John Mnyika
JF-Expert Member
- Jun 16, 2006
- 713
- 1,245
Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?
Nilizikuta enzi za kuimba nyimbo za kizalendo zikiwa ukingoni, wakati huo nikiwa kinda. Bendera ya taifa ikipandishwa, tulisimama wima! Hata nzi akikugusa, hakuna kutikisika. Bendera ikipanda, kichwani ulisikika mwangwi wa mirindimo ya nyimbo za kusifia bendera yetu ya taifa. Nyimbo inayotaja idadi na rangi za bendera yetu. Ama kwa hakika ilikuwa njia nzuri ya kukariri na kuamini. Rangi ya kijani, ikiwasilisha misitu yetu. Rangi ya manjano ikibeba madini na rasilimali zingine. Bluu ikiwasilisha bahari, mawaziwa na maji. Huku nyeusi, ikisadifu uafrika na rangi yetu. Naam, hiyo ndio bendera ya taifa la Tanzania.
Naandika makala haya, nikiitazama picha ya mtoto wa kitanzania! Ambayo kwa upekee wake nimeiweka katika kumbukumbu zangu. Picha hii imepigwa Mwanza, wakati wa mechi ya kandanda kati ya Taifa Stars na Simba wa Teranga-Senegali!. Picha zinazoshabihiana na hii ndio zilikuwa picha za wiki, mara baada ya mechi hiyo. Pengine ni hamasa kama hii ndiyo iliwasukuma vijana kufanya kile ambacho wengine tulijua hakiwezekani "Kuifunga Burkina Faso nyumbani kwao!". Naam; tuliwalamba bao moja kwa nunge. Naikumbuka tena Picha ya Mtoto iliyotoka baada ya mechi na Senegali, akiwa amepambwa au amejipamba kwa rangi za bendera ya Taifa letu, huku ameshikilia bendera ya Taifa letu, kifuani ameandikwa herufi "JK".
Naitazama picha hii nikiwa na hisia mbili zinazokinzana! Mosi, hisia ya furaha, kwamba uzalendo umeanza kurejea katika taifa letu. Hizi ni kelele ambazo tumeguwa tukizipiga sana; kwamba bila uzalendo, hakuna utaifa, bila utaifa hakuna kutanguliza mbele maslahi ya taifa; bila kutanguliza mbele maslahi ya taifa; maendeleo ya nchi yanawekwa rehani! Ishara mojawapo ya uzalendo ni matumizi ya alama za kitaifa. Suala ambalo huko nyuma limekuwa likiminywa.
Nakumbuka jinsi ambavyo serikali iliijua juu CHADEMA kwa kutumia rangi za bendera ya Taifa katika mabango yake. Baadaye, Disemba 30 mwaka huohuo 2005 baada ya uchaguzi, Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake ya kuzindua bunge, akakubaliana na sera hii ya uzalendo pamoja na kwamba haikuwepo katika ilani ya CCM-na kutangaza rasmi kwamba ni ruksa kwa raia kuvaa rangi za bendera ya taifa, ni muhimu kwa wananchi kuwa wazalendo. Binafsi nilipiga makofi katika hili. Upinzani ni visima vya fikra mbadala; zinapokubalika na serikali; maslahi ni ya wote bila kujali itikadi- hata katika hili la matumizi ya rangi na taswira za bendera katika maisha ya kila siku ya wananchi. Naam, nilipoona mtoto huyu alivyojipamba, niliona kabisa ameitika mwito!
Pili; hisia ya huzuni- kwa kuona herufi "JK" kifuani pake. Si kwamba sizipendi herufi "JK", na wala sijui kama ni kifupi cha jina la mtoto yule ama ni kifupi cha jina la Rais wetu Jakaya Kikwete kama ilivyozoeleka. Lakini jambo moja lilinipa huzuni, nalo ni "kufikisha ujumbe tofauti, katika mazingira tofauti". Katika mazingira yale, nilitaraji lengo la uzalendo wetu ni taifa letu.
