Rais Samia usilalamike, unachokisikia ndio kinasemwa nchi nzima, kubali tu yaishe!

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,148
Leo kwa mara ya kwanza Rais Samia amekuja hadharani na kukiri wazi kuwa anaongoza serikali iliyogawanyika vibaya, amezungukwa na wasaidizi wanao mhujumu wazi wazi na yuko kwenye vita kali ya kuupambania urais wake kwa hali na mali. Hali ni tete mnoo kwake, na hatakubali!

Bila kumumunya maneno, wacha tuuseme ukweli ili kumsaidia Rais Samia popote alipo na ikibidi utafute njia ya kutokea.

Kwanza niweke wazi jambo moja kubwa na muhimu, kwa sasa Rais Samia amepoteza uungwaji mkono kutoka makundi yote muhimu ya kijamii na kisiasa, yaani umechokwa. Hili halina ubishi na halihitaji takafari yote yote kubwa.

Kitendo cha mama Samia kuja hadharani na kukiri kuwa 'wenzake wanamzunguka' hivyo hatakubali! Hapo tunaona picha kubwa moja tu, maji yamezidi unga na mama Samia anahitaji msaada ili avuke.

Sasa kuna jambo moja kubwa pekee linaloweza kumuokoa mama Samia mahali alipo, hana ujanja inabidi alikimbilie. Kwa ufupi, jambo hilo ni;

Kutafuta muafaka wa kitaifa ili kuweza kuiunganisha nchi iliyoparaganyika vibaya kisiasa. Kama Samia hataweza kukaa na kumaliza tofauti zake na kundi kubwa la wafuasi wa Magufuli (sukuma gang) au wapinzani (hususani Chadema) basi ajue hawezi kutoboa. Hayo ndio makundi yenye nguvu kwenye siasa za Tanzania kwa sasa, na kwa sasa yote mawili kwa pamoja (pasipo kuongozwa na mtu yoyote) yanasema wazi wazi kuwa mama Samia hafai, hatoshei kwenye kiti cha urais na hayamtaki tena. Huo ni uasi wa kisiasa.

Wakati ukuta, na majuto ni mjukuu, wenye hekima wameshaelewa!
 
Ningelipata nafasi ya kumshauri Mama neno moja tu, ningemshauri ahamishie alichokifanya Karume Jr, afanye kampeni ya muafaka wa kitaifa, serikali ya umoja wa kitaifa, katiba ibadilishwe kuwapatia room wapinzani.

In that case, CCM itajihakikishia kubaki na wapinzani watajihakikishia nafasi ya ushiriki kwenye serikali.

Kuongoza watanganyika ni rahisi sana, coz wengi wao wanalilia maslahi tu! Agawe keki ya taifa kwa wote.
 
Uzuri wa watz huwa hawajali nani yuko madarakani na ni wa chama gani, wao wanachojali ni maisha yao yaende tuu.

Uzuri wa watz hawaandamani road ila huo msusio watakaokupa utajuta mwenyewe, utapigwa vita ya kidiplomasia ndani kwa ndani mpaka ukome.

Sasa mama walimuingiza chaka kwenye haya mambo:


1. Tozo za miamala
2. Kuwafurusha wamachinga
3. Mfumuko wa bei unaopanda kila mwezi hasa mafuta
4. Kubwa kuliko ni kesi ya ugaidi ya FAM, ambayo hata darasa la 7 anaona "hapa hamna kitu".
5. Kuendelea kufanya kazi na 90% ya awamu iliyopita.


Hayo mambo juu yasiposawazishwa 2025 % ya kushinda ni <20% hata atumie goli la mkono.
 
Uzuri wa watz huwa hawajali nani yuko madarakani na ni wa chama gani, wao wanachojali ni maisha yao yaende tuu.

Uzuri wa watz hawaandamani road ila huo msusio watakaokupa utajuta mwenyewe, utapigwa vita ya kidiplomasia ndani kwa ndani mpaka ukome.

