BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
- Thread starter
- #21
Kabisa Mkuu juzi nimeona tena Mo Ibrahim karudisha bulungutu lake Bungeni kwa kukosa Kiongozi mstaafu wa Afrika akiwemo Kikwete kushindwa kutimiza vigezo vya utawala bora walipokuwa madarakani.
Inashangaza sana kuona mtu anachukua uongozi wa nchi na kuahidi mazuri mengi ikiwemo kulinda maslahi ya Tanzania na Watanzania lakini akishaingia tu Ikulu basi anageuka na kulinda maslahi ya wezi, mafisadi, watoa rushwa na wapokea rushwa na huyu wa sasa kaingia na jipya la kukandamiza haki zetu za kikatiba katika kujadili mambo mbali mbali nchini ikiwemo mustakabali wa nchi yetu. Anataka tuwe mazombie na maovu yote nchini tuyanyamazie. Inasikitisha sana kusema kweli. Na hivyo vyama vya upinzani watangaze rasmi kwamba vimefutwa.
Inashangaza sana kuona mtu anachukua uongozi wa nchi na kuahidi mazuri mengi ikiwemo kulinda maslahi ya Tanzania na Watanzania lakini akishaingia tu Ikulu basi anageuka na kulinda maslahi ya wezi, mafisadi, watoa rushwa na wapokea rushwa na huyu wa sasa kaingia na jipya la kukandamiza haki zetu za kikatiba katika kujadili mambo mbali mbali nchini ikiwemo mustakabali wa nchi yetu. Anataka tuwe mazombie na maovu yote nchini tuyanyamazie. Inasikitisha sana kusema kweli. Na hivyo vyama vya upinzani watangaze rasmi kwamba vimefutwa.
Tuzo za Mo zitaendelea kukosa wakupewa kwa miaka mingi sana ijayo mkuu, utawala bora, haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, uwajibikaji vinazidi kuwa bidhaa adimu sana kwenye hizi nchi zetu.