Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Mkuu wa majeshi alishasema,TZ kuna wageni wengi mno serikalini na kwenye vyombo vya usalama,nadhani ndio uhamiaji ikaja na operesheni mjue jirani yako,ila ajabu operesheni yenyewe iko kule instagram na x,mitaani aionekani hapo ndio utajua sisi watanzania uzalendo ni sifuri,admin wa uhamiaji yy anapost tu,mwisho wa mwezi mshahara unaingia 😃utekelezaji hamna
 
Ndugu yangu! Usilo lijua ni Sawa na usiku kiza! TPDF si dhaifa kama unavyodhani, lipo more advance,kuna mengi yamefanyika na yanaendelea kufanyika kimyakimya, kama bado unamtazamo wa jeshi lileee lililopigana vita ya Kagera! Basi unakosea Sanaa,kuna Idadi kubwa ya vijana wenye uwezo wamekuwa walipelekwa urusi kwa mafunzo ya muda mrefu,takriban miaka 6 kwa bechi ya kozi moja,TPDF inafanya kazi zake kwa usiri na umakini mkubwa Sanaa,Tofauti na watu wanavyoifikiria.
Ila mkuu kwa dunia ya sasa kwenye suala la silaha hakuna usiri
 

View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0

General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.

Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.

Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.

Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"

Povu Ruksa, Karibu Sana......

SADC ya sasa imekuwa dhaifu mno ndio maana Kagame anavimba, sio kama enzi za kina Mugabe (Rip) na Dos Santos(Rip) waliomtia adabu yeye na M7.

JokaKuu zitto junior Nguruvi3
 
Hii kauli inaonyesha jinsi gani wamejipanga. Vyombo vya Ulinzi na Usalama viwe macho muda wote
Ishu inakuja wanyarwanda ni wengi sana Tz na wanazaliana sana na hata kama wamezaliwa na kukulia TZ, still wapo royal kwa nchi yao. Kama alivyosemaga mkuu wa majeshi wetu kwamba wapo raia wakigeni serikalini au kwenye taasisi zake na wengine wakiwa wameshika nafasi za kufanya maamuzi, basi hakika anachokisema PK kwamba anauwezo wa kukufata ulipo ni ukweli mtupu.
Lakini naiamini sana Nchi yangu TZ
 
Iliku
Hiyo mikwara tu mkuu,kwa anayejua huyo hapati shida.
Kipindi cha Jakaya alipiga mikwara sana aisee,JAKAYA akampiga mkwara wa askari wa mpakani kwa paredi akaufyata.
Ilikuwa wakati huo!
 
Mkuu wa majeshi alishasema,TZ kuna wageni wengi mno serikalini na kwenye vyombo vya usalama,nadhani ndio uhamiaji ikaja na operesheni mjue jirani yako,ila ajabu operesheni yenyewe iko kule instagram na x,mitaani aionekani hapo ndio utajua sisi watanzania uzalendo ni sifuri,admin wa uhamiaji yy anapost tu,mwisho wa mwezi mshahara unaingia 😃utekelezaji hamna
Tatizo linalotusumbua Tz ni uccm.Hata jambazi akiwa CCM anakuwa Salama.
 
Nyie mmeinvest kwenye wizi na propaganda za kuwasifia wanasiasa lkn hiki kinchi kidogo masikini kinawatukana watu waliokizi maendeleo mpaka idadi ya watu mara mia.

Kuna siku East Afrika tutakuja kulia kisa kuifumbia macho hii migogoro ambayo inawakumba jirani zetu lkn hatuoneshi udhibiti zaidi ya kutegemea wageni wa ulaya watusaidie.

Nina imani hiki kinchi(Rwanda) hakifanyi mambo kwa kukurupuka wala kwa mihemko, bali ni uhalisia, pia nina uhakika kwa Rwanda ilipofika ina intelligence kubwa mpaka huku tusikofikiria, vile vile kina technologia ambazo baadhi yetu bado hatuna na hatuna mipango nazo kwa kujidanganya sisi taifa lenye amani

Ipo siku hii amani fake itawaliza watu na tutaumbuka vibaya sana, nguvu zetu tumeziwekeza ktk siasa chafu za kuuwana, kuchafuana na kupora mali za umma, lkn mambo ya msingi bado tuko nyuma.

Jeshi letu linaweza kuwa bora ktk uiamara wa kuwaandaa na kuwapa ukakamavu askari na wanajeshi lkn kwa technolojia hili tusidanganyane, technolojia haifichiki, bado tuko nyuma sana, nyuma saana.

