Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,814
- 11,991
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki kilele cha sikuku ya Nane Nane jijini Mbeya, leo Agosti 8, 2023.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson amesema wakazi wa Mbeya wanaunga mkono uwekezaji unaofanywa na Serikali kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia kampuni ya DP World.
Amesema Jiji la Mbeya ni jiji pekee linalopatikana nyanda za juu kusini, hata hivyo barabara zake sio nzuri hivyo zinapaswa kutazamwa ili kuliongezea hadhi jiji hilo.
Akizungumza kwenye Maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema uzalishaji wa chakula umeongezeka sana msimu huu kwa zaidi ya tani milioni 3. Aidha, kutokana na ruzuku ya dawa za kuua fangasi kwenye Parachichi iliyotolewa na Rais, zao hilo limepanda ubora wake pamoja na kiasi cha uuzaji nje ya nchi.
Mwaka huu wa kilimo, Serikali itatumia zaidi Bilioni 200 kwa ajili ya ruzuku ya mbolea nchini ili kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima.
Waziri Bashe amebainisha pia uwepo wa uvamizi kwenye maeneno ya utafiti wa kilimo, amewaomba wananchi kuacha tabia hiyo na wale waliovamia wanapaswa kuachia maeneo hayo ili yafanye kazi iliyokusudiwa.
Rais Samia anazungumza
Lengo la maadhimisho haya ni kutambua na kuenzi mchango wa sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji pamoja na kutangaza shughuli mbalimbali za uzalishaji pamoja na kutoa fursa ya kutafakari na kutathimini sekta hizi muhimu.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni Vijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula, kwa kutambua umuhimu wa makundi haya, Serikali inaongeza jitihada za makundi haya katika kushiriki shughuli za kilimo.
Serikali haijafunga mipaka kuuza mazao nje ya nchi bali tunataka kuwa na mfumo rasmi ili uwezeshe serikali kujua kiasi cha mazao yanayouzwa nje ya nchi.
Uzoefu wa sasa unasema Magari yanatoka nje ya nchi na kuingia moja kwa moja kwa wakulima, wanalipa kwa fedha za ndani. Haya ni mazao yanayoweza kuuzwa kwa fedha za nje
Taasisi za utafiti zilinde vizuri maeneo yao, na waliomiwa wanapaswa kufahamika ili tatizo liondolewe. Kilimo bila itafiti hatuwezi kwenda vizuri. Tukiachia maeneo haya yachukuliwe tunaenda kudumaza utafiti na uzalishaji wa mbegu.
Niwaombe washirika wetu wa maendeleo bado tunahitaji msaada kwenye sekta ya miundombinu ya umwagiliaji.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson amesema wakazi wa Mbeya wanaunga mkono uwekezaji unaofanywa na Serikali kwenye Bandari ya Dar es Salaam kupitia kampuni ya DP World.
Amesema Jiji la Mbeya ni jiji pekee linalopatikana nyanda za juu kusini, hata hivyo barabara zake sio nzuri hivyo zinapaswa kutazamwa ili kuliongezea hadhi jiji hilo.
Akizungumza kwenye Maadhimisho hayo, Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema uzalishaji wa chakula umeongezeka sana msimu huu kwa zaidi ya tani milioni 3. Aidha, kutokana na ruzuku ya dawa za kuua fangasi kwenye Parachichi iliyotolewa na Rais, zao hilo limepanda ubora wake pamoja na kiasi cha uuzaji nje ya nchi.
Mwaka huu wa kilimo, Serikali itatumia zaidi Bilioni 200 kwa ajili ya ruzuku ya mbolea nchini ili kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima.
Waziri Bashe amebainisha pia uwepo wa uvamizi kwenye maeneno ya utafiti wa kilimo, amewaomba wananchi kuacha tabia hiyo na wale waliovamia wanapaswa kuachia maeneo hayo ili yafanye kazi iliyokusudiwa.
Rais Samia anazungumza
Lengo la maadhimisho haya ni kutambua na kuenzi mchango wa sekta za kilimo, uvuvi na ufugaji pamoja na kutangaza shughuli mbalimbali za uzalishaji pamoja na kutoa fursa ya kutafakari na kutathimini sekta hizi muhimu.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni Vijana na wanawake ni msingi imara wa mifumo endelevu ya chakula, kwa kutambua umuhimu wa makundi haya, Serikali inaongeza jitihada za makundi haya katika kushiriki shughuli za kilimo.
Serikali haijafunga mipaka kuuza mazao nje ya nchi bali tunataka kuwa na mfumo rasmi ili uwezeshe serikali kujua kiasi cha mazao yanayouzwa nje ya nchi.
Uzoefu wa sasa unasema Magari yanatoka nje ya nchi na kuingia moja kwa moja kwa wakulima, wanalipa kwa fedha za ndani. Haya ni mazao yanayoweza kuuzwa kwa fedha za nje
Taasisi za utafiti zilinde vizuri maeneo yao, na waliomiwa wanapaswa kufahamika ili tatizo liondolewe. Kilimo bila itafiti hatuwezi kwenda vizuri. Tukiachia maeneo haya yachukuliwe tunaenda kudumaza utafiti na uzalishaji wa mbegu.
Niwaombe washirika wetu wa maendeleo bado tunahitaji msaada kwenye sekta ya miundombinu ya umwagiliaji.