Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Possibly huwa wanapeperusha bendera ya Zanzibar ikiwa tu Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar yumo ndani ya office kwa wakati huo, na katika kikao cha BARAZA kuu lao alikuwapo.
 
Juzi nilipita mahali Bendera ya Taifa inashushwa...sasa mind yangu ikakumbuka haraka miaka ya zamani tulikatisha kituo cha polisi saa kumi na mbili wanashusha Bendera almanusura turushwe vichura kisa hatukusimama imeadiately....cha ajabu hii ya juzi naona hata polisi wenyewe wanaendelea na shughuli zao ndipo nimeamua kuuliza hii sheria imekuwa zilipendwa ama?
 
Kama watu wanataka uraia wa nchi mbili at per ndo itaheshimiwa kitambaa yenye rangi inayoitwa bendera!!!!!

Mpasuko ni mkubwa ati
 
Tangu ilipogeuzwa kapet bungeni sihangaiki nayo tena.
 
Siku hizi haiheshimiwi kabisa, na kuna baadhi ya ofisi za serikali walinzi wamekuwa wavivu kiasi cha kuamua kutokushusha kabisa hiyo bendera ya taifa, inapepea 24 hrs hakuna kushusha wala kupandisha.
Kuna ofisi nyingine wanashusha hadi saa 1 usiku.
Uzalendo umeshakwisha katika hii nchi,
 
Siku hizi haiheshimiwi kabisa, na kuna baadhi ya ofisi za serikali walinzi wamekuwa wavivu kiasi cha kuamua kutokushusha kabisa hiyo bendera ya taifa, inapepea 24 hrs hakuna kushusha wala kupandisha.
Kuna ofisi nyingine wanashusha hadi saa 1 usiku.
Uzalendo umeshakwisha katika hii nchi,
yaani na kwingine unapita imepaukaaaaaaaaaa mvua,jua twende,,,while zamani tulikuwa tunapigiwa filimbi kabisa kila mtu anasimama inaposhushwa na kupandishwa
 
Tuache utani lakini ule ulikuwa uzalendo wa kipekee uko wapi siku hizi?sijui watoto wetu watajifunza nini...so vitabu vya siasa aka civics vitakuwa vimebadilishwa maana swali hilo lilikuwa halikosekani std III ...
 
Kama Kada fulani wa Chama fulani anavaa bendera ya Taifa shingoni na kupangusia jasho, hapo kuna thamani tena ya bendera?
 
yaani na kwingine unapita imepaukaaaaaaaaaa mvua,jua twende,,,while zamani tulikuwa tunapigiwa filimbi kabisa kila mtu anasimama inaposhushwa na kupandishwa
kweli kabisa, sehemu nyingine zimechanika zipo nusu yaani aibu kweli.
 
Juzi nilipita mahali Bendera ya Taifa inashushwa...sasa mind yangu ikakumbuka haraka miaka ya zamani tulikatisha kituo cha polisi saa kumi na mbili wanashusha Bendera almanusura turushwe vichura kisa hatukusimama imeadiately....cha ajabu hii ya juzi naona hata polisi wenyewe wanaendelea na shughuli zao ndipo nimeamua kuuliza hii sheria imekuwa zilipendwa ama?

mkuu umenikumbusha mbali sana.
kwa hakika siku hizi heshima kwa tunu za taifa imeshuka na kibaya zaidi hakuna wa kuzisimamia. viongozi wenyewe wanachukulia poa. ni mwalimu peke yake aliweza kufanya watu wakaheshimu vitu vinavyotambulisha utaifa wetu.
siku hizi mambo yako tofauti sana na sisi tunaona sawa tu. ila si sawa hata kidogo.
 
watu wa mataifa mengine wanaheshimu sana bendera zao na kuzithamini na kuzipenda. nchini kwetu kuna wengine wanazipenda lakini zengwe nyingi mfano wanamichezo wanaokwenda nje kuwakilisha nchi yetu wamekuwa wakilalamika kunyimwa bendera wakiwa wanakwenda mbali kimashindano,wengine wanazizadharu bila kuchukuliwa hatua dhidi yao. yani hatujielewi kwa kifupi.
 
siku hizi hata nyimbo ya taifa kuwakuta waiwezayo ni mtihani. nakwambia kama kigezo cha uhamiaji haramu kingekuwa kujua kuuimba wimbo wa taifa wachache sana wangekuwa watanzania halisi wengi wangeitwa wahamiaji haramu na kufukuzwa.
ipo haja ya kuhifadhi tunu zetu za taifa kwa vizazi hadi vizazi.
 
Uzalendo umekwisha. Leo hii angalia shule za msingi nyingi ni za binafsi (English Academy) hakuna mchakamchaka, mambo mengi ni ya mataifa ya ulaya tu, unategemea kutakuwa na uzalendo? Yani Tanzania majanga sana.
 
siku hizi hata nyimbo ya taifa kuwakuwa waiwezayo ni mtihani. nakwambia kama kigezo cha uhamiaji haramu kingekuwa kujua kuuimba wimbo wa taifa wachache sana wangekuwa watanzania halisi wengi wangeitwa wahamiaji haramu na kufukuzwa.
ipo haja ya kuhifadhi tunu zetu za taifa kwa vizazi hadi vizazi.
Kwakweli,ni kitendo kinachotakiwa tukiongee namna hii kiuchungu kabisa yaani hiii si jambo la mzaha hata kidogo la wala hatutakiwi kulichanganya na itikadi za vyama hili ni la Utaifa
 
Back
Top Bottom