Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

Rangi za bendera ni ujumbe, uzalendo au urembo?

"wimbo wa taifa la Zambia unafana na wetu kwenye baadhi ya sehemu, ikumbukwe Zambia ni taifa la kikristo" mwisho wa kunukuu.

Umenisoma vibaya ndg au labda kuna kitu unafikiria kuhusu tofauti za kidini, lakini maana yangu ni kwamba tubadili hivi vitu kwa vile ni vya kuiga labda kwa umuhimu wa wakati huo. Lakini kama taifa sasa tuwe huru kutunga wimbo wetu. Kuhusu Zambia ni kweli ni taifa la kikristo yaani linalo-base katika msaafu wa kikristo ambao sisi hatuwezi kuufuata maana nchi yetu haina dini, lakini hoja yangu hapa ilikuwa melody zaidi maana hata tukiimba wimbo wetu nje ya nchi hakuna anayeelewa tunaimba nini lakini atasikia melody kwamba infanana na ya South Africa au Zambia.
 
Umenisoma vibaya ndg au labda
kuna kitu unafikiria kuhusu tofauti za kidini, lakini maana yangu ni
kwamba tubadili hivi vitu kwa vile ni vya kuiga labda kwa umuhimu wa
wakati huo. Lakini kama taifa sasa tuwe huru kutunga wimbo wetu. Kuhusu
Zambia ni kweli ni taifa la kikristo yaani linalo-base katika msaafu wa
kikristo ambao sisi hatuwezi kuufuata maana nchi yetu haina dini, lakini
hoja yangu hapa ilikuwa melody zaidi maana hata tukiimba wimbo wetu nje
ya nchi hakuna anayeelewa tunaimba nini lakini atasikia melody kwamba
infanana na ya South Africa au Zambia.

Jf ni jukwaa huru, sasa sioni sababu ya kuuzunguka mbuyu. Kama hoja yako ni bendera na wimbo, kwanini umeuingiza Ukristo?
 
Wandugu habari za leo.
Jana katika pita pita zangu nilipita makao makuu ya Jeshi la Magereza majira ya saa 12 jioni. Kipyenga kilipulizwa bendera ikaanza kushushwa. Lakini kuna watu walikua wanapita maeneo hayo na kile kipyenga hawakukisiakia kwa hakika na waliendelea na safari zao. Ghafla bin Vuup akaja askari magereza mmoja na kutoa amri wale mabwana waingie ndani ya uzio.

Jamaa walitii na kuanza kuhojiwa kwanini walitembea wakati bendera ilikua inashushwa? Kwa ukarimu sana wale jamaa waliwaambia hawakusikia filimbi ndio mana waliendelea na safari. Mjadala ukawa mzito sana hadi jamaa wakaomba msamaha na kupewa vitisho vingi sana juu ya kutoheshimu bendera. Naomba wana jamvi kufahamishwa juu ya hili je ni lazima bendera ikishushwa au kupandishwa kusimama?Kwanini wanapuliza filimbi??Je kuna sheria yoyote inayoamrisha hili?Au Kwenye katiba? au kuna muongozo wowote upo?Kama nitapa vitu hivi nitafurahi na nitawapelekea wale walinzi wa jana wasome hii kitu na waelimike au nielimike.

Naomba kuwasilisha na kusubiri wanasheria na watu wenye ufahamu mzuri juu ya hili na sio kukariri mambo ya zamani au?
 
Wandugu habari za leo,

Jana katika pita pita zangu nilipita makao makuu ya Jeshi la Magereza majira ya saa 12 jioni. Kipyenga kilipulizwa bendera ikaanza kushushwa.

Lakini kuna watu walikua wanapita maeneo hayo na kile kipyenga hawakukisiakia kwa hakika na waliendelea na safari zao. Ghafla bin Vuup akaja askari magereza mmoja na kutoa amri wale mabwana waingie ndani ya uzio. Jamaa walitii na kuanza kuhojiwa kwanini walitembea wakati bendera ilikua inashushwa?

Kwa ukarimu sana wale jamaa waliwaambia hawakusikia filimbi ndio mana waliendelea na safari. Mjadala ukawa mzito sana hadi jamaa wakaomba msamaha na kupewa vitisho vingi sana juu ya kutoheshimu bendera.

