Rais Samia Afanya Mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Reli Tanzania (TRC)

Hujui shirika la anga liko taabani hadi sasa! Nani muhusika na anayepaswa kuhojiwa na kulipa hasara ya billioni 60??

Kulikua kuna sababu gani chanya za kiuchumi kupeleka route ya ndege Chato?

Unaongelea habari za SGR je hufahamu ule ni mkopo wa $1.46 Billion ambao wewe pia utaulipa kwa kodi unazochangia kwenye kuuza au kununua huduma kadhaa?

Je Jiwe alitoa pesa yake mfukoni kufinance ujenzi wa Reli? Alikatwa hata asilimia 5% ya mshahara wake kusaidia ujenzi wa hii reli! ?

Hata angekuwepo Mzee Mwinyi ndio mtawala kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia nchi ilihitaji kuwa na reli ya mwendokasi na bado angetafuta vyanzo vya kusaidia ujenzi na ndio mikopo itakayolipwa na kodi za wananchi ila mwisho wa siku wananchi watafaidika na reli kupitia hizo kodi zao!

Sijawahi kusikia huku kwa wenzetu wanaisifu serikali mara imewajengea daraja mara sijui barabara! Ila kwa kua watanzania wengi bado wapo usingizini wanashindwa kujua zipi ni haki zao na zipi ni hisani.....

Link hii hapo kaone tulivyokopeshwa ila MATAGA mmegeuzwa praise team
Kusifu serikali hakujaandikwa kwenye katiba ni maamuzi ya watu kwa mapenzi yao. JPM alikuwa na nidhamu ya kazi alikuwa na uwezo mkubwa wa kufuatilia masuala anayoanzisha.

Kuna suala la kipaji cha mtu cha kufanya kazi, hayati alikuwa nacho. Kuhamia Dodoma ni suala la tangu 1973 wamepita marais wakilishindwa.

Suala la ndege ni la kiuchumi zaidi wewe umeliongelea kimtaani zaidi. Hasara ilanza mwaka 2016 ikiwa ni bilioni 300 mwaka jana imefikia bilioni 55 kumbuka kuwa inakwenda inashuka na kama sio corona kuipiga dunia sasa hivi isingekuwepo kabisa.

Ni rahisi kumkejeli JPM lakini wapo wengi wanaoujua uwezo wake wa kung'ang'ana mpaka jambo likaweza kufanyika.
 
Ingekuwa bora hako ka hela kangemalizia hiki kipande cha Dar-Moro ili watu angalau waanze kuonja matunda ya SGR kwa safari za Dar-Moro.
Kwa sisi tunaopita pale kihonda mchepuko na kitungwa ndio tunajua adha ya kutokamilika .yaani lami iliwekwa na ikabanduka ndani ya siku tati tu.
Tukasikia tanroad wamemkata mil 300 yule mkandarasi,lakini TANROAD wangekuwa na busara kama wangevijenga badala ya kumsubiria mkandarasi wa SGR amalize sijui lini.
Nimesema busara hayo maeneo ya michepuko yakamilike ili tusipate mavumbi na magari kuzimika au kuharibika kutokana na ubovu kwa karibu miaka 2. Ssasa.
 
Natabiri mama ndio atakuwa hero wa mradi wa ujenzi wa sgr

Jakaya+
Wazo la mradi,upembuzi yakinifu,kutafuta fedha (kuingiza kwenye mfumo wa kodi,mkopo).Utiaji saini mkataba wa awali.

Magufuli+
Utiaji saini mkataba,utekelezaji na ujenzi wa mradi awamu ya kwanza Dar- Moro, Moro- Makutopola

Samia Suluhu
Utekelezaji na Ujenzii wa mradi Morogoro-Dodoma,Dodoma-Isaka, Isaka - Mwanza

Hongera kwao Marais wetu.
 
Kusifu serikali hakujaandikwa kwenye katiba ni maamuzi ya watu kwa mapenzi yao. JPM alikuwa na nidhamu ya kazi alikuwa na uwezo mkubwa wa kufuatilia masuala anayoanzisha.

Kuna suala la kipaji cha mtu cha kufanya kazi, hayati alikuwa nacho. Kuhamia Dodoma ni suala la tangu 1973 wamepita marais wakilishindwa.

Suala la ndege ni la kiuchumi zaidi wewe umeliongelea kimtaani zaidi. Hasara ilanza mwaka 2016 ikiwa ni bilioni 300 mwaka jana imefikia bilioni 55 kumbuka kuwa inakwenda inashuka na kama sio corona kuipiga dunia sasa hivi isingekuwepo kabisa.

Ni rahisi kumkejeli JPM lakini wapo wengi wanaoujua uwezo wake wa kung'ang'ana mpaka jambo likaweza kufanyika.
Endeleeni kumsifia na mkamjengee kaburi vizuri sio kumuwekea mabati kama banda la wanyama
 
Nampongeza sana Mh. Rais Kwa kuhakikisha kuwa mradi huu muhimu sana Kwa Taifa letu unakamilika.
 
Nyie CHADEMA changieni sasa mbona mmekaa kimya na hilo genge lenu la akina Nape,,Kikwete,,Ridhiwani,,,January...

Mnakodoa mimacho
Tunaomba kwanza kabisa tulipwe fidia kuanzia Kimara Hadi Kiluvia kwa kuvunjiwa nyumba zetu bila utu, ndio tukae nanyi tujadili Mambo mengine ili kazi iendelee.
 
Hakika KAZI IENDELEE
Masanja Kadogosa amekiri kuwa wamepokea kiasi cha Tsh bilioni 273 ambazo zinaenda kujenga mradi wa reli SGR kutoka Mwanza hadi Isaka.
Tsh billion 273 ziliacha zimetolewa na mwenda zake kwaajili ya SGR Mwanza- Isaka, kwahivyo Mama ameongeza zingine au!?
 
Back
Top Bottom