A
Anonymous
Guest
➤ Sisi ni Watumishi wa Umma Wastaafu tuliokuwa tunafanyia kazi vikosi mbalimbali vya Jeshi, tuliajiriwa kila mtu na CV namba yake na kila mtu alipewa barua ya kuajiriwa pia kila Mwajiriwa alikuwa na C/NO yake ya kupatia Mshahara kutoka Hazina (Pay Slip tunazo).
➤ Tukiwa katika ajira tulikuwa tunapandishwa Vyeo na pia tukapewa barua za kuthibitishwa kazini.
➤ Pamoja na hayo tulifanya kazi katika mazingira magumu, miaka ya mwanzo tulipoanza kazi tulikuwa tunapewa ‘unform’, Viatu na Pesa na Likizo.
➤ Kuanzia Miaka ya 1998 mambo yakabadilika tukawa hatupewi tena, ikawa inapita hadi miaka mitatu au minne ndio mnapewa tena ya mwaka mmoja.
➤ Kabla ya kustaafu tuliandika barua kuomba tupatiwe haki hizo lakini mpaka leo (Agosti 11, 2023) hatujajibiwa.
Baadhi yetu tulikuwa katika Mifuko ya NPF, tukahamishiwa NSSF baadaye tukahamishiwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).
➤ Mfano kuna Mtumishi ambaye ametumikia miezi 495 lakini kwenye malipo akapewa miezi 272, kisha miezi 223 iliyosalia haijulikani malipo yake yamepotelea wapi, hata alipouliza hakupata majibu ya kueleweka zaidi ya kuambiwa amuulize Mwajiri wake.
➤ Muda wa Kustaafu ulipofika tukawekwa kwenye kikokotoo, pesa tulizojiwekea kwenye Mifuko ya Hifadhi tukakuta zimekatwa, tukapewa nusu ya kile kilichokuwa tumechangia.
➤ Tulipohoji mbona pesa zetu zimekatwa tukajibiwa kuwa ‘ndizo mtakazo kuwa mnalipwa kwa mwezi’. Yote tumevumilia lakini maisha yanazidi kuwa magumu.
➤ Wakati tumelipwa malipo pungufu kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia malipo ya Kiinua Mgongo hatujapata kabisa, tulipouliza tukaambiwa hatutapewa, tulipohoji tukaambiwa ni maelekezo kutoka juu, kwamba hatutakiwi kulipwa na Hazina.
➤ Tumeenda kwa Afisa Utumishi ili atuandalie malipo ya Kiinua Mgongo tukaambiwa hatupaswi kulipwa kiinua mgongo kwa kuwa sisi ni vibarua.
➤ Tunapatwa na mshangao wa majibu hayo, tukamuuliza Afisa Utumishi wetu kuwa ‘mbona tulikuwa tunapanda vyeo na Pay Slip tunazo’, akatujibu ‘tusihangaike hii ndio amri imetolewa’.
➤ Cha kushangaza waliopewa barua za kutokulipwa ni wachache zinazoonyesha hawastahili kulipwa Kiinua Mgongo, tukahoji mbona wengine hawajapewa hizo barua, wala hatujajulishwa, tulijibiwa tufuate barua walizotumiwa wenzetu.
➤ Tumebaki na mshangao wala hatujui hatima yetu.
➤ Tumefanya jitihada nyingi za kukutana na Waziri wa Ulinzi kupitia wasaidizi wake lakini imeshindikana.
➤ Tulipotaka kulalamika kwenye Vyombo vya Habari, wakasema masuala yetu hayatolewi kwenye Vyombo vya Habari.
➤ Aprili 2023 tulikutana na Mbunge mmoja, akaahidi kutusaidia kutukutanisha na Waziri wa Ulinzi lakini tangu wakati huo mchakato haujafanikiwa, tukijulishwa kuwa ratiba za Waziri zinambana.
➤ Wastaafu tuko wengi kuanzia wa Mwaka 2019.
➤ Wastaafu wenzetu wa miaka ya nyuma walilipwa vizuri kwenye Mifuko ya Hifadhi na kiinua mgongo wakapewa, leo sisi tunaambiwa vibarua Je? Kibarua anapata mshahara wa Hazina na anapandishwa cheo na kuthibitishwa kazini?
➤ Tunapewa majibu ya mdomo, kinachoumiza zaidi ni kuwa wakati wa kuajiriwa tulipewa barua, leo tunajibiwa mdomoni tu kwamba sisi ni vibarua, ukiuliza zaidi wanasema kuna wenzetu wachache wametumiwa barua, hivyo wengine wote tufuate kile kilichoandikwa katika barua za wenzetu wachache, hii si sawa.
➤ Tunaomba huruma yako kuna Watumishi wa Umma waliumwa maradhi mbalimbali wakiwa kazini mfano, TB, HIV na Corona hawakulipwa chochote na muda wa kustaafu umefika walivumilia yote hayo walijua watafika mwisho wa ajira yao watalipwa, leo wanaambiwa hawapaswi kulipwa kiinua mgongo je, hii ni haki?
