Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Rais Kagame anailenga Tanzania katika ujumbe huu?

Drone ni hela zako tu, ukiingia hapo China na bilioni 100 unazichukua za kutosha. So Rwanda kuzimiliki sio kwamba Tanzania ni dhaifu
Kutumia drones sio suala la pesa tu pekee, kutengeneza hao wataalamu wa kuziendesha ni gharama na inachukua muda..
hizo drones ziahitaji pia wataalamu wa kuzifanyia service..
Vita ya drones ina technics zake, ina ugumu wake na utaalamu..

Mfano Russia walianza kutumia jammers, hizo jammers ni magari yamebeba antenna kubwa very powerful, ni gari kama hilux, hilo gari likisimama mahala hilo eneo karibu 30KM/40KM au pengine zaidi mawasiliano hakuna, drone ikiingia hio zone ujue umeipoteza... na hayo magari si moja..

Ukraine walichofanya walianza kurusha drones wanazifunga fiber optics cable, drone inaruka lakini ina wire mwembamba sana, inaruka kilomita za kutosha, hii inasaidia drone kuwa resistant na electronic warfare systems... hizi drones zimetumika sana kulipua magari ya kirusi yenye jammers...

Vita za drones ni sehemu nyingine pana, inabidi mnakuwa full package, wawepo vijana wanajua masuala ya electronic warfare systems, hizi vita ni za kitaalamu zaidi....

Rwanda wanawekeza huko sana huko na wanatoa vijana wao wakasome.... silaha kama huna utaalamu nayo utapigwa tu...
 
Hii ni wake up call kwa mataifa yote duniani kwa sasa
Alichofanya Iran imefanya EU wakae dharura na hata waliemkataa ambae ni Trump alikuja na wakakubaliana waongeze bajeti ya Ulinzi

Sasa sisi acha tukaze fuvu tu
Huyu mzee anajiamini na nini?

Kama UK wameamua kununua ndege za kivita F-35 Stealth jets 12 ambazo zina uwezo wa kubeba mabomu ya Nuclear

Ili ikitokea tukashambuliwa basi nao waangamize maelfu ya watu bila huruma

Tusidharau maneno yake
Lazima tununue hata kwa mkopo dege moja tu la kuangamiza bila huruma

Natamani Mkuu wa majeshi ajibu
 
Niliona na Kainerugaba wa Uganda anatamba eti Eneo la Afrika lenye watu weusi majeshi IMARA ni UPDF na Jeshi la Rwanda. Huyu dingi siku baba yake M7 akimuachia Uganda sidhani kama east Afrika itakuwa salama sana maana anajikubali kupitiliza.

Kagame ni kibaraka wa US labda anajua anabackup
 
Ila tuwe wa kweli , japo Rwanda itazidiwa au kushindwa lakini TPDF hivi sasa ipo weak katika historia ya hii nchi, very weak...

Mbinu za kivita duniani zimebadilika sana asee, vita ya Ukraine damage kubwa zinafanywa na drones, karibu asilimia 70...

Na jeshi la Rwanda wamejiingiza kwenye hizo drones, operators wa drones sio wanapasua matofali kwa kichwa, wao ni kama gamers tu, kama mtu anacheza playstation... vita imebadilika sana..

Hao jamaa kujiamini hivyo inabidi iwe wake up call, itakuwa hawajiamini bure... mnakwenda na Artillery guns/mambomu ya mizinga ya enzi za Kagera war, unatumiwa ki drone kidogo kinawalipua na silaha zenu zote...
Ndugu yangu! Usilo lijua ni Sawa na usiku kiza! TPDF si dhaifa kama unavyodhani, lipo more advance,kuna mengi yamefanyika na yanaendelea kufanyika kimyakimya, kama bado unamtazamo wa jeshi lileee lililopigana vita ya Kagera! Basi unakosea Sanaa,kuna Idadi kubwa ya vijana wenye uwezo wamekuwa walipelekwa urusi kwa mafunzo ya muda mrefu,takriban miaka 6 kwa bechi ya kozi moja,TPDF inafanya kazi zake kwa usiri na umakini mkubwa Sanaa,Tofauti na watu wanavyoifikiria.
 