Naomba wana jamvi kufahamishwa juu ya hili je ni lazima bendera ikishushwa au kupandishwa kusimama?

Kwanini wanapuliza filimbi??Je kuna sheria yoyote inayoamrisha hili?Au Kwenye katiba? au kuna muongozo wowote upo?

Kama nitapa vitu hivi nitafurahi na nitawapelekea wale walinzi wa jana wasome hii kitu na waelimike au nielimike. Naomba kuwasilisha na kusubiri wanasheria na watu wenye ufahamu mzuri juu ya hili na sio kukariri mambo ya zamani au la?
 
Naomba wana jamvi kufahamishwa juu ya hili je ni lazima bendera ikishushwa au kupandishwa kusimama?Kwanini wanapuliza filimbi?

Je kuna sheria yoyote inayoamrisha hili? Au Kwenye katiba? au kuna muongozo wowote upo?

Mambo ya kijinga tu.
 
Hahaha inaonekana watanzania mmechoka na nchi yenu. Nataka kujua ni sheria au mazoe tu???Kama sheria tuifahamu wandugu maana naona kama vitu vingine umuhimu uliishia vyama vingi vilipoanza.
 
Zamani ilikuwa bendera huwezi hata kushona shati, Kikwete kabadili, nakumbuka alivyoingia madarakani aliliongea hilo, lakini bado kuna wajinga wanafanya mambo kijinga na kikoloni.

Wasimame wao wako ndani ya uzio wao, wewe unapita nje kwanini usimame? na ikiwa unapita na gari? nalo usimamishe?

Hizo zilikuwa sheria za kikoloni ili watutawale vizuri na sisi tumerithi. Ni ujinga tu.

Nakumbuka zamani tukiingia cinema kwanza inaoneshwa bendera ya taifa na nyimbo ya taifa, wote lazima tusimame, Dah, wametutesa kweli hawa wakoloni mambo leo.

Miafrika Ndivyo Tulivyo - Nyani Ngabu
 
Zamani ilikuwa bendera huwezi hata kushona shati, Kikwete kabadili, nakumbuka alivyoingia madarakani aliliongea hilo, lakini bado kuna wajinga wanafanya mambo kijinga na kikoloni.

Wasimame wao wako ndani ya uzio wao, wewe unapita nje kwanini usimame? na ikiwa unapita na gari? nalo usimamishe?

Hizo zilikuwa sheria za kikoloni ili watutawale vizuri na sisi tumerithi. Ni ujinga tu.

Nakumbuka zamani tukiingia cinema kwanza inaoneshwa bendera ya taifa na nyimbo ya taifa, wote lazima tusimame, Dah, wametutesa kweli hawa wakoloni mambo leo.

Miafrika Ndivyo Tulivyo - Nyani Ngabu

Ah mi najioneaga ushetani tuu,wafanye hayo kambini!
 
Kwel mkuu.ni upuuz wa hali ya juu.bendera utii kwa nch gan hasaa!

Bendera ya nchi kuiheshimu ni sawa, kwa nchi yeyote ile hata iwe si ya nchi yako inabidi uiheshimu kuwa ni bendera ya nchi fulani, lakini si kiwango cha kuiabudu, ikapandishwa watu wasimame, ikishushwa watu wasimame, siioni mantiki yake nje ya makambi yao ya kijeshi.
 
Bendera ya Taifa haitakiwi kushushwa kabisa labda tu kumetokea janga, msiba ama tukio la kusababisha ishushwe nusu mlingoti. Hii mila na utamaduni wa Muingereza hautufai kabisa kwa sababu Taifa letu halilali wala hatuko huru mchana tu. Kwao wao unaposhusha bendera jioni ina maana kwamba kazi zote za serikali zimelala, na hii sii lazima iwe maana yetu sisi kwani bendera inapopepea ni ishara kubwa ya UHURU wetu iwe usiku ama mchana. Bendera ya taifa haishushwi na inaposhushwa ni kwa sababu ambayo kweli filimbi au King'ora kitapigwa ktk janga lilotokea.
 
Miaka Ya Sasa Hivi Bendera Imegeuzwa Leso Ya Kufutia Jasho. Tuwaige Wa Marekani Hakuna Kitu Wanacho Kiheshimu Kama Bendera Ya Taifa. Sisi Huku Bendera Inashushwa Majitu Yanazidi Kutembea Kwa Kwa Kifupi Uzalendo Hakuna.
 
