Rais kaishiwa pumzi, karudi square one

Rais kaishiwa pumzi, karudi square one

Kila kitu alichodhani atakirekebisha kimeanza kurudia hali yake ya zamani.

Moto wa kupambana na mafisadi ni kama umezimika baada ya kuambiwa mahakama ya mafisadi imekosa kesi, tumerudi palepale.

Wakati anaingia alikuta TRA inakusanya bn 900 hadi tn1, yakaongezeka hadi tn1.5 leo yamerudi kule kule bn 900 sijui ya Nov inawezekana yameshuka zaidi.

Spidi ya kubomoa nyumba zilizojengwa mabondeni na kinyume cha sheria ulianza kwa mkwara ukapiga breki kwa mama Lwakatare, leo tumerudi kule kule.

Machinga ni vurugu mechi, ondoa rudisha ondoa, tatizo halijatatuliwa limebaki palepale.

Tumbua tengua teua mwisho tumeishia kuteua walewale tuliowatumbua hatuja solve kitu tumerudi kule kule.

Mikopo ya wanafunzi sio tu tumerudi tulipokuwa yaani square one bali hata uwezo wa serikali kulipa umepungua kulinganisha na serikali iliyopita.

Serikali imeshindwa hata kuajiri na kupandisha madaraja watumishi wake, ni kama tumerudi square one.

Alipoingia alizuia safari za nje akazuia sikukuu za kitaifa, leo watumishi wanasafiri kama kawaida na juzi tumesherehekea sikukuu ya Uhuru aliyoikataa mwaka jana, mambo yamekuwa business as usual.

Mapigano kati ya wakulima na wafugaji ni kama ndiyo yamezidi, pamoja na ahadi ya serikali yake kutatua kadhia hiyo ni kama tumerudi kule kule.

Kuna mengi ambayo alidhani rahisi kuyafanya yameanza kumshinda mfano, sukari ya Bharesa, pembe za ndovu, madawa ya kulevya, majangili. Nina uhakika anaweza kumaliza muda wake akayacha kama alivyoyakuta.

Naomba kutoa hoja.

Quinine.

Quinine Rais amepewa na wanancchi mandate ya miaka mitano kuongoza nchi na kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM. Ndio kwanza tumemaliza mwaka mmoja, kutoa hukumu kwamba Rais atamaliza muda wake akayaacha kama alivyoyakuta ni upotoshaji or rather wishful thinking.

wakati ni muamuzi sahihi wa kufanikiwa kwa Rais...na wakati huo ni miaka mitano na sio mwaka mmoja. Lakini hata ukiamua kumpima kwa mwaka mmoja, umechagua kuyaacha mambo ya msingi yaliyokwishafanyika yenye manufaa kwa wananchi wengi.

Jambo la kwanza na kubwa lililofanyika ni kutoa ELIMU BURE kuanzia msingi hadi sekondari. usipoangalia jambo hili kwa upana,waweza kudhani ni jambo dogo,lakini ukweli ni kwamba familia zote mijini na vijijini zenye watoto wenye umri wa kwenda shule, sasa wana uhakika wa elimu ya watoto wao katika ngazi hiyo ya msingi.

Eneo jingine ambalo Serikali inachukua hatua ambalo watu wengi hawalizungumzi ni kulipa madeni. Tunaposoma habari kwamba serikali imekopa fedha kujenga barabara, hospitali n.k maana yake ipo siku tutatakiwa kulipa. Serikali ya Awamu ya tano imeingia madarakani katika kipindi ambacho madeni yaliyokopwa miaka ya nyuma yamemature na yanatakiwa kulipwa. Kwa kuweza kulipa madeni hayo ndiko kunakoifanyTanzania iendelee kuaminiwa na mashirika ya fedha ya kimataifa kuendelea kukopeshwa fedha kwa ajiili ya kutekeleza miradi mipya ambayo itawagusa wanachi walio wengi

Kuanza hatua za Kutekeleza miradi yenye tija kwa wananchi wengi. hivi sasa Serikali ipo kwenye hatua ya kupata mkandarasi wa kujenga Reli ya Kati katika Kiwango cha kimataifa. Mradi huu utafungua upya fursa za uchumi kwa wananchi wa dar es salaam, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Kigoma, Mwanza.....Reli itakapojengwa itatoa ajira kwa maelfu ya wanannchi, na itakapokamilika itarahisisha usafirishaji wa mizigo na kupunguza gharama za kufannya biashara kutokana na urahisi iwa usafiri...lakini sio hivyo tu ikikamilika itapungusa kasi ya uharibifu wa barabara zetu ambazo zimejengwa kwa pesa nyingi za walipakodi na mikopo tunayoendelea kuilipia