Mimi nilisha wambia humu Rwanda anaweza kuitandika Tanzania wengine wakasema mimi ni mtusi eti 😆 😂
Naweza kusema kwenye modern warfare Rwanda wanaweza kutuzidi..
Na vita ya kileo ili ushinde lazima upigane kileo...
Matatizo ya kileo ili uyatatue inabidi utumie solutions za leo....
Huwezi tatua changamoto ya 2025 kwa kutumia njia ya mwaka 1961...
 
Namaanisha pamoja na hayo mapungufu, drone sio kitu cha kuringia kwa dunia ya sasa.

Hivi ujajua kuna ma engineers wa silaha kutoka Asian countries wapo wameajiriwa na nchi za ki Africa?

Sio issue kabisa hata kwenye drone, ukiwa na central command ukawaweka wachina 10 wanatosha kabisa kuipa joto Rwanda
Swala ni kwa kuangalia raia wa kawaida wa Tanzania na Rwanda yupi ana uzalendo na nchi yake ? Haya basi tuje wafanyakazi wa serikalini ? Halafu tumalizie na wanajeshi. Asset ya kwanza ya nchi ni watu au wananchi ukitaka kujifunza kajaribu kuhonga trafiki au polisi wa Rwanda na Tanzania halafu ulinganishe. Serikali yetu imeoza sana kiasi cha kwamba hata tutumie pesa kiasi gani hatua tutapiga ndogo sana. Pesa nyingi utapotea njiani kabla haijafika kwenye lengo.

Mfano mdogo sisi tunanunua silaha kwa Lugumi na Lugumi anaagiza kwa mtu na kuweka cha juu. Rwanda inazalisha silaha zake latest mwenyewe. Tulipofika kila mtu anajali tumbo lake.
 
Nyie mmeinvest kwenye wizi na propaganda za kuwasifia wanasiasa lkn hiki kinchi kidogo masikini kinawatukana watu waliokizi maendeleo mpaka idadi ya watu mara mia.

Kuna siku East Afrika tutakuja kulia kisa kuifumbia macho hii migogoro ambayo inawakumba jirani zetu lkn hatuoneshi udhibiti zaidi ya kutegemea wageni wa ulaya watusaidie.

Nina imani hiki kinchi(Rwanda) hakifanyi mambo kwa kukurupuka wala kwa mihemko, bali ni uhalisia, pia nina uhakika kwa Rwanda ilipofika ina intelligence kubwa mpaka huku tusikofikiria, vile vile kina technologia ambazo baadhi yetu bado hatuna na hatuna mipango nazo kwa kujidanganya sisi taifa lenye amani

Ipo siku hii amani fake itawaliza watu na tutaumbuka vibaya sana, nguvu zetu tumeziwekeza ktk siasa chafu za kuuwana, kuchafuana na kupora mali za umma, lkn mambo ya msingi bado tuko nyuma.

Jeshi letu linaweza kuwa bora ktk uiamara wa kuwaandaa na kuwapa ukakamavu askari na wanajeshi lkn kwa technolojia hili tusidanganyane, technolojia haifichiki, bado tuko nyuma sana, nyuma saana.

Ushahidi mnao, kambi zetu si mnazijua? Maonesho ya siraha zetu si huwa tunayaona?, basi hata wakisema wanaficha baadhi ya siraha ushahidi mnao wenyewe kuwa Tanzania kitechnolojia bado tuko nyuma sana,
Tutafichwa vingine lakin nyenzo za kivita hasa ktk ulimwengu wa leo Tanzania bado hatujafika huko tumebaki ktk matumizi ya nyenzo za generation ya 3 huko ambayo ni outdated zingine zilitumika vita ya pili ya dunia na zingine kipindi cha akina Idd amin.

