Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Uzalendo ilikuwa zamani kabla ya watu kuanza kuChukua Chao Mapema.
 
Ndugu zangu,


Ni kweli, Watanzania tunaendekeza sana siasa za vyama na kuiasahau Tanzania yetu. Leo asubuhi sana niliianza safari yangu kutoa Msamvu , Morogoro kuja Iringa. Ni kawaida kando ya barabara kwenye makazi ya watu au vibanda vya biashara kukuta ikipepea, ama, bendera ya CCM, Chadema, CUF, Simba au Yanga. Lakini, ni nadra sana kuiona ikiperushwa bendera ya taifa letu.

Leo pale kijijini Mtandika, nje kidogo ya Ruaha Mbuyuni niliona kwenye banda moja la biashara ikipepea bendera ya taifa. Nilishtuka kuiona , niliguswa pia. Nlipunguza hata mwendo kumwangalia kijana yule aliyekuwa akifanya biashara yake ya vitunguu huku bendera ya nchi yake ikipepea.

Maana, bila shaka kijana yule kwa mapenzi ya nchi yake aliitafuta mwenyewe bendera ile ya taifa. Kwa vile, unapoona mahali kuna vijana wanapeperusha bendera za vyama yaweza kuwa na tafsiri ya ama, ni wapenzi wa vyama hivyo, na kuwa wamezitafuta wenyewe, au kuna kada wa chama husika aliyekuja na kugawa bendera hizo kwa vijana hao.

Ndio, tunahitaji kufanya jitihada za kuwafanya watu wetu waipende nchi yao waliyozaliwa, kutoka ndani ya mioyo yao. Na moja ya jitihada hizo ni kuwapa maarifa yatakayowawezesha kujitambua, kujiamini na kuthubutu.

Maggid,
Iringa.
 
Brother Maggid Wakati baadhi ya Wananchi wanahangaika kujenga nchi kwa maana ya Utanzania kwanza, wengine wako busy kujenga udini, uchama, ukabila na ukanda. Tunahitaji masiah wakututoa huku shimoni tunakoelekea vinginevyo hali itakuwa tete sana huko mbele ya safari haya makundi yatakapokuwa yamekomaa
 
..wakati CCM inatamba hamkukumba kuhusu utaifa.

..leo mnaona CDM imeshika kasi ndiyo mnakumbuka kuhubiri utaifa.
 
Lakini hairuhusiwi kupeperusha bendera ya taifa kwa mtu yoyote isipokuwa ofisi za serikali na nyumba za viongozi wakuu.
huku ni kutokujua maana ya uzalendo ukweli natamani kila mtanzania awe na bendera ya taifa nyumbani kwake kukosekana kwa uzalendo ndio kumefikisha taifa hapa nchi ambazo bendera ya taifa iko huru wanaipenda sana nchi yao maana wanajua uzalendo kuliko sisi ambao tuliaminishwa bendera utaiona kwenye ofisi za serikali au sehemu muhimu tu matokeo yake ndio haya hatuna uzalendo wa kutetea hata mali, zetu wananchi wetu nk.
 
We Mjengwa, hapo sasa unamwingiza matatani kijana wa watu. Tanzania sio USA ambako kuonyesha mapenzi kwa nchi yako unaweza hata kushona shati lenye bendera ya taifa, kofia na suruali yake na viatu ati. Kwa Tanzania nakumbuka sana tangu enzi za Ng'walimu ni kosa la jinai kuona umevaa au kupeperusha bendera ya Taifa eneo ambalo sio ofisi rasmi ya serikali, unaweza kufungwa. Sasa watamfuatilia kijana kijijini hapo wamdaudi. Bora utundike bendera ya CCM ukauza gongo chini yake utatetewa. Tanzania hatujakomboka kifikra bado, ndo maana wanasiasa ambao ndo viongozi wetu wanatukanana kuhusu nani ni mtanzania halisi mwenye halali ya kuishi na kufanya biashara. Hukumbuki kwamba ukitaka kufanikiwa mambo yako lazima uwe ccm? Ama sivyo utafilisiwa njomba, hata mashamba ya kwenu Ludewa utayasikia kutoka kaburini. Watamwambia kaiba ofisini kwa serikali bendera hiyo na mlolongo wa vitu vingine vilivyopotea pamoja na bendera hiyo. Subiri.
 
kuna kpindi walipiga marufuku kupeperusha bendera hovyo, kutumia kama vtambaa, mapazia au shuka sababu etu tunadharirisha bendera ya nchi, ina maana wamesharusu saizi bcoz n rahs zaidi kupata bendera ya US kuliko ya tz
 
Tulifundishwa shule kuwa bendera ya taifa hupepea kwenye ofisi na taasisi za kiserikali. Hizi jezi amezileta Marcio Maximo. Mgeni kaona umuhimu wa bendera ya nchi isiyo yake... Kwa hiyo brother usishangae, hii ndo bongo zaidi uijuavyo.
 
