Rais Dr. Hussein Mwinyi awasili Cuba kwa mkutano wa G77 na China

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,321
24,228
Havana, Cuba

Cumbre de Jefes de Estado y de Gobierno del Grupo de los 77 y China

tarehe 14 September 2023
Mwandishi
Na Pedro Rioseco


View: https://m.youtube.com/watch?v=Lhxm7jatf5U

Mh. Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa na balozi wa Tanzania nchini Cuba Mh. Humphrey Hesron Polepole uwanja wa ndege wa Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana nchini Cuba.


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Mwinyi amewasili nchi Cuba kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan katika mkutano wa nchi za kundi la G77

Rais wa Cuba Miguel Díaz Canel Bermúdez ataongoza Ijumaa hii tarehe 15 hadi Jumamosi tarehe 16 September 2023 Mkutano muhimu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China kujadili mada "Changamoto za sasa za maendeleo: Jukumu la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu" .

Likiwa limeitishwa na Cuba, katika nafasi yake kama mwenyekiti wa muda nchi za G77 tangu Januari iliyopita, Kundi hili G77 ndilo kambi kubwa zaidi ya nchi zinazoendelea ndani ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa na kundi la mashauriano tofauti zaidi katika nyanja ya kimataifa.

Inajumuisha nchi wanachama 134 ambazo zinawakilisha theluthi mbili ya wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa na asilimia 80 ya idadi ya watu duniani, ambayo inaonyesha jukumu lake muhimu.


G77 Ilianzishwa mnamo Juni 15, 1964 kama kikundi cha nchi zinazoendelea na ambazo hazijaendelea kwa madhumuni ya kusaidiana, kudumisha na kusaidiana katika mijadala ya Umoja wa Mataifa, jukumu lake katika nyanja ya kimataifa lilikua na ujumuishaji uliofuata wa nchi za Ulimwengu wa Tatu.
Source : https://www.contraloria.gob.cu/noti...te-reunion-cumbre-del-grupo-de-los-77-y-china


15 September 2023
Havana, Cuba

RAIS DR. HUSSEIN MWINYI AKIHUTUBIA MKUTANO WA G77+CHINA MJINI HAVANA CUBA
1694962842999.png

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundo la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.



Akihutubia katika Mkutano huo, Dkt. Mwinyi amesema Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nguzo muhimu kwa nchi zinazoendelea kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza kuwa nchi hizo zinaweza kuendelea kiuchumi kupitia maendeleo katika sekta muhimu za kilimo, nishati, elimu, afya, madini, maendeleo ya muindombinu, maji na mazingira.

Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha namna nchi zinazoendelea zilivyoathirika na janga la maradhi ya UVIKO-19, bidhaa kupanda bei, mizozo ya kisiasa na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa baadhi ya changamoto zilisababisha kupanda kwa gharama za maisha na kudhoofisha jitahada za kujikwamua kiuchumi.



Mhe. Dkt. Mwinyi alikumbushia namna nchi zilizoendelea zilivyobanwa na teknolojia ya kutengeneza chanjo na kunyimwa msaada wa kiteknolojia ili zitengeneze chanjo zao na kusababisha kampuni za kutengeneza dawa za mataifa tajiri kupata faida kubwa kwa kuziuzia nchi zinazoendelea chanjo ya UVIKO-19.å

Mhe.Dkt. Mwinyi amezitanabaisha nchi za kundi la G77+China kuchukua changamoto hizo kama somo na zisibweteke kusubiri msaada kutoka mataifa yaliyoendelea.



Mkutano huo unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 15-16 Septemba 2023 unayakutanisha mataifa yanayoendelea unajadili changamoto zinazoikabili dunia baada ya kuathirika na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.



Mkutano huo umejikita kutafuta namna bora ya kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu ili kundi la G77+China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.



Kaulimbiu ya Mkutani inasema, “Changamoto za Maendeleo: Nafasi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu”.
 
Nakumbuka mkutano huu alipouleta Tanzania nyerere ndiyo akajenga hoteli ya 77 Arusha na akanunuwa Benz mpya 77 ili kupokea wageni huku Watanzania wanakaa foleni ya kula.