Kwanza bendera ya taifa haina rangi ya njano, pole mwalimu wako wa shule ya msingi alikudanganya!

Ukweli replace rangi ya njano kwa rangi ya dhahabu... tulijua tuna dhahabu na madini mengine tangu miaka hiyo; kamata ukweli huu hapa

au kula kilaini hapa

The National Flag



Ratio length to breadth: Three to two, e.g. 3ft. x 2ft., 6ft. x 4ft. 12ft. x 8ft.
Description: Green - Golden - Black and Blue, having the black center stripe centred on diagonal rising from flag-mast to top edge of the fly, two smaller golden stripes dividing the upper triangle portion which is green and the lower triangle portion which is blue.
Proportions of colours: Black center stripe, centred on diagonal of flag of 6ft. x 4ft., is 13/48 of fly and 13" wide. Golden stripes are each 1/16 of fly and 3" wide.
Colour Code and Significance: B.S. No. 2660: 1955

Black: B.S. No. 9-103 - the People

Green: B.S. No. 0-010 - the Land

Blue: B.S. No. 0-012 - the Adjoining Sea

Golden: B.S. No. 0-002 - the Mineral wealth

Uwiano wa Urefu
Kwa Upana:-

Maelezo:
Tatu kwa mbili, mfano ft.3 x ft.2, ft.6 x ft.4, ft.12 x ft.8
Ina rangi za Kijani, Dhahabu, Nyeusi na Bluu ambapo rangi nyeusi imepita katikati ya bendera kuanzia pembe ya chini kwenye mlingoti na kuishia pembe ya juu kulia. Rangi hii huigawa bendera katika sehemu mbili zenye umbo la pembe tatu. Rangi nyeusi imetenganishwa na pember tatu ya juu yenye rangi ya kijani na pembe tatu ya chini yenye rangi ya bluu kwa mistari miwili midogo yenye rangi ya dhahabu.

Viwango vya rangi na maana zake.
Nyeusi - Kiwango na. 9-103 - Watu

Kijani - Kiwango na. 0-010 - Ardhi

Bluu - Kiwango na. 0-012 - Bahari + Maziwa

Dhahabu - Kiwango na. 0-002 - Madini
Uwiano wa Rangi:
Rangi nyeusi kwa bender ya

Ft.6 x ft.4 ni 13/48 kwenda juu na

Ft.13 upana. Mistari ya dhahabu ni 1/16 kwenda juu na 3" upana kila mmoja.
Tatizo lako ni uelewa, katika kiswahili rangi ya dhahabu ni njano. hivyo wanafunzi wanapofundishwa rangi hawafundishwi kwa mfano wa muonekano wa kitu ila Mwalimu anapotaka kuelezea rangi ieleweke ndipo hutaja kitu ambacho aghalabu huwa na rangi husika.
mfao Rangi nyekundu wanafunzi huambiwa mfano wa rangi nyekundu ni damu, ama nyeusi hutolewa mfano wa masinzi(masizi), nk. hivyo rangi halisi ya bendera yetu sio rangi ya masinzi bali ni nyeusi,ama ya dhahabu bali ni njano, pia si rangi ya majani bali ya kijani pia si rangi ya mbingu bali ya kijani. nafikiri utakuwa umefahamu vizuri.
 
Bendera ya nchi kuiheshimu ni sawa, kwa nchi yeyote ile hata iwe si ya nchi yako inabidi uiheshimu kuwa ni bendera ya nchi fulani, lakini si kiwango cha kuiabudu, ikapandishwa watu wasimame, ikishushwa watu wasimame, siioni mantiki yake nje ya makambi yao ya kijeshi.

kwani bendera ni ya jeshi peke yao? ni bendera ya taifa, hivyo desturi ya kuheshimu bendera yapasa kuwa kwa wananchi wote. Na kuheshimu bendera kunadhihirishwa kwa kufuata itifaki zilizowekwa kwa ajili hiyo na kukubalika katika taifa husika na kwa kufuata misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa kuhusu suala hilo. Vinginevyo tutajuaje kwamba mtu anaheshimu bendera ya taifa lake?
 
Back
Top Bottom