Ushahidi mnao, kambi zetu si mnazijua? Maonesho ya siraha zetu si huwa tunayaona?, basi hata wakisema wanaficha baadhi ya siraha ushahidi mnao wenyewe kuwa Tanzania kitechnolojia bado tuko nyuma sana,
Tutafichwa vingine lakin nyenzo za kivita hasa ktk ulimwengu wa leo Tanzania bado hatujafika huko tumebaki ktk matumizi ya nyenzo za generation ya 3 huko ambayo ni outdated zingine zilitumika vita ya pili ya dunia na zingine kipindi cha akina Idd amin.

We need to improve, si tunajifunza vita za Ukraine+ Russia, Israel+ Iran kuwa vita vya sasa ni technolojia na kupunguza matumizi ya wanajeshi, yaani unapigwa nchini mwako kwa shambulio kubwa bila matumizi makubwa ya askari wa kijeshi, muda na fedha, na gharama za maandalizi ya plan.
Wenzetu wanatumia pesa kuwekeza kwenye teknolojia ya kujilinda, sisi tunajilinda kwa kusisitizana kuwa eti tuendelee kuwa taifa la amani tu basi, huku pesa tukizepeleka kwenye mambo ya ovyo ovyo.
 
Ktk mambo kama haya ni vema serikali yetu iendelee kujali thamani ya raia wake kiukweli ukweli na sio kama kutafta kiki au kama kuigiza igiza hivi.

Ktk kufanya hilo kuna baraka zake, na ktk hizo hizo baraka kuna utisho na heshima dhidi ya adui wa taifa.

Huo mchezo wa kutafta ukakamavu kwa kuwafosi watu kuwa wazalendo wa chama tawala kuna tofauti gani na kuwalazmisha watu kuwa wa imani moja ya kidini wakati nchi ina imani zaid ya moja?

Au kuna tofauti gani na kuwafosi watu kuwa kabila moja?
Kuna namna serikali inakosa baraka za raia wake. Hata hao wanaonekana kuunga mkono wengi hufanya hivyo kinafiki, kuhofia usalama wao na kuwinda fedha na madaraka.

Mazingira kama hayo sio salama hata mkiwa na jeshi imara bado haiwez kuwa salama mnapoingia vitani na adui hasa jirani.
 
Warwanda wako well organised

Ova
Wanaongozwa na watu wanaojitambua
Tunajua mpaka wamefika hapa wame sacrifice pakubwa sana na wengi wamemalizwa kwa maslahi ya Taifa lao.

Lakini kututisha hivyo sijui anajiamini vipi

Kama umeamua kuwa na maendelea kwa nchi yako, kwanini uanze kutafuta vita ilhali unajua utarudi nyuma miaka 20?

Leo Israel waliaminishwa ni nchi nzuri na wakaitwa waje kuwekeza na wakawekeza haswa na hata kuwadhurumu Palestinians ardhi Yao

Kosa kubwa kumpiga Iran sasa wayahudi hawatarudi tena kwao na wameondoka mpaka sasa zaidi ya 40,000 tena matajiri na wenye elimu zao

Wanajuta sasa
Ila kama Mr Slim nae anataka kuonyesha Ubabe kama Netanyahu, basi ajue vita Ina madhara na sio faida
 
Kila mwaka mnazika ila hamjielewi

Kila mwaka mnazika ila hamjielewi kama nyumbu.

Habari ya miaka 12 ndiyo unaileta leo unafikiri watu watakuwa hawajajifunza tu
 
Ishu inakuja wanyarwanda ni wengi sana Tz na wanazaliana sana na hata kama wamezaliwa na kukulia TZ, still wapo royal kwa nchi yao. Kama alivyosemaga mkuu wa majeshi wetu kwamba wapo raia wakigeni serikalini au kwenye taasisi zake na wengine wakiwa wameshika nafasi za kufanya maamuzi, basi hakika anachokisema PK kwamba anauwezo wa kukufata ulipo ni ukweli mtupu.
Lakini naiamini sana Nchi yangu TZ
Kwani Watanzania sio wengi Rwanda?
 

View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0

General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.

Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.

Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.

Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"

Povu Ruksa, Karibu Sana......

Nchi imekufa kabisa. IKO UCHIIIIIII

Wazalendo wamebaki UVCCM

20250707_230106.jpg
20250707_225931.jpg
20250707_230018.jpg
20250707_230018.jpg

 
Back
Top Bottom