We need to improve, si tunajifunza vita za Ukraine+ Russia, Israel+ Iran kuwa vita vya sasa ni technolojia na kupunguza matumizi ya wanajeshi, yaani unapigwa nchini mwako kwa shambulio kubwa bila matumizi makubwa ya askari wa kijeshi, muda na fedha, na gharama za maandalizi ya plan.
Hapo umenena mkuu. Jwtz ukuionekana una akili unatengenezewa kesi feki. Unatimliwa au kusitaafishwa.

Alafu jeshi lina muundo kama wa CCM
1. Kujuana / familia/ kurithishana
2. Ukanda/ukabila
3. Ujinga mwingine ni majungu au umbea.
 
Hii ni wake up call kwa mataifa yote duniani kwa sasa
Alichofanya Iran imefanya EU wakae dharura na hata waliemkataa ambae ni Trump alikuja na wakakubaliana waongeze bajeti ya Ulinzi

Sasa sisi acha tukaze fuvu tu
Huyu mzee anajiamini na nini?

Kama UK wameamua kununua ndege za kivita F-35 Stealth jets 12 ambazo zina uwezo wa kubeba mabomu ya Nuclear

Ili ikitokea tukashambuliwa basi nao waangamize maelfu ya watu bila huruma

Tusidharau maneno yake
Lazima tununue hata kwa mkopo dege moja tu la kuangamiza bila huruma

Natamani Mkuu wa majeshi ajibu
Kweli aisee vita vya Middle east na Ukraine vinafundisha ili uheshimiwe, jitahidi uwe na ngumi moja umeificha ambayo Adui yako anajua akikuchokoza kupitiliza ukimuwasha lazima Aombe Po.
 
Ndugu yangu! Usilo lijua ni Sawa na usiku kiza! TPDF si dhaifa kama unavyodhani, lipo more advance,kuna mengi yamefanyika na yanaendelea kufanyika kimyakimya, kama bado unamtazamo wa jeshi lileee lililopigana vita ya Kagera! Basi unakosea Sanaa,kuna Idadi kubwa ya vijana wenye uwezo wamekuwa walipelekwa urusi kwa mafunzo ya muda mrefu,takriban miaka 6 kwa bechi ya kozi moja,TPDF inafanya kazi zake kwa usiri na umakini mkubwa Sanaa,Tofauti na watu wanavyoifikiria.
Hivi huo usiri husaidia nini? ikiwa mataifa yenye nguvu za kijeshi kama China, Russia, Iran, Israel, Turkey n.k huonyesha uwezo wao kijeshi, hii Tanzania kuna siri gani?

Hio siri inasaidia nini?
 
Ila tuwe wa kweli , japo Rwanda itazidiwa au kushindwa lakini TPDF hivi sasa ipo weak katika historia ya hii nchi, very weak...

Mbinu za kivita duniani zimebadilika sana asee, vita ya Ukraine damage kubwa zinafanywa na drones, karibu asilimia 70...

Na jeshi la Rwanda wamejiingiza kwenye hizo drones, operators wa drones sio wanapasua matofali kwa kichwa, wao ni kama gamers tu, kama mtu anacheza playstation... vita imebadilika sana..

Hao jamaa kujiamini hivyo inabidi iwe wake up call, itakuwa hawajiamini bure... mnakwenda na Artillery guns/mambomu ya mizinga ya enzi za Kagera war, unatumiwa ki drone kidogo kinawalipua na silaha zenu zote...
Watasema sio mzalendo kisa ujasifia jeshi letu, lkn uzalendo pia ni kuyakemea maovu na kuyasema mapungufu ili wanaohusika wawajibike.

Nchi ya Rwanda huenda haina cha kupoteza, ipo siku itaondoka na nchi yoyote kubwa hapa East Afrika ili kushikisha adabu au kuonesha uwezo wake, au kutoa onyo au vile vile kuaibisha maana kwa mtu wa cheo cha rais hawezi kuropoka maneno kama hayo bila kuwa na maana, haijalishi yanauma kiasi gani, lkn uhakika ni kuwa Tanzania na baadhi ya nchi za East Africa mpaka SADC zipo uchi kiintellegencia mpaka umiliki wa nyenzo za kivita.

