Tindikali
JF-Expert Member
- Mar 26, 2010
- 2,015
- 2,667
Mzee, hujatutendea haki, hujarudisha heshima tuliyokupa.
The biggest day of your life haiwezi kuwa siku uliyokutana na Rihanna na Michael Jackson... Jamani!
Kwa miaka kumi ukiingia bafuni Mikocheni sisi tunaanza kusimamishwa Kiwalani kujiandaa kukupisha unaenda Airport, ukija msibani na harusini tunasimamisha kusali, kulia, kula, kuongea, mpaka we ukasaini kitabu ukakae chini, umestaafu unatumia jumba la serikali bure, petroli bure, vocha ya simu bure, mlinzi bure, mpishi, karani, dereva, shamba boy, and so forth and so forth and so forth.... Kijana wako na mke wako tumewapa ubunge na uwaziri si kwa lolote la kiuongozi walilofanya kabla ya hapo bali kwa heshima yako wewe.....
Lakini the greatest day of your life ni kukutana na Rihanna!
Hukumbuki hata siku moja uliyolala na amani kwa kupata majawabu ya tatizo moja la Mtanzania? Tanzania tuna shida milioni 60, kila mtu ana msongo, jana umetangazwa mgao wa umeme D'Salaam, kwa hiyo hata kwa Mo Dewji nako wamelala na mikelele ya genereta. Walobaki milioni 59 wamelala na mlo mmoja. Hukumbuki hata siku ulioapishwa Rais wetu? Basi ungevunga kwa kutaja siku uliyomuoa Salma, manake nae kakufumbia macho kwa makandokando kibao! Unampaisha Rihanna and your wife is sitting right next to you!
Halafu huna noma unasema ulikutana na Michael Jackson hotelini Spain ukiwa Waziri wa Madini. Hoteli pendwa ya Michael Jackson akiwa Spain ilikuwa ni WESTIN PALACE MADRID, jina lake lingine ni "the icon of luxury!"
Waziri na Rais wa nchi ambayo wasafiri tunasimamishwa vichakani "kuchimba dawa" kwa saab hatuna rest areas zenye vyoo njiani, unatumia viji tozo vyetu kukodi hoteli anayofikia Michael Jackson! Jamani! Na sijui kampuni gani la Spain ulilileta lije kutupiga makinikia..... Msalie Mtume!
Waafrika, nani atatuokoa????