Kupunguza mianya ya upotevu wa fedha za umma kwa njia ya ukwepaji kodi, malipo hewa (mishahara hewa, wanafunzi hewa, zabuni hewa) pamoja na overpricing/overcharging zilizokuwa zinafanywa kwenye manunuzi ya umma ambayo mwisho wake mzigo ulikuwa unabebwa na walipakodi. Juhudi zilizokwishafanyika zinastahili kuungwa mkono,lakini zaidi ushirikiano wa wananchi wazalendo, wenye nia njema ya kuona maovu yanatoweka unahitajika sana....Rais hawezi kujua kila kitu kinachotokea kila mahala.....anahitaji ushirikiano wa wananchi, anahitaji utendaji bora wa vyombo vyake.....


Mnyonge mnyongeni,haki yake mpeni.....ndani ya muda mfupi tumeona ndege yetu iliyokuwa inachechemea miaka nennda rudi inaruka.....tena ikiwa na ndege mbili mpya tunazomiliki wenyewe. Wapo watu wanabeza mafanikio hayo....pengine ni kwakuwa tumesahau tulikotoka......hivi mnajua ATCL iliwahi kukodikukodisha ndege ya zamani na kulipia mabilioni ya shilingi? leo hii tunamiliki ndege,hatudaiwi na mtu...si jambo la kubeza.


Kwa vyovyote vile, yapo mapungufu na changamoto mbalimbali zilizojitokeza ndani ya mwaka mmoja, lakini hazitoshi kutoa hukumu ya kushindwa kazi wakati kuna mafanikio mengi na muda wa miaka minnne wa kutekeleza zaidi. Tumpe nafasi Rais wetu atekeleze wajibu aliopewa na wananchi ili tutoe verdict yetu vizuri baada ya miaka mitano. pale penye mapungufu tuwe wazalendo kutoa solutions zifanyiwe kazi na sio kupinga tu maana nchi hii ni yetu sote.
 
Mahakama ya mafisadi itafanyaje kazi wakati vibaka wote mmenyooka? Thats the whole point....unapaswa kulalamika ikiwa ufisadi unaendelea huku watuhumiwa hawafikishwi mahakamani
Naomba nikuulize swla ndogo.je hiyo mahakama ya mafisadi inawasuhu mfisadi wapya au hata waliopita.mh.anasema alikuwa serikalin zaid ya miaka 20,hivo ufisadi huu anaujua na mengine yamejitokeza akiwemo.
1:epa
2.;Richmond
3:desi
4,rada
5:esrow
6:lugumi
Kama mnawasubiri wapya basis subirini shetani aje
 
Ni humu humu mlikuwa mnalalamika na issue za bandari na kwengine, leo wametumbuliwa wale tulokuwa tunalalamika bado mnalaumu, Nadhani kuna wengine wametumbuliwa kihaki hasa hata mwanzoni mlikuwa mna msifu, iweje sasa mnakuwa na kigeugeu.

Nadhani tatizo kuna mtu amekimbia amepitiliza hata kwao mkuu. Yani hata kanuni za mchezo hajali ila zinazotoka kichwani mwake ndio zinakuwa zenyewe. Yaani hata hela za wadhamini sasa zinatumika bila mpango uliokubalika ni vululu vululu tu.

Sasa matokeo yake wadhamini wanateseka ndio maana kelele haziishi.

Pamoja na tabia ya kuua mende kwa gobole, inadisturb hadi watoto ndani. Ingawa na mazuri yapo pia, hayaonekani vizuri, mfano ndege wanapanda wangapi pamoja na kwamba inaweza ikawa na faida kiuchumi ikiendeshwa vizuri!?!? What if it fails??

Lakini kubwa kuliko yote, utu. Hata kwa vitu vidogo tu, mfano wakurugenzi wa halmashauri na ma ras angalau watoke kwenye mfumo wa utumishi. Pia utumishi uheshimiwe jamani, kuna kiongozi anatukana watumishi hadharani lakini mkulu anasema jamaa ana support yake %100!!! Hivi vitu ni vidogo ila kwa wengine vinatia hasira mnoo!
 
Kila kitu alichodhani atakirekebisha kimeanza kurudia hali yake ya zamani.