Nilitaraji, hamasa ya msingi wapewe vijana wetu wa taifa stars. Ningefurahi zaidi kama herufi zile zingekuwa "TZ", yaani Tanzania au "JMT" yaani Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Ama zingekuwa "TS" kifupi cha Taifa Stars. Hapo ujumbe wa uzalendo ungefika vizuri zaidi.! Utaifa ungewekwa mbele zaidi. Naamini watanzania walijumuika pale Kirumba kushangilia taifa lao, na si kumshangilia "JK"! Sina umalaika wa kujua nia ya herufi zile; lakini najua katika maisha-wapo ambao hubeba mabango ya sifa; kwa lengo la kupata fadhila. Natumaini mtoto yule malaika wa Mungu hayupo katika kundi hilo. Walau akikua ataitazama picha ile na kukumbuka uzalendo uliotukuka!
Picha hii imenifanya nitafakari. Nikumbuke bendera mbalimbali. Na kuanza kujiuliza; je, zinabeba ujumbe, uzalendo ama ni urembo tu? Naitafakari bendera ya chama kinachotawala hivi sasa Tanzania- CCM. Rangi zake, alama yake!. Bendera hii ina rangi mbili; Kijani na Njano. Kijani ambayo wengi ya wanachama wake hupenda kuivaa. Nafakari, hivi inawakilisha kitu gani-Je, ni misitu katika nchi ambayo imeanza kugeuka jangwa kutokana na uharibifu wa mazingira? Je, ni misitu katika nchi ambayo wazawa wawindaji wanaendelea 'kuswagwa' toka misitu hiyo kupisha 'wawindaji wawekezaji'; je ni misitu katika nchi ambayo mkazi wa pembeni ya mbuga ya wanyama hajui mapato yanayotokana na idadi lukuki ya wageni wanaokuja kutembelea mbuga za wanyama yanakwenda wapi?
Watalii hawa wengi wao fedha za malipo yao hubaki nchini mwao kutokana na utaratibu wa kulipa huko huko(package tourism)! Je, inawasilisha kilimo katika nchi ambayo serikali ya awamu ya tatu chini ya chama hicho imekiri kwamba haikutoa kipaumbele katika kilimo huku serikali ya awamu ya nne ikiwa imetenga asilimia sita tu ya bajeti katika kilimo kwa mujibu wa makidirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2007/08 iliyowasilishwa bungeni? Kwa miaka 30 toka chama hiki kianzishwe, wakulima sehemu kubwa ya nchi yetu hawajaona matunda ya rangi hii ya kijani. Labda, ipo siku; ile alama ya jembe, itageuka kuwa zana ya ukombozi kwao katika karne hii ya sayansi na teknolojia!.
Halafu kuna rangi ya njano, rangi ambayo Timu ya Simba, hupenda kuwatania watani zao Yanga kwamba ni 'Yebo Yebo', nayo inawakilisha nini? Je, ni zile rasilimali na madini ambayo huchimbwa na makampuni makubwa ya kigeni na watanzania kuambulia mrahaba wa asilimia tatu huku tukiachwa na mashimo? Wapo wapi wale wafanyakazi bora watumie zana ile ya nyundo; kuvunja miamba ya unyonyaji- na kuhakikisha watanzania wananufaika na yale ambayo mwenyezi Mungu amelijalia Taifa hili tajiri wa rasilimali?Je, tuna umaskini wa uongozi na fikra mbadala? Ndio maana, niamua kufungua huu mjadala-Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo ama urembo?
Naendelea kutafakari; nakikumbuka Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na bendera yake. Mara baada ya uchaguzi, CHADEMA ilituma timu katika wilaya teule, kukusanya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba na kanuni za chama hicho. Moja ya mambo yaliyoguswa katika mabadiliko hayo ni pamoja na bendera yake. Hatimaye katiba na kanuni mpya zikapitishwa na Mkutano Mkuu wake uliofanyika mwaka 2006, na Bendera Mpya ya CHADEMA ikazinduliwa ikiwa ni ishara ya Tumaini Jipya! Nikiitafakari bendera hii nayo.
Bendera ya CHADEMA ina nembo ya kiganya cha mkono kilichonyoosha vidole viwili katika mfumo wa V kama ishara ya USHINDI. CHADEMA ni chama kinacholenga kushinda kidemokrasia na hatimaye kuleta ushindi wa maendeleo ya taifa. Bendera ya CHADEMA ina rangi nne: Nyeusi, Bluu bahari (light blue), nyeupe na nyekundu.
