Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,239
Nchini mwetu kuna matukio Makubwa mawili ya ushushwaji na Upandishwaji wa Bendera. Tukio la Kwanza ni lile la kila siku ambapo Bendera hupandishwa Asubuhi na Kushushwa usiku. Mtindo huu tumeuiga toka kwa waingereza na hauhusishi bendera zilizozimikwa kwa ulalo bali unahusisha bendera zilizo kwenye milingoti wima.
Zamani bendera zilitumika kwa makundi ya kivita au majeshi ya nchi na usiku zilikuwa zinatembezwa na wabeba bendera maalumu na ndiyo maana kwenye Magwaride kuna kile kikosi kinaitwa "kikosi cha bendera" ambacho hubeba bendera tatu". Majeshi au vikundi vya kivita vilikuwa vikiteka maeneo husimika bendera ya Kikundi chao au ya nchi kama utambulisho kwa makundi au majeshi ya nchi nyingine yakifika kuwa eneo hilo linamilikiwa na kikundi au nchi hiyo.
Mitindo ya upeperushaji na upandishaji bendera hutofautiana kati ya nchi na nchi. Kwa Tanzania bendera hupandishwa Asubuhi kuonyesha kwamba Utawala wa kiraia unaofuata sheria unaanza na kushushwa jioni kuonyesha kinyume chake!! Tukio la pili ni anapoapishwa Rais Mpya.
Kabla ya Rais Kuapishwa, Rais anayemaliza muhula wake (hata kama ni huyohuyo) hukagua gwaride la Heshima. Wakati anapokwenda kuapishwa bendera ya Rais hushushwa kuashiria kwamba kisheria nchi haina Rais. Na kama hapo yule anayetarajiwa kuapishwa akifa ghafla yule aliyemaliza muda wake hawezi kuurudia urais kwani atakuwa ameshauvua kwa kiashiria cha bendera kushushwa.
Zamani bendera zilitumika kwa makundi ya kivita au majeshi ya nchi na usiku zilikuwa zinatembezwa na wabeba bendera maalumu na ndiyo maana kwenye Magwaride kuna kile kikosi kinaitwa "kikosi cha bendera" ambacho hubeba bendera tatu". Majeshi au vikundi vya kivita vilikuwa vikiteka maeneo husimika bendera ya Kikundi chao au ya nchi kama utambulisho kwa makundi au majeshi ya nchi nyingine yakifika kuwa eneo hilo linamilikiwa na kikundi au nchi hiyo.
Mitindo ya upeperushaji na upandishaji bendera hutofautiana kati ya nchi na nchi. Kwa Tanzania bendera hupandishwa Asubuhi kuonyesha kwamba Utawala wa kiraia unaofuata sheria unaanza na kushushwa jioni kuonyesha kinyume chake!! Tukio la pili ni anapoapishwa Rais Mpya.
Kabla ya Rais Kuapishwa, Rais anayemaliza muhula wake (hata kama ni huyohuyo) hukagua gwaride la Heshima. Wakati anapokwenda kuapishwa bendera ya Rais hushushwa kuashiria kwamba kisheria nchi haina Rais. Na kama hapo yule anayetarajiwa kuapishwa akifa ghafla yule aliyemaliza muda wake hawezi kuurudia urais kwani atakuwa ameshauvua kwa kiashiria cha bendera kushushwa.