Polisi wamsaka ...

Polisi wamsaka ...

Natamani kumsikia John Mnyika arudie tena ule usemi Raisi Magufuli ni Dhai##### halafu nione hatua gani itachukuliwa kwake! By the way nchi inavyoendeshwa kwa utawala huu wa JPM Libya is coming very soon!
 
Hivi toka lini mtu akawa dikteta wakati anajua baada ya miaka kumi atarudi uraiani? Magufuli sheria mnalinda, nyie kama mna hoja mpingeni kwa hoja siyo kulalama kama watoto wadogo

Kwa sababu ana uhakika atakayemrithi ndo yule yule kutoka CCM ile ile....wanalindana.
 
Uzi huu unaweza kabisa kuwa muafaka kuhusu unyanyaswaji mkubwa unaofanywa na Polisi nchini katika kubaka demokrasi ili kutimiza lengo la Dikteta la Watanzania kuishi kwenye nchi iliyojaa vitisho vya hali ya juu. Kufungua uzi mwingine pia wa manyanyaso ya Polisi nchini RUKHSA.
Huu uzi sijui kama utadumu sana bila kupigwa panga
 
Ngoja kwanza niendelee kula bapa na nyama mbuzi choma si mnajua leo ni weekend wakuu!!
 
Unadhani polisi wanapaswa kufanya nini au kuchukua hatua gani kama watu hawatii sheria bila shuruti?
 
Hilo nalijua Mkuu, uzi huu hauna maisha marefu utapotezwa muda si mrefu ujao. JF ya siku hizi si JF ile ya zamani. Wakiufuta basi nitaamua kupumzika maana haina maana ya kuja hapa jamvini kujadili kuhusu mustakabali wa nchi yetu huku tukiwa hatuna uhuru wa kufanya hivyo.

Huu uzi sijui kama utadumu sana bila kupigwa panga
 
Wanashindwa kuelewa kuwa na wao wana ndugu hivyo wanawaumiza pia
 
Kamata piga risasi wachochezi wote Si MDA wa siasa Ni kazi tuu Na kujenga uchumi
Mkuu naona umevimbiwa na kuchoshwa na amani tuliyo nayo,inakuwaje unaongea mambo ya simanzi namna hiyo?huo ndiyo uhuru kweli?unaichonganisha serikali na wananchi bila hata aibu?ukikamatwa na kushitakiwa utalalamika?ebu kuweni na utaifa kwanza
 
walaaniwe sana viongozi wetu wastaafu na viongozi wetu wa dini kwa kukaa kimya. hawa wanasubiri maafa ndipo waje kusuluhisha....
 
kinya19062016.jpg



Tuzo za Mo zitaendelea kukosa wakupewa kwa miaka mingi sana ijayo mkuu, utawala bora, haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, uwajibikaji vinazidi kuwa bidhaa adimu sana kwenye hizi nchi zetu.
 
Mkuu Samaritan hakuna aliye salama, labda kama maovu yote unayoyaona nchini mwetu uyafumbie macho na kuamua kukaa kimya. Kitu ambacho si sawa. Kwanini Watanzania tukae kimya kama tunaona nchi yetu inaharibika? Kwanini tukae kimya kama haturidhiki na uongozi wa nchi na maamuzi yao mbali mbali ambayo yanatuathiri Watanzania? Je, hao wanaotaka kutunyamazisha tusiwakosoe na kukemea maovu mbali mbali nchini wao wana hati miliki ya Tanzania? Jibu ni HAPANA Tanzania ni yetu sote.
Uhuru wa kuwasiliana na kuongea ni msingi wa demokrasia.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom