Tujionee kwanza haya maajabu ya Kikokotoo kwa Watumishi wa Umma

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Jan 24, 2019
28,388
81,849
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30. Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 kama mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa kupitia mshahara wake kwa miaka yote hiyo 30+), basi atapatiwa kiasi cha shilingi milioni 33 tu. Na kiasi kinachobakia analipwa kila mwisho wa mwezi kwa muda wa miaka 12! Ikitokea mstaafu akafariki wakati wowote ule baada tu ya kustaafu, na hicho kiasi nacho kinakomea hapo hapo (Wizi wa mchana huu 🤭)
Halafu kichekesho zaidi ni kwamba hiki kikokotoo ni kwa baadhi tu ya Watumishi wa umma! Mfano walimu, Manesi, Maafisa ugani, nk.

Ukija kwa Vigogo wa ngazi za juu, mfano Wabunge; eti wenyewe hawahusiki na hiki kikokotoo! (Ona ubaguzi na upendeleo wa wazi huu 🤭) Ingawa na wenyewe eti ni watumishi wa umma!! Yaani wenyewe kila baada ya miaka 5 ya Ubunge wao, wanapatiwa mafao yao yote yanayokadiriwa kuwa kiasi cha shilingi milioni 250 za Kitanzania!

Ukija kwa vigogo wengine wa juu zaidi; mfano Rais, Makamu, Waziri Mkuu, Spika, na sasa wake wa hao vigogo; ikitokea wamestaafu! Wanapewa mafao yao yote! Na kila mwezi wanalipwa mshahara wa 80% kama ule wa Kigogo aliyeko madarakani kwa wakati huo kwa maisha yake yote! (Ubaguzi mwingine huu 🤭)

Swali la kujiuliza!! Kwa nini serikali mnawafanyia wafanyakazi wenu uonevu na wizi wa mchana kiasi hiki?

Mkiulizwa, mnatoa sababu za kipuuzi tu; eti wafanyakazi wakipewa hela zao zote kwa mkupuo wanaishia kuzitapanya na kutapeliwa, na mwisho wa siku wanakuwa masikini!! Sasa hao wafanyakazi wastaafu wakizitapanya hizo hela zao, nyinyi mnapata athari gani? Je, waliwaomba muwatunzie kupitia hicho kikokotoo chenu cha wizi?

Na kama mnaona ni muhimu kufanya hivyo, kwa nini msifanye mpaka kwa Wabunge? Je, ni kwa mini msitoe uhuru kwa Wastaafu kuchagua kama wanataka kupewa 33% pekee, au mafao yao yote?

Binafsi nimeandika haya malalamiko baada ya kushuhudia wastaafu fulani hivi niliopanda nao daladala sehemu fulani, wakilalamika kwa uchungu baada ya kulipwa mafao kiduchu kwa mfumo wenu huu kandamizi wa 33%.

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30! Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 ka mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa otoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
Ni maumivu na dhuluma tu ndio imelengwa hapo. Sio kumsaidia mstaafu.
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30! Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 ka mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa a mfumo wenu huu kandamizi wa 33%.

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
Daah ila kuna vitu vinaumiza!!
Mama ajiangalie hili.
 
Unaambiwa Mtumishi wa uuma wa ngazi ya chini aliyefanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 30! Anapostaafu analipwa 33% tu ya mafao yake.

Yaani kama mtumishi hiyo wa umma alistahili kupata milioni 100 kama mafao (kumbuka hii ni pesa yake halali aliyokatwa

Ushauri wangu kwa serikali; rejesheni mara moja kikokotoo cha zamani. Acheni kuwadhulumu wastaafu pesa zao.
Wewe huna elimu ya kikokotoo. Kikokotoo ni kizuri sana. Imagine anayelipwa mil 1,300,000 kwa mwezi anakuja kupokea 46 mil kama lumpsum, na bado kila mwezi atapata kama 500k, hivi huyu mtu akiamua kuiwekeza hiyo 46m kwenye duka au mifugo si atatengeneza kama laki tano zingine ukijumlisha anapata kama mil moja, compare na wakati wa ajira ana pungukiwa hela kidogo tu. Na hapo anakuwa na uhakika na cashflow yake.
 
