Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Hii ni wake up call kwa mataifa yote duniani kwa sasa
Alichofanya Iran imefanya EU wakae dharura na hata waliemkataa ambae ni Trump alikuja na wakakubaliana waongeze bajeti ya Ulinzi

Sasa sisi acha tukaze fuvu tu
Huyu mzee anajiamini na nini?

Kama UK wameamua kununua ndege za kivita F-35 Stealth jets 12 ambazo zina uwezo wa kubeba mabomu ya Nuclear

Ili ikitokea tukashambuliwa basi nao waangamize maelfu ya watu bila huruma

Tusidharau maneno yake
Lazima tununue hata kwa mkopo dege moja tu la kuangamiza bila huruma

Natamani Mkuu wa majeshi ajibu
No,kuna nchi wao ni kuilinda mbogamboga tu,mawazo nguvu zao ziko hapo tu

Ova
 
Kweli aisee vita vya Middle east na Ukraine vinafundisha ili uheshimiwe, Ajitahidi uwe na ngumi moja umeifucha ambayo Adui yako anajua akikuchokoza kupitiliza ukimuwasha lazima Aombe Po.
Ni kweli kabisa
Huku watu wameona ni sawa tuwe na hizo ndege 12 ambazo zikishambulia wanahakikisha nusu ya population inakwisha

Sio onyo bali ni pigo takatifu

Iran kampiga Myahudi bila kumuogopa mtu na kapiga haswa ili kumuonyesha myahudi na kumuambia UKOME kabisa

Sasa huyu jirani anatuona tunapasua matofali ya udongo na commandos kuvaa manati anacheka sana

Ila tungekuwa tuna display drones 2000 kwenye maonyesha sidhani kama angefungua domo hilo

Leo Netanyahu wa kukubali suluhu na Hamas huko Qatar

Kuonyeaha silaha hadharani ni ubabe na kujiamini. Asikuambie mtu
Angalia US na hata Kiduku
 
Acheni maneno, Rwanda anazalisha silaha latest zipi hizo? Hizo ni assembling tu, bado sioni kwamba Rwanda imeizidi Tanzania wapi, sawa wanaweza kuwa mbele kwenye drone ila hiyo sio factor ya kushinda vita na Tanzania, siku wakijichanganya akati wao ni landlocked country watajutia sana, itakuwa ndo mwisho wa Kagame, war of attrition itawatosha, baada ya mwezi mmoja hiyo stock ya drone hawataikumbuka imeisha vipi
We una zalisha nini 😄
Au ndiyo top secret

Ova
 

View: https://youtu.be/wUu2W2Mk3k0

General Paul Kagame amezungumzia mgogoro wake na Congo. Moja ya vitu alivyovisema ni kwamba wale wote ambao wanaamini kwamba wanaweza kuitishia Kigali wakiwa mbali anao uwezo wa kuwafuata hukohuko makwao.

Akaendelea kusema kwamba, wale waliokuwa wanaiunga mkono serikali ya Congo, Rwanda iliwasamehe na kuwaacha wapite nchini Rwanda na kurudi makwao. Katika watu ambao waliruhusiwa kupita Rwanda ni pamoja na askari wa JWTZ ambao kuna video inaonesha wanasachiwa ili kurudi nyumbani.

Paul Kagame amesema, kama wale wanajeshi wangethubutu kutunisha misuli bila kusalimu amri basi wangeangamizwa wote. Tena kama kuna wengine wataendelea kufikiria kwamba wataitishia Rwanda basi watafuatwa hukohuko makwao.

Maneno ya Dikteta Paul Kagame yameanzia dakika ya 14 ya hii video niliyoambatanisha hapa. Ni ujumbe wa vitisho kwa mataifa ya SADC, ikiwemo Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

Kuna msemo husema hivi, "Usipokuwa makini, hata mbwa atakucheka"

Povu Ruksa, Karibu Sana......

Hii NI security dilemma 😂😂😂
 
Ndugu yangu! Usilo lijua ni Sawa na usiku kiza! TPDF si dhaifa kama unavyodhani, lipo more advance,kuna mengi yamefanyika na yanaendelea kufanyika kimyakimya, kama bado unamtazamo wa jeshi lileee lililopigana vita ya Kagera! Basi unakosea Sanaa,kuna Idadi kubwa ya vijana wenye uwezo wamekuwa walipelekwa urusi kwa mafunzo ya muda mrefu,takriban miaka 6 kwa bechi ya kozi moja,TPDF inafanya kazi zake kwa usiri na umakini mkubwa Sanaa,Tofauti na watu wanavyoifikiria.

kwa nini wanawapeleka urusi na siyo USA au western country nyingine yoyote? …
 
Ila tuwe wa kweli , japo Rwanda itazidiwa au kushindwa lakini TPDF hivi sasa ipo weak katika historia ya hii nchi, very weak...

Mbinu za kivita duniani zimebadilika sana asee, vita ya Ukraine damage kubwa zinafanywa na drones, karibu asilimia 70...

Na jeshi la Rwanda wamejiingiza kwenye hizo drones, operators wa drones sio wanapasua matofali kwa kichwa, wao ni kama gamers tu, kama mtu anacheza playstation... vita imebadilika sana..

