Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,099
- 10,145
Jeshi la polisi limesema limeona baadhi ya viongozi wa CHADEMA wakihamasisha kukusanyika ili kumpokea mmoja wa kiongozi wanayetarajia kurejea nchini Julai 27, 2020.
Polisi wamesema hawana taarifa rasmi ya mikusanyiko hiyo inayohamasishwa mitandaoni. Wamesema ni haki yao kukusanyika lakini hakuna haki bila wajibu, hivyo wamewataka viongozi hao kufuata sheria.
Aidha jeshi la polisi limesema linafuatilia wanaosambaza ujumbe wa kuhamasisha wanafunzikugoma kwa kutoingia madarasani ili kushinikiza Bodi ya Mikopo kurejea masharti ya mkataba ya fedha ya kujikimu.
Polisi wamesema hawatasita kuwachukulia hatua wanaokiuka sheria, kwa kuitisha mikusanyiko na maandamano yasiyo na Baraka za kisheria, hivyo wamewataka wanafunzi wafuate njia stahiki za kufikisha malalamiko yao na sio kukiuka sheria.
Polisi wamesema hawana taarifa rasmi ya mikusanyiko hiyo inayohamasishwa mitandaoni. Wamesema ni haki yao kukusanyika lakini hakuna haki bila wajibu, hivyo wamewataka viongozi hao kufuata sheria.
Aidha jeshi la polisi limesema linafuatilia wanaosambaza ujumbe wa kuhamasisha wanafunzikugoma kwa kutoingia madarasani ili kushinikiza Bodi ya Mikopo kurejea masharti ya mkataba ya fedha ya kujikimu.
Polisi wamesema hawatasita kuwachukulia hatua wanaokiuka sheria, kwa kuitisha mikusanyiko na maandamano yasiyo na Baraka za kisheria, hivyo wamewataka wanafunzi wafuate njia stahiki za kufikisha malalamiko yao na sio kukiuka sheria.