Havana, Cuba
Cumbre de Jefes de Estado y de Gobierno del Grupo de los 77 y China
tarehe 14 September 2023
Mwandishi
Na Pedro Rioseco
View: https://m.youtube.com/watch?v=Lhxm7jatf5U
Mh. Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa na balozi wa Tanzania nchini Cuba Mh. Humphrey Hesron Polepole uwanja wa ndege wa Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana nchini Cuba.
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Mwinyi amewasili nchi Cuba kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan katika mkutano wa nchi za kundi la G77
Rais wa Cuba Miguel Díaz Canel Bermúdez ataongoza Ijumaa hii tarehe 15 hadi Jumamosi tarehe 16 September 2023 Mkutano muhimu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China kujadili mada "Changamoto za sasa za maendeleo: Jukumu la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu" .
Likiwa limeitishwa na Cuba, katika nafasi yake kama mwenyekiti wa muda nchi za G77 tangu Januari iliyopita, Kundi hili G77 ndilo kambi kubwa zaidi ya nchi zinazoendelea ndani ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa na kundi la mashauriano tofauti zaidi katika nyanja ya kimataifa.
Inajumuisha nchi wanachama 134 ambazo zinawakilisha theluthi mbili ya wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa na asilimia 80 ya idadi ya watu duniani, ambayo inaonyesha jukumu lake muhimu.
G77 Ilianzishwa mnamo Juni 15, 1964 kama kikundi cha nchi zinazoendelea na ambazo hazijaendelea kwa madhumuni ya kusaidiana, kudumisha na kusaidiana katika mijadala ya Umoja wa Mataifa, jukumu lake katika nyanja ya kimataifa lilikua na ujumuishaji uliofuata wa nchi za Ulimwengu wa Tatu.
Source : https://www.contraloria.gob.cu/noti...te-reunion-cumbre-del-grupo-de-los-77-y-china
15 September 2023
Havana, Cuba
RAIS DR. HUSSEIN MWINYI AKIHUTUBIA MKUTANO WA G77+CHINA MJINI HAVANA CUBA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundo la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akihutubia katika Mkutano huo, Dkt. Mwinyi amesema Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nguzo muhimu kwa nchi zinazoendelea kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza kuwa nchi hizo zinaweza kuendelea kiuchumi kupitia maendeleo katika sekta muhimu za kilimo, nishati, elimu, afya, madini, maendeleo ya muindombinu, maji na mazingira.
Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha namna nchi zinazoendelea zilivyoathirika na janga la maradhi ya UVIKO-19, bidhaa kupanda bei, mizozo ya kisiasa na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa baadhi ya changamoto zilisababisha kupanda kwa gharama za maisha na kudhoofisha jitahada za kujikwamua kiuchumi.
Mhe. Dkt. Mwinyi alikumbushia namna nchi zilizoendelea zilivyobanwa na teknolojia ya kutengeneza chanjo na kunyimwa msaada wa kiteknolojia ili zitengeneze chanjo zao na kusababisha kampuni za kutengeneza dawa za mataifa tajiri kupata faida kubwa kwa kuziuzia nchi zinazoendelea chanjo ya UVIKO-19.å
Mhe.Dkt. Mwinyi amezitanabaisha nchi za kundi la G77+China kuchukua changamoto hizo kama somo na zisibweteke kusubiri msaada kutoka mataifa yaliyoendelea.
Mkutano huo unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 15-16 Septemba 2023 unayakutanisha mataifa yanayoendelea unajadili changamoto zinazoikabili dunia baada ya kuathirika na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.
Mkutano huo umejikita kutafuta namna bora ya kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu ili kundi la G77+China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.
Kaulimbiu ya Mkutani inasema, “Changamoto za Maendeleo: Nafasi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu”.
Cumbre de Jefes de Estado y de Gobierno del Grupo de los 77 y China
tarehe 14 September 2023
Mwandishi
Na Pedro Rioseco
View: https://m.youtube.com/watch?v=Lhxm7jatf5U
Mh. Rais Dr. Hussein Mwinyi akiwa na balozi wa Tanzania nchini Cuba Mh. Humphrey Hesron Polepole uwanja wa ndege wa Aeropuerto Internacional José Martí de La Habana nchini Cuba.
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Hussein Mwinyi amewasili nchi Cuba kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Hassan katika mkutano wa nchi za kundi la G77
Rais wa Cuba Miguel Díaz Canel Bermúdez ataongoza Ijumaa hii tarehe 15 hadi Jumamosi tarehe 16 September 2023 Mkutano muhimu wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la 77 na China kujadili mada "Changamoto za sasa za maendeleo: Jukumu la Sayansi, Teknolojia na Ubunifu" .
Likiwa limeitishwa na Cuba, katika nafasi yake kama mwenyekiti wa muda nchi za G77 tangu Januari iliyopita, Kundi hili G77 ndilo kambi kubwa zaidi ya nchi zinazoendelea ndani ya Mfumo wa Umoja wa Mataifa na kundi la mashauriano tofauti zaidi katika nyanja ya kimataifa.
Inajumuisha nchi wanachama 134 ambazo zinawakilisha theluthi mbili ya wanachama wa Shirika la Umoja wa Mataifa na asilimia 80 ya idadi ya watu duniani, ambayo inaonyesha jukumu lake muhimu.
G77 Ilianzishwa mnamo Juni 15, 1964 kama kikundi cha nchi zinazoendelea na ambazo hazijaendelea kwa madhumuni ya kusaidiana, kudumisha na kusaidiana katika mijadala ya Umoja wa Mataifa, jukumu lake katika nyanja ya kimataifa lilikua na ujumuishaji uliofuata wa nchi za Ulimwengu wa Tatu.
Source : https://www.contraloria.gob.cu/noti...te-reunion-cumbre-del-grupo-de-los-77-y-china
15 September 2023
Havana, Cuba
RAIS DR. HUSSEIN MWINYI AKIHUTUBIA MKUTANO WA G77+CHINA MJINI HAVANA CUBA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundo la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akihutubia katika Mkutano huo, Dkt. Mwinyi amesema Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nguzo muhimu kwa nchi zinazoendelea kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza kuwa nchi hizo zinaweza kuendelea kiuchumi kupitia maendeleo katika sekta muhimu za kilimo, nishati, elimu, afya, madini, maendeleo ya muindombinu, maji na mazingira.
Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha namna nchi zinazoendelea zilivyoathirika na janga la maradhi ya UVIKO-19, bidhaa kupanda bei, mizozo ya kisiasa na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa baadhi ya changamoto zilisababisha kupanda kwa gharama za maisha na kudhoofisha jitahada za kujikwamua kiuchumi.
Mhe. Dkt. Mwinyi alikumbushia namna nchi zilizoendelea zilivyobanwa na teknolojia ya kutengeneza chanjo na kunyimwa msaada wa kiteknolojia ili zitengeneze chanjo zao na kusababisha kampuni za kutengeneza dawa za mataifa tajiri kupata faida kubwa kwa kuziuzia nchi zinazoendelea chanjo ya UVIKO-19.å
Mhe.Dkt. Mwinyi amezitanabaisha nchi za kundi la G77+China kuchukua changamoto hizo kama somo na zisibweteke kusubiri msaada kutoka mataifa yaliyoendelea.
Mkutano huo unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 15-16 Septemba 2023 unayakutanisha mataifa yanayoendelea unajadili changamoto zinazoikabili dunia baada ya kuathirika na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.
Mkutano huo umejikita kutafuta namna bora ya kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu ili kundi la G77+China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.
Kaulimbiu ya Mkutani inasema, “Changamoto za Maendeleo: Nafasi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu”.