➤ Mheshimiwa Rais, kwa nafasi yako tunaomba utusaidie; maisha yetu sasa yamekuwa magumu kwa mtihani huu tulioupata.
➤ Tukiwa katika ajira tulikuwa tunapandishwa Vyeo na pia tukapewa barua za kuthibitishwa kazini.
➤ Pamoja na hayo tulifanya kazi katika mazingira magumu, miaka ya mwanzo tulipoanza kazi tulikuwa tunapewa ‘unform’, Viatu na Pesa na Likizo.
➤ Kuanzia Miaka ya 1998 mambo yakabadilika tukawa hatupewi tena, ikawa inapita hadi miaka mitatu au minne ndio mnapewa tena ya mwaka mmoja.
➤ Kabla ya kustaafu tuliandika barua kuomba tupatiwe haki hizo lakini mpaka leo (Agosti 11, 2023) hatujajibiwa.
Baadhi yetu tulikuwa katika Mifuko ya NPF, tukahamishiwa NSSF baadaye tukahamishiwa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).
➤ Mfano kuna Mtumishi ambaye ametumikia miezi 495 lakini kwenye malipo akapewa miezi 272, kisha miezi 223 iliyosalia haijulikani malipo yake yamepotelea wapi, hata alipouliza hakupata majibu ya kueleweka zaidi ya kuambiwa amuulize Mwajiri wake.
➤ Muda wa Kustaafu ulipofika tukawekwa kwenye kikokotoo, pesa tulizojiwekea kwenye Mifuko ya Hifadhi tukakuta zimekatwa, tukapewa nusu ya kile kilichokuwa tumechangia.
➤ Tulipohoji mbona pesa zetu zimekatwa tukajibiwa kuwa ‘ndizo mtakazo kuwa mnalipwa kwa mwezi’. Yote tumevumilia lakini maisha yanazidi kuwa magumu.
➤ Wakati tumelipwa malipo pungufu kutoka katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pia malipo ya Kiinua Mgongo hatujapata kabisa, tulipouliza tukaambiwa hatutapewa, tulipohoji tukaambiwa ni maelekezo kutoka juu, kwamba hatutakiwi kulipwa na Hazina.
➤ Tumeenda kwa Afisa Utumishi ili atuandalie malipo ya Kiinua Mgongo tukaambiwa hatupaswi kulipwa kiinua mgongo kwa kuwa sisi ni vibarua.
➤ Tunapatwa na mshangao wa majibu hayo, tukamuuliza Afisa Utumishi wetu kuwa ‘mbona tulikuwa tunapanda vyeo na Pay Slip tunazo’, akatujibu ‘tusihangaike hii ndio amri imetolewa’.
➤ Cha kushangaza waliopewa barua za kutokulipwa ni wachache zinazoonyesha hawastahili kulipwa Kiinua Mgongo, tukahoji mbona wengine hawajapewa hizo barua, wala hatujajulishwa, tulijibiwa tufuate barua walizotumiwa wenzetu.
➤ Tumebaki na mshangao wala hatujui hatima yetu.
➤ Tumefanya jitihada nyingi za kukutana na Waziri wa Ulinzi kupitia wasaidizi wake lakini imeshindikana.
➤ Tulipotaka kulalamika kwenye Vyombo vya Habari, wakasema masuala yetu hayatolewi kwenye Vyombo vya Habari.
➤ Aprili 2023 tulikutana na Mbunge mmoja, akaahidi kutusaidia kutukutanisha na Waziri wa Ulinzi lakini tangu wakati huo mchakato haujafanikiwa, tukijulishwa kuwa ratiba za Waziri zinambana.
➤ Wastaafu tuko wengi kuanzia wa Mwaka 2019.
➤ Wastaafu wenzetu wa miaka ya nyuma walilipwa vizuri kwenye Mifuko ya Hifadhi na kiinua mgongo wakapewa, leo sisi tunaambiwa vibarua Je? Kibarua anapata mshahara wa Hazina na anapandishwa cheo na kuthibitishwa kazini?
➤ Tunapewa majibu ya mdomo, kinachoumiza zaidi ni kuwa wakati wa kuajiriwa tulipewa barua, leo tunajibiwa mdomoni tu kwamba sisi ni vibarua, ukiuliza zaidi wanasema kuna wenzetu wachache wametumiwa barua, hivyo wengine wote tufuate kile kilichoandikwa katika barua za wenzetu wachache, hii si sawa.
➤ Tunaomba huruma yako kuna Watumishi wa Umma waliumwa maradhi mbalimbali wakiwa kazini mfano, TB, HIV na Corona hawakulipwa chochote na muda wa kustaafu umefika walivumilia yote hayo walijua watafika mwisho wa ajira yao watalipwa, leo wanaambiwa hawapaswi kulipwa kiinua mgongo je, hii ni haki?
➤ Mheshimiwa Rais, kwa nafasi yako tunaomba utusaidie; maisha yetu sasa yamekuwa magumu kwa mtihani huu tulioupata.