Rais Kikwete na safari za nje

Rais Kikwete na safari za nje

Sitaki kuamini kwamba kila mtu anaweza kuwa waziri katika nchi hii, lakini kwa hoja ya Waziri Meghji, ambaye ni miongoni mwa mawaziri wazoefu katika baraza letu, inatosha kabisa kutia shaka kwamba kumbe yeyote anaweza kuteuliwa kuwa waziri, kama uwaziri unamaanisha kuwapo kwa mtu tu ambaye atasaini lolote atakaloambiwa na anaowaamini.

Mkuu Zalendo,

Heshima mbele mkuu, hapa hakuna cha kuongeza ila ubarikiwe tu!
 
Mkuu FM ES
Ni wazi kuwa kwa nchi yenye volume ya uchumi na biashara kama Afrika Kusini, naweza kusema Mbeki kusafiri mara 27 kwa mwaka ni mara chache sana, kama safari zake zinakuwa za kikazi. Na kwa nchi kama Tanzania ambayo uchumi wala biashara zake hata kwa Afrika Mashiriki havina impact kubwa naona kusafiri mara 21 ni kwingi sana. Sijui ni kigezo gani alichotumia Mh Membe kuwafananisha marais hawa wawili,
Na hatujui who foots the bill when RSA President travels, maana kwenye nchi za wenzetu watu huwa hawapandi ndege ya rais au kusafiri na rais kwa pesa za umma!
 
maneo yte sasa ni Davos lakini hadi muda huu Jakaya yuko mtaani anasogoa .Je huko Davos si maeneo yake ? Si muhimu yeye kuwepo au kamtuma Membe ?
 
Kwa mtaji wa mambo yanavyoenda sasa si JK wala Membe, wote ajali kubwa tu.
 
Uchumi wa South Afrika, unajua ni mkubwa kuliko hata wa Portugal, tena mara mbili, sasa leo unawezaje kuilinganisha na bongo in terms of safari za marais wake? Mbona kuna watu hapa JF walituambia kuwa Membe ni kichwa sana tena wakaanzisha mpaka topics hapa za kumpamba what happened? au!
 
Uchumi wa South Afrika, unajua ni mkubwa kuliko hata wa Portugal, tena mara mbili, sasa leo unawezaje kuilinganisha na bongo in terms of safari za marais wake? Mbona kuna watu hapa JF walituambia kuwa Membe ni kichwa sana tena wakaanzisha mpaka topics hapa za kumpamba what happened? au!

Ebwana kuna kipindi niiinyaka Thesis yake aliyoandika Membe huko John Hopkins...huwezi kuamini kama huyo mtu leo kawa waziri

lakini ndio Africa

all in all mara mia wangempa yule Mahiga kuliko Membe lakini Membe ni mwansiasa hivyo mahiga sidhani kama angeweza hizi Fitna anazoendeleza huyu Membe

Nitaitafuta ile link yenye thesis yake niliisevu kwenye bookmarks yangu

just bear with me
 
1. SA is the 20th Largest economy in the world- wako mbele ya nchi nyingi za Ulaya!

Sasa Tz- hata watu wetu hatuwezi kuwalisha kwa chakula na SA ni tofauti!!!

2. Kwani Membe ndo anaandaliwa kuwa Raisi 2015? manake ukiangalia BWM na JK wote waliwahii huwa Mawaziri wa Foreign kabla ya kuteuliwa na CCM kugombea! Na pia anatoka ktk kabila ndogo kama JK, AHM, BWM na JKN!

I dont think he is the kind of presidential material we want kwani vile naona ana uwezo kidogo!

We wait and see!!
 
Makinda ndiye anasimamia asubuhi hii Kikao cha muda huu . Hoja ni kumpongeza JK kwa kuwa Rais wa AU. Sifa zinamwagwa na Malecelea asema mnao lia na safari za JK mlie tu lakini yeye lazioma atasafiri sana for AU purpose .

Malecela kamaliza kuzoza na sasa Zungu anaitwa kutoa hoja then watu wahojiwe .

Sasa Safari halali mnasemaje ?
 
Huyo mzee kweli amechoka, maana hizo ni kejeli na pia ushabiki amabao nisingeutegemea kwa heshima aliyonayo. Anyway hivyo ndivyo viongozi wa kibongo walivyo. Huwa hawajali kabisa matamshi yao maana huwa haina effect!!!!!!!!
 
Lunyungu,Vipi kuhusu suala la Ripoti ya Richmond?