Wewe idiot huna elimu ya kikokotoo, ni mbumbu na lijinga. Kikokotoo ni kizuri sana. Imagine anayelipwa mil 1,300,000 kwa mwezi anakuja kupokea 46 mil kama lumpsum, na bado kila mwezi atapata kama 500k, hivi huyu mtu akiamua kuiwekeza hiyo 46m kwenye duka au mifugo si atatengeneza kama laki tano zingine ukijumlisha anapata kama mil moja, compare na wakati wa ajira ana pungukiwa hela kidogo tu. Na hapo anakuwa na uhakika na cashflow yake.
Usimtukane. Kikotoo cha zamani mtu akistaafu mfano hai alilipwa milioni 150 kwa mkupuo kwa mtu aliyekuwa na mshagara mil karibu 2 kwa nwezi na amefanyakazi muda usiopungua miaka 30 na anendelea kulipwa laki 8 kila mwezi kwa maisha yake yote sio kwa miaka 12 tu baada ya kustaafu. Baada ya miaka 12 huyo mstaafu ataaga dunia kwa kukosa maisha. Ikumbukwe wengi wa wastaafu hutmia pesa ya mkupuo kujenga nyumba na kulipia ada za watoto wanakuwa vyuoni. Bila shaka hawezi kuanza biashara kwani hata wafanyabiashara kwa umri huo huwa wanawarithisha watoto biashara kama hufahamu hilo.
 
Usimtukane. Kikotoo cha zamani mtu akistaafu mfano hai alilipwa milioni 150 kwa mkupuo kwa mtu aliyekuwa na mshagara mil karibu 2 kwa nwezi na amefanyakazi muda usiopungua miaka 30 na anendelea kulipwa laki 8 kila mwezi kwa maisha yake yote sio kwa miaka 12 tu baada ya kustaafu. Baada ya miaka 12 huyo mstaafu ataaga dunia kwa kukosa maisha. Ikumbukwe wengi wa wastaafu hutmia pesa ya mkupuo kujenga nyumba na kulipia ada za watoto wanakuwa vyuoni. Bila shaka hawezi kuanza biashara kwani hata wafanyabiashara kwa umri huo huwa wanawarithisha watoto biashara kama hufahamu hilo.
Acha uongo, mfano ma prof vyuoni walipata mpaka mil 30 tu. Kwa ufupi kila mfuko ulikuwa na fomula yake, ila kwa sasa inatoa fursa sawa. Nimemtukana kwa sababu ni mjinga anapotosha watu. Kikokotoo cha sasa kinamuwezesha mstaafu kuishi bila wasiwasi kwa sababu monthly pension ni kubwa na mstaafu akiiwekeza vizuri lumpsum kwenye miradi mbali mbali inamlipa vizuri hata kama ikitokea lumpsum imeisha anaweza kuishi vizuri. Mleta maada aacha uzuzu
 
Acha uongo, mfano ma prof vyuoni walipata mpaka mil 30 tu. Kwa ufupi kila mfumo ulikuwa na fomula yake, ila kwa sasa inatoa fursa sawa. Nimemtukana kwa sababu ni mjinga anapotosha watu. Kikokotoo cha sasa kinamuwezesha mstaafu kuishi bila wasiwasi kwa sababu monthly pension ni kubwa na mstaafu akiiwekeza vizuri lumpsum kwenye miradi mbali mbali inamlipa vizuri hata kama ikitokea lumpsum imeisha anaweza kuishi vizuri. Mleta maada aacha uzuzu
Mbona kwa kikokotoo cha zamani alipata lumpsum kubwa na bado akaendelea kupata monthly pension kubwa kulinganisha na sasa, rudisheni kikokotoo cha zamani acheni huu unyonyaji.​
 
Back
Top Bottom