Rangi:
NYEUSI inawakilisha WATU WA TANZANIA. Hii ni rangi ya wazawa asili wa nchi yetu. Ni rangi ambayo inabeba pia falsafa ya NGUVU YA UMMA. Rangi ya BLUU BAHARI (LIGHT BLUE) ni rangi ya asili ya CHADEMA. Ni rangi ambayo inawasilisha HAKI. Rangi nyeupe inawasilisha UWAZI na UKWELI. Huu ni msingi muhimu wa CHADEMA. CHADEMA ni chama ambacho kitasimamia uwazi, ukweli na uadilifu kwa njia ya demokrasia.Rangi ya BLUU ISIYOKOZA iko juu ya rangi NYEKUNDU kama ishara kwamba kama taifa tumevushwa na mashujaa kuelekea katika jamii yenye haki, na hivyo CHADEMA ni chama cha siasa kinasimamia haki.
Rangi nyekundu inawakilisha MASHUJAA. CHADEMA inathamini historia ya nchi yetu ikiwemo damu ambayo imewahi kumwaga katika kutetea haki wakati wa vita dhidi ya mkoloni na matukio mengine ambayo ni chimbuko la uzalendo na nia yetu ya kuendeleza amani katika nchi yetu.
Mintaarafu bendera ya Tanzania imepatikana kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilihali visiwani kuna historia ya damu kumwagika ama kumwagwa wakati wa mapinduzi? Kama kweli tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na utawala wa Chama cha Mapinduzi(CCM), je ni mapinduzi yasiyo na ‘rangi nyekundu'?.
Rangi nyekundu ni hidaya kwao waliomwaga damu wakati mapambano kadhaa na Mreno na Mwarabu. Tuzo kwao waliopigana na Ujerumani wakati wa utawala na mliomwaga damu katika vita vya dunia. Heko kwao ambao damu walisafisha safari ya kumng'oa Nduli Amin. Heri yake Sethi Benjamini na wote waliopotesha maisha katika hekaheka za kueneza Azimio la Arusha. Kumbukumbu kwao waliotoa damu katika mikikimikiki ya mfumo wa vyama vingi kutoka Zanzibar mpaka bara. Damu yao iliyomwagika haizoleki, ukiwa waliouacha hauzoeleki lakini fikra walizosimamia hazizeeki. Mapambano bado yanaendelea!
Kwake Bushiri bin Salim wa Tanga, suriama wa kiarabu na kiafrika, pamoja na nia yake tenge ya kulinda maslahi katika biashara ya utumwa ulimwaga damu kwa kunyogwa Pangani baada ya kuongoza maasi makali dhidi ya kuingia kwa ukoloni wa Kijeruamani-damu yake ilimwagika pamoja na damu za wapiganaji wa Pwani, Morogoro mpaka uhehe. Kwake Mtemi Meli, uliyewashinda wadachi mpaka mwenzake Sina alipomsaliti hatimaye yeye na mashujaa wenzake wakamwaga damu kaskazini wakilinda uhuru.
Tunamkumbuka Chifu Mkwawa, aliovyowaunganisha wahehe-toka Kalenga, Tosamaganga mpaka ulipoamua kuimwaga damu yake mwenyewe kuliko uhuru upotee mikononi mwake. Mtemi Isiki wa Tabora uliendesha mashambulizi ya kishujaa, hatimaye akaamua kumwaga damu yake na ya familia yake kwa kujilipua na baruti ili tu asipate aibu ya uhuru kuchukuliwa mbele ya macho yake. Tunamkumbuka Mtemi Makongoro wa Musoma, alipambana kwa ushujaa mpaka ilibidi kikosi cha wanamaji kiletwe kupitia miji ya Mombasa na Kisumu kummaliza.
