Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,250
- 113,634
Mjinga mimi nina swali. Ni swali kumhusu Rais Samia [baadhi yenu ni mama yenu].
Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.
Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.
Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.
Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.
Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?
Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.
Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.
Sina takwimu wala taarifa zingine zozote za kuufuta huu ujinga wangu.
Na hata sijui niende wapi ili kuzipata takwimu na taarifa hizo.
Hivyo basi, JamiiForums ndiyo kimbilio langu nitakapo kupata baadhi ya taarifa.
Kwa namna fulani, JF imekuwa ni injini ya utafutaji wa baadhi ya taarifa.
Sasa ni hivi; huyu Rais wetu tokea achukue madaraka, ameshakaa nchini kwa hata mwezi mzima [mmoja] bila kusafiri kwenda nje ya nchi?
Nauliza hivyo kwa sababu naona kama vile kila baada ya wiki mbili hivi huwa ni lazima asafiri kwenda nje ya nchi, jambo ambalo sidhani kama lina tija sana kitaifa.
Wajuzi nijuzeni, tafadhalini sana.