Hao jamaa kujiamini hivyo inabidi iwe wake up call, itakuwa hawajiamini bure... mnakwenda na Artillery guns/mambomu ya mizinga ya enzi za Kagera war, unatumiwa ki drone kidogo kinawalipua na silaha zenu zote...
Ujinga wako ni tatizo lako. Kwani kuna Jeshi la nchi yoyote Afrika isiyo na drone? Kuna Jeshi la nchi yoyote lisio na mazoezi ya kupasua tofali? Yale maonesho ya uwanja wa uhuru yanaitwa 'Military show-off' ambayo hata mataifa yaliyoendelea huyafanya kwa ajili ya kuburudisha tu.

Kwenye link hiyo ni Royal marine Commandos wakifanya show-off.

View: https://youtu.be/SLQCWouUgHU?si=4jcR1KwHt6qXEq5i
 
Kuna watu watafurahia Tanzania kupigwa ili tupate serikali mpya itakayothamini kila mchango wa Kila mtanzania
Mimi ni mmoja wapo ya hao watu, tena nitafurahi mno siku hili likitokea..!! Kuliko kuendelea kuona nchi wakiifaidi watu wachache ni heri tupigwe kisha kila mtu akimbilie anapojua yeye.
 
Acheni maneno, Rwanda anazalisha silaha latest zipi hizo? Hizo ni assembling tu, bado sioni kwamba Rwanda imeizidi Tanzania wapi, sawa wanaweza kuwa mbele kwenye drone ila hiyo sio factor ya kushinda vita na Tanzania, siku wakijichanganya akati wao ni landlocked country watajutia sana, itakuwa ndo mwisho wa Kagame, war of attrition itawatosha, baada ya mwezi mmoja hiyo stock ya drone hawataikumbuka imeisha vipi

👆🏿👆🏿👆🏿Ndugu yangu hizi sio SMG au AK47 za ngerengere 92 kj Morogoro
 
Nyie mmeinvest kwenye wizi na propaganda za kuwasifia wanasiasa lkn hiki kinchi kidogo masikini kinawatukana watu waliokizi maendeleo mpaka idadi ya watu mara mia.

Kuna siku East Afrika tutakuja kulia kisa kuifumbia macho hii migogoro ambayo inawakumba jirani zetu lkn hatuoneshi udhibiti zaidi ya kutegemea wageni wa ulaya watusaidie.

Nina imani hiki kinchi(Rwanda) hakifanyi mambo kwa kukurupuka wala kwa mihemko, bali ni uhalisia, pia nina uhakika kwa Rwanda ilipofika ina intelligence kubwa mpaka huku tusikofikiria, vile vile kina technologia ambazo baadhi yetu bado hatuna na hatuna mipango nazo kwa kujidanganya sisi taifa lenye amani

Ipo siku hii amani fake itawaliza watu na tutaumbuka vibaya sana, nguvu zetu tumeziwekeza ktk siasa chafu za kuuwana, kuchafuana na kupora mali za umma, lkn mambo ya msingi bado tuko nyuma.

Jeshi letu linaweza kuwa bora ktk uiamara wa kuwaandaa na kuwapa ukakamavu askari na wanajeshi lkn kwa technolojia hili tusidanganyane, technolojia haifichiki, bado tuko nyuma sana, nyuma saana.

Ushahidi mnao, kambi zetu si mnazijua? Maonesho ya siraha zetu si huwa tunayaona?, basi hata wakisema wanaficha baadhi ya siraha ushahidi mnao wenyewe kuwa Tanzania kitechnolojia bado tuko nyuma sana,
Tutafichwa vingine lakin nyenzo za kivita hasa ktk ulimwengu wa leo Tanzania bado hatujafika huko tumebaki ktk matumizi ya nyenzo za generation ya 3 huko ambayo ni outdated zingine zilitumika vita ya pili ya dunia na zingine kipindi cha akina Idd amin.

We need to improve, si tunajifunza vita za Ukraine+ Russia, Israel+ Iran kuwa vita vya sasa ni technolojia na kupunguza matumizi ya wanajeshi, yaani unapigwa nchini mwako kwa shambulio kubwa bila matumizi makubwa ya askari wa kijeshi, muda na fedha, na gharama za maandalizi ya plan.
Mkuu wa majeshi alishasema,TZ kuna wageni wengi mno serikalini na kwenye vyombo vya usalama,nadhani ndio uhamiaji ikaja na operesheni mjue jirani yako,ila ajabu operesheni yenyewe iko kule instagram na x,mitaani aionekani hapo ndio utajua sisi watanzania uzalendo ni sifuri,admin wa uhamiaji yy anapost tu,mwisho wa mwezi mshahara unaingia 😃utekelezaji hamna
 
Toa upumbavu wako na wewe unadhani hizo propoganda zenu za kijinga zitafanikiwa
Kila mwaka mnazika ila hamjielewi kama nyumbu.

 
Mkuu wa majeshi alishasema,TZ kuna wageni wengi mno serikalini na kwenye vyombo vya usalama,nadhani ndio uhamiaji ikaja na operesheni mjue jirani yako,ila ajabu operesheni yenyewe iko kule instagram na x,mitaani aionekani hapo ndio utajua sisi watanzania uzalendo ni sifuri,admin wa uhamiaji yy anapost tu,mwisho wa mwezi mshahara unaingia 😃utekelezaji hamna
Sikuwahi jua kuna operation ka hiyo
 
Toa upumbavu wako na wewe unadhani hizo propoganda zenu za kijinga zitafanikiwa
 
Back
Top Bottom