Tunamkumbuka Kinjeketile kwa kuongoza vita vya kutisha vya Maji Maji kwa miaka kadhaa vilivyoanzia vilima vya Matumbi karibu na Kilwa. Wao walitaka kumwondoa mkoloni kwa nguvu na walikuwa tayari kumwaga damu kuliko kuendelea kuishi bila ya uhuru. Mapambano yao yalisambaa maeneo mengi ya ardhi yetu. Hawa walikuwa mashujaa kweli kweli waliojua umuhimu wa imani na falsafa katika mapambano-wakawapa watu ujasiri kwa dawa ya "Kugeuza risasi, Kuwa maji". Pamoja na kushindwa vita na wazalendo zaidi ya laki moja kupoteza maisha katika wakati ambao ardhi ilikuwa na watu wachache yapo mapigano ambayo walishinda. Pamoja na machifu 47 wa Kingoni kunyongwa damu yao ilileta mabadiliko katika utawala. Kwa vyovyote vile damu nyingi kiasi hiki iliyomwagika kwa sababu ya kudai uhuru haiwezi kupuuzwa. Hivyo rangi nyekundu ni kumbukumbu yao.
Karibu kila eneo katika nchi yetu yupo shujaa ambaye anaweza kukumbukwa laiti kama historia zenu zingejulikana kizazi hata kizazi na kuwa chimbuko la kujiamini, kujithamini na uzalendo miongoni mwa Watanzania. Kushindwa kwao na hatimaye ukoloni kuingia ama kuendelea hakuondoi historia kuwa mlimwaga damu kwa ajili ya kulinda uhuru wa ardhi hii tukiyoirithi! Rangi nyekundu ni ishara kwamba; sio siri, kwa sera bila silaha, mapambano bado yanaendelea mpaka mabadiliko ya kweli yatakapopatikana!
Rangi nyeupe iko mbele ya rangi zote kama ishara kwamba chama kinatanguliza UWAZI na UKWELI katika nyanja zote. Pia rangi nyeupe imebeba nembo ya chama kwa kuwa usafi ni msingi muhimu sana kwa chama. Nembo ya chama iko mbele kama kama ishara ya CHADEMA kuwa chama kiongozi katika kuchochea misingi muhimu katika kuleta mabadiliko na maendeleo katika Taifa. Nafungua mjadala; rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?
Nilizikuta enzi za kuimba nyimbo za kizalendo zikiwa ukingoni, wakati huo nikiwa kinda. Bendera ya taifa ikipandishwa, tulisimama wima! Hata nzi akikugusa, hakuna kutikisika. Bendera ikipanda, kichwani ulisikika mwangwi wa mirindimo ya nyimbo za kusifia bendera yetu ya taifa. Nyimbo inayotaja idadi na rangi za bendera yetu. Ama kwa hakika ilikuwa njia nzuri ya kukariri na kuamini. Rangi ya kijani, ikiwasilisha misitu yetu. Rangi ya manjano ikibeba madini na rasilimali zingine. Bluu ikiwasilisha bahari, mawaziwa na maji. Huku nyeusi, ikisadifu uafrika na rangi yetu. Naam, hiyo ndio bendera ya taifa la Tanzania.
Naandika makala haya, nikiitazama picha ya mtoto wa kitanzania! Ambayo kwa upekee wake nimeiweka katika kumbukumbu zangu. Picha hii imepigwa Mwanza, wakati wa mechi ya kandanda kati ya Taifa Stars na Simba wa Teranga-Senegali!. Picha zinazoshabihiana na hii ndio zilikuwa picha za wiki, mara baada ya mechi hiyo. Pengine ni hamasa kama hii ndiyo iliwasukuma vijana kufanya kile ambacho wengine tulijua hakiwezekani "Kuifunga Burkina Faso nyumbani kwao!". Naam; tuliwalamba bao moja kwa nunge. Naikumbuka tena Picha ya Mtoto iliyotoka baada ya mechi na Senegali, akiwa amepambwa au amejipamba kwa rangi za bendera ya Taifa letu, huku ameshikilia bendera ya Taifa letu, kifuani ameandikwa herufi "JK".
