Rais Samia aitisha kikao cha dharura usiku huu (Mei, 08 2022) Ikulu Dar Es Salaam kujadili mafuta

Hakuwa na dini na epuka sana matapeli watakaokuambia alikuwa na dini.
Unamaanisha alikuwa pagani, hana dini? Ndivyo elimu yako ilipoishia hapo?

kwi kwi kwi teh teh teh. Tutakuelimisha tu, kidogo kidogo utaelewa tu.
 
Unamaanisha alikuwa pagani, hana dini? Ndivyo elimu yako ilipoishia hapo?

kwi kwi kwi teh teh teh. Tutakuelimisha tu, kidogo kidogo utaelewa tu.
😂 eti na ww unacheka. Dini ni yenu wanaadamu yeye hakuwa mfuasi wa dini. Kwani mpagani ni nani? Asokuwa na dini iloanzishwa na binadamu au asiyemjua Mungu muumba mbingu na ardhi??
 
Ishu ni kutokuwa na dini?

Kama kwa neno "udini" unamaanisha ni Uislam, basi "ishu" yote ni Uislam. Nje ya hapo ndipo hakuna "ishu".
Unaudhlilisha uislam unapouweka kwenye utetezi wa hoja zako! Na pengine unatetea kwa nia ya kuendeleza matabaka tu, lakini hata imani na maadili ya dini hiyo, huna!
 
Unaona donge tu. Kama "udini" ni Uislam basi ni lazima uone aibu, kwa kuwa wewe unaabudu binaadam mwenzio kwa kudanganywa na wazungu.
Jamaniiiiiii...aibu jaman.
Mwendazake simpendi laini hivi huko shuleni ulienda kujifunza ujinga???!!!😀
 
Kwetu huku mkoa nimeshangaa bei kupanda kwa sh 300 nzima kwa lita ya Petrol hii sijawahi kuiona tangu nipate ufahamu wa matumizi ya mafuta.
 
Hizo themosi zingetumiwa kama mfano wa kubana matumizi kwenye aina ya magari yanayotumiwa na serikali. Au zina masharti ya mtaalamu maana hazina hadhi ya Ikulu.
 
Nimemsikiliza Waziri Bashe muda mfupi uliopita alipokuwa akichangia hoja ya wizara ya viwanda na uwekezaji, yule kijana ni hazina maana variables zote za kilimo na viwanda kwa hakia viko mdomoni kwake. Nigependa sana awe waziri wetu wa fedha going forward.
Maneno tu hayo. Alisema watu wamepandisha Bei ya mbolea kiholela. Ila Hadi Leo hakuna alichofanya Wala kuchukua hatua na bei bado ipo vilevile
 
Hizo themosi zingetumiwa kama mfano wa kubana matumizi kwenye aina ya magari yanayotumiwa na serikali. Au zina masharti ya mtaalamu maana wazina hadhi ya Ikulu.

Screenshot_20220509-144407.png
 
Maisha yatapanda na yatazidi kupanda MILELE, na wala hayajawahi kuwa RAHISI, tatizo ni kwamba VIONGOZI wa NCHI hawana MIPANGO endelevu ya kuinua PATO la MTU mmoja mmoja. SERIKALI badala ya kupigana kuinua KIPATO cha yule MTANZANIA wa MWISHO kule ambaye anabeba MZIGO wote wa hizi BEI mnahangaika na BEI yenyewe.. Hiyo BEI siyo tatizo, bali NGUVU YA MANUNUZI ya WATANZANIA ndo TATIZO…

Jibu la haya yote ni SEKTA ya KILIMO ambayo mmeamua KUISIGINA kwa MAKUSUDI. Ni kweli kuna UWEKEZAJI wa SEKTA zingine kama UTALII, VIWANDA na MADINI unafanyika ila ni SERIKALI ndo inafaidika ZAIDI kwa KODI moja kwa moja lakini WANANCHI WENGI hawafaidiki moja kwa moja pamoja na ajira chache wanazopata ambazo haziwezi kuinua asilimia kubwa ya wananchi walio na hali duni kimaisha… Kwanini kwa dhati kabisa KILIMO kisifanyiwe MKAKATI kwenye UWEKEZAJI uliotukuka na siyo GERESHA kama zile za KILIMO KWANZA ambayo mpaka leo hatujawahi pewa mrejesho wowote?

KILIMO ndo SEKTA pekee duniani inayotoa ajira kwa WATU WENGI wa HALI zote za kimaisha bila kutegemea MAHALI husika,,,

Nchi yetu ina KANDA nyingi za KILIMO ambazo zinaweza kugawanywa kutokana na ZAO husika, halafu SERIKALI au WAWEKEZAJI wakatengeneza MIUNDOMBINU ya KUMWAGILIA tukaachana na KUTEGEMEA MVUA. MIPANGO mingi mizuri inaozea kwenye makabati na hii inasababishwa na 10% zinazopatikana kwenye UWEKEZAJI wa CHAP CHAP na RAHISI kufanyika kwenye SEKTA nyingine kwakuwa VIONGOZI hawataki kuhangaika na KILIMO ambacho kinaonekana KIGUMU kwenye UWEKEZAJI lakini kina MATUNDA mazuri kwa TAIFA hili..

Leo tunaagiza MAFUTA ya KULA wakati nchi hii ina ardhi ya CHIKICHI, SOYA na ALIZETI.. Tunaagiza SUKARI wakati tuna ardhi ya MIWA,, tunaagiza NGANO wakati tuna ardhi ya kuilima hiyo NGANO.. Hivi vyote vingekuwa vinalimwa kwa UKAMILIFU wake hakika vilio vyote hivi visingelikuwa kwa UKUBWA uliopo.. Kwasababu tusingukuwa tunaagiza bidhaa nyingi nje kwahiyo hela yetu ingekuwa na NGUVU sokoni…

Hivi VIKAO vya Saa 10 usiku mtakaa sana huko tuendako maana VIONGOZI ni wale wale wenye FIKRA zile zile za kuongeza KODI na TOZO kwenye MAFUTA yale yale na VITU vyenye URAHISI wa MALIPO badala ya kutafuta NJIA MBADALA.
 
Wanakaa kujadili nini? Maana sababu wamezitoa kuwa Ni Vita ya Ukraine hivyo basi kwa mujibu wa majibu yao ya awali Kama Serikali, hakuna namna Bei itashuka mpaka Vita iishe.

Wangefanya la maana Kama wangeenda kuzungumza na Putin na Zelensky ili Vita viishe Bei ishuke. Kama kikao hicho kitazaa matunda hii itakua na maana kwamba sio Vita vya Ukraine Ni chanzo Cha kupanda Bei, hivyo watakua walituchukulia poa watz na kuonesha kutokuwa serious.

TIME HEALS ALL WOUNDS
 
Back
Top Bottom