Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,701
- 9,779
Baada ya kumaliza sala za asubuhi naingia zangu kwa mama Pima kupata chai. Nakuwa mteja wa kwanza kufika hapo. Mama Pima anabaki akinikodolea macho! Namuuliza chai vipi? Au hauuzi? Anaamua kunichemshia kikombe kimoja cha chai ya majani machungu na kiporo cha chapati mbili. Nampisha afanye usafi, naamua kulia nje. Watu wote wanapita huku wakinishangaa kama mchawi vile. Naamua kuacha chapati moja na kutokomea zangu
Njiani nakutana na kijana wa kahawa. Katika Hali ya kujuliana Hali, ananipakulia kikombe cha gahawa. Wakati nakitwanga nikiwa sina hili wala lile, anapita mzee moja ndani ya kanzu na kibandiko. Kwa sauti nzito ya koromeo ambalo halijasafishwa anatamka "Astakafuli". Loo! Naamua kuimwaga gahawa ile kisha kurudisha kikombe cha watu
Karibu na maeneo ya nyumbani, nakutana na Mama Grace, huyu huwa ananikubali sana, na anaamini kuwa ipo siku nitamuoa mwanae. " Afadhari nimekuona mwanangu, naomba unipitishie hii mikate nyumbani kwangu. Lahaula, njia nzima na mikate mkononi, zinasikika sauti za taratibu zikitamka "Lione hilo Kobe" Naamua kuvumilia
Njiani nakutana na Aisha chupi kubwa akiwa ndani ya vazi la heshima hadi naogopa kumpa salamu, napitiliza mbele kisha nacheka mwenyewe
Naondoka malangoni mwa mama Grace, nakutana na mabinti wawili ambao huwa wananikubali, nawapa salamu wanaishia kuninunia na kuchongoa midomo. Najaribu kumtangiza mmoja wao, anaishia kunambia, nimekustahi, usiniharibie swaumu.
Kwani salamu imekatazwa katika mfungo huu? Natikisa kichwa kisha nacheka mwenyewe kila nikikumbuka migugumio
Ndipo nafika maeneo ya gheto. Nasikia goma la amapiano linatoka kwenye moja ya chumba cha mule ndani. Kwa sauti ya jazba nauliza, "Ni shaitwani gani anataka kutuharibia swaumu humu ndani?" Afanaleki! Kumbe goma la Amapiano linachomozea chumbani kwangu, ooh! Kumbe sikuzima bufa nilipikuwa naondoka gheto. Kumbe qaswida kwenye flash yangu zilikwisha, ndipo Ngoma za Amapiano zikaunga mstari
Na hili nalo mkalitizame kwa kina
Njiani nakutana na kijana wa kahawa. Katika Hali ya kujuliana Hali, ananipakulia kikombe cha gahawa. Wakati nakitwanga nikiwa sina hili wala lile, anapita mzee moja ndani ya kanzu na kibandiko. Kwa sauti nzito ya koromeo ambalo halijasafishwa anatamka "Astakafuli". Loo! Naamua kuimwaga gahawa ile kisha kurudisha kikombe cha watu
Karibu na maeneo ya nyumbani, nakutana na Mama Grace, huyu huwa ananikubali sana, na anaamini kuwa ipo siku nitamuoa mwanae. " Afadhari nimekuona mwanangu, naomba unipitishie hii mikate nyumbani kwangu. Lahaula, njia nzima na mikate mkononi, zinasikika sauti za taratibu zikitamka "Lione hilo Kobe" Naamua kuvumilia
Njiani nakutana na Aisha chupi kubwa akiwa ndani ya vazi la heshima hadi naogopa kumpa salamu, napitiliza mbele kisha nacheka mwenyewe
Naondoka malangoni mwa mama Grace, nakutana na mabinti wawili ambao huwa wananikubali, nawapa salamu wanaishia kuninunia na kuchongoa midomo. Najaribu kumtangiza mmoja wao, anaishia kunambia, nimekustahi, usiniharibie swaumu.
Kwani salamu imekatazwa katika mfungo huu? Natikisa kichwa kisha nacheka mwenyewe kila nikikumbuka migugumio
Ndipo nafika maeneo ya gheto. Nasikia goma la amapiano linatoka kwenye moja ya chumba cha mule ndani. Kwa sauti ya jazba nauliza, "Ni shaitwani gani anataka kutuharibia swaumu humu ndani?" Afanaleki! Kumbe goma la Amapiano linachomozea chumbani kwangu, ooh! Kumbe sikuzima bufa nilipikuwa naondoka gheto. Kumbe qaswida kwenye flash yangu zilikwisha, ndipo Ngoma za Amapiano zikaunga mstari
Na hili nalo mkalitizame kwa kina