Yule mzee alikuwa na mambo ya kijinga jinga sana. kazi kujichekesha chekesha tu.
 
14 September 2023
Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana, Cuba and

En Cuba presidente de Ruanda para participar en la Cumbre del G77 y China

Mkutano huo unahudhuriwa na marais wa Rwanda, Paul Kagame; Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva; kutoka Argentina, Alberto Fernandez; kutoka Colombia, Gustavo Petro; kutoka Iraq, Abdelatif Rashid; kutoka Palestina, Mahmud Abás, kutoka Angola, João Lourenço; kutoka Burundi, Évariste Ndayishimiye, na kutoka Honduras, Xiomara Castro.

View: https://m.youtube.com/watch?v=kfJZdQrWwaY
Wakuu wengine ni kutoka mataifa Bolivia, Luis Arce, pia walithibitisha ushiriki wao; Sri Lanka, Ranil Wickremesinghe; Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi; Laos, Thongloun Sisoulith; Equatorial Guinea, Obiang Nguema, na Waziri Mkuu wa Saint Vincent na Grenadines, Ralph Gonsalves, pamoja na wawakilishi wakuu wa nchi zingine za Kundi la G77.

Aidha, maafisa wakuu kama vile Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa UN , António Guterres, watahudhuria hafla hiyo; katibu mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano, Doreen Bogdan-Martin, na mkurugenzi mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, Qu Dongyu.

View: https://m.youtube.com/watch?v=eRFQZzMmTYU
Source : canal caribe
 

Attachments

  • 1694879351458.png
    1694879351458.png
    182.1 KB · Views: 2
Mkutano huo unahudhuriwa na marais wa Brazil, Luiz Inacio Lula da Silva; kutoka Argentina, Alberto Fernandez; kutoka Colombia, Gustavo Petro; kutoka Iraq, Abdelatif Rashid; kutoka Palestina, Mahmud Abás, kutoka Angola, João Lourenço; kutoka Burundi, Évariste Ndayishimiye, na kutoka Honduras, Xiomara Castro.

Wakuu wengine ni kutoka mataifa Bolivia, Luis Arce, pia walithibitisha ushiriki wao; Sri Lanka, Ranil Wickremesinghe; Msumbiji, Filipe Jacinto Nyusi; Laos, Thongloun Sisoulith; Equatorial Guinea, Obiang Nguema, na Waziri Mkuu wa Saint Vincent na Grenadines, Ralph Gonsalves, pamoja na wawakilishi wakuu wa nchi zingine za Kundi.

Aidha, maafisa wakuu kama vile Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa UN , António Guterres, watahudhuria hafla hiyo; katibu mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Mawasiliano, Doreen Bogdan-Martin, na mkurugenzi mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, Qu Dongyu.
Hao wote wanafik ni wengi, walishindwa kumtetea Salim Ahmed Salim awe Katibu Mkuu UN, alitetewa na China tu katika hao.

Unafik mtupu hapo.
 
14 September 2023
Havana, Cuba

RAIS HUSSEIN MWINYI AZINDUA JENGO LA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI CUBA
1694739716526.png

Rais Dr. Hussein Mwinyi na makamu wa rais wa Cuba Mh. Salvador Valdés Mesa wakikata utepe kuashiria ufunguzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania Havana Cuba. Pia mikataba kadhaa ya makubaliano imesainiwa baina ya Cuba na Tanzania .


View: https://m.youtube.com/watch?v=F7OZdp4wGJU
El vicepresidente de Cuba, Salvador Valdés, asistió hoy a la apertura de la embajada de la República Unida de Tanzania en el contexto del inminente inicio mañana aquí de la Cumbre del G77 y China. Vicepresidente de Cuba asiste apertura de embajada de Tanzania (+Fotos) - Prensa Latina
1694739650215.png


Source : Prensa Latina TV
 
Nakumbuka mkutano huu alipouleta Tanzania nyerere ndiyo akajenga hoteli ya 77 Arusha na aakanunuwa Benz mpya 77 ili kupokea wageni huku Watanzania wanakaa foleni ya kula.
Hii mikutano ya kimataifa imeisaidia sana Tanzania, mpaka sasa iliyokuwa Hotel 77, sasa imegeuka Grand Malia ndio the best hotel ya 5 star Arusha, na Grand Malia ya Zanzibar ndio the 2nd best baada ya Verde!.
Take time kuisoma hii attached Doc uone umuhimu wa mikutano ya kimataifa kwa Tanzania.
P
 