Naitazama picha hii nikiwa na hisia mbili zinazokinzana! Mosi, hisia ya furaha, kwamba uzalendo umeanza kurejea katika taifa letu. Hizi ni kelele ambazo tumeguwa tukizipiga sana; kwamba bila uzalendo, hakuna utaifa, bila utaifa hakuna kutanguliza mbele maslahi ya taifa; bila kutanguliza mbele maslahi ya taifa; maendeleo ya nchi yanawekwa rehani! Ishara mojawapo ya uzalendo ni matumizi ya alama za kitaifa. Suala ambalo huko nyuma limekuwa likiminywa.
Nakumbuka jinsi ambavyo serikali iliijua juu CHADEMA kwa kutumia rangi za bendera ya Taifa katika mabango yake. Baadaye, Disemba 30 mwaka huohuo 2005 baada ya uchaguzi, Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake ya kuzindua bunge, akakubaliana na sera hii ya uzalendo pamoja na kwamba haikuwepo katika ilani ya CCM-na kutangaza rasmi kwamba ni ruksa kwa raia kuvaa rangi za bendera ya taifa, ni muhimu kwa wananchi kuwa wazalendo. Binafsi nilipiga makofi katika hili. Upinzani ni visima vya fikra mbadala; zinapokubalika na serikali; maslahi ni ya wote bila kujali itikadi- hata katika hili la matumizi ya rangi na taswira za bendera katika maisha ya kila siku ya wananchi. Naam, nilipoona mtoto huyu alivyojipamba, niliona kabisa ameitika mwito!
Pili; hisia ya huzuni- kwa kuona herufi "JK" kifuani pake. Si kwamba sizipendi herufi "JK", na wala sijui kama ni kifupi cha jina la mtoto yule ama ni kifupi cha jina la Rais wetu Jakaya Kikwete kama ilivyozoeleka. Lakini jambo moja lilinipa huzuni, nalo ni "kufikisha ujumbe tofauti, katika mazingira tofauti". Katika mazingira yale, nilitaraji lengo la uzalendo wetu ni taifa letu.
Nilitaraji, hamasa ya msingi wapewe vijana wetu wa taifa stars. Ningefurahi zaidi kama herufi zile zingekuwa "TZ", yaani Tanzania au "JMT" yaani Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Ama zingekuwa "TS" kifupi cha Taifa Stars. Hapo ujumbe wa uzalendo ungefika vizuri zaidi.! Utaifa ungewekwa mbele zaidi. Naamini watanzania walijumuika pale Kirumba kushangilia taifa lao, na si kumshangilia "JK"! Sina umalaika wa kujua nia ya herufi zile; lakini najua katika maisha-wapo ambao hubeba mabango ya sifa; kwa lengo la kupata fadhila. Natumaini mtoto yule malaika wa Mungu hayupo katika kundi hilo. Walau akikua ataitazama picha ile na kukumbuka uzalendo uliotukuka!
Picha hii imenifanya nitafakari. Nikumbuke bendera mbalimbali. Na kuanza kujiuliza; je, zinabeba ujumbe, uzalendo ama ni urembo tu? Naitafakari bendera ya chama kinachotawala hivi sasa Tanzania- CCM. Rangi zake, alama yake!. Bendera hii ina rangi mbili; Kijani na Njano. Kijani ambayo wengi ya wanachama wake hupenda kuivaa. Nafakari, hivi inawakilisha kitu gani-Je, ni misitu katika nchi ambayo imeanza kugeuka jangwa kutokana na uharibifu wa mazingira? Je, ni misitu katika nchi ambayo wazawa wawindaji wanaendelea 'kuswagwa' toka misitu hiyo kupisha 'wawindaji wawekezaji'; je ni misitu katika nchi ambayo mkazi wa pembeni ya mbuga ya wanyama hajui mapato yanayotokana na idadi lukuki ya wageni wanaokuja kutembelea mbuga za wanyama yanakwenda wapi?
Watalii hawa wengi wao fedha za malipo yao hubaki nchini mwao kutokana na utaratibu wa kulipa huko huko(package tourism)! Je, inawasilisha kilimo katika nchi ambayo serikali ya awamu ya tatu chini ya chama hicho imekiri kwamba haikutoa kipaumbele katika kilimo huku serikali ya awamu ya nne ikiwa imetenga asilimia sita tu ya bajeti katika kilimo kwa mujibu wa makidirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2007/08 iliyowasilishwa bungeni? Kwa miaka 30 toka chama hiki kianzishwe, wakulima sehemu kubwa ya nchi yetu hawajaona matunda ya rangi hii ya kijani. Labda, ipo siku; ile alama ya jembe, itageuka kuwa zana ya ukombozi kwao katika karne hii ya sayansi na teknolojia!.
