Polisi wamsaka ...

Polisi wamsaka ...

Hilo la idara ya polisi ni nzuri sana Watanzania wengi hawawezi kukubaliana nawe hata siku moja.

Tatizo mnalaumu idara ya polisi bila kufahamu kuwa polisi wanafanya kazi yao ya kila siku nayo ni kutekeleza maagizo kutoka kwa watawala, nashauri tusiwalaumu polisi wetu bali lawama zote zipelekwe kwa wanaotoa hizi ORDERS. Idara yetu ya Polisi ni nzuri sana sema aina ya wanasiasa tulionao ndio wanawaingiza matatizoni.
 
Magu hawezi pingana na historia ya dunia.

Hakujawahi kutokea kwa Taifa lolote tokea kuumbwa kwa dunia hii ambapo nguvu ya dola iliwahi kushinda nguvu ya Umma uliojizatiti.

Ajikumbushe kidogo tu kwa hali iliyojitokeza miaka michache tu iliyopita kule Misri, ambapo vifaru vilivyokuwa vimeamrishwa na Mubarak ili vikawapondeponde wananchi, badala yake vifaru hivyo havikuweza kuwapondaponda wananchi hao na badala yake wananchi hao 'walivikwea' vifaru hivyo kama sisi tunavyoyapanda mabasi ya mwendokasi!
 
Magu pia asijidanganye, itakuwa ndoto kwa Tanzania yetu kuingia kwenye uchumi wa kati wa nchi ya viwanda kama nchi itaendeshwa na mfumo wa ONE MAN SHOW.

Kwa maana ya kutoruhusu mawazo mbadala na badala yake nchi iendeshwe kwa staili ya zidumu fikra za Mwenyekiti!
 
Du ! Inawezekana kweli?hivi ni kwa nini polisi polisi lakini vitro byao vinavamiwa kwa majanga na marungu?
 
Mkuu Hao Mapolisi Ni Lazima Wafanye Hivyo Kwa Kukitumikia Chama Cha Green, Coz Wakisha retire tu huwa Wanategemea Kuteuliwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya
 
Inawezekana kabisa akawa na lengo zuri,ila njia anayotumia ni mbaya Sana! Nafikiri tumpe ushauri wa njia za kufanya kazi vizuri kuliko kupo
nda mda wote
Unataka kumshauri JPM? Are you sane?
 
BAK yanayoendelea kwenye nchi yetu ukiyawaza unaweza kupasuka kichwa bila kufanikiwa kupata majibu ngoja niende kunywa ndovu yangu baridii
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Friday, June 24, 2016
Polisi wafunguka minong’ono kuwa wanaipendelea CCM

By Herieth Makwetta, Mwananchi hmakweta@mwananchi.co.tz


Dar es Salaam. Jeshi la Polisi limekanusha taarifa kuwa linakipendelea chama tawala cha CCM, bali limesema litaendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo cha luninga cha TBC usiku huu, Kamishna wa oparesheni na mafunzo wa Jeshi hilo, CP Nsato Marijani amesema Polisi ni taasisi inayofanya kazi kwa mujibu wa sheria bila kushinikizwa na mtu, watu au taasisi yoyote ile.

Amesema taarifa mbalimbali zimekuwa zikienezwa na watu wasio na uelewa kuhusu kazi za jeshi hilo kinyume na hali iliyopo.

“Polisi hatuko juu ya sheria na hata tunapofanya kazi tunakuwa makini ili kuepuka kukiuka miiko ya kazi yetu,” amesema.

Amesema jeshi hilo linaweza kushtakiwa Mahakamani kama litakuwa limetenda kinyume cha Sheria.

“Kazi yetu ni kuhakikisha tunawalinda raia na mali zao, na hatuwezi kwenda kinyume na hapo.”

Amesema polisi hawezi kuua watu au kuwanyanyasa eti kwa lengo la kukipendelea chama tawala.