Moto wa kupambana na mafisadi ni kama umezimika baada ya kuambiwa mahakama ya mafisadi imekosa kesi, tumerudi palepale.

Wakati anaingia alikuta TRA inakusanya bn 900 hadi tn1, yakaongezeka hadi tn1.5 leo yamerudi kule kule bn 900 sijui ya Nov inawezekana yameshuka zaidi.

Spidi ya kubomoa nyumba zilizojengwa mabondeni na kinyume cha sheria ulianza kwa mkwara ukapiga breki kwa mama Lwakatare, leo tumerudi kule kule.

Machinga ni vurugu mechi, ondoa rudisha ondoa, tatizo halijatatuliwa limebaki palepale.

Tumbua tengua teua mwisho tumeishia kuteua walewale tuliowatumbua hatuja solve kitu tumerudi kule kule.

Mikopo ya wanafunzi sio tu tumerudi tulipokuwa yaani square one bali hata uwezo wa serikali kulipa umepungua kulinganisha na serikali iliyopita.

Serikali imeshindwa hata kuajiri na kupandisha madaraja watumishi wake, ni kama tumerudi square one.

Alipoingia alizuia safari za nje akazuia sikukuu za kitaifa, leo watumishi wanasafiri kama kawaida na juzi tumesherehekea sikukuu ya Uhuru aliyoikataa mwaka jana, mambo yamekuwa business as usual.

Mapigano kati ya wakulima na wafugaji ni kama ndiyo yamezidi, pamoja na ahadi ya serikali yake kutatua kadhia hiyo ni kama tumerudi kule kule.

Kuna mengi ambayo alidhani rahisi kuyafanya yameanza kumshinda mfano, sukari ya Bharesa, pembe za ndovu, madawa ya kulevya, majangili. Nina uhakika anaweza kumaliza muda wake akayacha kama alivyoyakuta.

Naomba kutoa hoja.

Quinine.

ukifanya nchi kama familia yako ndo matokeo yake

nchi ya kwetu sote
 
Ukiwa na akili ndogo kazi sana
Mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutendaji yaliyofanyika huyaoni au unajitia upofu

Dhana ya kujitegemea pia huioni kbs kwmba ime gain momentum kwa kipindi hiki kifupi

Mianya ya rushwa ilivyopunguzwa kama sio kuzibwa kabisa huoni nalo

Uwahibikaji wa watumishi wa umma pia umefumba macho bado

Bado tuna safari ndefu
Mkuu wafanyakaz wa umma hawapo km unavyojidanganya kwanza wana madai kibao hlf hawajapandishwa madaraja sambamba na mshahara kwa muda sasa,zaidi wanafanya kazi kwa kinyongo na ilimradi aonekane anawajibika lkn ukweli hapana,nadhan kwenye nyanja ya Elimu,Afya majibu utayapata time will tell
 
Nami mwenyewe nakuwa na mashaka na mwenendo wa haya mambo. Kinachonisikitisha zaidi ni kuwa lile kundi la mumiani waliotufikisha hapa wanaonekana kujipanga ili kurejea kwenye madili makubwa na wizi wa makontena!
 
Kwa
Mahakama ya mafisadi itafanyaje kazi wakati vibaka wote mmenyooka? Thats the whole point....unapaswa kulalamika ikiwa ufisadi unaendelea huku watuhumiwa hawafikishwi mahakamani
Kwani ilivyoanzishwa kulikuwa na matarajio ya Ufisadi kushamiri? Ina maana alivyosema atainyoosha Nchi alikuwa anatusanifu wananchi? Kwani majipu aliyotumbua mwanzoni yalikuwa yametendeka away hii? Usituletee hoja za Mwakyembe hapa Kwa kukosa majibu
 
Jamaa alijua anaweza endesha kwa mikwara na biti...chaliii aiseee....
 
Ukiwa na akili ndogo kazi sana
Mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutendaji yaliyofanyika huyaoni au unajitia upofu

Dhana ya kujitegemea pia huioni kbs kwmba ime gain momentum kwa kipindi hiki kifupi

Mianya ya rushwa ilivyopunguzwa kama sio kuzibwa kabisa huoni nalo

Uwahibikaji wa watumishi wa umma pia umefumba macho bado

Bado tuna safari ndefu
Yepi hayo yataje. Hayo mabadiliko ni yepi hayo?

Jikiteni kwenye hoja sio mnatoa toa tu maneno matupu. Yataje hayo mabadiliko ya kimfumo na kiutendaji.
 
Back
Top Bottom