Halafu kuna rangi ya njano, rangi ambayo Timu ya Simba, hupenda kuwatania watani zao Yanga kwamba ni 'Yebo Yebo', nayo inawakilisha nini? Je, ni zile rasilimali na madini ambayo huchimbwa na makampuni makubwa ya kigeni na watanzania kuambulia mrahaba wa asilimia tatu huku tukiachwa na mashimo? Wapo wapi wale wafanyakazi bora watumie zana ile ya nyundo; kuvunja miamba ya unyonyaji- na kuhakikisha watanzania wananufaika na yale ambayo mwenyezi Mungu amelijalia Taifa hili tajiri wa rasilimali?Je, tuna umaskini wa uongozi na fikra mbadala? Ndio maana, niamua kufungua huu mjadala-Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo ama urembo?
Naendelea kutafakari; nakikumbuka Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) na bendera yake. Mara baada ya uchaguzi, CHADEMA ilituma timu katika wilaya teule, kukusanya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba na kanuni za chama hicho. Moja ya mambo yaliyoguswa katika mabadiliko hayo ni pamoja na bendera yake. Hatimaye katiba na kanuni mpya zikapitishwa na Mkutano Mkuu wake uliofanyika mwaka 2006, na Bendera Mpya ya CHADEMA ikazinduliwa ikiwa ni ishara ya Tumaini Jipya! Nikiitafakari bendera hii nayo.
Bendera ya CHADEMA ina nembo ya kiganya cha mkono kilichonyoosha vidole viwili katika mfumo wa V kama ishara ya USHINDI. CHADEMA ni chama kinacholenga kushinda kidemokrasia na hatimaye kuleta ushindi wa maendeleo ya taifa. Bendera ya CHADEMA ina rangi nne: Nyeusi, Bluu bahari (light blue), nyeupe na nyekundu.
Rangi:
NYEUSI inawakilisha WATU WA TANZANIA. Hii ni rangi ya wazawa asili wa nchi yetu. Ni rangi ambayo inabeba pia falsafa ya NGUVU YA UMMA. Rangi ya BLUU BAHARI (LIGHT BLUE) ni rangi ya asili ya CHADEMA. Ni rangi ambayo inawasilisha HAKI. Rangi nyeupe inawasilisha UWAZI na UKWELI. Huu ni msingi muhimu wa CHADEMA. CHADEMA ni chama ambacho kitasimamia uwazi, ukweli na uadilifu kwa njia ya demokrasia.Rangi ya BLUU ISIYOKOZA iko juu ya rangi NYEKUNDU kama ishara kwamba kama taifa tumevushwa na mashujaa kuelekea katika jamii yenye haki, na hivyo CHADEMA ni chama cha siasa kinasimamia haki.
Rangi nyekundu inawakilisha MASHUJAA. CHADEMA inathamini historia ya nchi yetu ikiwemo damu ambayo imewahi kumwaga katika kutetea haki wakati wa vita dhidi ya mkoloni na matukio mengine ambayo ni chimbuko la uzalendo na nia yetu ya kuendeleza amani katika nchi yetu.
Mintaarafu bendera ya Tanzania imepatikana kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilihali visiwani kuna historia ya damu kumwagika ama kumwagwa wakati wa mapinduzi? Kama kweli tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na utawala wa Chama cha Mapinduzi(CCM), je ni mapinduzi yasiyo na ‘rangi nyekundu'?.