Attachments

  • Strategy Update Editors Forum 2023.ppt
    53.2 MB · Views: 2
Hii mikutano ya kimataifa imeisaidia sana Tanzania, mpaka sasa iliyokuwa Hotel 77, sasa imegeuka Grand Malia ndio the best hotel ya 5 star Arusha, na Grand Malia ya Zanzibar ndio the 2nd best baada ya Verde!.
Take time kuisoma hii attached Doc uone umuhimu wa mikutano ya kimataifa kwa Tanzania.
P
Ilikuwa nyang'a nyang'a mpaka ikauziwa mtu binafsi ndiyo kaibadilisha.

Kipi alichokifanya nyerere kwenye uchumi kikawana baraka? Katika 100 labda kimoja. Kipo?

Mzee yule alikuwa mwongeaji mzuri sana, yule angefanya kazi ya u salesman ingemfaa sana, he was mesmerizing lakini Urais ni 0.
 
Nakumbuka mkutano huu alipouleta Tanzania nyerere ndiyo akajenga hoteli ya 77 Arusha na akanunuwa Benz mpya 77 ili kupokea wageni huku Watanzania wanakaa foleni ya kula.

Yule mzee alikuwa na mambo ya kijinga jinga sana. kazi kujichekesha chekesha tu.
Hukumbuki kitu; sema Nyerere alikuwa mgalatia kwa hiyo msimamo wako kwake unaeleweka. Nyerere hakuwa anajichekesha chekesha kama unavyodai; mtu wa kujichekesha hadi leo ni Kikwete.

Mkutano wa G77 uliofanyika Tanzania ulikuwa ni mwanzoni mwa mwaka 1979 na ulikuwa wa mawaziri wa nchi za nje tu; haukuwa Summit ya marais. Wakati huo Tanzania ilikuwa bado iko kwenye vita ya Kagera, isingefanya matumizi unayodai eti kwa sababu ya mkutano wa Mawaziri twa nchi za nje tu. Hotel 77 ilijengwa mwaka 1977 wakati wa miaka kumi ya Azimio na kuzaliwa kwa CCM kabla hata ya vita yenyewe na mkutano huo unaolaani.
 
Hukumbuki kitu; sema Nyerere alikuwa mgalatia kwa hiyo umsimamo wako kwake unaeleweka. Nyerere hakuwa anajichekesha chekesha kama unavyodaia; mtu wa kujichekesha hadi leo ni Kikwete.

Mkutano wa G77 uliofanyika Tanzania ulikuwa ni mwanzoni mwa mwaka 1979 na ulikuwa wa mawaziri wa nchi za nje tu; haukuwa Summit ya marais. Wakati huo Tanzania ilikuwa bado iko kwenye vita ya Kagera, isingefny matumiz unayodai eti kwa sababu ya mkutano wa Mawazir twa nchi za nje tu. Hotel 77 ilijengwa mwaka 1977 wakwti wa miaka kumi ya Azimio na kuzaliwa kwa CCM kabla hata ya vita yenyewe na mkutano huo unaolaani.
Kikwete hacheki anatabasamu ya asili.

Naona huelewi tofauti ya kucheka na kutabasamu. Ni wazi Kiswahili siyo lugha mama kwako.

Tusiandikie na mate na wino upo, zaidi ya kujuwa kupiga porojo ni kipi cha maana ulichokikuta wewe cha Nyerere, AlhamduliLlah mimi nimeishi wakati wake wote.
 
