nautaka tena
Senior Member
- Jun 29, 2021
- 182
- 213
Viongozi wa hii nchi hivi hawaoni umuhim au ni ushenzi tuu kula like umemaliza uziNafikiri akili sasa zitatukaa vizuri. Tunaposema Katiba Mpya ni muhimu tunamaanisha.
Nchi ni lazima iwe na dira ya maendeleo na si kama hivi sasa inavyoongozwa Kwa kufuata mawazo ya mtu mmoja. Yawe mazuri au ya hovyo. Anaweza kuamua lolote bila kushauriana na yeyote yule. Mbaya zaidi hakuna chombo Chenye Mamlaka ya kuhoji.
Nije kwenye mada. Rais aliamua Bandari ijengwe. Kwa mawazo yake aliona/aliamini ina faida kubwa kwa Taifa na hata kwa mataifa jirani zetu kusini mwa nchi. Makofi alipigiwa na kupongezwa kwa moyo wake wa kizalendo.
Rais aliyefuata akaja na mawazo yake binafsi. Akasema Bandari ile ni wizi na unyonyaji mkubwa kwa Taifa. Mikataba ya hovyo kabisa ni wapumbavu pekee ndio wanaweza kukubaliana na mikataba hii. Nae kapigiwa makofi na kupongezwa kwa moyo wake wa kizalendo ktk kuwatetea raia wa nchi yake.
Kaja mwingine Kwa mbinu mpya eti ile mikataba haikuwa kweli kama tulivyoaminishwa. Hivyo ni muhimu sana kuwa na Bandari ile kwani ina manufaa makubwa Kwa nchi yetu.
Bwawa la Mwl Nyerere tuliambiwa ndiyo mwarobaini wa tatizo la umeme nchini. Kulingana na hali ilivyo kwa sasa wakati wowote tutaambiwa, kulingana na mabadiliko ya tabia ya nchi umeme wa kutegemea maji siyo ishu. Nalo likapigwa pending.
Ni Nani mkweli kati ya hawa wote?? Mimi sina jibu kwani wenye uwezo na mamlaka ya kupitia mikataba yote ni Wabunge.
Bunge lenyewe ndiyo hilo. Limegeuzwa kuwa kichaka cha kupitishia mawazo ya mtu mmoja kwa mgongo wa Serikali.
Bila kuwa na Katiba Mpya itakayompunguzia Rais Mamlaka/Madaraka basi hatutaweza kuwa na Mihimili mitatu itakayoweza kujisimamia yenyewe bila kuingiliana ktk kutekeleza majukumu yao.
Kwanini isijengwe mtwaraHuyu 'Jamaa' alikuwa mwongo na muovu kwa mambo mengi; lakini huwezi ku'dismiss' kila kitu alichokisema kuwa kweli hakikuwepo kwenye mkataba huo.
Hawa wanaochochea sasa hivi bandari ijengwe kwa njia yoyote ile, hawa nao ni waovu kama huyo jamaa kwa njia zao wenyewe, kama siyo waovu zaidi ya Magufuli.
Bandari ya Bagamoyo ni muhimu sana kwa nchi hii, na ni muhimu ijengwe, lakini umuhimu huo ni lazima ulindwe kwa manufaa ya nchi yetu.
Mkuu, ndiyo maana nimesema awali kuwa sisi tuwepesi sana kusahau na tunazowea maumivu kirahisi sana. Wengine tunapojaribu to raise alarm kuhusu michezo inayoendelea tunaambiwa ni MATAGA na SUKUMA GAN.Kwani ni lazima tukubali 'kuigwa'?
"...to sit back and watch...", ndio kukubali kwenyewe huko.
No, we cannot just sit back and watch, we will do everything in our power to stop these ruffians.
Kenya walipigwa kwenye SGR, na sehemu nyingi nyingine, lakini kidogo sasa wameanza nao kutoka tongotongo.
Umesikia wanavyofurumusha 'wapigaji' kwenye shirika lao la umeme "Kenya Power and Transmission co"?
Kinachoshangaza, wakati wao waking'amua jinsi wanavyonyongwa na wawekezaji wa miradi ya ufuaji umeme, sisi ndio kwanza tunachangamkia upigaji huo!
Ina maana sisi hatujifunzi lolote.