Rangi nyekundu ni hidaya kwao waliomwaga damu wakati mapambano kadhaa na Mreno na Mwarabu. Tuzo kwao waliopigana na Ujerumani wakati wa utawala na mliomwaga damu katika vita vya dunia. Heko kwao ambao damu walisafisha safari ya kumng'oa Nduli Amin. Heri yake Sethi Benjamini na wote waliopotesha maisha katika hekaheka za kueneza Azimio la Arusha. Kumbukumbu kwao waliotoa damu katika mikikimikiki ya mfumo wa vyama vingi kutoka Zanzibar mpaka bara. Damu yao iliyomwagika haizoleki, ukiwa waliouacha hauzoeleki lakini fikra walizosimamia hazizeeki. Mapambano bado yanaendelea!
Kwake Bushiri bin Salim wa Tanga, suriama wa kiarabu na kiafrika, pamoja na nia yake tenge ya kulinda maslahi katika biashara ya utumwa ulimwaga damu kwa kunyogwa Pangani baada ya kuongoza maasi makali dhidi ya kuingia kwa ukoloni wa Kijeruamani-damu yake ilimwagika pamoja na damu za wapiganaji wa Pwani, Morogoro mpaka uhehe. Kwake Mtemi Meli, uliyewashinda wadachi mpaka mwenzake Sina alipomsaliti hatimaye yeye na mashujaa wenzake wakamwaga damu kaskazini wakilinda uhuru.
Tunamkumbuka Chifu Mkwawa, aliovyowaunganisha wahehe-toka Kalenga, Tosamaganga mpaka ulipoamua kuimwaga damu yake mwenyewe kuliko uhuru upotee mikononi mwake. Mtemi Isiki wa Tabora uliendesha mashambulizi ya kishujaa, hatimaye akaamua kumwaga damu yake na ya familia yake kwa kujilipua na baruti ili tu asipate aibu ya uhuru kuchukuliwa mbele ya macho yake. Tunamkumbuka Mtemi Makongoro wa Musoma, alipambana kwa ushujaa mpaka ilibidi kikosi cha wanamaji kiletwe kupitia miji ya Mombasa na Kisumu kummaliza.
Tunamkumbuka Kinjeketile kwa kuongoza vita vya kutisha vya Maji Maji kwa miaka kadhaa vilivyoanzia vilima vya Matumbi karibu na Kilwa. Wao walitaka kumwondoa mkoloni kwa nguvu na walikuwa tayari kumwaga damu kuliko kuendelea kuishi bila ya uhuru. Mapambano yao yalisambaa maeneo mengi ya ardhi yetu. Hawa walikuwa mashujaa kweli kweli waliojua umuhimu wa imani na falsafa katika mapambano-wakawapa watu ujasiri kwa dawa ya "Kugeuza risasi, Kuwa maji". Pamoja na kushindwa vita na wazalendo zaidi ya laki moja kupoteza maisha katika wakati ambao ardhi ilikuwa na watu wachache yapo mapigano ambayo walishinda. Pamoja na machifu 47 wa Kingoni kunyongwa damu yao ilileta mabadiliko katika utawala. Kwa vyovyote vile damu nyingi kiasi hiki iliyomwagika kwa sababu ya kudai uhuru haiwezi kupuuzwa. Hivyo rangi nyekundu ni kumbukumbu yao.
Karibu kila eneo katika nchi yetu yupo shujaa ambaye anaweza kukumbukwa laiti kama historia zenu zingejulikana kizazi hata kizazi na kuwa chimbuko la kujiamini, kujithamini na uzalendo miongoni mwa Watanzania. Kushindwa kwao na hatimaye ukoloni kuingia ama kuendelea hakuondoi historia kuwa mlimwaga damu kwa ajili ya kulinda uhuru wa ardhi hii tukiyoirithi! Rangi nyekundu ni ishara kwamba; sio siri, kwa sera bila silaha, mapambano bado yanaendelea mpaka mabadiliko ya kweli yatakapopatikana!
Rangi nyeupe iko mbele ya rangi zote kama ishara kwamba chama kinatanguliza UWAZI na UKWELI katika nyanja zote. Pia rangi nyeupe imebeba nembo ya chama kwa kuwa usafi ni msingi muhimu sana kwa chama. Nembo ya chama iko mbele kama kama ishara ya CHADEMA kuwa chama kiongozi katika kuchochea misingi muhimu katika kuleta mabadiliko na maendeleo katika Taifa. Nafungua mjadala; rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?