Mzee Malecela naye ana Mambo,Sasa safari wapi na wapi na utendaji wa Mwenyekiti wa AU.
Je safari ndio zinapunguza matatizo yanayoikabili afrika?
Je akisafiri sana machafuko yaliyoko Somalia na Sudan yatakwisha?
Je Kenya patakuwa Salama?
Je Maisha Bor yatapatikana kwa safari?

Waache kutufanya Mazuzu.Bila kubadili mfumo wa uongozi katika nchi za Afrika maendeleo yatakuwa magumu.Watu kama Muungwana ni hasara kubwa katika taifa letu.Watu wanakosa pesa ya mikopo ya elimu ya juu then wao kila siku wanapanga safari?

nimesikitiwsha sana na Mzee John.hivi nani ana Kitabu cha Uongozi na Hatma ya Tanzania.Nadhani kuna haja ya kukisambaza kwa watanzania wote na tena hasa wabunge wasio na faida kama mzee Malecele.

Mzee ES naona sasa unaweza kuamini kwamba huu mzee amelewa na mvinyo wa damu ya kijana ya kifisadi ambayo mkewe haitaki kuinywa.au anamkebehi Mkuu wa kaya?

Kuhusu suala la Wabunge kukataa ishu ya Mswaada mpya wa Sekta Ya umeme,Ukiangalia kwa Undani utagundua kuna mgongano wa kimaslahi kama uliotokea wakati Vodacom inaanzishwa,Kuna jambo hapa.Je ni kweli wabgunge hawajatumiwa?Tumsiangalie karamagi kwa jicho moja bali tuangalia on both eyes.

Siku zote watu wa kucheka cheka na wakimya wanaopenda kusifiwa ni watu wabaya sana katika suala linalohusu Rushwa manaa huwa wanafanya mambo yao kwa siri kubwa sana na baadaye kuwachomekea watu.

Ipo siku,siku imekaribia ,siku ambayo watanzania wataujua ukweli wa Ubia wa Urais wa JK.
 
Wameacha kujadili mambo ya maana wamekalia soga na porojo tu na hatimaye session itapita na hakuna la maana watakalo fanya.

Yaani session nzima inajadili kumpongeza JK kwa kuchaguliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa AU? Au ndiyo style ya kupoteza muda ili siku ziishe halafu wasijadili zile report ambazo wanakwepa kuzijadili?
 
Sina hakika kama leo itakuja mbele ya wakuu hawa maana naona ni muswada wa Utalii baada ya kumpongeza na kumwaga sifa kibao kwa JK . Kimiti kaanzia mbali na Malecela akafunga kazi kwa kusema mnao lia na safari basi sasa yuko AU safari zitakuwa zaidi ina maana ujumbe wa JF unawafikia . Mhagama kaongea pumba sana leo .Sijui wale wabunge wako Dunia gani .
 
Sasa hivi Mzee Malecela na Kingunge wakiongea tunapaswa kusikiliza na kusahau. Siasa zao zimepitwa na wakati, na watanzania wa sasa sio wa kudanganywa kwa pilitiki kama alivyojaribu mzee kingunge kwenye issue ya ufisadi.
Wazee wetu wanatakuwa kupumzika na kuondoka kwenye scene kwa kheri na sio kwa vijembe visivyo na maana. Anayosema mzee ukiyapima hata kwa kipimo chochote, hayana maana.
Angesema tunashukuru kwa nchi yetu kupewa nafasi hiyo ambayo tumeipata bure na ambayo ni ceremonial tu!!
 
Usimshangae Malecela, CCM woooote wapo hivyo hivyo, by the way who in CCM said differently not only today but even when BoT saga started inside this very Bunge ? CCM ukusifia hata ujinga unakula, lakini ukisema ukweli utakula mafi yako (Makweta, Ulimwengu, Kombe n.k)
 
Makinda ndiye anasimamia asubuhi hii Kikao cha muda huu . Hoja ni kumpongeza JK kwa kuwa Rais wa AU. Sifa zinamwagwa na Malecelea asema mnao lia na safari za JK mlie tu lakini yeye lazioma atasafiri sana for AU purpose .

Malecela kamaliza kuzoza na

Naungana na Mhe. Malecela katika Kumpongeza Mhe. JK kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa AU.
Aidha napenda kuchukua nafasi hii kumkaribisha Mhe. rais hapa Finland

Kidumu Chama Cha Mapinduzi..
 
Hili Zee litachoka limeshachoka,inbidi likapumzike. Muda wao hawa CCM ndio waelekea ukingoni. Malecela ovyooooooooooooooooooooooooo
 
Back
Top Bottom