hivyo hutoa taswira ya mkoa ilivyo kwahiyo ni lazima utajiri wa dhahabu utumike kujenga stendi kuu ya kisasa na siyo hiyo ya kwenye matope.

Rose aliyasema hayo mbele ya wananchi na watendaji alipowasili mkoani Geita tayari kukabidhiwa ofisi.

Chanzo: ITV habari!
Halafu hapo si yule mkurugenzi alininua v8 ya 460ml
 
Mkuu mpya wa mkoa wa Geita Mheshimiwa Rose amesema ameshangazwa sana kukuta mkoa wa Geita una stendi kuu ya mabasi ya matope.

RC Rose amesema stendi ndio reception hivyo hutoa taswira ya mkoa ilivyo kwahiyo ni lazima utajiri wa dhahabu utumike kujenga stendi kuu ya kisasa na siyo hiyo ya kwenye matope.

Rose aliyasema hayo mbele ya wananchi na watendaji alipowasili mkoani Geita tayari kukabidhiwa ofisi.

Chanzo: ITV habari!
CHADEMA walikuwa wanongoza hii nchi, wameshindwa hata kujenga stendi ya chngarawe achilia mbali lami.

Hii nchi bhana, alafu CHADEMA wakaenda kujenga uwanja wa ndege huko porini CHATO na mbuga ya Burigi badala ya kuanza na maendeleo ya stendi ili wapate kodi.

"mwendazake"
 
Hawapiti stand hawa. Huyu alikuwa mkuu wa wilaya ya Same kabla hajateuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Geita. Stand ya wilaya ya Same ina lami. Stand ya makao makuu ya mkoa kuwa ya vumbi ni aibu. Sijafika mikoa yote Tanzania, lakini stand nyingi makao makuu ya mikoa ni lami.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nadhani mikoa ya kanda ya ziwa imelaaniwa... Shinyanga pekee ndio ina lami labda kidogo na Bariadi aka Simiyu hiyo mi-Mwanza, Kagera, Mara, Geita... vumbi mpaka....
 
CHADEMA walikuwa wanongoza hii nchi, wameshindwa hata kujenga stendi ya chngarawe achilia mbali lami.

Hii nchi bhana, alafu CHADEMA wakaenda kujenga uwanja wa ndege huko porini CHATO na mbuga ya Burigi badala ya kuanza na maendeleo ya stendi ili wapate kodi.

"mwendazake"
Sababu ni kutumiwa na mabeberu..
 
Back
Top Bottom