Sasa mama walimuingiza chaka kwenye haya mambo:


1. Tozo za miamala
2. Kuwafurusha wamachinga
3. Mfumuko wa bei unaopanda kila mwezi hasa mafuta
4. Kubwa kuliko ni kesi ya ugaidi ya FAM, ambayo hata darasa la 7 anaona "hapa hamna kitu".
5. Kuendelea kufanya kazi na 90% ya awamu iliyopita.


Hayo mambo juu yasiposawazishwa 2025 % ya kushinda ni <20% hata atumie goli la mkono.
Mnapokosea ni ile kusema ati asifanye kazi na watu wa Maguguli.I can tell you hapo mnakosea sana na mnataka kumwangusha.Wabunge wote waliyopo ni wa Magufuli.sasa unaposema ati asifanye kazi na watu wamagufuli what do you mean ?Hivi wakitaka kumwangusha si ni kupitisha azimio kule bugeni kuwa hawana Imani na Rais?

What is so wrong akifanya kazi na watu wa Magufuli? Guys acheni kumpotosha rais wetu.Na akifanya vita na watu wa Magufuli vita hii itamshinda vibaya sana.Yawezekana kuna mahara JPM alikosea lakini makosa yake ni 5% ya mabaya yake compared to 95 % ya mazuri aliyoifanyia nchi hii.She better be careful na watu wa Magufuli. Mnapokosea etu watu wa Magufuli ni wasukuma.you are 100% wrong.

Hata wabunge wanaojifanya kuwa wanamchukia JPM wakati yeye ndiye aliyewapitisha na kuwanadi kwa waanchi,nao mwisho wao 2025.Nawashauri wafanye kazi kwa kufuata ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020 ,mambo mengini hayana faida kwa taifa letu.

Mama ukifanya vita na watu wa Magufuli iko siku watakurushia bomu la shutuma hutapona walahi.
 
Mi sioni kigumu hapo,ushauri wangu ni kuwa tu achangamshe yale waliyoyaanzisha awamu ya 5 kwani inaonekana kama kuna kupungua kwa speed kidogo,otherwise she is still on right track,lastly asiwe mvivu kumfyatua mtu ambaye anahisi kutokwenda na speed yake hii itamsaidia sana,itajenga discipline...
 
Mama sijui anamlalamikia nani ikiwa aliyetoka ni ccm, na nyuma nyuma yake walikuwapo ccm.

Atulie tuu miaka yake iishe waje wengine wale keki ya taifa. Maana kila akizichanga karata zake anaona kabisa ushawishi wake ni mdogo kuelekea 2025.

Kama yeye anajiamini atembed bila biti ya ccm aone kama kutoboa kupo.
 
Uzuri wa watz huwa hawajali nani yuko madarakani na ni wa chama gani, wao wanachojali ni maisha yao yaende tuu.

Uzuri wa watz hawaandamani road ila huo msusio watakaokupa utajuta mwenyewe, utapigwa vita ya kidiplomasia ndani kwa ndani mpaka ukome.

Sasa mama walimuingiza chaka kwenye haya mambo:


1. Tozo za miamala
2. Kuwafurusha wamachinga
3. Mfumuko wa bei unaopanda kila mwezi hasa mafuta
4. Kubwa kuliko ni kesi ya ugaidi ya FAM, ambayo hata darasa la 7 anaona "hapa hamna kitu".
5. Kuendelea kufanya kazi na 90% ya awamu iliyopita.


Hayo mambo juu yasiposawazishwa 2025 % ya kushinda ni <20% hata atumie goli la mkono.
Umesema uongo sana. Eti watanzania hawajali nani yuko madarakani na CHAMA gani!! Lini tulipata Rais kutoka nje ya ccm hata tujue watanzania hawajali ni wa Chama gani?
 
Back
Top Bottom