Mzalendo,

Asante sana. Nimefika salama Iringa. Na utalii nimeufanyia Ruaha Mbuyuni, kununua vitunguu!
Maggid,
Iringa.

huwa sipendi mtu anayetoa thread, halafu anajichagulia post chache sana za kujibu kwa faida yake badala ya kujibu hata hoja asizozipenda. not fair at all!!
 
kanuni ya nyaraka za serikali ambazo mtu huruhusiwi kumiliki binafsi ni pamoja na bendera ya taifa

kuwa makini na vitu vingine kumbuka kutokujua sheria siyo kinga
 
Ndugu zangu,


Ni kweli, Watanzania tunaendekeza sana siasa za vyama na kuiasahau Tanzania yetu. Leo asubuhi sana niliianza safari yangu kutoa Msamvu , Morogoro kuja Iringa. Ni kawaida kando ya barabara kwenye makazi ya watu au vibanda vya biashara kukuta ikipepea, ama, bendera ya CCM, Chadema, CUF, Simba au Yanga. Lakini, ni nadra sana kuiona ikiperushwa bendera ya taifa letu.

Leo pale kijijini Mtandika, nje kidogo ya Ruaha Mbuyuni niliona kwenye banda moja la biashara ikipepea bendera ya taifa. Nilishtuka kuiona , niliguswa pia. Nlipunguza hata mwendo kumwangalia kijana yule aliyekuwa akifanya biashara yake ya vitunguu huku bendera ya nchi yake ikipepea.

Maana, bila shaka kijana yule kwa mapenzi ya nchi yake aliitafuta mwenyewe bendera ile ya taifa. Kwa vile, unapoona mahali kuna vijana wanapeperusha bendera za vyama yaweza kuwa na tafsiri ya ama, ni wapenzi wa vyama hivyo, na kuwa wamezitafuta wenyewe, au kuna kada wa chama husika aliyekuja na kugawa bendera hizo kwa vijana hao.

Ndio, tunahitaji kufanya jitihada za kuwafanya watu wetu waipende nchi yao waliyozaliwa, kutoka ndani ya mioyo yao. Na moja ya jitihada hizo ni kuwapa maarifa yatakayowawezesha kujitambua, kujiamini na kuthubutu.

Maggid,
Iringa.
0788 111 765.

Mjengwa Blog::Habari,Picha,Matangazo
Mawazo mazuri, ila punguza kupersonalize blog yako. Tunajua ni ya kwako, lakini habari zingine kama kueleza safari zako, unelala kwa nani, amekupa chakula gani, huyu ni nani na mnahusiana naye vp, zinatuboa tunaotegemea blog kupata habari. Hilo tu.
 
Mawazo mazuri, ila punguza kupersonalize blog yako. Tunajua ni ya kwako, lakini habari zingine kama kueleza safari zako, unelala kwa nani, amekupa chakula gani, huyu ni nani na mnahusiana naye vp, zinatuboa tunaotegemea blog kupata habari. Hilo tu.

Hovyohovyo,

Asante sana.
Hizo taarifa za nimelala kwa nani, nimekula nini zimekujaje hapa? Mengine ya kwenye blogu ni ya kwenye blogu. Wanaonifuatilia kwenye blogu huwa wanajua imetokea wapi. Maana, mengine ya kwenye blogu yakifika hapa ni kuwachanganya wajao hapa. Yabaki huko huko Mjengwablog!
 
...kuna "mbwiga" mmoja kutoka pande za Singida anaidhalilisha sana hii bendera ya taifa kwani huitumia kufunika mba zilizomjaa shingoni...
 
maggid; nimeshindwa kuona picha hiyo kwa vile inaelekea kuwa website yako ime-expire. Ukishamliza kurenew website usi-update content kwa muda kidogo ili na sisi tupate muda wa kusoma thread hiyo; huwa napenda sana picha zako unazopiga kutoka vijijini.
 
Back
Top Bottom