Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Acheni kuchemsha na ushamba wa kusafiri kwani pesa za Bush zingekuja kwa JK kupiga simu????. Mnafikiria wawekezaji na misaada mtaletewa tu Raisi inabidi asafiri tena zaidi ya anavyosafiri sasa. Hakuna kitu cha maana kukaa ofisini kila siku wakati wakekezaji wanatoka nje.
 
Acheni kuchemsha na ushamba wa kusafiri kwani pesa za Bush zingekuja kwa JK kupiga simu????. Mnafikiria wawekezaji na misaada mtaletewa tu Raisi inabidi asafiri tena zaidi ya anavyosafiri sasa. Hakuna kitu cha maana kukaa ofisini kila siku wakati wakekezaji wanatoka nje.



WRONG:

Hakuna investtor anayekwenda kuinvest kwenye nchi kisa rais kaenda DOWNING STREET au WHITE HOUSE

ma investors wanaenda kuinvest kwenye nchi ambayo

TAX CODES ZINAELEWEKA

KUTOA CONTAINER BANDARINI HAKUCHUKUI MWEZI MZIMA

MAOFISA WA KODI WANAJUA TOFAUTI KATI YA APPLE MONITOR NA KIFAA CHA SINEMA

in short kama mazingira kuleta FDI kwenye nchi mazuri yatakuja tuuu na wanasiasa kazi yao iwe ni kuondoa URASIMU

HIVI UNAJUA KWA NINI WATANZANIA WANATUMIA BANDARI YA MOMBASA badala ya Dar?

kwa sababu ukishusha container lako kenya huwa unaliondoa on the same day tofauti na ule upuuzi unaoendelea Dar
 
Acheni kuchemsha na ushamba wa kusafiri kwani pesa za Bush zingekuja kwa JK kupiga simu????. Mnafikiria wawekezaji na misaada mtaletewa tu Raisi inabidi asafiri tena zaidi ya anavyosafiri sasa. Hakuna kitu cha maana kukaa ofisini kila siku wakati wakekezaji wanatoka nje.

Wale wale!
Nishachoka kufundisha sasa!
Kaaazi kweli kweli!
 
Rais Kikwete anatarajiwa kwenda China kuanzia tarehe 10-15 kwa ziara ya mwaliko wa Rais wa China Bw. Hu Jintao. Kufuatia hali inayoendelea Tibet yawezekana China inatafuta support ya Tanzania katika mkakati wake wa kuzima mwamko wa Tibet na itafanya hivyo kwa kuingia mikataba ya Nishati, kilimo na viwanda ili Tanzania itoe statement of support au kwa namna moja kuipa baraka Uchina.
 
Ushauri wa bure kwa wataoongozana na JK....wafanya biashara....na serikali mpiganie sana kuwaomba wafanye biashara na kuleta vitu huku africa vyenye ubora wasifanye jalala la ku jaribia bidhaa zao mbovu.......mbona ulaya wanapeleka high quality products?pia waingane mikataba na serikali kuleta wataalam waloiobobea sio wanakuja kupata uzoefuu......ni wazo langu tuu
 
yawezekana huu ndio mwanzo wa ziara zile ndefu ambazo zilikuwa kama sahihi ya JK kwa 2007
 
Alijisemea MWK kuwa huyu ni Vasco da Gama!!From hero in 2005 to zero by 2010!! He is really making a fool out of himself!!Ndugu yako Edward alituletea dili la kutengeneza mvua toka Thailand, sasa na wewe tuletee ajabu lingine la dunia tusilolifahamu toka China!!
 
Ushauri wa bure kwa wataoongozana na JK....wafanya biashara....na serikali mpiganie sana kuwaomba wafanye biashara na kuleta vitu huku africa vyenye ubora wasifanye jalala la ku jaribia bidhaa zao mbovu.......mbona ulaya wanapeleka high quality products?pia waingane mikataba na serikali kuleta wataalam waloiobobea sio wanakuja kupata uzoefuu......ni wazo langu tuu

Sijui umesoma ulivyoandika? Kasi ya TBS ni nini?We unarushia mpira wachina?
 