Ume usoma mkataba? Mara nyingi kama huna taarifa za kutosha hakuna haja ya kupinga kitu
Mkuu 'chazachaza', nisome unielewe. Naona hujaelewa ninachokieleza mimi.
Nasema hivi: Bandari ya Bagamoyo kwa Tanzania ni muhimu sana, tena sana. Sijaandika popote kwamba ni muhimu ijengwe na mchina kwa masharti anayotaka yeye.
Umuhimu wa hiyo bandari kwa Tanzania ni hapo inapokuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa Tanzania na si vinginevyo.
Kalamu1 ndugu yangu bandari ya Bagamoyo ni uwekezaji wa hovyo kuliko uwekezaji mwingine wowote wa hovyo uliofanyika katika nchi yetu. Ni bora hilo eneo litumike kwa kilimo (kama linafaa kuliko kuwapa hao wachina. Wachina hawaji kucheza makida na wana mkakati mkali sana. Mradi ukiendelea kuna uwezekano mkubwa kabisa vizazi vijavyo vikajaanzisha vita vya kumuondoa mchina. Ni hatari kubwa kabisa kuikabidhi nchi nyingine lango la bandari ya nchi walimiliki. Watafanya chochote wanachotaka, wataingiza na kutoa chochote wanachotaka bila wa kuwauliza. Hata mimi Magufuli bado nasema alikuwa rais mbovu sana lakini kwenye hili la bandari alikuwa sahihi kabisa. Samia anahaha usiku na mchana ili ijengwe lakini atakuja kuingia kwenye rekodi kama rais aliyeuza nchi yetu. Najua wachina wanamwaga fedha nyingi sana kwa kila mtu anayeonekana ni kikwazo kwa sababu wanajua watapakuja kupata faidi kubwa na muda mrefu. Hili jambo linatakiwa lipinngwe kwa nguvu zote.
Point niliyoiona mimi, kwa kuzingatia mada zangu ni pale aliposema kulipa mabilion ya pesa kwamba Wachina wanataka kujenga viwanda Kigamboni, lakini hapo hapo akazungumzia suala la kujenga Bandari Kigamboni...cc Chige a.k.a .........
Yaani kwenye eneo lote kuanzia Tanga hadi Mtwara kusijengwe bandari yoyote. Bandari ya Kilwa tusiiendeleze, Bandari ya Mtwara ambayo itawezesha mikoa ya kusini kupokea mafuta badala yake Dar es Salaam kisha yarudi huko, hatutakiwi kuiendeleza, Barabara kutoka Mtwara hadi Bamba Bay ambayo itatuwezesha kusafirisha mizigo hadi Msumbiji tusiijenge.
Tunaendeleza Bandari ya Bagamoyo. Na bahati mzuri tunashirikiana na Serikali ya China. Tunataka pawe na viwanda vingi katika eneo la Bagamoyo. Tuwe na bandari nzuri na viwanda vingi. Tukishakuwa na viwanda vingi, tutatengeneza ajira, sio tu kwa wana-Bagamoyo bali kwa Watanzania wote. Mchakato wa masuala haya, yalianza kushughulikiwa vizuri sana na Rais wa Awamu ya IV, Mzee Kikwete. Na kazi zinaendelea vizuri. Nataka niwahakikishie kwamba, mpango wa kuendeleza eneo la Bagamoyo, haujabadilishwa. NI lazima tuwe na viwanda vingi, na sasa hivi tupo katika hatua nzuri tu za mwisho ili kusudi masuala haya yaanze kukamilika.
Lakini sasa kwenye ardhi, kule nje ya bandari ambako ndiko walikuwa wanatumia kwa ajili ya kujenga viwanda... kwa sababu ile bandari ilikuwa ya viwanda. Hilo nalo tuelewane. Kuna watu wanakosea na wengine ni watu wakubwa kabisa, wanafikiri bandari ile ilikuwa inakuja kushindana na bandari hii (ya Dar es salaam). Hapana.
