tpaul
Platinum Member
- Feb 3, 2008
- 27,181
- 27,781
Sasa huo usalama wa taifa hawataki watu watoe mawazo yao?Pole punguza hasira kuna usala wa taifa humu.
Sasa huo usalama wa taifa hawataki watu watoe mawazo yao?Pole punguza hasira kuna usala wa taifa humu.
Hana wasaidizi? Mwisho watatusahau na waache kutualika matokeo yake mtu ukienda ulaya wazungu wanakuuliza umetokea Nigeria au South Africa? Maana tz hawaijui
Pamoja na hilo la Wakimbizi na Wahamiaji, pia kutakuwa na kikao muhimu sana ambacho kitachukua takribani 70% ya mkutano wote kutokana na umuhimu wake. Huu ni mdahalo unaolenga kuzungumzia malengo ya maendeleo endelevu na nafasi yetu katika kusukuma mabadiliko ya kufikia malengo hayo.
Sasa huo usalama wa taifa hawataki watu watoe mawazo yao?
hizo pesa za safari kile ki gulf stream kinajazwa wese halafu yule maza anaenda na kurudi!!!!! hamna matumizi yaliyobanwa hapo!!!! jason bourne aliwahi kusema hapa ili ndege ya rais iende irudi kadirio la chini la mafuta ni milioni 250 mpaka milioni 300 maximum!!! sasa hapo angeenda baba mwenye nyumba angepungukiwa nini?Tuzoeee tu..mpaka 2020.... Kuna nini huko UN si kuongea tu na kurudi home. Bora hizo pesa za safari ajenge skuli bukoba
Toka nje ya box la ujinga. Hiyo mikopo mnayochukua kila siku kutoka IMF na World Bank unadhani inadondoka hewani? Ngoja wavute handbrakes kidogo ndo utaelewa kilichomtoa kanga manyoya.Huo mkutano una faida gani kwa Tanzania ? UNAIINGIZIA nchi pato la shilingi ngapi mwisho wa mkutano?
Kasome Taratibu za UN Ndo ujue wanaotakiwa kuhudhuria hvo vkao ndo urudi tena hapa ukiwa na uelewa Sahihi bro.HONGERA HN.RAIS,KAZI HII NI YA WIZARA YA MAMBO YA NJE.../
AENDE WAZIRI NA WASAIDIZI 2 TU,KUIWAKILISHA TANZANIA.
Mshana jr NINAKUUNGA mkono, awamu hii tuna tatizo kubwa sana katika mahusiano ya kimataifa, unajua mikutano kama hii huzaa matunda kwani maraisi hutumia kuonana na wenzao kando ya mikutano na kuzungumzia mahusiano ya kibiasha na yenye tija kwa nchi zao.Sio kweli kabisa tetemeko linatumika kama sababu tuu
Ninamshaka na kilichopo kichwani mwako, unafikiri kila anaekwenda UN anazungumza kiingereza?Tatizo sio kwenda au kutokwenda tatizo ni sababu iliyotolewa.
UN Sio lazima kwenda ila ni muhimu kwenda, Tanzania sio kisiwa.
Tunaanza kupata shaka kile kinachosemwa mitandaoni kuwa 'Kirengesa' tatizo, Waumini wa hili la Lugha tunazidi kuongezeka.
UN hatuendi, AU hatuendi, SADC hatuendi .... Hivi ni mkutano gani wenye faida kwa Tanzania!!? Au ni mikutano ya CCM tu ndiyo yenye faida kwa Taifa hili? Wajuzi mtueleweshe!!Aliyekuwa anaenda bila kukosa mahudhurio mlimuita Vasco Dagama. Anayebana matumizi....mnamponda humu. WaTanzania tunataka nini?
By the way UN New York.....ni kitu gani kipya anahitaji kwenda kufanya? maana maximum time ya kuongea kwa kila Kiongozi ni dakika tano! Na mara nyingi kumbi zinakuwa empty! wakubwa wameshaondoka.
WATANZANIA tuamke...Tanzania ya Magufuli ni ukurasa mwingine. You either adapt or perish!
Toka nje ya box la ujinga. Hiyo mikopo mayochukua kila siku kutoka IMF na World Bank unadhani inadondoka hewani? Ngoja wavute handbrakes kidogo ndo utaelewa kilichomtoa kanga manyoya.
Kwahiyo haendi kisa mdahalo au anashughulikia wahanga wa tetemeko?Ebo yaani 70% ya mkutano wote ni mdahalo!!! (debate) !!!! Tunarudi kule kule sekondary kwenye debates (midahalo)!!! Yaani Raisi mzima aende safari yote na gharama zote aende kuhudhuria mdahalo (debate)???
Hata watu wazima UN huwa wanafanya midahalo (debates) nilifikiri vitu hivyo ni kwa ajili ya watoto wa sekondari tu.Hata maraisi MWEEEE!!! Hivi Raisi anaweza shuka uwanja wa ndege wa nchi yake bila aibu akasema nilikuwa umoja wa mataifa kwenye mdahalo!!!! LOOOOO.Magufuli heri haendi yuko sahihi.
Angeenda mngekuwa wa kwanza kulaumu kwanini anasafiri wakati huku nyumbani kuna tetemeko lililosababisha maafa makubwa. Kuongoza hii nchi ni kazi sana.Sio kweli kabisa tetemeko linatumika kama sababu tuu