Ushauri wa bure kwa wataoongozana na JK....wafanya biashara....na serikali mpiganie sana kuwaomba wafanye biashara na kuleta vitu huku africa vyenye ubora wasifanye jalala la ku jaribia bidhaa zao mbovu.......mbona ulaya wanapeleka high quality products?pia waingane mikataba na serikali kuleta wataalam waloiobobea sio wanakuja kupata uzoefuu......ni wazo langu tuu


TATIZO SIO WACHINA TATIZO WAFANYA BIASHARA WETU MAANA WAO WANAENDA NA KUONA VILIVYO BORA NA HIVYO vilododa na kwa kupenda faida kubwa huchukua vilivyododa.


nilipokuwa india nikienda madukani wahindi wanavyojua waafrika ni watu wa feki hunipa viata vile feki vya bei rahisi, basi nikimwambi nnata ngozi huingia ndani na kunitolea ila hunambia bei huwa kubwa.


sasa hili ni tatizo letu ukiambiwa kiatu dola 150 unaanza kupiga mahesabu na kutafuta cha dola 60 au chini zaidi
 
Mkuu Mwanakijiji,

Kwa hili la safari za Rais kwa hakika nakuona kwamba huna hoja ya maana badala ya bifu tu!!!


Sounds interesting, lakini mkuu hebu fafanua kidogo hapa ili na wengine tuelewa hasa hilo "bifu" ambalo MKJJ analo na haya maziara!
 
....UWANJA WETU MPYA VIPI MBONA UMEKWAMA ....MAANA UMEBAKIA KUWEKWA TARTAN RUNWAY NA UZIO FULANI..JUST 5%..COMPLETION REMAIN TANGU MWAKA 2006 HADI LEO ..KILA SIKU WANASOGEZA UFUNGUZI MBELE..MKAPA KALA NGOMBE ..YAANI JK MKIA UTAMSHINDA???

PIA AONGEE NA WACHINA IKIBIDI AWAOMBE WAMALIZIE AWAMU YA PILI YA ULE UWANJA KAMA MSAADA..AWAMU YA PILI ITAHISISHA INDOOR SPORTS FACILITIES..IE swimming pool,basketball,hockey..ets..kama akiweza kufanya na awamu ya pili utakuwa FULL OLYMPIC STADIUM..
 
SIO CHINA TU, ushishangae kusikia baada ya wiki 2 na baada ya miezi miwili tena unasikia ameenda Japan, smart President working while he is overseas.
 
Sijui umesoma ulivyoandika? Kasi ya TBS ni nini?We unarushia mpira wachina?


Kuna wakati kwenye habari kulikuwa na taarifa ya condom fupi kutoka uchina......... china ndio wenyewe kwa mavitu si mnajua hata vitu vya ulaya vingi vinatengenezwa uchina? ni pesa yako tu maana wafanya biashara wanawajua Wabongo kwa kuomba kupunguziwa hata vitu mambavyo vipo kwenye SALE kwa kulijua hilo wakaamua kuwa wanaleta bidhaa hafifu za bei muswano! Mpo hapo wandugu?
 