Kwani chato wakaazi wake ni wakenya!!?Magufuli Nani kwenye hii nchi, kakataa bandari isijengwe bagamoyo,kaenda kujenga airport kwao isiyo na faida yoyote
🤣🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 Zitto alikuwa anasema jamani tukikataa tutakuwa tumepoteza bahati kubwa na wanakwenda kujenga sehemu nyingine. Mimi nilidhani walishakwenda huko kwingine zamani lakini kila nikisikia bado wanapambana kwa nguvu zote ili ''watusaidie'' ndipo nabaki hoi.Point niliyoiona mimi, kwa kuzingatia mada zangu ni pale aliposema kulipa mabilion ya pesa kwamba Wachina wanataka kujenga viwanda Kigamboni, lakini hapo hapo akazungumzia suala la kujenga Bandari Kigamboni...
Now tell me: NI Wachina gani walitaka kujenga Bandari Kigamboni?!
Au tuseme alikusudia kusema Bagamoyo, na hivyo viwanda of course, ilikuwa ni huko huko Bagamoyo kwenye Bagamoyo Special Economic Zone!!
Kwa mfuatiliaji anafahamu Bagamoyo Special Econmic Zone iliyokuwa inatarajiwa kujengwa viwanda, ni mradi uliokuwa uende pamoja na Ujenzi wa Bandari!! Sasa alitarajia aone viwanda gani wakati Mradi wa Bandari ulipigwa stop?!
On top of that, JPM anasema Wajenzi walitoa masharti ya kipumbavu kwamba:-
Huyo ndo JPM mmoja, but another version of JPM is here:-
Hivi yule aliyesema ni "ni mambo ya kipumbavu kabisa yamefanyika ndo huyo huyo hapo juu, au ni watu wawili tofauti?
Lakini kwa upande mwingine nao, Deusdedit Kakoko, aliyekuwa Mkurugenzi wa Bandari nae anasema kuanzia dakika ya 4 kwamba:-
Sasa nijuze wewe! Kumbe Bandari ya Bagamoyo ilikuwa iwe export port na sio competitor wa bandari zilizopo, na ndo maana hapo hapo palitakiwa kujengwa viwanda!!
Sasa how come tena unatoa masharti ya kutojenga bandari ingine ambazo zisingekuwa competitor?!
Na msikilize hata huyo Kakoko mwenyewe alivyo mwongo! Eti kule Sri Lanka hadi ikatokea vita! Na wengi wamekuwa wakihusisha Bandari ya Hambantonta (ya Sri Lanka) na umafia wa Wachina!!
Sasa ni lini Sri Lanka ilitokea vita inayohusishwa na hiyo bandari?!
Kila anayefuatilia mambo anafahamu vita ambavyo vilidumu Sri Lanka ni vile kati ya Serikali na Tamil Tiger!! Kama nawe ni mfuatiliaji... hivyo vita vilipiganwa lini hadi lini na Bandari ya Hambantonta ilijengwa lini?!
Na miongoni mwa propaganda ambazo zilisambazwa sana Tanzania na wale wale mliokuwa mnawashingilia, ni suala la Wachina kuichukua hiyo Bandari ya Sri Lanka ili kujilipa deni lao! Watu tukasema hapa hizo ni habari za uongo zilizoanzishwa na Trump Administration ili ku-discredit Belt & Road Initiative!!
Mkasema tumenunuliwa!
Hata Wamarekani nao waliingizwa chaka na propaganda za Trump Administration hadi pale Wasomi wa Harvard na John Hopkins University walivyoanza kutilia wasiwasi habari hizo! Ili kupata ukweli wa kile wanachoambiwa na serikali yao, wakaamua kupeleka watu field kufanya research ili kufahamu ukweli!
Abstract ya research husika inasema:-
View attachment 2016615
Hivi mlikuwa mnaambiwaje vile kuhusu Wachina na Bandari ya Sri Lanka?!
Nimeshasema uwe na jioni njema.Huwezi kunijua kwa sababu huna huo uwezo.
Hoja hujibiwa kwa hoja!China unayoisema iliwapa Waingereza miaka 200 kumiliki Hong Kong na ndio ikawa insipiration ya China unayoiona leo. Dubai Bandari yao kubwa ya Kwanza waliwapa wamarekani wajenge na waendeshe kwa miaka 50, leo hii wanashirika linaitwa Dubai Port World na sasa linaendesha Bandari Mbalimbali duniani ikiwemo Marekani mara baada ya kupata uzoefu mkubwa kwa Wamarekani. Ukiwa na mawazo ya kuibiwa kila siku utashindwa hata kufungua genge. Master plan ya Bandari tuandae sisi, wachina watoe hela kulalamike tuanze sisi. Maajabu sana!!
Imekuwa ni jioni mbaya, I am afraid!Nimeshasema uwe na jioni njema.
Bagamoyo ikijengwa bandari ya dar ndo itakuwa By By iwe kwa lazima au kwa hilariKwa sehemu kubwa sana tunakubaliana kati yako na mimi.
Mimi naamini kabisa kwamba bandari ya Bagamoyo ni muhimu sana kwa Tanzania, tatizo pekee lililopo ni, je, itajengwa vipi, na nani na kwa masharti gani.
Kenya wameanza ujenzi wa bandari yao ya Lamu, wao wenyewe. Tayari ghati tatu zitakuwepo pale. Hiyo ni bandari yao. Uwekezaji mwingine wa ziada katika eneo hilo wa miradi mbalimbali, huko wanaalika wawekezaji. Sisi hapa tumekomalia waChina wajenge, kwa masharti magumu wanayotupa sisi. Hapo ndipo penye tatizo.
Nilishauliza humu JF mara kadhaa, lakini sijawahi kujibiwa. Hivi haiwezekani mradi huo wa Bagamoyo ikawa 'Joint Venture' kati yetu na wawekezaji, huku mradi ukiwa bado ni wa Tanzania? Mbona bomba la mafuta ya Uganda tuna umiliki kule, kwa nini isiwezekane kwenye mradi huu wa Bagamoyo.
Niseme wazi, kama wewe ulivyo na wasiwasi na Mchina, nami nina wasiwasi mkubwa sana juu yake. Huyu ndiye anayekuja kuwa mkuu wa mabepari duniani kote, tena anakiu kubwa sana, ukichukulia na wingi wa wananchi wake. Mahusiano ya huyu na nchi atakazokuwa ameziingilia utakuwa ni tofauti sana na hawa mabepari tuliowazoea kwa miaka mingi.
Samia lazima awe makini sana, vinginevyo ninakubaliana na uliyoandika juu yake.
Mkuu, unazungumzia miaka 200 na miaka 50 kwa Hong Kong na Dubai mtawalia. Je, unaweza kutueleza covenants/ terms ambazo zilikuwemo kwenye mikataba ya uwekezaji huko Hong Kong na Dubai?China unayoisema iliwapa Waingereza miaka 200 kumiliki Hong Kong na ndio ikawa insipiration ya China unayoiona leo. Dubai Bandari yao kubwa ya Kwanza waliwapa wamarekani wajenge na waendeshe kwa miaka 50, leo hii wanashirika linaitwa Dubai Port World na sasa linaendesha Bandari Mbalimbali duniani ikiwemo Marekani mara baada ya kupata uzoefu mkubwa kwa Wamarekani. Ukiwa na mawazo ya kuibiwa kila siku utashindwa hata kufungua genge. Master plan ya Bandari tuandae sisi, wachina watoe hela kulalamike tuanze sisi. Maajabu sana!!
Kazi iendelee ,tupigwe tu tushazoeaSerikali ni ile ile
Ndo unavyojidanganya kwamba wanapambana, sio?!🤣🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 Zitto alikuwa anasema jamani tukikataa tutakuwa tumepoteza bahati kubwa na wanakwenda kujenga sehemu nyingine. Mimi nilidhani walishakwenda huko kwingine zamani lakini kila nikisikia bado wanapambana kwa nguvu zote ili ''watusaidie'' ndipo nabaki hoi.
The Chinese port operator is also developing a $3.5 billion Djibouti International Free Trade Zone, expected to be Africa’s largest free-trade zone. Other investment projects backed by Chinese firms include port facilities, a railway, and two airports, as well as a pipeline to supply water from neighboring Ethiopia.
Most of China’s imports derive from the Middle East and Angola. Currently, eighty percent of China’s oil has to pass through the Strait of Malacca, a narrow stretch of water between the Indonesian island of Sumatra and the Malay Peninsula. With Singapore, a major US ally that frequently participates in US naval drills, located at the mouth of the strait’s eastern opening, the Strait of Malacca becomes a natural strategic chokepoint. In the event of a conflict, the Malacca Strait could easily be blocked by a rival nation, cutting off China from crucial energy resources.