Tunaweza kuwa bora kwa idadi kubwa ya wanajeshi na matumizi ya ukakamavu lkn linapoja suala la matumizi ya technolojia asee tutapigwa mchana kweupe.

Ushahidi mnao, hivi tuna hata mafunzo ya matumizi ya drones kwa majeshi yetu?, siraha za anga je? au siraha za kujilinga na mashambulizi ya anga tupo vizuri?, au ndio yale yale tunasubiri tuvamiwe ili tukaombe msaada kwa wafadhiri wetu kama ilivyokuwa vita ile?.

Narudia tena, Tanzania kijeshi tunahitaji improvement kubwa sana, na kwa ukubwa wa nchi yetu basi hata bajeti yake inatakiwa kuwa imara haswa.
 
Ndugu yangu! Usilo lijua ni Sawa na usiku kiza! TPDF si dhaifa kama unavyodhani, lipo more advance,kuna mengi yamefanyika na yanaendelea kufanyika kimyakimya, kama bado unamtazamo wa jeshi lileee lililopigana vita ya Kagera! Basi unakosea Sanaa,kuna Idadi kubwa ya vijana wenye uwezo wamekuwa walipelekwa urusi kwa mafunzo ya muda mrefu,takriban miaka 6 kwa bechi ya kozi moja,TPDF inafanya kazi zake kwa usiri na umakini mkubwa Sanaa,Tofauti na watu wanavyoifikiria.
Sasa urussi wana teknolojia gani ?Wanasumbuliwa na Ukraine mpaka kesho vita haishi. Nilitegemea useme walipelekwa Israel. Urussi hawana system wala jeshi kama zamani rushwa iliyokithiri imeharibu nchi yao pia. Hili ni tatizo la Tanzania pia.
 
rwanda-bayraktar-turkey-baykar.png

Rwanda hivi sasa wana process za kuanza kutumia stealth drones na zina AI..
Lets be careful... huyu mzee akiachiwa hivi pasipo kuchukua tahadhari, miaka 10/20 baadae tukikaa kifala tutashindwa hata kumgusa..
Ile nchi imewekeza kwenye nini
Zaidi ya uchawa tu,kujikombakomba,umbea,udaku

Ova
 
In short, Kagame akiamua unaweza kuamka ukakuta huyo Rahisi wako kafa.

Siraha zenu zenyewe DALALI ni LUGUMI ambaye ni mtu wa Kagame.
Toa upumbavu wako na wewe unadhani hizo propoganda zenu za kijinga zitafanikiwa
 
Swala ni kwa kuangalia raia wa kawaida nmwa Tanzania na Rwanda yupi ana uzalendo na nchi yake ? Haya basi tujue wafanyakazi wa serikalini ? Halafu tumalizie na wanajeshi. Asset ya kwanza ya nchi ni watum ukitaka kujifunza majaribu kuongea trafiki au polisi wa Rwanda na Tanzania ndio utajua tofauti. Serikali yetu imeoza sana kiasi cha kwamba hata tutumie pesa kiasi gani hatua tutapiga ndogo sana.

Mfano mdogo sisi tunanunua silaha kwa Lugumi na Lugumi anaagiza kwa mtu na kuweka cha juu. Rwanda inazalisha silaha zake latest mwenyewe. Tulipofika kila mtu anajali tumbo lake.
Acheni maneno, Rwanda anazalisha silaha latest zipi hizo? Hizo ni assembling tu, bado sioni kwamba Rwanda imeizidi Tanzania wapi, sawa wanaweza kuwa mbele kwenye drone ila hiyo sio factor ya kushinda vita na Tanzania, siku wakijichanganya akati wao ni landlocked country watajutia sana, itakuwa ndo mwisho wa Kagame, war of attrition itawatosha, baada ya mwezi mmoja hiyo stock ya drone hawataikumbuka imeisha vipi
 
Back
Top Bottom