Ni kweli kwa asilimia fulani kwani wachina wao wenyewe huwa wanasema sisi waafrica sio soko lao wanalolitegemea ila ni moja ya masupplier wakubwa wa row material kwa bei cheap,sasa kwa upande wa marketing huwa tunakeep profitable customer hii inamaanisha kuwa kwa mchina kukuingiza bogi sio hatari kwake kwani anajua wewe sio tegemezi kubwa sana katika soko lake ila atakung'ang'ania katika uhusiano ili uweze kumletea malighafi,kwa mfano kwa wale mnaofuatilia mutajua kuwa China anachukua Copper toka Zambia na Brazil ila ya Zambia ni cheap mno na wakati huohuo anachukua migogo toka kongo(DRC) yote hayo anategemea bandari ya DSM sasa utaona ni jinsi gani kwake yeye Tanzania muhimu. Hawa jamaa ni wajanja sana kwani wanakuja na Viji Scholarship mchwala then kwakuwa viongozi wetu huwa wanaona ni bora Scholarship kuliko Scholarship bora na hulizika kwa idadi ya wanafunzi na hapo mchina hupeta kiulaini kabisa.
Kwa upande wa pili wa shilingi,ni kweli kuwa hawa jamaa kutokana na Technolojia yao kuna bidhaa nyingi huwa ni bomu sasa kwa zile ambazo ni swafi ina maana nyingi wamechukua baadhi ya parts toka nje so kama wanatengeneza na kuuza huwa bei ni kubwa kimtindo kwa watu wa kwetu kuafford so ndio maana wafanyabiashara wetu huwa wanaishia kuchukua bidhaa za bei chee,sasa kinachotokea ni kuwa kipindi wanataka hizo chee mchina nae anakubambikia hapohapo.
La muhimu ni kuwa kama wafanyabiashara wetu watakuwa makini nina imani wanaweza kupata bidhaa nzuri kwa bei yenye nafuu(sio ya kutupa) na sidhani kama kuna matatizo kwani sisi tulio huku ndio tunajua nini ni nini.
 
..leo jioni hii rais anatua india ambako juzi pia makamu wa rais alipita hapo kutalii ....atakuwa india kwa siku tatu.....
 
Jamani naomba nimtetee Mtalii wetu maarufu.

Hii Safari ilipangwa na Wachina kumkaribisha kwenye mkutano fulani mkubwa kuhusu msuala ya biashara na maendeleo na mahusiano kati ya China na Africa. Kama sijakosea sana Kikwete ndio mgeni rasmi na atafungua huo mkutano.

Labda mjiulize Wachina wameona nini kwa Tanzania watupe heshima kubwa kiasi hicho? je wamegundua kuwa viongozi wetu na watendaji wa Serikali ni wepesi wa kulewa mvinyo na kusaini mikataba harakaharaka ambayo ni bei poa kwa wawekezaji?

Kingine ambacho najiuliza kwa ziara hii, ni kusikia kuwa Musharaf na jamaa wa Chile watakuwapo huko. Je China wanajenga hoja gani ya kimataifa?

Jamani tunataka Tanzania itangazwe kwa ari, kasi na nguvu mpya. Nendeni Galilaya Karpenaumu na pande zote za dunia mtangaze Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu, njoo danganya unauwezo na pesa kuwa mwekezaji, tutakupa mkataba wa kudumu na kukulipa capacity charge nono, tutakusamehe kodi na ushuru jinsi upendavyo!

Angalia sana mradi mipya ya uwekezaji utasikia Pakistan na Chile ndio wawekezaji wapya!
 
Kikwete nenda, nenda hata huko Uchina nenda!!!

Nitakuwa wa ajabu nikianza kupinga ziara za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nje ya Nchi kwani hiyo ni moja kati ya kazi zake. Ninamtakia mafanikio katika ziara hizo.

Bidhaa duni:
Kawaida bidhaa kabla hazijazalishwa kinachoangaliwa ni akina nani watakuwa walengwa wa bidhaa hizo. China kama nchi iliyoendelea inazalisha bidhaa nyingi kwa ajili ya masoko yake mbalimbali duniani ikiwemo masoko ya third world. Ubora wa bidhaa huendana pia na gharama za uzalishaji, kadri bidhaa inavyokuwa bora na gharama za uzalishaji ndivyo zinavyokuwa juu zaidi. Kwa mfano, kuna Furniture ambazo huzalishwa China za high quality zinauzwa USA kwa takribani $4000, je unadhani hiyo furniture mfanya biashara anayenunua toka China atafikiria kuileta kuiuza Tanzania? Jibu ni kwamba itabidi atafute Furniture ambayo wateja wake wanaweza kuafford na si vinginevyo. Bidhaa za ubora wa hali ya juu zipo isipokuwa wateja Tanzania hawapo wa kukidhi mahitaji ya kibiashara.
 
Back
Top Bottom