14 September 2023
Uwanja wa ndege wa kimataifa José Martí wa Havana, Cuba

Vingozi zaidi wa nchi na serikali wapokewa tayari kwa mkutano wa Kundi la 77


View: https://m.youtube.com/watch?v=TzGB2BZuvks
Dominica , Roosevelt Skerrit, fue recibido esta tarde en el Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana, por el ministro de Industrias, Eloy Álvarez Martínez. Por su parte, el titular de Finanzas y Precios, Vladimir Regueiro Ale, dio la bienvenida al primer ministro de Granada, Dickon Mitchell, en horas de la tarde de hoy. Posteriormente, arribó a nuestro país el primer ministro de San Vicente y las Granadinas, Ralph Gonsalves, quien fue recibido por Marta Elena Feito Cabrera, Ministra de Trabajo y Seguridad Social. Los tres líderes caribeños representarán a sus países en la Cumbre del G-77 y China, que sesionará los días 15 y 16 de septiembre en La Habana
 
Kikwete hacheki anatabasamu ya asili.

Naona huelewi tofauti ya kucheka na kutabasamu. Ni wazi Kiswahili siyo lugha mama kwako.

Tusiandikie na mate na wino upo, zaidi ya kujuwa kupiga porojo ni kipi cha maana ulichokikuta wewe cha Nyerere, AlhamduliLlah mimi nimeishi wakati wake wote.
Mtu akitabasamu huwa hatoi sauti; kiswahili chako cha gengeni usikifanye formal. Ndio nyinyi mnaosmea "nyimbo hii ni nzuri" badala ya kusema "wimbo huu ni mzuri" halafu mnajifanya eti mnajua kiswahili sana. Elewa tofauti ya smile na laugh!
 
Nakumbuka mkutano huu alipouleta Tanzania nyerere ndiyo akajenga hoteli ya 77 Arusha na akanunuwa Benz mpya 77 ili kupokea wageni huku Watanzania wanakaa foleni ya kula.

Yule mzee alikuwa na mambo ya kijinga jinga sana. kazi kujichekesha chekesha tu.
Leo ndio nimeujua upumbavu wako vizuri.@faizafox.


Sisi vijana wa zamani tulikuwa na kiswahili chetu miaka hiyo Malaya tulimuita Fox.
Kama unadiriki kumuita Baba wa Taifa "mjinga"mtu ambaye ameacha heshima yake,ikienziwa kote Duniani.
Huyu mama yenu anastahili kuitwa nani kwa anayoyafanya sasa hivi?
Upumbavu mwingine hatufai kuuvumilia bali kuukataa na kuwaambieni live kwamba nyinyi ndio wajinga wa karne na ndio maana mnafanya mambo ya kijimga namna hii.
 
Havana, Cuba

Cumbre de Jefes de Estado y de Gobierno del Grupo de los 77 y China

tarehe 14 September 2023
Mwandishi
Na Pedro Rioseco

View: https://m.youtube.com/watch?v=D8AK5C46fx4
Mh. Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa na balozi wa Tanzania nchini Cuba Mh. Humphrey Hesron Polepole uwanja wa ndege wa Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana nchini Cuba.


Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Mwinyi amewasili nchi Cuba kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan katika mkutano wa nchi za kundi la G77

Rais wa Cuba Miguel Díaz Canel Bermúdez ataongoza Ijumaa hii tarehe 15 hadi Jumamosi tarehe 16 September 2023 Mkutano muhimu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China kujadili mada "Changamoto za sasa za maendeleo: Jukumu la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu" .

Likiwa limeitishwa na Cuba, katika nafasi yake kama mwenyekiti wa muda nchi za G77 tangu Januari iliyopita, Kundi hili G77 ndilo kambi kubwa zaidi ya nchi zinazoendelea ndani ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa na kundi la mashauriano tofauti zaidi katika nyanja ya kimataifa.

Inajumuisha nchi wanachama 134 ambazo zinawakilisha theluthi mbili ya wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa na asilimia 80 ya idadi ya watu duniani, ambayo inaonyesha jukumu lake muhimu.


G77 Ilianzishwa mnamo Juni 15, 1964 kama kikundi cha nchi zinazoendelea na ambazo hazijaendelea kwa madhumuni ya kusaidiana, kudumisha na kusaidiana katika mijadala ya Umoja wa Mataifa, jukumu lake katika nyanja ya kimataifa lilikua na ujumuishaji uliofuata wa nchi za Ulimwengu wa Tatu.
Source : https://www.contraloria.gob.cu/noti...te-reunion-cumbre-del-grupo-de-los-77-y-china

sawa HUMPHREY POLEPOLE tumekuelewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom