Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,499
Rais Samia ametoa maagizo mazito kwa Lazaro Jacob Twange, Mkurugenzi Mtendaji mpya wa TANESCO, akimtaka kuiongoza taasisi hiyo nyeti kwa weledi, uzalendo, na ufanisi mkubwa. Akimwelekeza rasmi kuanza majukumu, Rais Samia amesema TANESCO ni taasisi ya kimkakati inayohusiana moja kwa moja na usalama wa taifa kwa kuwa umeme ni uti wa mgongo wa uchumi wa nchi.
Amesisitiza kuwa licha ya Tanzania kuwa na uzalishaji wa umeme wa kutosha kupitia miradi mikubwa kama Julius Nyerere Hydropower Project (JNHPP), changamoto kubwa iliyopo ni usambazaji na uambukizaji wa umeme kwenda kanda ya kaskazini na nyanda za juu kusini, hivyo Twange anatakiwa kuhakikisha miradi ya miundombinu ya usambazaji inakamilika kwa wakati.
Soma, Pia: Rais Samia: Umeme ni Usalama wa Taifa, TANESCO isimamie vema; watumishi wa umma wazingatie maadili na uzalendo
Rais pia ametaka Twange asimamie kwa karibu matumizi ya vyanzo mbadala vya nishati ikiwemo gesi na uranium, akieleza kuwa nchi ina akiba kubwa ya uranium Tunduru (takriban tani 58,500) ambayo inaweza kutumika kuzalisha umeme kama ilivyo kwa mataifa mengine. Ameagiza mradi huo uanze mara moja ili Tanzania inufaike na rasilimali hiyo kabla ya kuruhusu usafirishaji nje.
"Ndani ya nchi yetu Mungu ametubariki Uranium kwa muda mrefu sana tuliaminishwa kwamba kutengeneza umeme wa Uranium ni hatari lakini nchi zinazoendelea wanatumia na ndio chazno kikubwa cha umeme wao, sisi tuna low material hapa ndani wanatuambia hatari ili wachote wapeleke kwao wakatengeneze umeme kwao, sasa pamoja na wizara ni vyema kusimamia mradi wetu ule wa Uranium kule Tunduru kwamba sasa wale wawekezaji waanze kazi na tufaidike na rasilimali ile nchini na kama wanataka kuchukua nje wachukue lakini kwanza tufaidike ndani ya nchi nategemea kuna matani mengi tu (makadirio ya sasa hivi kama tani 58,500 za uranium zimelala pale) huu mradi uende na tuanze"
"Umeme wa Nyukilia kama wao wanautumia, tunaweza kuutumia na tukawa na umeme wakutosha nchini lakini na kuuza nchi jirani kama tunavyotaka kuuza sasa kwa Zambia lakini nasi tunanunua kutoka Ethiopia. Sasa tukijitosheleza hatutakwenda kununua"
Amesisitiza kuwa licha ya Tanzania kuwa na uzalishaji wa umeme wa kutosha kupitia miradi mikubwa kama Julius Nyerere Hydropower Project (JNHPP), changamoto kubwa iliyopo ni usambazaji na uambukizaji wa umeme kwenda kanda ya kaskazini na nyanda za juu kusini, hivyo Twange anatakiwa kuhakikisha miradi ya miundombinu ya usambazaji inakamilika kwa wakati.
Soma, Pia: Rais Samia: Umeme ni Usalama wa Taifa, TANESCO isimamie vema; watumishi wa umma wazingatie maadili na uzalendo
Rais pia ametaka Twange asimamie kwa karibu matumizi ya vyanzo mbadala vya nishati ikiwemo gesi na uranium, akieleza kuwa nchi ina akiba kubwa ya uranium Tunduru (takriban tani 58,500) ambayo inaweza kutumika kuzalisha umeme kama ilivyo kwa mataifa mengine. Ameagiza mradi huo uanze mara moja ili Tanzania inufaike na rasilimali hiyo kabla ya kuruhusu usafirishaji nje.
"Ndani ya nchi yetu Mungu ametubariki Uranium kwa muda mrefu sana tuliaminishwa kwamba kutengeneza umeme wa Uranium ni hatari lakini nchi zinazoendelea wanatumia na ndio chazno kikubwa cha umeme wao, sisi tuna low material hapa ndani wanatuambia hatari ili wachote wapeleke kwao wakatengeneze umeme kwao, sasa pamoja na wizara ni vyema kusimamia mradi wetu ule wa Uranium kule Tunduru kwamba sasa wale wawekezaji waanze kazi na tufaidike na rasilimali ile nchini na kama wanataka kuchukua nje wachukue lakini kwanza tufaidike ndani ya nchi nategemea kuna matani mengi tu (makadirio ya sasa hivi kama tani 58,500 za uranium zimelala pale) huu mradi uende na tuanze"
"Umeme wa Nyukilia kama wao wanautumia, tunaweza kuutumia na tukawa na umeme wakutosha nchini lakini na kuuza nchi jirani kama tunavyotaka kuuza sasa kwa Zambia lakini nasi tunanunua kutoka Ethiopia. Sasa tukijitosheleza hatutakwenda kununua"