Rais Samia Amewatetemesha Watanzania

Rais Samia Amewatetemesha Watanzania

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
39,280
Reaction score
25,361
Ndugu zangu Watanzania,

Ni kishindo, ni gumzo mtaani, ni kila mtu na neno lake, ni kila mtu na uchambuzi wake, ni kila mtu na mtizamo wake. Nchi imesimama, nchi imetetemeka, nchi imepiga saluti kwa Rais Samia, Watanzania wanatetemeka. Lakini Taifa ni Salama na watanzania ni Salama salimini. Ni uteuzi na utenguzi wa aina yake uliofanywa na Rais wetu na Jemedari wetu mpendwa na kipenzi cha watanzania katika namna iliyozima habari zote kuanzia za michezo mpaka siasa, watu wamekesha macho mitandaoni utafikiri kengele au filimbi ya hatari imepigwa katikati ya makazi ya watu.Tangia uteuzi na utenguzi ulipotoka mitandaoni kwote kumetekwa na Rais Samia.

Kwa kweli Rais Samia ameisapraizi Tanzania Katika wakati ambao watanzania walikuwa wapo Bize na habari za Simba na Yanga lakini ghafla habari zikabadilika na kuzisahau kabisa habari hizo na kubakia na habari moja tu kuu ya Rais Samia na uteuzi pamoja na utenguzi. Ni mama wa Aina yake, ni Rais Wa maamuzi, Ni Rais wa mipango, mikakati, mbinu na medani za kivita. Ni Rais jasusi wa kiwango cha DUNIA, Ni komando wa siasa na mipango mikakati ya kisiasa. Ni Rais aliyeiva na kukamilika katika kila idara, ni Rais aliye mbele ya wakati.

Ni Mwenyekiti imara,hodari, shupavu na madhubuti sana.ni kiongozi na nusu,Rais Samia anabakia kuwa Rais Samia asiye na mfano wake.mpime katika mizani ya aina yoyote ile utamkuta anabakia kuwa yeye kama yeye Mwamba usio tikisika,field Marshall kutoka Tanzania, jasiri muongoza njia, simba wa nyika na shujaa wa Afrika. Ni nahodha imara anayeijuwa vyema bahari anayopita na aina ya mawimbi yake.

Taifa lipo katika mikono Salama ya Daktari Samia Suluhu Hasssan likiwa na afya njema na utulivu mkubwa sana. Huwezi ukatamani kuhama Tanzania ya Rais Samia. Uende wapi? Ukatafute nini kisichopatikana katika ardhi ya Rais Samia? Songa mbele Mama yetu na Rais wetu, Taifa lina imani kubwa sana na wewe.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

IMG-20240315-WA0027.jpg
IMG-20240309-WA0024.jpg
 

Attachments

  • IMG-20240208-WA0009.jpg
    IMG-20240208-WA0009.jpg
    52.8 KB · Views: 6
Yalikuwa makosa tokea mwanzo kumteua Makonda, tupo tuliosema waziwazi.

Ni vyema amerekebisha, japo hakufaa kupewa ofisi ya umma hivyo hakuna jema katika hayo yote mawili ya utenguzi na uteuzi.
Makonda NI mtu anayostahili kuwa gerezani na si vinginevyo.

Nilikuwa namsapoti Sana huyu mama lakini baada ya kuleta hii takataka nimemuona ni walewale tu.
 
Yalikuwa makosa tokea mwanzo kumteua Makonda, tupo tuliosema waziwazi.

Ni vyema amerekebisha, japo hakufaa kupewa ofisi ya umma hivyo hakuna jema katika hayo yote mawili ya utenguzi na uteuzi.
Huyo bado yupo sana lazima alipeleke jahazi hadi 2025
 
Umeandika maneno mengi ila yote hayana maana uzi umejaa tu shupavu, kipenzi chetu, nguli kweli kweli, jasusi , shujaa sijui jemedari

Punguza kuna muda unaweza kumsifu mtu hadi ukawa kero hata mbele ya unaemsifia
 
48 Laws of Power, kitabu muhimu sana, pia kile kinaitwa The Art of war by Sun Tzu, ukivimudu hivi, umemaliza.

Makonda alikuwa anajiona boss wa Chongolo, hajamaliza hata kuzoea ofisi, kapigwa teke la makende
 
Yalikuwa makosa tokea mwanzo kumteua Makonda, tupo tuliosema waziwazi.

Ni vyema amerekebisha, japo hakufaa kupewa ofisi ya umma hivyo hakuna jema katika hayo yote mawili ya utenguzi na uteuzi.
Mheshimiwa Makonda ni mchapakazi sana tena sana na ndio maana anaendelea kuaminiwa na Mheshimiwa Rais na kupewa jukumu la kumsaidia kuongoza jiji la Arusha.jiji la kitalii na la kipekee kabisa na la kimkakati kabisa katika uchumi wetu
 
Pamoja na kulia kwenye kaburi la JPM lakini waaaapi, kaenda mpaka kwenye kaburi la Nyerere, lakini waaapi, mpaka la Mzindakaya lakini waaapi
 
48 Laws of Power, kitabu muhimu sana, pia kile kinaitwa The Art of Law, ukivimudu hivi, umemaliza.

Makonda alikuwa anajiona boss wa Chongolo, hajamaliza hata kuzoea ofisi, kapigwa teke la makende
[/QUOTE
Kwani Mheshimiwa Chongolo si alikuwa nje ya uongozi wakati wa uenezi wa Mheshimiwa Makonda.
 
Mtego wa Makonda unamfanya kila mtu asahau mambo ya msingi, yaani ccm haitoki leo au kesho, wanajua kucheza na akili zetu. Mambo ya CAG na report yake yenye uchafu sehemu zote imefunikwa na teuziya Makonda.

Bado safari yetu ni ndefu.
 
Back
Top Bottom