Amesema kile kinacho endelea katika Kisiwa cha Pemba, Zanzibar kwa sasa, hakiwezi kufumbiwa macho na jeshi hilo kwani kinaashiria uvunjifu wa amani.

Kamishna Marijani amesema:

“Polisi hawawezi kukaa kimya pale wanapobaini mali za raia zinaharibiwa na kundi la watu fulani kwa makusudi, hiyo ni hujuma, lazima tufanye kazi ya kulinda mali hizo kama kanuni yetu inavyotutaka, kulinda usalama wa raia na mali zao.”
 
Ndugu watanzania, naomba mniombee. Nimejitoa mhanga kuwakomboa watu wa hali ya chini ambao naamini ndiyo walionipa kura nyingi. Mimi sikuchaguliwa na matajiri. Mnataka nimtumbue hapa hapa au? Namlipia huyu kijana akapate huduma huko regency. Hivi mlitarajia serikali iendelee kuwalipia na kuwakumbatia hawa va la za ? Haiwezekani kabisa hao wanaowatetea nao ni va li za. Hakuna siasa vyuoni. Nakumbuka hata JK hakuwa hata na kadi ya TANU alipokuwa chuo. MTAJIJU.
Mwongo mkubwa.

Kikwete na Lowasa walikuwa viongozi wa TANU YOUTH LEAGUE wakati wanasoma UDSM. Hivi unaweza kuwa kiongozi bila ya kuwa na kadi?? Kuna watu ni waongo hadi wanatia kinyaa.
 
Duh wangeweza kusema ukweli
Friday, June 24, 2016
Polisi wafunguka minong’ono kuwa wanaipendelea CCM

By Herieth Makwetta, Mwananchi hmakweta@mwananchi.co.tz


Dar es Salaam. Jeshi la Polisi limekanusha taarifa kuwa linakipendelea chama tawala cha CCM, bali limesema litaendelea kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na kituo cha luninga cha TBC usiku huu, Kamishna wa oparesheni na mafunzo wa Jeshi hilo, CP Nsato Marijani amesema Polisi ni taasisi inayofanya kazi kwa mujibu wa sheria bila kushinikizwa na mtu, watu au taasisi yoyote ile.

Amesema taarifa mbalimbali zimekuwa zikienezwa na watu wasio na uelewa kuhusu kazi za jeshi hilo kinyume na hali iliyopo.

“Polisi hatuko juu ya sheria na hata tunapofanya kazi tunakuwa makini ili kuepuka kukiuka miiko ya kazi yetu,” amesema.

Amesema jeshi hilo linaweza kushtakiwa Mahakamani kama litakuwa limetenda kinyume cha Sheria.

“Kazi yetu ni kuhakikisha tunawalinda raia na mali zao, na hatuwezi kwenda kinyume na hapo.”

Amesema polisi hawezi kuua watu au kuwanyanyasa eti kwa lengo la kukipendelea chama tawala.

Amesema kile kinacho endelea katika Kisiwa cha Pemba, Zanzibar kwa sasa, hakiwezi kufumbiwa macho na jeshi hilo kwani kinaashiria uvunjifu wa amani.

Kamishna Marijani amesema:

“Polisi hawawezi kukaa kimya pale wanapobaini mali za raia zinaharibiwa na kundi la watu fulani kwa makusudi, hiyo ni hujuma, lazima tufanye kazi ya kulinda mali hizo kama kanuni yetu inavyotutaka, kulinda usalama wa raia na mali zao.”
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mwongo mkubwa.

Kikwete na Lowasa walikuwa viongozi wa TANU YOUTH LEAGUE wakati wanasoma UDSM. Hivi unaweza kuwa kiongozi bila ya kuwa na kadi?? Kuna watu ni waongo hadi wanatia kinyaa.
Ulijifunza lugha? Unajua maana ya kejeri?
 
Back
Top Bottom